08/02/2026
Tasnia ya muziki nchini Burundi 🇧🇮 ipo kwenye majonzi mazito kufuatia kifo cha msanii mkongwe wa Hip Hop na Rap, Jeez-B, aliyekuwa akiheshimika sana katika muziki wa kizazi kipya.
Kwa mujibu wa taarifa, Jeez-B alifariki dunia kutokana na maradhi ya figo, baada ya kuwa amelazwa kwa siku kadhaa katika Hospitali ya Kijeshi ya Kamenge (Hôpital Militaire de Kamenge HMK).
📌 Marehemu Jeez-B alikuwa na mashabiki wengi kutokana na nyimbo zake zilizogusa maisha halisi ya kijamii, na aliwahi kushirikiana na wasanii wakubwa akiwemo Big Fizzo pamoja na T-Max.
Kifo chake ni pigo kubwa kwa muziki wa Burundi, hususan kwa Hip Hop na Rap, ambapo alichukuliwa k**a kielelezo na msanii mwenye uzoefu mkubwa.
🕯🕊 Mungu ailaze roho ya marehemu Jeez-B mahali pema peponi.