Wababu Maarifa

Wababu Maarifa Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Wababu Maarifa, Arts and entertainment, Pangani.

Ukurasa huu ni kwaajili ya sanaa,utunzi wa kazi za fasihi mashairi,riwaya,stori fupi n.k, na taarifa za burudani, dawati la kuchangia mawazo kwa jinsi zote,rika zote.

katika maisha yetu humu tunamoishi yanatukuta mambo mengi magumu na sisi tunaoishi maisha yetu ndio tunaojua wapi na nin...
04/01/2023

katika maisha yetu humu tunamoishi yanatukuta mambo mengi magumu na sisi tunaoishi maisha yetu ndio tunaojua wapi na nini tunapitia na kipi ni kweli na kipi ni uongo na nini ukweli na nini ni uongo katika maisha yetu,ukipata muda wa walau wa dakika 1 kuweza kufurahi na nafsi yako jitahidi kufanya hivyo kwani kesho unaweza ukapita katika magumu zaidi na ukakumbuka nyakati ambazo ulikuwa umepata muda huru wa kufanya mambo yako na haukuutumia ipasavyo.

Usiogope kuwa peke yako katika ku-enjoy huko kwani watu uja na kuondoka na mwisho wa siku pia wakija wanaweza wakaondoka huku wakikuvunjia heshima yako,wakikukosea adabu,wakakushusha thamani,wakaiondoa amani ya moyo wako na maisha kwa ujumla,kutokuwa na shukurani.

Husiwategemee watu sana katika maisha yako kwani watu huja na kuondoka na hawatokusaidia katika kutafuta hicho ulichokipata ila wao watakunyang'anya chako ulichokipata kwani wao hawawezi na hawana maarifa ya kutafuta k**a uliyokuwa nayo wewe,husitegemee kukupa ila tegemea kukupora ama kunyang'anywa kwa kutumia kila namna sababu wao wana maarifa madogo na ni WADHAIFU kupitiliza.

Usimtegemee mtu anayefanya ujinga ama upumbavu wowote kwako bila ya ridhaa yako na akaonesha kiburi juu yako,majivuno na ubabe k**a ana uwezo wa kukusaidia,mtu huyo mjinga na MPUMBAVU hawezi kukusaidia nae anahitajika kusaidiwa katika kila namna hawezi kukusaidia.

ukimsikia siku anasema anataka kukusaidia huyo ni muongo anakudanganya anataka ajue wapi unapatia mkate wako ili akuharibie.

Mwaka 2023 ni mwaka mpya.Tunauanza mwaka huu mpya wa 2023 pengine hata tukiwa na mafurushi (bundles) ya matatizo tuliyok...
02/01/2023

Mwaka 2023 ni mwaka mpya.

Tunauanza mwaka huu mpya wa 2023 pengine hata tukiwa na mafurushi (bundles) ya matatizo tuliyokuwa nayo tangu mwaka haujabadilika na kuwa 2023,kilichofanyika hapa ni kuongezeka kwa idadi ya ukubwa wa miaka kwa tarakimu moja na kufanya maelfu kusomeka katika mtindo mwingine kwa majumuisho ya kuongezeka kwa tarakimu hiyo moja na kuleta maana nyingine tofauti kabisa kwa kutazama,kusoma,kutenda,mipango na mikakati kwa taasisi,jamii ama mtu binafsi kwa kuandaa mpango kazi uliokuwa tofauti na ule wa mwanzo na kuweka matarajio makubwa katika kufanikiwa zaidi ya mwaka uliopita la kuboresha ama kuanza upya pia vyote vinawezekana.

Mwaka 2023 umetukuta tukiwa bado tunapambana na wale waovu wetu wa tangu mwaka uliopita,husije ukajisahau kwamba kwa sababu mwaka umebadilika na yule aliyekuwa muovu kwako atabadilika,mwaka umebadilika lakini fikra,tabia,maamuzi yake ya uovu kwako bado hayajabadilika.

Tunasherehekea kwa pamoja na ndugu,jamaa na marafiki si kwamba tuna furaha sana,hapana ila ni kwasababu ya ukubwa wa tukio lenyewe limetukutanisha pamoja k**a tulivyokutana kipindi hicho ila matatizo yapo pale pale,utafurahi siku moja siku zinazofuata kupambana kupo pale.

Kinachonifariji mimi ni kuamini ya kwamba k**a sio langu aliwezi likanitafuna na kunimaliza wote na k**a langu nitalibeba na kupambana nalo na k**a litakuwa linahitaji suluhu nitalipatia ufumbuzi.

Ninachoamini mimi ni uwepo wa Mungu,kuamini kwamba anatenda,anaamua,anabadili na kuzuia hasichokitana yeye kikufike kwako na kukupatia kila ambacho unastahili kukipata kwa wakati wako aliyepanga yeye manani na hata pasi na kutumia nguvu.

Ninachokiamini mimi ni kukaza,kutokubali kwa urahisi,kutokuwa mnyonge kwa sababu ya kuogopa kukosa kitu fulani kuna watu walipoteza na sasa wana gain zaidi ya kile walichokipoteza.

Unyonge, masikitiko,makasiriko,malalamiko,hayawezi yakanitoa mimi ama wewe pahala A na kukupeleka pahala B amabapo ni pazuri zaidi ya pahala A,tunatakiwa tupambane,tukaze,tujitume,tutumie hakili katika kuamua huku ukikumbuka ya kuwa unapokuwa katika kutafuta ujue kuna mtu ama watu nao wanakutafuta wewe,be care.

23/08/2022

FURSA YA KILIMO CHA NYOKA

Kilimo cha nyoka ni moja ya kilimo chenye faida sana ,mmoja anaweza akaanzisha kilimo hichi ukizingatia thamani ya "snake venom" ipo juu sana.Sumu ya nyoka inatumika kwa wingi kwenye viwanda vya famasia na viwanda vya vipodozi hivyo thamani ya "snake venom " ipo juu sana kutokana na uhitaji wake.

Gram moja ya "snake venom " kwa soko la kimataifa inauzwa $1880 ,na kwenye soko la Afrika kusini inauzwa kwa makadirio ya Rand 25,000
*K**a unafikiria kuanzisha shamba lako la nyoka ,yafuatayo ni mambo muhimu ya kuzingatia ili uweze kupata faida ya kutosha kutokana na venom wanayozalisha Nyoka

1.Zingatia hali ya joto na hewa .
Nyoka wanahitaji joto ya kiwango cha 24-29 degrees Celsius nyakati ya siku na 21-24 nyakati za usiku.

2.Mabanda na nyumba za nyoka zinahitaji kusafishwa mara kwa Mara
Hali hiyo itasaidia kukuza uzalishaji wa nyoka kwa wingi.Nyoka wanahitaji kuwekwa mahali salama kuzuia matatizo yeyote ile ya kiafya kuwapata.

3.Nyoka kwa kawaida hula panya 3-4 na hulishwa kwa wiki 3-4 .Nyoka hula panya walio hai lakini wanaweza kula waliokufa pia ,Nyoka hupenda kucheza na panya mwanzo kabla ya kuwala hivyo ni vema kuwapatia walio hai.

Faida za ufugaji wa nyoka

1.Uzalishaji wa venom ambayo ukiuza unapata kiasi kikubwa cha pesa.

2.Hupunguza na kutokomeza wadudu waharibifu k**a panya nk.Nyoka chakula chao kikuu ni panya hivyo husaidia kutusafishia shamba au nyumba kwa kuwamaliza wadudu hawa.

**Mwisho nawashauri ndugu zangu sio kila tukiwaona nyoka tunawaua ,nyoka ni rafiki zetu na sio maadui.Tuwatumie ipasavyo watatusaidia sana.

23/08/2022
Wakati wewe ukiwa busy kutafuta kipato chako kila siku, kumbe kuna mtu/watu wanakutafuta,kukufuatilia na kushindana na w...
06/11/2020

Wakati wewe ukiwa busy kutafuta kipato chako kila siku, kumbe kuna mtu/watu wanakutafuta,kukufuatilia na kushindana na wewe hata bila ya wewe mwenyewe kujua.

Wakati wewe upo busy na kutafuta pesa kuna mtu yupo pahala akikuongelea wewe vibaya tu ili uharibikiwe na uyumbe kimaisha.

Mwengine atakesha kwa waganga ili kukuchawia(ushirikina) ili husifanikiwe katika unachokitafuta.

WAPO WENGINE WATAKAOHOJI KWA NINI FULANI HAPATI SHIDA,TABU WALA KARAHA NA WATATAKA KUJUA NA KUONA KILA UTAKACHOKIFANYA K**A WAO NDIO WATU WA KUKUPANDISHA DARAJA DUNIANI.

JIBU:SI KILA MTU ANAYEFANYA JAMBO LAKE AMA KUPITIA MAGUMU ATAJIDHIHIRISHA KWA KILA MTU HASA PALE TU UTAKAPOKUWA ENOUGH AND STRONG MATURED YANI KUKOMAA KIAKILI(MAARIFA) HATOFANYA SHUGHULI YAKE ILI KUWAONESHA WATU KWAMBA YEYE ANAFANYA NINI ILA UTAFANYA KWA AJILI YA MANUFAA YAKO BINAFSI.

MTU MWINGINE HAPENDI SIFA ZA SHOW OFF (KUJIONYESHA) KWAMBA ANAFANYA NINI ILA YUPO MWINGINE ANAYEPENDA SIFA TU AIDHA KWA TABIA AU MANUFAA YAKE BINAFSI.

NB:SI KILA MTU ANAYEONESHA WATU YA KWAMBA ANAFANYA NINI KWAMBA ANATAKA SIFA,HAPANA ILA INAWEZEKANA SHUGHULI,AJIRA AMA KAZI AIFANYAYO INAMTAKA AFANYE IVYO ILI KUPATA WASHIRIKI WENGI ZAIDI HATIMAYE KUONEKANA NA WAKUU WAKE NA KUWEZA KUPATA MASLAHI MAZURI ZAIDI,TUSIKARIRI.

Picha:Miaka kadhaa iliyopita.


Tende(Date) ni chakula namba moja safi na bora duniani kuwa na uwezo wa kutuliza shambulio la moyo linalosababishwa kwa ...
18/10/2020

Tende(Date) ni chakula namba moja safi na bora duniani kuwa na uwezo wa kutuliza shambulio la moyo linalosababishwa kwa kuziba kwa mirija ya kusukuma damu (cholesterol), hypertension, na stroke(kupooza kwa baadhi ya maeneo,viungo katika mwili wa binaadamu).
Pia ni chanzo kikuu cha madini chuma mwilini.

Chanzo:Scientific Facts


Huko nchini Japani kuna kampuni ambayo inamiliki shule ambazo umfundisha mtu ni jinsi gani anaweza kuwa mchekeshaji.Shul...
02/10/2020

Huko nchini Japani kuna kampuni ambayo inamiliki shule ambazo umfundisha mtu ni jinsi gani anaweza kuwa mchekeshaji.

Shule ya kwanza ilifunguliwa mnamo mwaka 1982 na kiasi cha wanafunzi 1,000 udahili kozi hiyo kila mwaka wa masomo unapowadia.

Source:Power of science


Itokeapo ukaongea,unauawaItokeapo ukanyamaza,unauawaKwahiyo ni bora kuongea na kuuawa(kufa) angalikuwa  taarifa ilishawa...
20/09/2020

Itokeapo ukaongea,unauawa
Itokeapo ukanyamaza,unauawa
Kwahiyo ni bora kuongea na kuuawa(kufa) angalikuwa taarifa ilishawafikia wananchi (watu).
MOHAMMAD KIRUMIRA
1984-2018

Mnamo miaka ya 1990-> klabu ya mpira wa miguu ya nchini Uingereza Arsenal kwa wakati huo iliwai kuwa na mchezaji aliyeit...
16/09/2020

Mnamo miaka ya 1990-> klabu ya mpira wa miguu ya nchini Uingereza Arsenal kwa wakati huo iliwai kuwa na mchezaji aliyeitwa David Dicks.
Mchezaji huyo alipopatwa na jeraha liliomfanya ashindwe kucheza mchezo wa ligi kwa wakati huo na kutokana na majeraha hayo,gazeti moja wapo liliandika taarifa ya kuumia kwake iliyosomeka hivi "Arsenal to play without Dicks”

Aliyekuwa kocha mkuu kwa wakati huo aliamua kuamuru gazeti hill kubadili kichwa hicho cha habari na kusomeka hivi " Arsenal to play with Dicks out".
Unaambiwa idadi ya namba ya maudhurio ya wanawake iliongezeka maradufu zaidi ya awali pale Arsenal ilipokuwa ikicheza😀😁.


Wanatueleza watu wenye uzoefu na bahari (majini) ya kwamba ikitokea umeona mahiti ikielea baharini huku sehemu ya mbele ...
01/09/2020

Wanatueleza watu wenye uzoefu na bahari (majini) ya kwamba ikitokea umeona mahiti ikielea baharini huku sehemu ya mbele ya mwili ukiwa umeelekea juu (umelala chali) huo utakuwa ni mwili wa jinsi ya k**e (mwanamke).

Na endapo mwili huo sehemu yake ya mbele itakuwa imeelekea chini (umelala kifudi fudi) huo utakuwa ni mwili wa jinsi ya kiume (mwanaume)

Wataalamu na wazoefu wa bahari utueleza kwamba sehemu ya mbele kifuani (matiti) ya mwanamke ugeuka kuwa boya linalomfanya kuelea kuelekea juu endapo amepoteza uhai akiwa majini.


Address

Pangani
103

Telephone

+255655372750

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Wababu Maarifa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to Wababu Maarifa:

Share