09/05/2026
UPDATES|| TANZANIA, AFRIKA KUSINI WAIBUKA WASHIDNI KATIKA UTALII.
Nchi kadhaa za Afrika zimeonesha ukuaji mzuri katika sekta ya utalii, huku ikitarajiwa ukuaji huo kuendelea kwa kasi na kuongeza mchango katika uchumi na jamii licha ya changamoto mbalimbali duniani.
Hayo yameelezwa katika ripoti mpya ya Baraza la Utalii na Usafiri Duniani (WTTC) ijulikanayo k**a Travel and Tourism Economic Impact 2025, iliyowasilishwa katika mkutano wa baraza hilo unaofanyika ndani ya meli ya kitalii ya Crystal Cruises, iliyowasili leo Jumamosi Mei 9, 2026 katika Bandari ya Alexandria nchini Misri.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, Afrika Kusini yenye asilimia 7.7 na Tanzania yenye asilimia 7.4 zimeongoza barani Afrika kwa kuvutia uwekezaji katika sekta ya utalii, zikiwa juu ya wastani wa dunia wa asilimia 3.8.
Aidha, Afrika Kusini, Tanzania na Kenya zimeonyesha mafanikio katika mapato yanayotokana na watalii kununua bidhaa na kuzipeleka nje ya nchi.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii wa Tanzania, Dkt. Hassan Abbasi ni miongoni mwa washiriki wa mkutano huo.