ARISE GOOD STORY

ARISE GOOD STORY ARISE GOOD STORY hapa utasoma simulizi nzury kutoka kwa waandishi wazuri

23/01/2021

Karibuni kwenye simulizi mpya kabisa, comment zenu na like ndio zitafanya niendelee kuipost humu. Karibuni

NIMETUMWA: 1
By: Atuganile Mwakalile
Whatsapp: 0714443433

Ilikuwa ni siku ya Ijumaa ambapo wanafunzi siku ya leo waliruhusiwa mapema sana kurudi nyumbani, na walikuwa na furaha sana ya kuwahi kurudi nyumbani k**a kawaida ya wanafunzi.
Berinda na Blenda walikuwa ni ndugu wa mama na baba mmoja ambao walipishana mwaka mmoja tu, hivyo watu wengi waliwaita mapacha na walifanana sana pia walisoma pamoja katika hii shule, kwahiyo siku ya leo ilikuwa ni furaha sana kwa upande wao pia.
Basi waliongozana na wenzao kurudi nyumbani, njiani waliachana na wenzao na kuanza safari wao wawili ya kurudi nyumbani kwao huku wakiongea ongea mambo yao mbalimbali yanayowafurahisha.
Walipokuwa njiani kukaribia na nyumbani kwao, Blenda alihisi haja ndogo na kumwambia mwenzie,
“Nataka nikajisaidia, ngoja niingie hapo”
Mwenzie akasema,
“Mmmh Blenda usiende peke yako, mama alishakataza kabisa hiyo tabia. Ngoja twende wote”
“Jamani na wewe Berinda, si unisubiri kidogo hapo”
“Hapana, mimi ni dada yako Blenda”
“Dada uliyenipita mwaka mmoja tu!!”
Kisha Blenda akacheka na kuingia kwenye kichaka kwaajili ya kujisaidia, wakati huo Berinda alikuwa akimsubiria ila alishangaa kuona ndugu yake amekawia kutoka kwenye kile kichaka ikabidi amfate na kumkuta amesimama huku ameshika karatasi, Berinda akamuuliza,
“Wewe Blenda hilo karatasi ni la nini? Tunachelewa nyumbani”
“Limeandikwa neno moja tu linanishangaza, nimeliokota hapo”
Berinda alisogea na kulisoma, liliandikwa kwa herufi kubwa,
“NIMETUMWA”
Berinda akamuangalia Blenda na kumuuliza,
“Umelipata wapi?”
Blenda alijibu bila wasiwasi,
“Nimeliokota hapo chini”
Akionyesha kwa nyuma yake, walipogeuka hapo nyuma walikuta mwili wa binadamu ukiwa umenyongwa, wakajikuta wakitupa lile karatasi na kupiga kelele halafu wakatoka kwenye kile kichaka.

Walikimbia sana hadi walipofika chini ya mti walisimama huku wakiwa wanahema sana, basi Berinda akamuuliza mdogo wake,
“Inamaana Blenda hukuona? Hukuona pale k**a pana tatizo?”
Blenda alikuwa anahema sana na kusema,
“Sikuona chochote, niliokota tu lile karatasi. Naogopa dada, naogopa sana”
“Inaogopesha sana Blenda, twende tukamwambie mama”
“Mmmmh dada sidhani k**a ni wazo jema kumwambia mama, tusimwambie kabisa kuhusu hili jambo. Mama atatupiga sana”
“Kwanini atupige? Tumeona kitu cha tofauti ni lazima kutoa taarifa”
“Hapana Berinda, tusifanye hivyo tafadhali. Kwanza mama atauliza tulikuwa tunatafuta nini huko porini si unamjua mama alivyo mkali! Halafu atanipiga sana mimi sababu anajua kuwa mimi ni mbishi sana”
Berinda akakubaliana pale na mdogo wake Blenda kuwa wasiende kumwambie mama yao kuhusu lile tukio.
Basi waliondoka pale na kufika nyumbani ambapo mama yao aliwashangaa pia kwa wao kuwahi kurudi,
“Mbon mmewahi sana kurudi? Mmeshadanganyana huko eeeh!!”
“Hapana mama leo tumetolewa mapema”
“Bora umejibu wewe Berinda maana angejibu huyu Blenda nisingeamini kabisa, ni mjanja mjanja sana huyu mdogo wako”
Wale watoto walikaa kimya tu kisha mama yao aliwaonyesha chakula cha wao kuweza kula na kufanya waende kuvua yale mavazi ya shule ili wapate kula.

Wakati Berinda na Blenda wakila, kuna mtu alimfata mama yao kisha mama yao akatoka kwa haraka sana pale nyumbani na kufanya wenyewe wasielewe chochote ila kuendelea kula tu pale.
Walipomaliza kula, Blenda alianza kumwambia dada yake,
“Au mama ameitwa kwenda kuona yule mtu aliyeuwawa?”
“Nadhani itakuwa hivyo Blenda, ila tusifikirie hayo sana yatatuchanganya akili mdogo wangu”
“Kweli dada yatatuchanganya akili”
Basi walipomaliza kula waliondoka zao na kwenda kucheza na watoto wa mitaani.
Waliwakuta watoto wakicheza mchezo wa kukimbia na kujificha, wakaungana nao, kwahiyo na wao walikuwa wanakimbia na kwenda kujificha.
Basi muda huu watoto wote walipatikana kasoro Blenda hadi walianza kuulizana,
“Jamani Blenda ameenda kujifichia wapi? Ni mambo gani haya mtu anajificha hadi haonekani?”
Ikabidi watoto wote waingie kwenye msako wa kumtafuta Blenda sasa, wakati wakiendelea kutafuta Berinda akaona kuna jumba ambalo halijaisha yani ni gofu tu akaamua kuingia humo huku akiita,
“Blenda, Blenda, Blenda”
Kweli kabisa Blenda akajibu,
“Nipo humu dada”
Basi Berinda alifata ile sauti ya Blenda ilipokuwa inatoka, alimkuta Blenda amesimama huku ameshika kipande cha karatasi, akamuuliza,
“Umeshika nini hiko?”
“Kimeandikwa k**a kule dada”
“Kivipi?”
Berinda akasogea ili kuangalia, akaona kile kipande cha karatasi kimeandikwa kwa herufi kubwa pia,
“NIMETUMWA”
Berinda akashtuka sana na kumuuliza Blenda,
“Umekitoa wapi?”
“Hapo”
Yani sehemu ambayo Blenda alionyeshea mkono kulikuwa na mwili wa mwanadamu umelazwa pale, na yeye alionekana amenyongwa.
Wote wawili walishtuka kisha Blenda alitupa kile kikaratasi na kukimbia pamoja na dada yake, walikimbia hadi walipofika nyumbani ndio walipumzika.

Berinda akamuuliza pale mdogo wake,
“Ulikuwa unatafuta nini kwenye lile lijumba Blenda? Mbona una hatari hivyo mdogo wangu?”
“Nilienda kujificha dada, hata sikujua k**a nitakutana na jambo k**a lile”
“Kujificha gani huko? Wenzio wote tunajificha karibu, wewe kwanini unaenda kujificha mafichoni k**avile? Ona sasa kwa ambacho tumeona kule? Tumwambie mama?”
“Uwiiii dada hapana, usimwambie mama. Atanipiga sana aniue jamani, mama alishatukataza kucheza michezo ya kujificha, dada usimwambie mama”
“Ni kweli mama katukataza michezo ya kujificha ila wewe nae umezidi, kujificha gani sasa kule? Kila mtoto alikuwa anakutafuta wewe Blenda maana wote walipatikana kasoro wewe, kumbe upo kwenye jumba ambalo lina mauaji. Haya mambo mbona yanatisha, wale watu wamekufa ujue!!”
“Najua ndio dada, ila mimi sikuona chochote wakati nashika lile karatasi dada yangu”
“Inaogopesha na kusikitisha, kwahiyo unasisitiza kuwa tusimwambie mama!”
“Ndio tusimwambie mama”
Basi wakaamua kunyamza maana wakaona wakisema itakuwa ni balaa tupu.

Muda kidogo mama yao alirudi pale nyumbani huku akisema kwa masikitiko,
“Jamani kuna mambo ya ajabu yameingia, kuna mtu amekutwa msituni ameuwawa halafu pembeni yake umekutwa ujumbe umeandikwa kuwa NIMETUMWA tena kwa herufi kubwa, hata sijui ni nani aliyefanya ufedhuli huu. Haya mambo yanaogopesha sana”
Berinda na Blenda walikuwa kimya kabisa, kisha mama yao akawaambia,
“Sasa Berinda utaosha vyombo maana wewe ndio mkubwa halafu Blenda utaenda dukani kununua mafuta ya kura ili nipike chakula cha usiku”
“Sawa mama”
Basi k**a walivyoambia, Berinda alisogea kwenye vyombo na kuanza kuosha vyombo wakati huo Blenda alienda zake dukani alikotumwa.

Hadi berinda alimaliza kuosha vyombo, mdogo wake Blenda alikuwa hajarudi, basi Berinda akaamua kwenda kumfatilia maana alijua wazi kuwa mama yao akijua kuwa hajarudi itakuwa ni msala zaidi.
Basi alienda hadi dukani ila hakumkuta Blenda na aliambiwa kuwa kaondoka muda mrefu tu, akajiuliza kuwa atakuwa kapitia wapi, basi akaanza kupita kwenye njia huku akiita,
“Blendaaa, Blendaaaa, Blendaaaa”
Kuna mahali alipita na kuisikia sauti ya Blenda,
“Nipo huku dada”
Basi Berinda alizunguka nyuma ya nyumba hiyo na kumkuta Blenda akiwa ameshika karatasi, kwanza Berinda alishtuka sana na kuanza kuangaza angaza labda ataona mwili mwingine wa binadamu ila hakuona chochote, akamsogelea mdogo wake na kumuuliza,
“Wewe Blenda, ni nini hiko umeshika”
“Soma dada”
Berinda aliangalia, lilikuwa ni karatasi lililoandikwa kwa herufi kubwa,
“NIMETUMWA”
Basi Berinda akamuuliza,
“Umelitoa wapi?”
“Hapo”
Walipoangalia wakauona mwili wa mtu akiwa amenyongwa k**a wale wawili, hapo waliogopa sana na kuanza kukimbia.

Walikimbia hadi nyumbani kwao huku wakiwa wanapumua sana hata kuingia ndani hawakuingia, ila Berinda alimsema mdogo wake,
“Una nini leo Blenda? Unaokota karatasi za ajabu na kuna mambo ya ajabu”
Mara Blenda akasema,
“Dada umeona ile karatasi pale chini, basi huwa naona k**a vile”
Kisha Blenda akainama na kuokota lile karatasi kisha wakakuta imeandikwa vilevile kwa herufi kubwa,
“NIMETUMWA”
Walijikuta wakiogopa kuangalia hata mahali ambapo wameokota lile karatasi maana walijua lazima kuna mtu kauwawa pia.

Itaendelea….!!!
Kwa mawasiliano 0714443433 au 0765692210
By, Atuganile Mwakalile.

23/01/2021

LIKE, COMMENT NA SHARE NDIO ZITAFANYA NIONE UMUHIMU WA KUENDELEA KUIPOST

NIMETUMWA: 2
By: Atuganile Mwakalile
Whatsapp: 0714443433

Walijikuta wakiogopa kuangalia hata mahali ambapo wameokota lile karatasi maana walijua lazima kuna mtu kauwawa pia.
Walikumbatiana kwa uoga sana, na aliyewashtua pale ni mama yao ambaye aliwaambia kwa ukali,
“Hivi nyie watoto mna akili timamu kweli? Hebu njooni upesi”
Hawakuangalia hata nyuma zaidi ya kumkimbilia mama yao na kumkumbatia, ambapo aliwauliza,
“Kuna nini kwani?”
Berinda akataka kumueleza mama yao ila Blenda alimfunga mdomo dada yake ili asiseme hadi mama yao akawaingiza ndani na kuwauliza kwa ukali,
“Kuna nini?”
Akajibu Blenda,
“Hakuna kitu mama”
“Wajinga nyie, subirini”
Mama yao akaingia chumbani, hapo Berinda akamwambia Blenda,
“Ujue mama atatupiga?”
“Ndio atatupiga ila tutafute uongo wa kumwambia”
“Uongo gani?”
Mara mama yao akatoka na mkanda wa suruali wa baba yao huku akiwaambia,
“Leo mtanieleza mnachokificha”
Ila kabla hajaanza kuwaadhibu, mlango uligongwa kwa nguvu na hivyo alienda kufungua na kukuta watu wengi wamejaa nje kwake, alistaajabu sana akiuliza,
“Kuna nini?”
“Yani mauaji yametokea nje ya nyumba yako hujui? Ni hatari hii mama B, tumeingiliwa jamani, mji wetu umeingiliwa huu”
Basi mama B alitoka nje kuungana na wengine kushangaa mambo yaliyotokea.

Ndani alibaki Berinda na Blenda ambapo walianza kuongea,
“Sasa Blenda mdogo wangu, haya mambo mbona ni makubwa sana!! Tunatakiwa kumwambia ukweli mama bila kujali kitu chochote kile”
“Tatizo tukimwambia ukweli atatupiga hadi tufe jamani, haswa mimi. Unajua mama yetu ni mkali sana eeeh!!”
“Kwahiyo tuendelee kukaa kimya?”
“Ndio dada, niokoe mdogo wako. Mama ni mkali sana”
“Mmmmh sawa, unajua nakupenda sana mdogo wangu Blenda”
Basi wakakumbatiana pale na kuanza mazungumzo yao mengine huku mama yao akiwa bado nje.

Mama B aliingia ndani wakati giza tayari limeingia na kuanza kuongea na watoto wake kuhusu mauwaji yaliyotokea,
“Hivi jamani mauwaji yanatokea nje ya nyumba yangu halafu mimi sijui? Natetemeka mimi jamani, naogopa sijui nini kinaendelea hapa”
Akatulia kidogo na kuwauliza,
“Wakati mnarudi hamkuona chochote?”
Blenda alijibu,
“Hatukuona chochote mama”
“Sawa, yani hapa kesho tumeambiwa kikao cha wanakijiji wote ili tujue kuwa hili jambo linasababishwa na nani na kwanini ipo hivi. Naogopa sana, kesho asubuhi ni kwenye kikao”
“Na watoto tutaruhusiwa?”
“Mmmmh sijui, tutajua huko huko”
“Sawa mama”
Kisha mama yao kwa huu muda ilibidi aandae chakula na waweze kula halafu kwenda kulala.

Wakati wamelala Blenda alijiwa na ndoto, katika hii ndoto alikuwa anayaona matukio yote ya mauwaji, yani alikuwa anaona kuna mtu akiwanyonga watu ila hakuona sura ya mtu huyo, pia alimuona huyu mtu ambavyo alikuwa akiacha ujumbe kwa kila aliyekuwa anamnyonga. Yani Blenda aliona kila kitu kwenye ndoto, kisha akasikia sauti ya huyu mtu,
“Kesho lazima niue watatu kwenye kijiji chako”
Blenda alishtuka kwa uoga sana hadi alikuwa akitetemeka, dada yake na yeye aliamka na kumuuliza,
“Tatizo ni nini Blenda?”
“Nimeota vibaya dada”
“Kuhusu nini?”
Blenda alimsimulia dada yake ndoto nzima, hapo hadi Berinda aliogopa pia na kumwambia,
“Blenda mdogo wangu, tumwambie mama kuhusu hili jambo”
“Mmmh dada tusimwambie, naogopa mama akijua itakuwa balaa kubwa sana”
“Sasa balaa kivipi wakati ni ndoto?”
“Unamsahau mama wewe, atauliza ni kwanini niote hivyo. Naogopa sana, tusimwambie mama”
“Kweli atauliza, basi tuendelee kulala mdogo wangu”
Ni kweli kabisa wakaamua kuendelea tu kulala kwa huu muda.

Mapema kabisa mama yao wakina Berinda alijiandaa kwaajili ya kikao cha wanakijiji wote, na aliwaaga pale wanae kuwa anaenda kwenye kikao,
“Sasa muhakikishe usafi wa nyumba, vyombo na kila kitu kiwe kisafi humu ndani. Nadhani tumeelewana?”
“Sawa mama”
Kisha mama yao akaondoka zake, walibaki pale wenyewe na kuanza kubishana kuhusu kazi za kufanya,
“Wewe Blenda utasafisha ndani halafu mimi nitaenda kuosha vyombo”
Blenda alimbishia dada yake pale,
“Hapana, wewe ndio mkubwa usafishe ndani halafu mimi nikaoshe vyombo”
“Ila Blenda wewe ni mbishi sana, kila siku mama analalamika kuwa hutakatishi vyombo vyako”
“Analalamika ndio ila huwa naosha au sioshi?”
“Unaosha”
“Basi na leo nataka nikaoshe vyombo halafu wewe safisha ndani”
Berinda hakumbishia mdogo wake maana yeye hakuwa mbishi sana, hivyo walitoa vyombo nje kwaajili ya Blenda kuanza kuviosha halafu Berinda alibaki ndani akisafisha nyumba.

Wakati Berinda akiendelea kusafisha nyumba akaisikia sauti ya Blenda ikiita kwa nguvu na mara Blenda aliingia ndani kwa kasi ya ajabu huku akihema na kumfanya Berinda amuulize,
“Kuna nini wewe?”
“Dada, nimeokota tena karatasi”
“Kheeee Blenda tena?”
“Ndio dada, hii hapa”
“Khaaaa umekuja nayo ndani?”
“Naogopa dada”
Basi Berinda aliisogelea ile karatasi iliandikwa vile vile kwa herufi kubwa,
“NIMETUMWA”
Berinda akashika kichwa na kusema,
“Inamaana kuna mtu ameuwawa hapa nyumbani kwetu?”
“Ndio dada”
“Naogopa, twende tukawaambie tu huko kwenye kikao, k**a mambo yenyewe ndio haya basi na sisi tutauwawa mdogo wangu”
Basi wakaamua kutoka ndani kwa kasi sana bila kuangalia sehemu yoyote ile maana waliogopa kubambana na maiti k**a ilivyokuwa jana yake.

Wakakimbia sana kuelekea ambapo kulikuwa na kikao cha watu wote pale kijijini, kisha waanza kusikiliza ambavyo pale walikuwa wakiongea,
“Mnajua hili sio jambo la kawaida eeeh!! Haiwezekani kabisa, watu wauwawe halafu kuwe na ujumbe kuwa nimetumwa, je ni nani anayefanya hayo mauwaji? Ametumwa na nani? Ni mambo ya ajabu sana haya”
Mwingine akaongea,
“Jamani hapa tutaongea tu bila kupata hitimisho, kila aliyeuwawa anakutwa na ujumbe kwenye karatasi. Kinachofaa kwasasa naona tumtafute mtaalamu anayejua kuangalia karatasi imeshikwa na nani, yani muhusika wa ile karatasi ni nani, hapo itakuwa rahisi kujua kuwa ni nani anayefanya hayo mauaji na kuacha ule ujumbe kwa marehemu”
Blenda aliogopa na kutupa kile kikaratasi, basi dada yake akamwambia,
“Unaona Blenda, nilikwambia kushika shika hilo karatasi sio swala zuri kabisa, sasa wakiangalia si wataona ni wewe unayeshikashika hizo karatasi?”
“Sasa tufanyeje dada?”
“Ile karatasi usingeitupa, tungeenda kuichoma moto”
“Sawa”
Blenda akageuka kuikota tena ile karatasi ila alishtuka sana pale na kumwambia,
“Dada, dada ona”
Berinda alipoangalia waliona ni mwili wa binadamu umelala pale, kwakweli waliogopa sana na kutetemeka, hapo hapo walikimbia na kuingia kwenye kile kikao kwa kasi sana hata wanakijiji waliwashangaa,
“Kuna nini nyie?”
Berinda alijibu kwa uoga,
“Kuna mtu ameuwawa hapo njiani na nyumbani kwetu nje kuna mtu ameuwawa”
Wale wanakijiji walishangaa sana na hapo waliamua kuambatana na hawa watoto ili kwenda eneo la tukio.
Walifika hapo njiani ambapo wakina Blenda waliona mwili ila hapakuwa na mwili wowote, walitingisha vichwa tu kisha wakaenda nao hadi nyumbani kwakina Blenda napo hapakuwa na mwili wowote ule.

Itaendelea….!!!
Kwa mawasiliano 0714443433 au 0765692210
By, Atuganile Mwakalile.

24/06/2020

WhatsApp Group Invite

Natural hair😝😝😝
01/03/2020

Natural hair😝😝😝

22/02/2020

Ndo maana nakupendaga charmingray Yan dah💖💖💖💖💖💖💖💖

21/02/2020

Karibu katika page hii ya ARISE GOOD STORY inahusu simulizi za kujifunza kuelimisha katika maisha ivo ndugu rafiki share like na comments katika page hii nawapenda vyote nyie ndo mchango ndo chachu ya mafanikio kwangu👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏👏
Tutaanza kusoma simulizi ivi punde

Address

Tabata

Telephone

+255692592780

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ARISE GOOD STORY posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to ARISE GOOD STORY:

Share

Category