Islamic knowledge Tanzania

Islamic knowledge Tanzania ﺑِﺴْﻢِ ٱﻟﻠَّﻪِ ٱﻟﺮَّﺣْﻤَٰﻦِ ٱﻟﺮَّﺣِﻴﻢِ
Bismi Allahi alrrahmani alrraheemi | Biashara na Uhusiano wa Kijamii. Biashara na Uhusiano wa Kijamii.

919. Riba,

2.

A PAGE CREATED FOR PROVIDING SOCIAL NETWORKING ISLAMIC REMINDER'S DAILY FROM QURAN-L -MAJID. Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w., Amesema Bihar al-Anwaar, J. 103, Uk. 89:

“Iwapo mtu atanunua bidhaa katika vyakula ambavyo ni muhimu katika jamii na akakificha kwa siku arobaini kwa matumaini kuwa bei yake itapanda miongoni mwa Waislam, na k**a atafanikiwa kukiuza kwa bei ya juu hicho chakula basi k**a f

edha zote atazigawa katika sadaka kwa na wenye kuhitaji misaada maskini, basi hiyo haitapunguza adhabu yoyote mbele ya Allah swt kwa kile alicho kitenda (kuhujumu uchumi).”

920. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s., amesema Bihar al-Anwaar, J. 103, Uk. 93:

“Yeyote yule anayefanya biashara bila ya kuzingatia sheria na kanuni za Islam, basi kwa hakika ataingia katika riba, (bila ya yeye mwenyewe kujijua).”

921. Al Imam 'Ali ibn Abi Talib a.s. ananakili kutoka Mtume Muhammad Mustafa s.a.w.w. kuwa Amesema, Khisal-i-Sadduq, J. 1, Uk. 286:

“Yeyote yule aliye katika biashara na anayenunua na kuuza vitu lazima ajiepushe mambo matano, ama sivyo asinunue wala asiuze kitu chochote:
1. Kula kiapo,

3. Kuficha ubaya na kasoro za mali,

4. Kusifu kitu k**a hakistahili hivyo wakati wa kuuza; na

5. kutafuta kasoro au ubaya wakati wa kununua.1”

922. Al Imam Muhammad al-Baquir a.s. Amesema, Al-Kafi, J. 5, Uk. 78:

“Yeyote yule anayetafuta riziki humu duniani ili aondokane na shida za kutegemea watu katika mahitaji yake, na ili kuwalisha na kuwasaidia wananyumba wake, na kueneza mapenzi yake kwa majirani zake basi atakutana na Allah swt siku ya Qiyamah huku uso wake ukiwa uking’ara k**a mwezi.”

27/09/2025

Maasha Allah karibu sana Ustaadha & Ustaadhat kwapamoja katika lengo la jifunza na kujikumbusha yale aliotuamrisha na kutukataza mwenyezimungu katika kuiendea pepo yake siku ya mwisho: Mohamed Kazungu, Husna Chota, Minaaa, Rama Hamisi

IBADA YA MWISHO YA MTUME KATIKA ZILE NYUSI 10 ZA MWISHO WA RAMADHAN.´Aliy ambaye amesema:”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi ...
19/03/2025

IBADA YA MWISHO YA MTUME KATIKA ZILE NYUSI 10 ZA MWISHO WA RAMADHAN.

´Aliy ambaye amesema:
”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akiiamsha familia yake katika zile nyusiku kumi za mwisho za Ramadhaan.”[1]

Hadiyth ni nzuri na Swahiyh.
796- Qutaybah ametuhadithia: ´Abdul-Waahid bin Ziyaad ametuhadithia,

kutoka kwa ´Aaishah aliyesema:
”Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akijitahidi katika zile nyusiku kumi za mwisho kuliko anavyojitahidi katika nyusiku zengine.”[2]

Muhusika: Imaam Abu ´Iysaa Muhammad bin ´Iysaa at-Tirmidhiy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: al-Jaami´ (795-796)
Imechapishwa: 15/05/2020
https://firqatunnajia.com/ibaadah-ya-mtume-katika-zile-nyusiku-kumi-za-mwisho-ramadhaan/

Uislamu kwa ufahamu wa Salaf

Usiku wa Qadr unakuwa katika zile nyusiku kumi za mwisho Ramadhaanal-Bukhaariy na Muslim wamepokea kutoka kwa Abu Sa´iyd...
18/03/2025

Usiku wa Qadr unakuwa katika zile nyusiku kumi za mwisho Ramadhaan

al-Bukhaariy na Muslim wamepokea kutoka kwa Abu Sa´iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ´anh) ambaye amesema:

“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifanya I´tikaaf lile kumi la katikati la Ramadhaan. Mwaka mmoja akafanya I´tikaaf mpaka ilipofika usiku wa tarehe ishirini na moja, asubuhi ambayo kikawaida ndio anatoka kwenye I´tikaaf yake,

*akasema: “Yule mwenye kutaka kufanya I´tikaaf basi afanye I´tikaaf katika zile siku kumi za mwisho. Nimeota juu ya usiku huo kisha nikausahau. Nimejiona asubuhi nikisujudu ndani ya maji na udongo. Utafuteni katika zile siku kumi za mwisho na utafuteni katika zile nyusiku za witiri.”*

Usiku huo kukanyesha. Msikiti ulikuwa k**a paa na maji yakanyesha juu yake. Nikaona namna ambavo paji la uso la Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) lilikuwa na athari ya maji na udongo baada ya asubuhi ya tarehe ishirini na moja.”
Hadiyth hii inajulisha kwamba Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akifanya I´tikaaf zile siku kumi za katikati za Ramadhaan ili kutafuta usiku wa Qadr.

Muundo huu unaonyesha kwamba alifanya hivo mara nyingi.
al-Bukhaariy na Muslim wako upokezi mwingine unaosema kwamba alifanya I´tikaaf zile siku kumi za mwanzo halafu ndio akafanya I´tikaaf katika zile siku kumi za katikati.

Kisha akasema:
*“Nimejiwa na kuambiwa kwamba ni katika zile siku kumi za mwisho* *Yule miongoni mwenu anayetaka kufanya I´tikaaf basi afanye hivo.”*

Haya yanajulisha kwamba yalifanyika kabla ya kubainikiwa kwamba ni katika zile siku kumi za mwisho. Baada ya kubainikiwa alikuwa akifanya I´tikaaf katika zile siku kumi za mwisho mpaka alipoondoka duniani.”

Muhusika: Imaam Zayn-ud-Diyn bin Rajab al-Hanbaliy
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Latwaa’if-ul-Ma´aarif, uk. 242
Imechapishwa: 16/05/2020
https://firqatunnajia.com/usiku-wa-qadr-unakuwa-katika-zile-nyusiku-kumi-za-mwisho-ramadhaan

01. Hukumu ya Tarawiyh na idadi ya Rak´ah zakeAliulizwa muheshimiwa Shaykh al-´Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) swali lifuata...
18/03/2025

01. Hukumu ya Tarawiyh na idadi ya Rak´ah zake

Aliulizwa muheshimiwa Shaykh al-´Uthaymiyn (Rahimahu Allaah) swali lifuatalo: Ni ipi hukumu ya swalah ya Tarawiyh? Ni ipi Sunnah juu ya idadi ya Rak´ah zake?

Akajibu ifuatavyo: Swalah ya Tarawiyh ni Sunnah aliyoisunisha Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) juu ya ummah wake. Alisimama kuswali na Maswahabah zake nyusiku tatu lakini baadaye (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaacha kufanya hivo kwa kuchelea isije kufaradhishwa juu yao.

Kisha baada ya hapo waislamu wakabaki katika hali hiyo katika zama za Abu Bakr na katika uongozi wa ´Umar. Baada ya hapo kiongozi wa waumini ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) akawakusanya kwa Tamiym-ud-Daariy na Ubay bin Ka´b. Wakawa ni wenye kuswali kwa mkusanyiko mpaka hii leo na himdi zote anastahiki Allaah.

Kwa hivyo imependekezwa katika Ramadhaan.
*Kuhusu idadi ya Rak´ah zake ni Rak´ah kumi na moja au Rak´ah kumi na mbili. Hii ndio Sunnah katika jambo hilo. Lakini endapo mtu atazidisha juu ya hizo hakuna neno wala ubaya*

Kwa sababu kumepokelewa juu ya hilo kutoka kwa Salaf aina mbalimbali katika kuongeza na kupunguza. Hakuna baadhi ambao waliwakemea wengine. Kwa hivyo asikaripiwe yule ambaye atazidisha ijapo bora ni kwa yule ambaye atakomeka na ile idadi iliopokelewa.

Isitoshe Sunnah pia imejulisha kwamba hakuna ubaya kuzidisha. al-Bukhaariy na wengineo wamepokea kupitia kwa Ibn ´Umar ambaye amesimulia kuwa kuna mtu alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kuhusu swalah ya usiku ambapo akajibu:
“Ni [Rak´ah] mbilimbili. Atakapochelea mmoja wenu Subh basi ataswali [Rak´ah] moja ili kuwitirisha yale aliyoswali.”[1]

Hakuweka kikomo cha idadi maalum (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambacho mtu atafupika kwacho. Lakini lililo muhimu katika swalah ya Tarawiyh ni unyenyekevu na utulivu katika Rukuu´, Sujuud na wakati wa kuinuka kutoka katika Rukuu´ na Sujuud.

*Mtu asifanye ile haraka ya spidi inayofanywa na baadhi ya watu ambayo inawakosesha waswaliji kufanya yale mambo yaliyosuniwa*

Bali huenda spidi yake ikawakosesha kufanya yale mambo yaliyowajibishwa kwa ajili ya kupupia awe wa kwanza kutoka kwenye misikiti ili watu wapate kukusanyika kwake kwa wingi zaidi. Kitendo hichi ni chenye kwenda kinyume na yale yaliyowekwa katika Shari´ah.

Ni lazima kwa imamu kumcha Allaah juu ya wale walioko nyuma yake na asirefushe urefushaji ambao unawatia uzito unaotoka nje ya Sunnah k**a ambavo pia asiwepesishe uwepesi ambao unaharibu yale mambo ya wajibu au yaliyosuniwa kwa wale walioko nyuma yake.

Kwa ajili hii wanachuoni wamesema:
“Imechukizwa kwa imamu kufanya haraka itakayowakosesha waswaliji kufanya yale yaliyopendekezwa.”
Tusemeje kwa wale wanaofanya haraka inayowakosesha waswaliji kufanya yale ambayo ni ya wajibu?

Hakika haraka k**a hii ni ya haramu juu ya imamu huyu. Tunamuomba Allaah atupe sisi na ndugu zetu msimamo na usalama.

[1] al-Bukhaariy (990) na Muslim (1695).
Muhusika: Imaam Muhammad bin Swaalih bin ´Uthaymiyn
Tarjama: Firqatunnajia.com
Marejeo: Fataawaa Swalaat-it-Taraawiyh, uk. 05-06
Imechapishwa: 02/04/2022
https://firqatunnajia.com/01-hukumu-ya-tarawiyh-na-idadi-ya-rakah-zake/

Uislamu kwa ufahamu wa Salaf

Assalamu alaykum warahmatullah wabarakatuFunga ya asiyeswali ni batili*Swali: Ni ipi hukumu ya swawm ya asiyeswali?*Jibu...
20/03/2024

Assalamu alaykum warahmatullah wabarakatu

Funga ya asiyeswali ni batili

*Swali: Ni ipi hukumu ya swawm ya asiyeswali?*

Jibu: Asiyeswali ni kafiri. Yanaharibika matendo yake yote:

وَلَوْ أَشْرَكُوا لَحَبِطَ عَنْهُم مَّا كَانُوا يَعْمَلُونَ

“Lau wangemshirikisha bila shaka yangeporomoka yale waliyokuwa wakitenda.”[1]

Tunamuomba Allaah usalama. Ambaye haswali ni kafiri na matendo yake ni batili mpaka atubie kwa Allaah.

[1] 06:88

Mhusika: Imaam ´Abdul-´Aziyz bin ´Abdillaah bin Baaz
Mfasiri: Firqatunnajia.com
Marejeo: https://binbaz.org.sa/audios/794/فتاوى-رمضانية
Imechapishwa: 30/03/2023

Sasa Jiunge na sisi Previous Next [metaslider id=”92474″] Makala Makala zaidi … Darsa Darsa zaidi … Video Video zaidi … Dawrah/Nad-wah Dawrah/Nad-wah zaidi … Khutbah Khutbah zaidi … Mihadhara Mawaidha zaidi … Ruduud Ruduud zaidi … [metaslider id=”27421″] Ratiba ya Darsa za live...

﷽Assalamu alaykum warahmatullah wabarakatu.*al-Waadi´iy kwamba mke aliyejamiiwa mchana wa Ramadhaan hatoi kafara**Swali:...
20/03/2024


Assalamu alaykum warahmatullah wabarakatu.

*al-Waadi´iy kwamba mke aliyejamiiwa mchana wa Ramadhaan hatoi kafara*

*Swali:* Vipi ikiwa mwanamke alijaamiwa kwa ridhaa yake na hakumzuia mume wake kutokana na hilo?

*Jibu:* Anapata dhambi ikiwa naye ameridhia. Kusema kwamba na yeye atatoa kafara Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakumwamrisha kufanya hivo. Wala hakumwambia yule bwana amwamrishe mke wake ikiwa na yeye aliridhia kufanya hivo. Hata hivyo naye anapata dhambi ikiwa yeye ndiye amesababisha mpaka mume wake akaingia katika aliyoingia.

*Mhusika:* ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
*Mfasiri:* Firqatunnajia.com
*Marejeo:* Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 81
*Imechapishwa:* 18/03/2024

https://firqatunnajia.com/al-waadiiy-kwamba-mke-aliyejamiiwa-mchana-wa-ramadhaan-hatoi-kafara/

Sasa Jiunge na sisi Previous Next [metaslider id=”92474″] Makala Makala zaidi … Darsa Darsa zaidi … Video Video zaidi … Dawrah/Nad-wah Dawrah/Nad-wah zaidi … Khutbah Khutbah zaidi … Mihadhara Mawaidha zaidi … Ruduud Ruduud zaidi … [metaslider id=”27421″] Ratiba ya Darsa za live...

﷽*al-Waadi´iy mgonjwa wa pumu kutumia sprei mchana wa Ramadhaan* *Swali:* Ni ipi hukumu ya kutumia sprei kwa watu wanaop...
20/03/2024



*al-Waadi´iy mgonjwa wa pumu kutumia sprei mchana wa Ramadhaan*

*Swali:* Ni ipi hukumu ya kutumia sprei kwa watu wanaopata ugumu wa kupumua?

*Jibu:* Udhahiri ni kwamba sio chakula wala kinywaji. Kwa hivyo sitambui kuwa inaharibu swawm.

*Mhusika:* ´Allaamah Muqbil bin Haadiy al-Waadi´iy
*Mfasiri:* Firqatunnajia.com
*Marejeo:* Fadhwaaih wa Naswaaih, uk. 80-81
*Imechapishwa:* 18/03/2024

https://firqatunnajia.com/al-waadiiy-mgonjwa-wa-pumu-kutumia-sprei-mchana-wa-ramadhaan/

Sasa Jiunge na sisi Previous Next [metaslider id=”92474″] Makala Makala zaidi … Darsa Darsa zaidi … Video Video zaidi … Dawrah/Nad-wah Dawrah/Nad-wah zaidi … Khutbah Khutbah zaidi … Mihadhara Mawaidha zaidi … Ruduud Ruduud zaidi … [metaslider id=”27421″] Ratiba ya Darsa za live...

15/04/2023

بسم الله الرحمن الرحيم
🌟🌙 = ZAKATUL-FITR =🌙🌟
🍒 🍛🍛🍛🍛🍛🍛🍛🍛🍛🍛🍛 🍒
عَنْ ابْنِ عَبَّاسٍ قَالَ
«فَرَضَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ زَكَاةَ الْفِطْرِ طُهْرَةً لِلصَّائِمِ مِنْ اللَّغْوِ وَالرَّفَثِ وَطُعْمَةً لِلْمَسَاكِينِ مَنْ أَدَّاهَا قَبْلَ الصَّلاةِ فَهِيَ زَكَاةٌ مَقْبُولَةٌ وَمَنْ أَدَّاهَا بَعْدَ الصَّلاةِ فَهِيَ صَدَقَةٌ مِنْ الصَّدَقَاتِ».🌙
رواه أبو داود 1371 قال النووي : رَوَاهُ أَبُو دَأوُد مِنْ رِوَايَةِ ابْنِ عَبَّاسٍ بِإِسْنَادٍ حَسَنٍ
_((Kutoka kwa Ibn 'Abbaas (R.A) ambaye amesema: "Mtume(ﷺ) amefaridhisha Zakaatul-Fitri kuwa ni twahara ya mwenye kufunga kutokana na maneno ya upuuzi na machafu, na kulisha masikini. Atakayeitoa kabla ya Swalah basi hiyo ni Zakaah iliyotakabaliwa, na atakayeitoa baada ya Swalah basi hiyo ni Sadaqah miongoni mwa Sadaqah"))_
☘. *UFAFANUZI WAKE.* ☘
**🔹**🔸**🔹**🔸**🔹**
Zakatul- fitr,faida Faida yake ni k**a ifuwatavyo chini:
🍛-N0 (1)
• _((Kumsafisha mfungaji katika yale yaliyompita au yaliyopungua katika funga yake.))_
🍛-N0 (2)
• _((Kumshukuru Mwenye ezi Mungu kwa neema ya kutuwezesha kumaliza mfungo wa mwezi wa Ramadhan))_
🍛-N0 (3)
• _((Kumshukuru Mwenye ezi Mungu kwa neema ya kutuwezesha kufika tena katika mwaka mwingine na ndani yake kutupa afya ya kuweza kufunga tena k**a tulivyofunga katika miaka iliyotangulia.))_
****
🍛-N0 (4)
• _((Kuwawezesha wenye shida katika jamii ya kiislamu siku ya Idd wawe katika hali nzuri ya furaha k**a wengine wao na familia zao na kwa hivyo kuongeza mapenzi kati yao .))_
****
🍛-.N0 (5)
• _((Kuwafanya waislamu wote masikini na matajiri siku ya Idd wawe ni wenye furaha wakifurahia sikukuu ya kumaliza mfungo ili hali kila mmoja akiwa na uwezo wa kumiliki chakula na mahitaji mengine ya siku ya Idd.))_
****
🍛-.N0 (6)
• _((Kuwalinda na kuwatosheleza wale masikini katika jamii ya kiislamu ili waweze kutulia na familia zao bila ya kuwaza juu ya mahitaji ya siku ile.))_
🍌******
عن ابن عمر رضي الله عنهما قال: فرض رسول الله صلى الله عليه وسلم زكاةَ الفطر ص

Pata maarifa na maelezo halisi kuhusu vitabu vya Kiislamu, matukio, maeneo, fiqh, sharia, sunnah, hadithi kutoka Islamic...
06/04/2023

Pata maarifa na maelezo halisi kuhusu vitabu vya Kiislamu, matukio, maeneo, fiqh, sharia, sunnah, hadithi kutoka Islamic knowledge Tanzania Maarifa ya Kiislamu.

31/03/2023

Fitina ya mwanamke iko usoni.
Allaah (Ta´ala) amemrukhusu mwanamke kuonesha mapambo yake yenye kufichikana kwa mtumishi mwanaume asiyekuwa tena na matamanio kwa wanawake na mtoto ambaye bado hajaelewa kitu kuhusiana na uke. Hili linatolea dalili kuonyesha mambo mawili:

1-Mapambo yenye kufichikana hayatakiwi kuonekana kwa wanaume ajinabi isipokuwa watu hawa aina mbili.

2- Hukumu hii inatok**ana na khatari ya fitina kwa mwanamke. Ni jambo lisilokuwa na shaka yoyote kuwa uzuri na fitina iko usoni. Hivyo inakuwa ni wajibu kuufunika mbele ya wanaume wenye matamanio kwa wanaume.

Address

FaruHost, Rock City Mall, 2nd Flor, Mwanza Ilemera
Mwanza

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Islamic knowledge Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category