08/01/2021
CHOZI LANGU.
Mtunzi;Juma Dali
0717 861 372.
Sehemu ya 01.
Ilikuwa ni majira ya usiku wa manane, nami k**a ilivyo kawaida yangu muda huo ndio muda maalumu wa kurejea maghetoni kwangu, katika pitapita zangu nilijikuta napita moja ya jumba lililopo, mitaa ya uswahilini Uswazi. nikiwa bado naendelea na safari yangu gafla nilisikia maongezi flani yaliotoka ndani ya nyumba ile, kanakwamba walikuwa wanabishana.
Kutokana na kuwa na tabia flani za ushilawadu maana nisijifiche sikutaka maongezi yale yanipite hivihivi. Hivyo nilijisogeza kwa kunyata kanakwamba simba anawinda swala, kwani nilizipiga hatua za polepole mno kiasi cha wenye nyumba kushindwa kunisikia, laiti k**a ungeniona ungeweza jiaminisha labda ni kibaka hivyo nilikuwa kwenye mpango wa kuvamia nyumba ile.
Na kukwapua kile kilicho kizuri kinachopatikana kwenye nyumba ile, lakini la! hasha haikuwa hivyo nilikuwa na lengo kupiga chabo tu na si vinginevyo.
Nilizichanganya kwato zangu hatimae nililifikia jumba lile, nilijisogeza dilishani ili kuyapata kwa uzuri maongezi yote yanayotokea ndani, akili zangu zilinituma huenda ndani kulikuwa na mchezo usio wa kawaida unafanyika.
Mchezo ambao hauna refalii wala rezimeni wala kamisaa wa mchezo, na hauna mashabiki, mchezo ambao hucheza baba na mama tu tena hucheza kwa siri bila ya mtu yeyote kufahamu.
Hivyo nilijitahidi zaidi kujibanza moja ya dirisha ambalo ndimo maongezi yalikuwa yanatokea, nilisogeza vyema sikio langu ili nipate kusikia kile kinachozungumzwa ndani.
nilijitega kwa uzuri sana nadhani hakuna siku ambao nilikuwa makini zaidi kusikiliza jambo k**a siku hii, na niliweza kuyapata kwa uzuri zaidi kabisa maongezi yote yaliokuwa yanaongelewa ndani "mkewngu majali mkewangu" "eenh mumewangu" aliitika kwa sauti ambayo wazi ilionekana kujawa na usingizi mzito, ila kwa kuwa aliitwa hakuwa na budi kuukatisha usingizi na kuamka ili kusikia kile kilichomfanya mumewe kumuamsha.
Alijiamsha na kukaa sawa ingawaje usingizi haukutaka kumuacha kwani bado ulizidi kumng'ang'ania, aliyafikicha macho yake kuondoa usingizi ulikoma kutoka.
Nami kwa ufinyu wangu wa akili kusikia mtu akiamka, nilizidi kukaa sawa sikusikia maumivu yoyote ya mbu waliokuwa wanagema damu yangu tamu niliwacha tu waendelee na shughuli yao zaidi niliwabadilishia mikao tu ili wafaidi vizuri, niliendelea na kazi yangu kanakwamba mpiga picha hivyo nilitaka nisihalibu kazi nikakosa wateja.
Akili yangu ilinituma huenda wanabadilishana upande yaani wanaingia kipindi cha pili cha mtanange usio na refalii nilijitahidi kuvutia taswira, jinsi mtanange huo ulivyo.
Dah! inaelekea ilikuwa mechi ya kukatana na shoka sio mechi ya kitoto niliongeza umakini zaidi ili nipate kusikia kwa uzuri zaidi.
Mazungumzo kwa upande wa ndani yaliendelea "nisamehe sana kwa kukatisha usingizi wako mkewngu" mume alianzisha maongezi "hapana Bidhim mumewangu hata hujanisumbua ni wajibu wako hivyo huna haja ya kuomba msamaha wewe endelea tu baba"alimaliza kwa kupoza sauti, hali iliopekea Bidhim kujisikia faraja.
"unajuwa tokea tufunge ndoa huu ni mwaka wa pili sasa hatuna mtoto na unajuwa ndoa bila mtoto haina maana kwani tunatafuta kwa shida unadhani nani atakuja kurithi hizi mali zote tunazozitafuta, haliakuwa hatuna mtoto na uwezo wa kumlea na kumpa mahitaji yote muhimu tunao".
Bidhim alionekana kuwa na kiu ya kupata mtoto nae siku moja aje kuitwa baba, ila ni ukweli usiopingika ndoa bila mtoto haiwi na radha kifupi haipenezi yaani hainogi, ukizingatia wamefunga ndoa kwa ajili ya kutekeleza abada mojawapo ilioelezwa kwenye vitabu mbalimbli vya muumba wa mbingu na ardhi.
"ni kweli mumewangu hata nami najisikia vibaya kila nikiwaona rafiki zangu wanavyocheza na watoto wao inaniuma mno, ni afadhali umeliwaza hilo ila ulikuwa unafikilia nini?" kumbe hata mke nae alihitaji mtoto "mimi naona sasa ni wakati wa kumtafuta mtoto" "hata nami naunga mkono hiyo kesho twende hospitali tukaangalie uzazi" alichangia "sawa langu lilikuwa ni hilo tu unaweza ukaendelea kupumzika" "haya sawa" kila mmoja alijilaza kivyake.
dah iliniuma mno kumbe yalikuwa maongezi ya kawaida tu hata wale mbu waliokuwa wanafaidi damu yangu niliwapa dozi tena sio ya kitoto, "dah watu wengine bhana mimi nilijuwa kuna mambo yetu wao wanajadili watoto dah" kisha nilimalizia na kusonya.
Sikuona haja ya kuendelea kubaki tena mahali pale hivyo niliamua kuondoka huku nikiwalaumu kwa kunipotezea muda.
Asubuhi ya siku iliofuata waliamka wakiwa wenye afya tele k**a walivyopanga kwenda hospitalini basi ilikuwa hivyo.
Baada ya majibu ya daktali ambayo yalionyesha uzazi wanao hivyo ni maamuzi yao kuzaa walifurahi, yaratibu mipango ya mtoto ilichukuwa nafasi yake.
Naam hii ndio hadithi yangu ya kwanza kuandika leo nimeileta kwenu je unaionaje tililika mdau je wanandoa hawa walifanikiwa kupata mtoto? swali la kujiuliza hayo na mengine mengi usikose kufutalia kigongo hiki.
Mnaosoma na kupita kimyakimya hamtendi haki k**a simulizi haipendezi sema k**a inapendeza sema maana huo ndio mtaji pekee unaonifanya niilete kwenu simulizi hii.
LIKE,COMENT NA SHARE KWA WINGI ILI IWAFIKIE WENGI IFANYE ISOMWE NA WENGI ONYESHA UPENDO WAKO.
Lakini like ukurasa huu ili uwe wa kwanza kuona kila kitakachopostiwa huko pia waalike rafiki zako ili familia izidi kuongezeka.
AHSANTE NA KWA HERI.
CHOZI LANGU NANI WAKULIFUTA?.