Juma Dali

Juma Dali Elimu Na Burudani

FURAHA YANGU.Mtunzi; Juma Dali0717 861 372.Sehemu ya 05.Safari yangu ilikomea nyumbani lakini ilikuwa k**a bahati kwani ...
02/08/2022

FURAHA YANGU.
Mtunzi; Juma Dali
0717 861 372.

Sehemu ya 05.

Safari yangu ilikomea nyumbani lakini ilikuwa k**a bahati kwani sikukuta mtu yeyote, nilipitiliza hadi ndani niliingia chumbani kwa wazazi wangu, hata sikujua ni nini nafuata kwenye chumba cha wazazi wangu, nilianza kupekua kanakwamba kuna cha kwangu nilisahau lakini sikupata chochote.
Yaani kila nilichokifanya nilifanya tu lakini ukweli sikufahamu nafanya kwa ajili gani "aaah mbona hamna chochote" nilijisemea baada ya kukosa kile nilichokuwa nakitafuta nilitoka hadi chumbani kwangu ambako nako sikupata chochote akili yangu ilikuwa k**a imechanganyikiwa yaani hakuna nilichokifanya kikatimia sikutaka kuendelea kubaki nyumbani nilitoka tena, akili yangu haikuwa sawa kabisa nililudi tena kijiweni k**a nilivyotoka ndivyo nilivyokuta hakukuwa na mtu yeyote nilikaa kwenye benchi ambalo kila nilipofika nilipendelea kuketi.
Mawazo tele yaliendelea kuusonga ufahamu wangu wa akili k**a kuna siku ambayo nilifanya vitu vya hovyo basi ni pamoja na hii niliingiza mkono mfukoni lakini sikupata nilichokitarajia "dah inamaana nimeacha nyumbani" nilijisemea mwenyewe huku nikiendelea kujipapasa mifukoni "dah leo" nilijisemea na kujisonya mwenyewe tu hakika nilikuwa chizi kasoro kuokota makopo.
Wakati nikiendelea kujisonya sonya nilisikia sauti iliyonifanya niache kile ninachokifanya "oya vipi mbona hivyo mkulungwa" niligeuka na kumtazama mtu alienisemesha "vipi msela mbona k**a umevulugwa" aliendelea kunisemesha.
Lakini sikujibu chochote zaidi ya kumtumbulia macho tu kanakwamba sikumsikia alichozungumza "Edu vipi msela mbona unaniangalia tu mshikaji wangu naongea lakini hunijali kulikoni msela" aliniuliza huku ak**eti karibu yangu sikumjibu chochote badala yake nilikaa kimya na kuendelea kujisonya mwenyewe.
Hali hii ilimshangaza sana rafiki yangu alitamani kujua kinachonisibu lakini alibaki kukaa kimya tu.
Alinitazama kwa dakika kadhaa bila shaka alijiuliza maswali mengi kuhusu mimi alijitahidi kuvumilia lakini moyo wa uvumilivu alimkana na kutomtambua kabisa "Edu mshikaji wangu vipi mbona husemi chochote kulikoni kuna mtu amekuzingua niambie mimi mshikaji wako peter" aliongea kwa upole sana.
Nilibaki njia panda na nisijue nini cha kumueleza kwani moyo wangu ulijaa kisasi ambacho sikikijua ningekilipaje kwani akili yangu ilikuwa mbali nilikuwa nawaza kisasi tu na sio kitu kingine.
Nilimuangalia rafiki ya peter ambaye alikuwa mpole mithili ya maji mtungini nilitamani kumueleza kile kinachonisibu lakini nafsi ilikataa na kunieleza utakuwa udhaifu mkubwa sana k**a nitaeleza kile kilichonikuta asubuhi ataniona ni bwege mzee k**a yule ananipigaje na kumuangalia ama kweli nilikuwa mjinga wa fikra sikuwaza chochote zaidi ya kisasi akili yangu iliniambia usimueleze chochote kaa nalo moyoni kwani ni aibu kubwa sana.
Nilimuangalia Peter ambaye alionyesha kiu ya kutaka kujua kila kinachonisibu, nilimuangalia sana mwishowe nilinyanyuka na kuanza kuzipiga hatua kwa ajili ya kuondoka hali hi ilimshangaza Peter "Eduu" aliniita.
Niligeuka na kumuangalia lakini sikuitika nilibaki kumuangalia tu "vipi lakini msela mbona umebadilika sana leo vipi hauko sawa kabisa" aliendelea kuniongelesha.

Je unadhani kwa hasira alizonazo Edward atafanya nini? usikose sehemu inayofuata.

Mnaosoma na kupita kimya kimya hamtendi haki k**a simulizi haipendezi sema k**a inapendeza sema maana huo ndio mtaji pekee unaonifanya niilete kwenu simulizi hii like, comment na share kwa wingi ili tuzidi kusonga mbele pia like ukurasa huu ili uwe wa kwanza kuona kila kitakachopostiwa humu.

Je nini kitaendelea?.
Ahsante na kwa heri.

FURAHA YANGU.Mtunzi; Juma Dali0717 861 372.Sehemu ya 04."hiki kinachosemwa na mwalimu ni kweli uhudhurii shuleni" dah ni...
31/07/2022

FURAHA YANGU.
Mtunzi; Juma Dali
0717 861 372.

Sehemu ya 04.

"hiki kinachosemwa na mwalimu ni kweli uhudhurii shuleni" dah nilibaki kumuangalia tu kwani lilikuwa swali gumu kwangu ni kweli sikuwa nahudhuria shuleni lakini ningetoa jibu gani mbele ya mwl. la kumlidhisha baba yangu "nijibu mbona uko kimya" awamu hii aliongea kwa ukali kiasi cha kunistusha pale nilopaa nililuka kidogo na kukaa sawa lakini kwa muda wote sikuwa wa kuzungumza chochote kwani hata uwongo niliokautunga wote ulishanikimbia kwa hofu na kuniacha pekeyangu.
Baada ya kuona si muongeaji baba yangu aligazibika na aliona ni dharau kubwa kwake anaongea na mimi halafu simjibu chochote "PAAAH" ilisikika sauti hiyo nilivyokuja kutahamaki nilikuwa naona kiza tu sioni chochote nikiwa bado najiuliza ni nini ilisikika sauti ya pili "PAAAH" ukitokea upande wa pili wa shavu langu la kushoto lilikosa ushilikiano wa kusikia na badala yake nilikuwa nasikia k**a mdudu analia sikioni mwangu.
Baba yangu aliamua kuniadhibu kwa kunitandika makofi mawili yaliochangamsha ubongo wangu na kuufanya ukae sawa nikiwa najiuliza ni kipi kimetokea ndipo nilipoisikia sauti ya baba yangu "yaani naongea na wewe halafu unakaa kimya" baba alikuwa amekasilika haswa kitendo cha kupigwa na baba yangu mbele ya mwl. wangu nilikiona k**a dharau kwangu.
Niliamua kutoka bila ya kuaga na kutokomea kabisa shuleni pale baba alikasilishwa zaidi na kitendo kile alitaka kunifuata lakini mwl. Jadhim alimshika mkono "hapana usiende usije ukaleta athali nyingine itakuwa ni aibu" baba alikuwa mgumu kukubaliana na wazo la mwl. Jadhim kuwa ainifuate ili kuepusha hatari lakini mwisho alikubaliana nae.
Baada ya kutulia waliongea mengi kuhusu mwenendo wangu ambapo baba yangu aliniombea radhi kwa kosa la kutohudhuria shuleni kuwa nisipewe adhabu hivyo nisamehewe na niendelee na shule.
Mwl. Jadhim alikubaliana nae hivyo nilisamehewa kosa langu la kutohudhuria shuleni baada ya kutoka shuleni nilikwenda moja kwa moja nyumbani na kubadili sare za shule na ilikuwa k**a bahati sikumkuta mama yangu hivyo sikupata bugha ya aina yeyote ile nilibadili na kuondoka.
Kichwani sikuwa sawa kabisa maswali mengi nilijiuliza bila ya ku kupata majibu laiti ungeniona huenda ungedhani ni kichaa niliekimbia milembe maana hata utembeaji wangu ulifanana na kichaa kabisa.
"yaani dingi anidande mbele ya mwalimu dah hii ni dharau sasa" kwangu niliona k**a nimedhalilishwa kupigwa mbele ya mwalimu japo kwa upande wa pili wa shilingi baba alikuwa sahihi kuniadhibu "yaani leo sikubali haiwezekani mzee k**a yule anidunde mbele ya mwalimu halafu nikae kimya lazima nimuonyeshe mzee maana hii ni dharau" kamwe sikutaka kukubaliana na kilichotokea kwa siku ile moyoni nilipania kumuonyesha baba yangu.
Ila sikujuwa ningefanya nini ili kumuonyesha mzee lakini moyoni nilipania tu lazima nimuonyeshe hakika kitendo kile kiliniumiza sana sikutaka kipite hivihivi kingipitaje kwa mfano wakati nimedhalilishwa.
Nilitembea sana siku hii na safari yangu ilikomea kijiweni nilifika na kuketi lakini hakukuwa na mtu yeyote yule bila shaka kila mmoja alikuwa kwenye harakati zake lakini kwangu hilo sikujali nilikaa japo nilikuwa mpweke.
Kutokana na utulivu uliokuwepo eneo lile ulinipa nafasi ya kutafakali kwa kina kila nilichopitia asubuhi kutoka kwa baba yangu.
Hasira zilizidi kunipanda taratibu machozi yalianza kunishuka, sasa ningefanyaje tena na limeshatokea.
Sikuwa na namna ya kulibadilisha zaidi ya kujipoza kwa kulia tu "aah sikubali leo mzee atanitambua lazima nimuonyeshe" nilijisemea kauli hiyo na kisha kufuta machozi yangu sikukaa sana nikaamua kuondoka huku hasira zikiwa zimenishika vilivyo.

Je unadhani Edward atamfanya nini mzee wake usikose mwendelezo huu uliojaa mafunzo lukuki pia nisamee kwa kutoposti changaoto ya umeme ila tunaendelea.

Mnaosoma na kupita kimya kimya hamtendi haki k**a simulizi haipendezi sema k**a inapendeza sema maana huo ndio mtaji pekee unaonifanya nilete kwenu simulizi hii, like, comment na share kwa wingi ili tuzidi kuongezeka tafadhali unyesheni upendo ili kumpa mwandishi hamasa.

Je nini kitandelea?
Furaha yangu
Ahsante na kwa heri.

FURAHA YANGU.Mtunzi; Juma Dali0717 861 372.Sehemu ya 03.Baada ya kumaliza kula nilitoka na kwenda kijiweni k**a ilivyo k...
28/07/2022

FURAHA YANGU.
Mtunzi; Juma Dali
0717 861 372.

Sehemu ya 03.

Baada ya kumaliza kula nilitoka na kwenda kijiweni k**a ilivyo kawaida yangu uko nilikutana na rafiki zangu tuliendelea kula ma*****na na baada ya kuona teali nimetosheka niliwaaga wenzangu "oya wadau mori ngoja nikampolomoti mzee maana mfuko umetoboka" sio kweli kwamba niliishiwa ila niliamua kutumia vivyo ili wenzangu wasiniombe pesa kwani ilikuwa kawaida ya kijiweni, nilielekea gengeni kununua bigijii ila kuindoa harufu ya ma*****na ili hata wazazi wangu wasitambue chochote nilifika nyumbani na kupitiliza hadi chumbani.
Sikumbuki saa ngapi usingizi ulinipitia nilikuja kustuka baada ya kuisikia sauti ya mama ikianiamsha "Edward Edward mwanangu" "mmmh" niliitika huku uchovu ukiwa umenishika vilivyo "amka ule chakula" nilijiamsha na kuitazama saa yangu ya mkononi ilikuwa inasoma saa mbili na dakika ishirini nilijisikia uchovu mno kiasi hata chakula hakikupanda nilikula tonge kazaa na kuludi tena ndani hali ile ilimpa wasiwasi mama yangu na kuamua kunifuata chumabani kwangu "Edward unaumwa mbona chakula hujala sana umemega tonge kazaa tu umeacha" aliniuliza baada ya kuona chakula hakipandi "hapana mama sijisikii kula kwa sasa" baada ya kusikia hivyo alinifunika shuka na kuondoka huku akiombea nilale salama sio siri mama alikuwa ananipenda.
Siku iliyofuata asubuhi mapema jua likianza safari yake ya kila siku ya kuitafuta magharibi japo haijulikani huwa linatumia njia gani wakati wa kuludi maana kila siku hilo ni kuitafuta magharibi tu niliamka na kuanza kujiandaa ili kwenda shule k**a ilivyo kawaida yangu lakini lengo halikuwa kwenda shule.
Nilivaa sare zangu za shule na kuchukua mkoba nikiwa nahitaji kutoka nilikutana na baba na alinieleza kuwa tunapaswa kuongozana kwenda shule ili kwenda kusikiliza wito.
Dah kwangu habari za barua nilishazisahau k**a siku iliyopita kuliletwa barua ya kumtaka mzazi wangu tuongozane nilichukia mno kufuatana na baba shuleni kwani niliamini kila kitu kinakwenda kuhalibika na ukweli wote kuwa hadharani na nilijitahidi mno kumruka ili tusiongozane lakini alikataa katakata na kunitaka tuongozane.
Kutokana kung'ang'ania sikuwa na budi kumsubiri alijiandaa na baada ya kumaliza tuliongozana hadi shuleni dah kila mwananfunzi alieniona alinishangaa kana kwamba kaonyeshwa mwezi wa sikukuu tena mwezi wa Eid-il-fitri inayofuata baada ya mfungo wa ramadhani.
Hili lilimshangaza baba yangu tulifika ofisini kwa mwalimu mkuu na kukaribishwa na secretary na kututaarifu tumsubiri yuko njiani "msuburini tu sasa hivi atakuwa njiani" tulielekezwa mahali pakukaa ili kumsubiri lakini kwa kipindi chote nilikuwa kimya tu nikitunga uwongo wa kujitetea pale nitakapoulizwa maswali.
Baada ya ya nusu saa mwl. Jadhim aliwasili shuleni alipaki gari yake aina ya rav 4 na kushuka baada ya kuzipiga hatua kazaa aliweza kuniona "eenh wewe doja" aliamua kuniatania nilibaki kumuangalia tu kwa kipindi chote mawazo hayakuwa shuleni kabisa niliona k**a napoteza muda tu.
Baada ya kusalimiana mwl. Jadhim alianza kuongea kile alichotuitia "aah mzee christopher kwanza pole sana kwa usumbufu kwa wakati huu huenda ungekuwa kwenye shughuli zingine za kujitafutia ridhiki na kushughulikia mambo yako" alianza kwa kumuomba radhi baba.
"ahsante sana lakini bila ya usumbufu haya ndio majukumu yangu hivyo hakuna shida" baba nae alimtoa wasiwasi kuwa hajamsumbua hivyo aendelee alitoa kikohozi chepesi kisha akaendelea "mzee wangu nimekuita hapa ili kujadili mwenendo wa maendeleo ya kijana wetu kwani mwenendo wake sio mzuri.
Edward amebadilika mno kiasi cha kubuluza mkia darasani wakati hakuwa na tabia hii kabla kuporomoka darasani lakini kubwa zaidi sasa hivi hahudhurii kabisa shuleni hii wiki ya pili sasa anajihusisha na uvutaji wa bangi kwa hiyo k**a walimu na wazazi pia tumeona tusitoe maamuzi bila ya kukuita ili kukueleza hili "baba alisikiliza kwa umakini na alinigeukia ambako akaniuliza swali ambalo sikuritarajia k**a baba yangu ataniuliza swali hilo.

Je mzee Christopher alimuuliza swali gani?.

Mnaosoma na kupita kimya kimya hamtendi haki k**a simulizi haipendezi sema k**a inapendeza sema maana huo ndio mtaji pekee unaonifanya niilete kwenu simulizi hii like,comment na share kwa wingi ili tuzidi kusonga mbele usisahau kulike ukurasa huu ili familia izidi kuongezeka.

Ahsante na kwa heri.
Furaha yangu.

27/07/2022

FURAHA YANGU.
Mtunzi; Juma Dali
0717 861 372.

Sehemu ya 02.

"yaani wewe dingi yako anakuchunga utafikili wa k**e kwamba anahofia utampelekea ujukuu usio na baba" Hamisi aliendelea kuchangia "si ndio hapo hata k**a ningekuwa wa k**e ndio anichunge kiasi hiki" "mmh inakoelekea atakufunga kamba ili usitoke nyumbani" ""oya shika hii hapa" pusha alimaliza mada " "dah poa umeiwasha au iwashe tu hapa sina kiberiti" haya ndio yalikuwa maisha yangu ya kila siku.
Lakini k**a ujuavyo tabia moja hujanga tabia nyingine na ndivyo ilivyokuwa kwangu baada ya kujiingiza kwenye uvutaji wa bangi tabia mbaya ziliznza kujionyesha kwenye macho yangu.
Nilianza kutohudhulia shuleni na badala yake muda wa shule kuutumia tukiwa porini na siku zingine kwenye majumba mabovu tukiendelea kula ma*****na wazazi wangu lakini sivyo.
Wanasema hakuna chenye siri ulimwengu fanya ufanyavyo ipo siku kila kitu kitakuwa hadharani ndivyo ilivyokuwa kwangu baada ya kukosa masomo takribani wiki mbili mfululizo mwalimu mkuu wa shule ya kitangali secondary school ambayo ndiyo shule niliekuwa nasoma na kwa wakati huo nilikuwa nasoma kidato cha nne aliamua kuandika barua na kumpa mwanafunzi mmoja alieitwa.
Naifat karim alikuwa mtiifu aliifikisha barua k**a ilivyotakiwa "hodi" "karibu" "shikamoo mama" "marahaba Naifat hujambo" "sijambo mama sio mkazi nimeleta barua" "barua!" mama alishangaa "ndio imetoka shuleni" "inahusu nini" "mimi sijuwi" mama alionyesha kushtushwa na barua ile lakini hakuwa na budi kuipokea alipokea na kuifungua Naifat baada ya kuona mama yangu ameanza kuifungua barua aliamua kuaga na kuondoka akihofia kuulizwa maswali endapo ataufahamu ukweli uliozungumzwa kwenye barua ile kwani yeye alikuwa akifahamu ni kipi dhumuni la barua ile "mama mimi naenda" "haya karibu tena mwanangu" baada ya kuondoka Naifat mama yangu aliendelea kuisoma na baada ya kumaliza hakuamini "inamaana Edward hii mwezi pili hajahudhulia shule!" "hapana mbona kila siku huwa anaondoka nyumabni akiwa na sare za shule" kutokana kilichoelezwa kwenye barua mama yangu alijikuta akiingia kwenye malumbano ya hoja moyo ukimueleza kuwa hapana na nafsi ikisema ni kweli kilichoandikwa kwenye barua hivyo alijikuta anadondosha chozi.
Lakini wakati akiendelea kudondosha chozi ndipo alipowasili baba yangu ambae alitoka kwa wakati huo kwenda kututafutia ridhiki na alimkuta mama akiwa analia "kulikoni mama Edward mbona unalia" mama hakuongea chochote badala yake alimkabidhi barua aliipokea na kuisoma na baada ya kuisoma aliishiwa nguvu "eenh inamaana siku zote hizi Edward anavyotoka nyumabni huwa haendi shule na badala yake anakwenda sehemu tofauti" "ndio hivyo k**a ulivyoona" mama alimjibu "sitaki kuamini" "ndio na mimi inaniuma mno yaani mwanangu kabadilka kawa teja sasa mimi ni mama wa aina gani" wazazi wangu walijikuta wakiishiwa nguvu walikuwa wananipenda mno hivyo kubadilika kwa tabia zangu kuliwapa wakati mgumu mno.
Muda wa kurudi shuleni nami nililudi nyumbani nikijifanya kuwa na mimi naludi shule kwani nilikuwa na sare za shule pamoja na mkoba wangu.
Nilipofika nyumbani wazazi wangu walinikalisha chini na kunihoji juu ya kile walichoelezwa nilijitetea kuwa ni uwongo tu hakuna ukweli wowote.
Nilibadilisha sare zangu za shule na mama alinipa chakula lakini kwa wakati wote mama yangu alikuwa akiniangalia tu asiamini k**a mwanae kweli ni teja kwani sikuwahi kutumia mbele ya wazazi wangu kitu ambacho kiliwafanya waweze kuniamini lakini la kuvunda halina ubani.

Poleni kwa kuchelewa kuposti tunaendelea.

Mnaosoma na kupita kimya hamtendi haki k**a simulizi haipendezi sema k**a inapendeza sema maana huo ndio mtaji pekee unaonifanya niilete kwenu simulizi hii like, comment na share kwa wingi ili tuzidi kusonga mbele.

Je nini kitaendelea? usikose mwendelezo huu.

Ahsante na kwa heri.
FURAHA YANGU.

25/07/2022

FURAHA YANGU.
Mtunzi; Juma Dali
0717 861 372.

Sehemu ya 01.

Furaha yangu ni kuishi vizuri, kula vizuri, kuvaa vizuri, kulala nyumba nzuri, kuwa na mke nzuri, kutembelea gari nzuri, kuwa na watoto wazuri na kumiliki vitu vikubwa na vidogo ikiwemo kampuni na nakadhalika hiyo ndio furaha yangu lakini kamwe sikuwahi kufikili ugumu na uhatari uliopo juu ya kuitimiza furaha yangu kwa imani yangu niliaminikuwa vitu hivyo nitavipata kirahisi mno bila ya kupata shida, mateso na misukosuko pale nitakapovihitaji vitu hivyo.
Niliamini maisha ni rahisi sana hivyo niliamini kila nimuonae anendesha gari basi amelipata kirahisi hajapitia changamoto yeyote juu ya kulipata gari hilo kwani niliona maisha ni rahisi mno hiyo ndio ilikuwa akili yangu na niliwalaumu mno wale ote walalamikao kuwa maisha ni magumu niliwaona hawana akili timamu lakini sivyo nilivyofikili wanasemaga kuwa uyaone k**a kinavyosema kitabu kimoja nilichowahi kukisoma hapo awali kiitwacho CHANZO CHA KUMBUKUMBU kilichoandikwa na mwandishi mahili Juma Dali nami ndivyo ilivyokuwa kwangu.
Ndugu msomaji nisikuchoshe sana na maneno ya kiswahili yasioisha naomba umakini nikueleze kile nilichopitia.
Naitwa Edward Christopher ni mzaliwa wa Kitangali A ni mtoto pekee kwa mzee Christopherna mkewe Janeth Ndauka kutokana kuwa ni mtoto wa pekee kwenye familia yangu nilipendwa mno na wazazi wangu kiasi cha kupewa kipaumbele kwa kila jambo lakini licha ya kupendwa na familia yangu na kuniona k**a dhahabu kwao kamwe sikuwa mwenye furaha hii ni kutokana kuishi maisha duni kwani familia yangu ilikuwa ni ya kawaida haikuwa familia ya kitajiri wala ya kimaskini ilikuwa kati na kwa kuwa nilikuwa mtoto pekee nililelewa kwenye mazingira ya kudekezwa naweza sema nilikuwa nalelewa k**a yai kwa kila kitu nilichokiomba nilipewa tena kwa wakati hali iliyopelekea kudeka mno kwa wazazi wangu.
Lakini licha ya hayo yote sikutosheka nilihitaji vingi zaidi ambavyo hatasikuwa na uwezo wa kuvipata kwa wakati na mara kwa mara baba yangu mzee Christopher alikuwa aninishauli kuwa maisha sio rahisi k**a ninavyofikili lakini kwangu nilimuona k**a anaimba ngonjera tu wala sikumtilia maanani mbona watu wengi wanamiliki magari wanatumia pesa vile watakavyo "mwanangu Edward leo kuna jambo nataka nikueleze" maana naona kadri siku zinavyoendelea hari inazidi kuwa mbaya unazidi kubadilika kila iitwayo leo "mwanangu huku unakoenda sasa siko nasikia ushaanza kutumia madawa shuleni huna nidhamu k**a ilivyokuwa awali nimeangalia ripoti yako ya maendeleo shuleni umefeli wewe wa kupata mswaki mbona hii tabia hukuwahi kuwa nayo kabla nakumbuka ukiwa shule ya msingi ulikuwa vizuri sana ulikuwa unashika nafasi ya kwanza au wapili akikosa wapili basi watatu lakini sasa umebadilika tatizo ni nini mwanangu kipi unachokikosa kila unachokihitaji unapewa" nilibaki kumuangalia tu k**a sanamu niliendelea kutafuna zangu bigijii kwani teali nilitoka kupuliza bangi muda sio mrefu hivyo nilikuwa natafuna bigijii kuondoa harufu "mbona hunijibu kwa nini" dah niliona mzee ananipotezea muda tu hivyo niliamua kuondoka zangu kwenda kijiweni mzee Christopher aliendelea kuniita ili niludi aendelee kunipa hadithi yake lakini hata sikugeuka badala yake niliendelea kuchanganya kwato zangu kuelekea kijiweni baada ya dakika kumi teali nilikuwa kijiweni "aah vipi mshikaji" "dah baridi barafu tia uzito kwanza mdau"hiyo ndio ilikuwa salamu kwa marafiki zangu "vipi k**a ama niaje" "k**a juzi tu mdau" nilisalimiana na mateja wenzangu k**a ilivyo kawaida yetu kila tunapokutana huwa tunasalimiana hivyo""oya pusha ninyongee moja kubwa yaani ile ngumu kumeza" "aah mbona haina noma haina kwere" niliagiza k**a kawaida yangu "eenh tupe story" "aah wanangu si nilikuwa kihome" huyu alikuwa mwanafunzi mwenzangu ambaye nilikuwa nasoma nae "eenh kulikoni" dingi ameongea porojo sijamuelewa hata nini" "wewe dingi yako anazingua" pusha alidakia "kweli washikaji anazingua"Abasi aliongeza huyu ni mwanafunzi mwingine hayo ndiyo yalikuwa maisha yangu ya kila siku.

Narudia naomba radhi kwa kutokuwa hewani kwa takribani miezi kadhaa sasa ila nashukuru nimepata vifaa na nimerudi hewani.

Je unadhani nini kitaendelea ungana nami kwenye simulizi hii ili kujua nini kitaendelea itaaisha hapahapa cha kufanya ni kulike na kukomenti ili tuzidi kusonga mbele lakini pia usiache kufollow ukurasa huu ili kupata hadithi tamu na za kusimumua zaidi waalike marafiki zako ili familia izidi kuongezeka.

Mnaosoma na kupita kimya kimya hamtendi haki k**a simulizi haipendezi sema k**a inapendeza sema maana huo ndio mtaji pekee unaonifanya niilete kwenu simulizi hii.

Je nini kitaendelea?
Ahsante na kwa heri.

19/07/2022

Naomba radhi kwa kutokuwa hewan kwa kipindi kirefu ila sasa nimerudi tena baada ya kusubiri zaidi ya miezi kadhaa changamoto ya vifaa ndio ilikuwa tatizo ila sasa nimerudi na tunaendelea k**a kawaida like, coment na share ili tuzidi kusonga mbele.

Ahsante sana.
Je utanipenda

Naomba radhi kwa kutokuwa hewani kwa kipindi kirefu ila sasa nimerudi hewani kuanzia kesho hadithi zitaanza kuruka k**a ...
19/07/2022

Naomba radhi kwa kutokuwa hewani kwa kipindi kirefu ila sasa nimerudi hewani kuanzia kesho hadithi zitaanza kuruka k**a kawaida like,coment na share kwa wingi ili tuzidi kusonga mbele.

Ahsante na kwa heri.
Je utanipenda?

PENZI LANGU MAUMIVU YANGU.Mtunzi; Juma Dali0717 861 372.Inakujia karibuni kuwa wa kwanza kuisoma kwa kulike na kushare u...
16/06/2022

PENZI LANGU MAUMIVU YANGU.
Mtunzi; Juma Dali
0717 861 372.

Inakujia karibuni kuwa wa kwanza kuisoma kwa kulike na kushare ukuraha kwa rafiki zako poleni kwa kuadimika hapa katikati hii ni kwa sababu ya changamoto zilizopo nje ya uwezo wangu na ahsante kwa kusubiri kwa kipindi chore niseme ahsanteni sana.

Ahsante na kwa heri.

CHAGUO LANGUMtunzi; Juma Dali0717 861 372.Sikubalikiwa utajiri wa mali na fedha nyingi kiasi cha kuitwa tajiri miongoni ...
20/04/2022

CHAGUO LANGU
Mtunzi; Juma Dali
0717 861 372.

Sikubalikiwa utajiri wa mali na fedha nyingi kiasi cha kuitwa tajiri miongoni mwao laaah! nilibalikiwa upendo hata pale nisipopendwa heshima hata nisipoeshimiwa kujali hata nisipojaliwa kuthamini hata nisipothaminiwa busara ndio siha yangu japo wachache nilibahatika kuwa nao hawakulipa kile nilichokionyesha kwao ila hilo halikatishia tamaa bado nitaendelea kusimamia msimamo wangu.

Dah nimewamisi sana mwana mpotevu amerudi niliwamisi sana wapendwa wangu mko salama humu ndani baada ya ukimya wa kipindi kirefu hatimae nimerudi tena tuwe pamoja hadi mwisho wa safari hii nimewakumbuka sana.

MKULUNGWA,
JE UTANIPENDA?

Ahsante na Kwa heri.

01/01/2022

JE UTANIPENDA?
Mtunzi; Juma Dali
0717 861 372.

Mnanikatisha tamaa ushiliki wenu ni mdogo hadith inaonekana inafikisha wasomaji elfu moja ila like hazifiki hata mia jamani jitahidini kulike ili kunipa faraja kuwa kile ninachokifanya watu wanakiunga mkono. Pia usiache kunikosoa pale unapooona makosa maana ndio kwanza mwandishi mchanga kwenye tasnia hii hivyo nahitaji sana ushauli ili niweze kuleta kazi nzuri zaidi.
Mnaosoma na kupita kimya kimya hamtendi haki k**a simulizi haipendezi sema k**a inapendeza sema maana huo ndio mtaji pekee unaonifanya niilete kwenu simulizi hii like comment na share kwa wingi ili tuzidi kusonga mbele.

Je utanipenda?
Ahsante na kwaheri.

19/11/2021
JE UTANIPENDA?Mtunzi; Juma Dali0717 861 372.Sehemu ya 30.Alishindwa kuzungumza kila alipotaka kunyanyua mdomo kuzungumza...
10/11/2021

JE UTANIPENDA?
Mtunzi; Juma Dali
0717 861 372.

Sehemu ya 30.

Alishindwa kuzungumza kila alipotaka kunyanyua mdomo kuzungumza chochote mdomo ulikuwa nzito, sio siri hasira zilimshika kisawasawa, hakuona tena sababu za kuendelea kukaa mahali pale alinyanyuka na kuzama ndani, kila mmoja alishikwa na bumbuwazi, hawakujua ni nini kinaendelea ni k**a walipigwa shoti.
Baada ya kimya kidogo kupita mzee Robert alianzisha tena maongezi "nadhani hili swala kwa sasa sio wakati sahihi wa kulizungumzia zaidi nafikili tutafute tena muda mwingine tukae ili tulizungumzie kwa undani zaidi maana ni nzito sana" aliweka ukomo na kuwaangalia wenzie k**a wanamsikiliza ama laa "ni kweli mzee Robert ulivyosema maana limekuwa gafla sana hakuna alietarajia kwa hiyo kutengwe muda ili kulizungumzia kwa mapana zaidi, hali aliyoiyonyesha mama yake sio nzuri kwa hiyo tutafute siku nyingine ili tulizungumzie" aliongeza mama Witness.
Kisha alimuangalia Vanessa ambae kwa wakati ote aliinamia chini kwa hofu hakuwa wa kuongea chochote, "umeelewa kilichozungumzwa na wakubwa zako lakini?" aliuliza shangazi yake kumuuliza Vanessa maana wakati ote uso wake aliutazamisha chini tu.
Vanessa hakujibu chochote zaidi ya kukaa kimya tu taratibu sauti ya chinichini ya kilio ilianza kusikika, hali hii iliwashangaza sana hawakujuwa Vanessa analia nini, shangazi yake aliamka alipokaa na kumfuata, alimuinua uso wake ambao kwa wakati ote alitazama ardhi "nini kinachokuliza mwanangu?" aliambatanisha na swali, kimya "Vanessa nini mama kinachokuliza hebu niambie mimi shangazi yako usiogope niambie nini mama kinachokusumbua" alirudia tena kumuuliza, ila hakupata jawabu lolote lile zaidi ya ukimya ulioendelea kutamalaki maeneo yale, shangazi yake alishindwa kumuelewa zaidi ya maswali mengi alioendelea kujiuliza, mama Witness nae aliungana na mama Baraka kumuhoji lakini hawakufanikiwa.
Moyoni Vanessa aliendelea kujutia kwakile alichokifanya, kila alipomuaza mama yake hakuwahi kumkwaza kiasi cha kuchukia kiasi kile ila leo kwa mara ya kwanza amemkwaza.
Hivyo alijiuliza maswali mengi sana kiasi cha kushindwa kumsikiliza shangazi yake na mama yake mama Witness "Vanessa!!" aliita mama Witness "eenh eenh" aliitika kanakwamba amekurupushwa kutoka usingizini "duh inamaana muda ote tunaongea na wewe ila mawazo hayakuwa hapa mwanangu" shangazi aliuliza kinyonge "hapana shangazi" alijitetea.
"jamani nadhani muda umekwenda sana hili jambo tulifunike tutaliongelea vizuri kesho maana kila mmoja ana lake" aliongea mze Robert, hakukuwa na wa kupinga kila mmoja alikubaliana nae.
******
Kwa Kenedy hali ilizidi kuwa tofauti sana maana hata chakula alichoagiza hakikupanda licha ya njaa kumshika ila mawazo mengi yaliyomzonga kichwani mwake yalipelekea kukata hata hamu ya kula, alijilazimisha ili kuupa mwili nguvu angalau alifikisha nusu ya chakula asikuambie mtu mapenzi yanauma sana hususani unapompenda mtu na kuwekeza kila kitu chako, muda wako, moyo wako, akili yako na mali zako ukiamini siku moja atakuja kuwa miongoni mwa watakaounda familia yako halafu mwishoni mambo yanabadilika inauma sana, ila bado hakutaka kujiaminisha moja kwa moja kwamba Vanessa sio wake tena aliendelea kuweka matumaini yaleyale japo mambo yalibadilika kiasi, alikula chakula na kurejea nyumbani kujipumzisha.

Je nini kitaendelea usikose sehemu ijayo.

Mnaosoma na kupita kimya kimya hamtendi haki k**a simulizi haipendezi sema k**a inapendeza sema maana huo ndio mtaji pekee unaonifanya niilete kwenu simulizi hii msione k**a nachelewa kuposti hadothi hii nikiposti mapema kuna mwandishi fulani anaidukua na kuigeuza k**a yake yaani badae anaposti kwenye kurasa zake na ndio maana huwa nachelewa sana kuposti ila itaruka mpaka mwisho mahali hapa hapa. cha kufanya nikulike ukurasa huu ili uweze kuona kila kitakachopostiwa humu.

Je utanipenda?
AHSANTE NA KWAHERI.

JE UTANIPENDA?Mtunzi; Juma Dali0717 861 372.Sehemu ya 29.Alikuja kuzinduka majira ya saa mbili usiku, njaa nayo haikumua...
08/11/2021

JE UTANIPENDA?
Mtunzi; Juma Dali
0717 861 372.

Sehemu ya 29.

Alikuja kuzinduka majira ya saa mbili usiku, njaa nayo haikumuacha salama, ukizingatia na dawa alizomeza bila ya kula chochote ndio ilizidi kukwangua zaidi.
Aliamka na kukaa kitako, "duh njaa inauma ngoja niende kwa mama Ally nikapate japo ugali maana mmh" alijisemea na hakutaka kupoteza muda, aliamka lakini alihisi kizunguzungu hakuweza hata kunyanyua mguu wake hatua moja mbele alibaki kusimama, huku akiwa amefumba macho yake alifanya hivyo kwa dakika kadhaa mpaka pale hali ilipokaa sawa na kisha kutoweka nyumbani kwenda kujipatia ridhki.
******
Upande wa pili kwa Vanessa hali ilikuwa shwari hakuwaza chochote kwake kila kilichotokea jioni ya siku hiyo aliona ni sawa tu wala hakuwaza kwa kile kitakachotokea mbeleni, mbaya zaidi hakutaka kukaa nalo pekee yake aliamua kuishilikisha familia yake, "jamani baba mdogo, shangazi, mama na mama Witness nimewaita ili niwaeleze jambo naamini mtalipokea na mtalifurahia", aliwaangalia kila mmoja usoni, ambapo kila mmoja alinyaonyesha hamu ya kutaka kufahamu jambo lenyewe "eenh tuambie shangazi una nini maana leo unafuraha sana hebu tuweke wazi" aliongea shangazi yake huku akionyesha shauku ya kutaka kufahamu kile alichonacho shangazi yake.
Alitabasamu kidogo kisha akaendelea "mama nisamehe sana k**a nitakukwaza" alitanguliza kwa kuomba radhi hali iliyopelekea ote kupatwa na taharuki "eenh mbona unaanza kuomba radhi kulikoni tena Vanessa mbona unatustua" alisema mama Witness "eenh hata na mimi nashangaa kuna nini?" aliongeza mama yake "hapana mama ila nimetanguliza tu k**a nitakukwaza ila jambo lenyewe ni la heri tu mama wala msiwe na hofu" aliwatoa hofu kisha akaendelea "mmh aah nikiwa chuo mama nimekutana na watu tofauti tofauti na kizuri zaidi ni kuwa nimepata mchumba" aliweka ukomo.
Aliwaangalia tena usoni kila mmoja alionyesha kushangazwa na kile walichokisikia, mama yake hakuamini "unasema umepata mchumba eenh" aliuliza kwa taharuki "ndio mama nimepata mchumba" aliludia bila haya "kwa hiyo umepata mchumba eenh huyo mchumba anaitwa nani?" aliuliza mama Witness huku akiwa ameshika tama "anaitwa Dominick ni mtoto wa waziri mkuu ananipenda na mimi nampenda tena ana nia ya dhati ya kunioa, alitaka kuja kujitambulisha ila mimi tu ndio niliemzuia nimemuambia mpaka niwaeleze kwanza ndiyo aje vizuri" aliweka tena ukomo.
Ila awamu hii kila mmoja alionyesha kushangazwa zaidi hasa kwa mama yake ambae hakufahamu nini cha kusema, mawazo mengi yalipita kwenye ufahamu wake wa akili alijalibu kuwaza wasifu wa mwanaume huyo ambae amempata mwanae lakini hakuapata majibu alijalibu kuvaa viatu vya Kenedy pale atakaposikia taarifa hizi atajisikiaje hakupata jawabu alijikuta anashindwa cha kusema badala yake aliduwaa tu k**a mtu aliepigwa shoti ya umeme.
"Vanessa unasema kweli" aliuliza mzee Robert ambae kwa wakati ote alikaa kimya bila ya kuongea chochote, "ndio baba tena nampenda sana" aliongea kinyonge "na Kenedy je" aliuliza shangazi yake "Kenedy mimi simpendi kwanza hana elimu hana pesa mimi wa nini" aliongea bila woga wowote "unasemaje Vanessa "mama yake alipandwa na hasira "inamaana ndicho ulichoenda kusomea huko chuoni si ndio inamaana ndiyo unachojifunza umesahau Kenedy amekutoa wapi hawa unaowaona si walikutelekeza hawa Kenedy amekufanyia mangapi wewe mtoto usitake kunichanganya" hasira zilimzidi kiasi cha kushindwa kuvumilia, mikono ilianza kutetema, machozi yalianza kushuka taratibu, uso wake ulibadilika na kuwa k**a mbogo sio siri alichukia sawa.

Haya unadhani kwa hasira alizonazo mama Vanessa unadhani atachukua maamuzi gani.
Mnaosoma na kupita kimya kimya hamtendi haki k**a simulizi haipendezi sema k**a inapendeza sema maana huo ndio mtaji pekee unaonifanya niilete kwenu simulizi hii. Like,Coment na share kwa wingi ili tuzudi kusonga mbele usisahau ku-like ukurasa huu ili uwe wa kwanza kuona kila kitakachopostiwa humu.

Je utanipenda?
AHSANTE NA KWAHERI.

Address

Newala

Telephone

+255717861372

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Juma Dali posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to Juma Dali:

Share