Asoupestudioz

Asoupestudioz The Blessing Voice Singers under asoupestudioz from Seka SDA church Musoma-Mara, Tanzania

24/07/2023

Somo: SIKU ZA MWANADAMU

Katika dunia tunayoishi, zimekuwepo siku za aina nyingi sana, mathalani siku ya watoto,
siku ya akina mama, siku ya wazee n.k. Kwa kawaida, kwa kila siku za aina hii, jamii
hukusanyika na kuadhimisha tukio la hiyo siku. Siku nzima ni mjumuisho wa saa
24. Mwanadamu naye anazo siku zake za kuishi hapa duniani kwa mujibu wa maandiko.

MWANZO 6:1-3.....”Ikawa wanadamu walipoanza kuzidi usoni pa nchi na
wana wa k**e walizaliwa kwao,2 wana wa Mungu waliwaona hao binti za
wanadamu ya kuwa ni wazuri; wakajitwalia wake wo wote
waliowachagua. 3 Bwana akasema, Roho yangu haitashindana na
mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni nyama; basi siku zake
zitakuwa miaka mia na ishirini.”.....Mungu alipomuumba mwanadamu,
hakumwekea ukomo wa maisha yake. Maasi na dhambi zilipoongezeka,
Mungu aliamua kuweka kipimo cha kuishi kwa mwanadamu huyo
aliyemuumba, kwa kuwa hawezi kushindana na mwanadamu milele.
AYUBU 14:1-2... “Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za
kuishi si nyingi, naye hujaa taabu. 2 Yeye huchanua k**a vile ua, kisha
hukatwa; Hukimbia k**a kivuli, wala hakai kamwe”... Mwanadamu hana
siku nyingi za kuishi hata abweteke. Hata hivyo pamoja na uchache wa siku
za mwanadamu, Ayubu anasema zimejaa taabu (magonjwa, mikosi, vifo vya
utata n.k.). Leo Mungu anataka kuuleta ukombozi katika maisha ya watu kwa
Jina la Yesu.
Maandiko yanasema katika ZABURI 103:15...”Mwanadamu siku zake zi
k**a majani; K**a ua la kondeni ndivyo asitawivyo.”
AYUBU 10:20.....”Je! Siku zangu si chache? Acha basi, Usinisumbue,
nipate ngaa kutuzwa moyo kidogo.”....Mungu leo anataka alete matumaini
kwa uliyepoteza tumaini kwa Jina la Yesu.
Maandiko mengine yanasema katika ZABURI 144:44....”Binadamu
amefanana na ubatili, Siku zake ni k**a kivuli kipitacho..”..
KWA NINI TUJIFUNZE KUHUSU SIKU ZA MWANADAMU?

1. Ni kwa sababu Mungu tayari ametupangia muda wa siku za kuishi, na
hivyo ndani ya siku hizi wapo wanaotaka kuzipunguza ili zisitimie k**a
ambavyo Mungu wetu amekusudia.

Endapo mtu anakufa katika kifo cha utata, maana yake mwanadamu huyu
ambaye ni roho iliyopanga katika nyumba iitwayo mwili, atakuwa
hakuzitimiza zile siku za kushi alizompangia Mungu. Katika 1WAKORINTHO
15:40...”Tena kuna miili ya mbinguni, na miili ya duniani; lakini fahari
yake ile ya mbinguni ni mbali, na fahari yake ile ya duniani ni mbali.”....

Maandiko yanasema katika KUTOKA 23:25-26...”Nanyi mtamtumikia
Bwana, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako;
nami nitakuondolea ugonjwa kati yako. 26 Hapatakuwa na mwenye
kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku
zako nitaitimiza..”.... Kumbe inawezekana kabisa kwa siku zako kutotimia
endapo haumtumikii Bwana. Siku za mtu kuna uwezekano zisitimie. Hata
katika kazi yako, unaweza kujikuta unapunguziwa siku za ajira yako endapo
hujamtumikia Bwana inavyopaswa.

AYUBU 15:20.....”Mtu mwovu huwa na uchungu siku zake zote, Hata
hesabu ya miaka aliyowekewa mwenye kuonea.”....

Ndiyo maana katika WAEFEZO 6:10-12 imeandikwa ....”Hatimaye, mzidi
kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. 11 Vaeni
silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. 12 Kwa
maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya
falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo
wabaya katika ulimwengu wa roho.”...tunafundishwa namna ya kushindana
na siku ya uovu. Hii ni ile siku ambyo imewekwa ili kumsababishia mtu
matatizo ya aina fulani.

MHUBIRI 7:1.....”Heri sifa njema kuliko marhamu nzuri; Na siku ya kufa
kuliko siku ya kuzaliwa.”........

Maandiko yanasema katika AYUBU 7:1....”Je! Mtu hana wakati wake wa
vita juu ya nchi? Na siku zake, je! Si k**a siku za mwajiriwa?”....... Kila
mtu ana wakati wake wa vita. Usimcheke yeyote unapomuona anapigana
vita, ukasema eti hajui kupigana, kwa sababu kila mtu anao wakati wake wa
vita. Na kila mtu ni kana kwamba ni mwajiriwa aliye kazini, na usipofanya
vizuri utaondolewa kwenye ajira yako. Yesu vivyo hivyo alisema mkulima
anapoliona tawi lisiilozaa, hulikata na kulitupa nje. Msingi wa kuishi hapa
duniani siyo ufanye kazi, au biashara au kuoa na kuolewa,
lahasha‼. Hayo yote ni ya ziada, bali lengo kuu la kuwekwa hapa duniani
ni KUMTUMIKIA BWANA na hivyo usipofanya vizuri utaondolewa na kutupwa
nje.

AYUBU 14:15.....”Kwa kuwa siku zake zimeamriwa, hesabu ya miezi yake
unayo wewe, Nawe umemwekea mipaka yake asiyoweza kuipita;”.....
Kumbe maisha ya mtu yanaweza kuwekewa “mpaka”, na ambayo
huwezi kuuvuka. Hata uwe na fedha namna gani, huwezi kuuvuka huo
mpaka. Maisha ya yule tajiri na maskini Lazaro yanatufundisha kuhusiana na
huu mpaka. Tajiri akiwa kuzimu na Lazaro akiwa kifuani mwa Ibrahimu, na
katikati yao ulikuwepo mpaka.

2. Ni kwa sababu Tunataka kuzijua idadi ya siku zetu. Ule wakati wa kukaa
mashimoni umekwisha kwa Jina la Yesu. Danieli aliposoma vitabu aligundua
idadi ya siku za kukaa utumwani zimekwisha. Na hata sisi lazima tusome
vitabu na kwamba zile siku za kukaa chini ya utmwa wa shetani zinakoma
kwa Jina la Yesu.

Mungu wa dunia hii (ibilisi) naye hupenda kuweka mipaka ya siku zetu.
Endapo mtu angeweza kuona mbele ya maisha yake na kuziona balaa
zilizoandaliwa juu yake, hakika hayupo ambaye angesukumwa kuja kanisani
ili kumuomba Mungu amuepushie hizo balaa.

3. Ni kwa sababu Tunataka kuzijua siku za mwanadamu ili tujipime
na kujua jinsi gani tumekuwa dhaifu. Wakati mwingi hata waajiriwa
huchekwa pale wanapostaafu lakini huko mtaani unawakuta

hawajajenga hata kibanda cha kuishi.‼ Ni kwanini? Walipokuwa
ajirani walijisahau, wakaacha kujua kuwa siku za ajira zao zimepimwa.

ZABURI 139:4....”Bwana, unijulishe mwisho wangu, Na kiasi cha siku
zangu ni kiasi gani; Nijue jinsi nilivyo dhaifu.”.... Mtunga Zaburi anataka
kuangalia umri wake wa kuishi na kazi alizomfanyia Bwana ili kujua je
zinalingana?

Usifungwe na kazi au ndugu katika kumtumikia Bwana. K**a alivyofanya
Yusufu, vivyo hivyo na wewe ufanye vivyo hivyo, kwa kumuachia joho yeypte
anayekuvuta ili kukurudisha nyuma katika kumtumikia Bwana.

Imeandikwa katika 1WAKORINTHO 3:9....”Maana sisi tu wafanya kazi
pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.”......
Kuna mwingine ni k**a shamba la Mungu, lakini endapo Mungu anataka
kupanda chochote humtumia.

1WAFALME 16:34.....”Katika siku zake, Hieli Mbetheli akajenga Yeriko;
akatia misingi yake kwa kufiwa na Abiramu mzaliwa wake wa
kwanza, na kuyaweka malango yake kwa kufiwa na mwana wake mdogo
Segubu; sawasawa na neno la Bwana alilolinena kwa Yoshua mwana wa
Nuni.”.... Katika siku za mtu ujenzi unaweza kuendelea. Kuna mtu anaishi,
lakini kuna ujenzi anaoendeleza kuufanya ili magonjwa yampate mtu
mwingine. Kuna mtu anaishi lakini ameandaa mpango mbaya katika maisha
ya watu wengine.

Mungu anataka tuwe na siku nyingi, katika ndoa, familia, ajira n.k. Mungu
wetu siyo Mungu wa siku chache. Anapoponya uponyaji anaoutoa unakuwa
endelevu.

Katika siku za mtu fulani, mabaya yaweza kuletwa kutoka upande mmoja
kwenda mwingine.

Imeandikwa katika 1WAFALME 21:29....”Huoni jinsi Ahabu alivyojidhili
mbele yangu? Basi kwa sababu amejidhili mbele yangu, sitayaleta yale
mabaya katika siku zake; ila katika siku za mwanawe nitayaleta mabaya
hayo juu ya nyumba yake.”.... Mungu alikuwa ameshaahidi mabaya kumpata
Ahabu,lakini kwa kuwa Ahabu alijidhili Mungu akabadili msimamo wake, ila
mabaya yale yakaelekezwa kwa wana wa Ahabu.

Imeandikwa katika MAOMBOLEZO 5:7....”Baba zetu walitenda dhambi
hata hawako; Na sisi tumeyachukua maovu yao.”.... Katika maisha ya
mtu, kuna wakati uovu ulitendwa na waliomtangulia, lakini mateso yanampata
mtu mwingine ambaye hakuhusika na yale maovu.

Ni kweli Mungu alikusudia uishi miaka 120. Lakini shetani naye [k**a
mungu wa dunia hii] anaweza kuingilia kati ilisiku zako hizi zisitimie, endapo
wewe utakuwa mtenda dhambi.

Asoupe Family






Kusamehe niTabia ya MunguMahali sahihi pa kuanzia kujifunzahabari za kusamehe ni Mungu mwenyewe. Naweza kusema kwa ujasi...
24/07/2023

Kusamehe ni
Tabia ya Mungu
Mahali sahihi pa kuanzia kujifunza
habari za kusamehe ni Mungu mwenyewe. Naweza kusema kwa ujasiri na kw aushahidi
wa kimaandiko kwamba, Mungu sio tu ni chanzo bali kwake ni tabia. Ni tabia yake
Mungu kusamehe, na hufanya hivyo bila masharti. Tunaweza kupata aushahidi huu
kutokana na Neno la Mungu mwenyewe aliposema:
“Mimi, naam, mimi, ndimi
niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi
zako.” (Isa.43:25)
Maandiko haya yanatudhihirishia
kwamba, Mungu husamehe sio kwa sababu tumestahili kusamehewa, au sio kwamba
sisi tumemwomba sasa msamaha mpaka akashawishika, badala yake Mungu huamua
kusamehe kwa sababu ndiyo tabia yake. Anaposema “niyafutaye makosa yako kwa
ajili yangu mwenyewe” maana ni kwa rehema zake, huruma zake, upendo wake, na
ndiyo asili yake.
Ukifuatulia tangu binadamu wa kwanza
alipokosa, waliamua kujificha ili kwamba Mungu asiwaone. Mungu akawa
anawatafuta japo sio kuwa alikuwa hawaoni, ila wao walifikiri Mungu hawaoni.
Adamu Uko wapi? Adamu anajibu akisema:
“Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nikajificha.”
(Mw.3:8)
Unaona? Badala ya Adamu kumtafuta
Mungu baada ya kukosa ili aombe msamaha kwake, akaamua kujificha. Ndivyo
binadamu tulivyo hata sasa. Hatujitumi kumtafuta Mungu ili kutubu na
kutengeneza njia zetu. Lakini amemtuma Roho Mtakatifu ambaye ndiye
anayetufuatilia huku akituhukumu kupitia dhamiri zetu tugeuke na kutubu ili
tupate kudumisha uhusiano wetu na Mungu.
Haya tunapokuja kwa habari ya historia
ya dhabihu ya dhambi, ni Mungu mwenyewe aliyeweka taratibu na kanuni kwa wana wa Israeli za kuomba msamaha.
Dhabihu ni kielelezo cha kuomba msamaha toka kwa Mungu. Hii pia ni ishara
nyingine kwamba “kusamehe” ni tabia ya Mungu.
Hata suala la ujio wa Yesu duniani,
bado ni Mungu mwenyewe katika kutimiza ahadi yake ya ukombozi wa binadamu.
Tunaona Mungu ndiye aliyeupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe pekee ili kila
amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele. (YH.3:16)
Suala zima la wokovu wa Yesu Kristo
ni jitihadamu zake Mungu za kusamehe. Na ni jitihada anazifanya wakati binadamu
wenyewe ndio kwanza tumezama katika uasi na dhambi. Hatun habari na hata
tukipata habara hatujali.
Sasa tukirejea kwenye mada ya msingi
ya KWANINI LAZIMA TUSAMEHE. Ni kwa sababu wote tuliokubali kupokea msamaha
wake, tukafanyika watoto wake, tunawiwa kuwa na TABIA YA BABA YETU ambayo ni
KUSAMEHE bila masharti.
“lakini mimi nawaambia, wapendeni adui zenu,
waombeeni wanaowaudhi, ili mpate kuwa wana wa Baba yenu aliye mbinguni; maana
yeye huwaangazia jua lake waovu na wema, huwanyeshea mvua wenye haki na wasio
haki.” (MT.5:45)
Kwa agizo hili ni dhahiri kwamba,
haiwezekani kuwapenda adui zetu; na hata kuwaombea wanaotuudhi, k**a
hatujajenga au kuwa na tabia ya KUSAMEHE bila masharti k**a Mungu Baba yetu.
Mpendwa msikilizaji wangu, kwa leo tunajifunza kwamba, kusamehe ni tabia ya
Mungu. Na kwamba sisi k**a kweli ni watoto wake lazima tuwe na tabia ya Baba
yetu ya KUSAMEHE bila masharti.
Binadamu wote ni wakosaji
Sababu ya pili ya ni kwanini ni lazima kusamehe ni kwa sababu BINADAMU
WOTE NI WAKOSAJI. Sasa hapa naomba tuvue vazi la unafiki tuukabili ukweli
kwamba binadamu wote ni wakosaji ikiwa ni pamoja na wewe na mimi na binadamu
wenzetu.
Kwa hiyo, hakuna mwenye haki ya kumhukumu mwenzake hata k**a
anayo sababu ya kufanya hivyo, kwa kuwa mwenye kutaka kuhukumu yeye mwenyewe ni
mkosaji vile vile.
Naomba nijenge hoja yangu kwa mifano hai ya Biblia. Maandiko
yanasema kwamba, “walakini mauti ilitawala tangu Adamu mpaka Musa, nayo iliwatawala hata
wao wasiofanya dhambi ifananayo na kos ala Adamu, aliye mfano wake
atakayekuja.” (Rum. 5:14)
Unaona? Kosa la binadamu wa kwanza lilisababisha uzao wa
binadamu wote waliofuata kuathiriwa na tabia ya kukosa japokuwa sio kosa lile
lile walilokosea binadamu wa kwanza.
Ni kweli unaweza kuwa na madai tofauti au umetendewa isivyo haki
wala halali na wengine na ukawa na madai tofauti yanayojitegemea. Lakini hii
haifuti kwamba na wewe unao uliowakosea kivingine na kwamba nao wana madai
dhidi yako ambayo ni tofauti na madai yako dhidi ya wengine. K**a unavyokosewa
na watu ndivyo na wewe kwa kutaka au kutokukusudia unawakosea wengine.
Lakini hii hali ya kukosa haikuasisiwa na sisi wa kizazi hiki bali
imetokea mbali kwa binadamu wa kwanza k**a iilivyoandikwa kwamba: “Kwa
sababu k**a kwa kuasi kwake mtu mmoja
watu wengi waliinngizwa katika hali ya wenye dhambi,……” (Rum.5:19)
K**a tulivyojifunza kipengele cha jana kwamba Mungu ana tabia ya
kusameme bila masharti, leo kwenye kipengele hiki cha BINADAMU WOTE NI
WAKOSAJI, ni lazima tujenge tabia ya kusamehe wengine kwa sababu kwanza hatuna
haki ya kutoa hukumu dhidi wanaotukosea wakati sisi wenyewe tuna watu
wanaotuhesabu wakosaji wao.
Hapa sina maana ya kwamba tufumbie macho maovu na kwamba
tusiwaguse wakosaji kwa mujibu wa sharia zilizopo. Kusamehe sio kufumbia macho
uovu. Kusamehe ni kutokumhesabu mkosaji k**a binadamu anayestahili kupewa
second chance ya kujirekebisha. Lakini pia kusamehe kunakotajwa hapa ni
kutokuwa na kinyongo pamoja na visasi dhidi ya wakosaji wako, badala yake
kumbuka na wewe umesimamaje machoni pa wengine ambao wanakuhesabu umewakosea.
Kabla ya kutunga kidole wakosaji wako angalia vidole
vinakuelekea wewe mwenyewe na kujihoji k**a unatenda haki stahili. Na mwisho
vile inavyotaka kuwatendea wakosaji wako ndivyo unavyotaka na wewe utendewe na
wenye madai dhidi yako?
Turejee kisa cha Yesu kuletetewa mwananke aliyek**atwa akizini
na washtaki wake wakataka sharia ichukue mkondo wake, Yesu naye akawajibu
ambaye hana dhambi k**a hiyo awe wa kwanza kutoa adhabu, na wote wakatoweka bil
akuaga. Yesu akamwambia mwanamke yule enenda zako USITENDE DHAMBI TENA.
Kusamehe ni Sharti la
kusamehewa
Kipengele cha tatu ambacho ni KUSAMEHE NI SHARTI LA KUSAMEMEWA. Sababu
hii inatokana na kauli ya Yesu Kristo mwenyewe aliposema: “Lakini k**a ninyi hamsamehe,
wala Baba yenu aliye mbinguni hatawasamehe ninyi makosa yenu.” (Mk.11:26)
Haya ni maneno ya Yesu Kristo mwenyewe. Kuna kisa ambacho Yesu
alisimulia kuhusu mtu aliyekuwa anadaiwa na akak**atwa ili aadhibiwe akaomba
msamaha apewe nafasi ya kulipa deni lake, na akasamehewa deni hilo. Kumbe mtu
yule yule alipokutana na mtu ambaye anamdai tena kiasi kidogo kuliko madeni
anayodaiwa yeye, aliamua kumwadhibu mdeni wake bila huruma na akasahau kwamba
yeye amesamehewa madai k**a yale.
Unyama wake huyu ulimfikia yule aliyekuwa amemsamehe na akamwita
na akaamua kumwadhibu vikali kwa sababu yeye alishindwa kuonyesha ubinadamu kwa
mwenzake.
Kutokana na kisa hiki Yesu aliweka waziwazi msimamo wa Mungu
kuhusu KUSAMEHE. Licha ya kwanza anataka sisi k**a watoto wake tuwe na tabia ya
KUSAMEHE bila masharti; bado Mungu amekufanya KUSAMEHE k**a sharti la
KUSAMEHEWA.
Bila shaka Mungu anajua kwamba sisi binadamu tuna ubinafsi na
kujipendelea pamoja na kujisahau kwa habari za mahitaji ya wengine. Tunapofikia
kiasi ambacho hatuko tayari KUSAMEHE wengine, njia peke ya kuturejesha kwenye
mstari ni KUTOKUSAMEHEWA makosa yetu wenyewe k**a hatutaku kuwasamehe wengine.
Hii ndiyo maana ya kipengele cha sala ya Bwana kinachosema;
“utusamehe makosa yetu k**a sisi tunavyowasamehe waliotukosea.” Unaona. Kiwango
kile kile tunachosamehe wengine ndicho kiwango tunachosamehewa na sisi mbele za
Mungu.

Asope Family





SOMO: Nguvu ya Maombi (The Power of Prayer). MADA: Jinsi Gani tuombe ili Mungu ajibu maombi yetu?SEHEMU YA KWANZA.Tunapa...
24/07/2023

SOMO: Nguvu ya Maombi (The Power of Prayer).
MADA: Jinsi Gani tuombe ili Mungu ajibu maombi yetu?

SEHEMU YA KWANZA.

Tunapaswa Kuomba Juu ya Mambo Gani? Inaendelea......

C. Kupeleka Mahitaji Yetu Mbele za Mungu na Kutoa Shukrani.

Tunapaswa kuomba kwa ajili ya Mahitaji ambayo sisi kweli tuna haja nayo na Mara nyingi tunafanya hivyo. Hata hivyo baadhi ya watu husahau kumshukuru Mungu kwa yale maombi wanayojibiwa na pokea.

Maombi yetu Mara kadhaa yanahusisha kuomba Mahitaji zaidi kila Sikh katika maisha yetu. Mungu ni mkarimu sana na yeye hutoa kile tunachohitaji kwa wakati unaostahili.

Pamoja na Mungu kujibu Maombi yetu, ni muhimu kujua kuwa Pia Mungu anatarajia tuthamini kile anachotoa kwaajili yetu kwa kusema asante.

Maandiko katika Biblia hutufundisha kuwa tunaweza kuomba kile tunachohitaji na Mungu akajibu maombi yetu:

Wafilipi 4: 6 maandiko yanasema

6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.

Badala ya kuwa na wasiwasi, ni muhimu maombi yako/ haja zako zijulikane na Mungu. Maandiko yamesisitiza kuwa kwa kila jambo majibu yamo katika kuomba na shukurani.

Mathayo 7: 7-11maandiko yanatukumbusha kuwa, Mungu ni Baba mwenye upendo ambaye huwapa watoto wake Mahitaji kwa kadri walivyoomba.

Anauliza je ni nani kati yenu mwanaye akiomba mkate atampa Jiwe? Au akiomba samaki atampa nyoka?

Anamalizia kwa kusema " k**a ninyi mlio waovu mwaweza kuwapa watoto wenu vipawa vyema je si zaidi sana Baba yenu Wa Mbinguni .........'' Hivyo kile tunachokiomba ndicho tutakachopokea.

1 Petro 5: 7 maandio yanasema wazi kuwa, Mungu hujishughulisha Zaidi na Mambo Yetu na hivyo tumpe yeye Fadhaa/haja zetu. Anasema.

7 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.

Tua wasiwasi wako kwa Mungu kwa kuwa anakujali sana kupita ulivyowahi kufukiri.

Yakobo 4: 2,3 maandiko yanatuweka wazi kuwa, Wakati mwingine hatuwezi kupokea majibu ya maombi yetu kwa sababu hatuombi, na k**a tunaomba basi tunaomba vibya yaani bila kufuata utaratibu. Anasema;

2 Mwatamani, wala hamna kitu, mwaua na kuona wivu, wala hamwezi kupata. Mwafanya vita na kupigana, wala hamna kitu kwa kuwa hamwombi!

3 Hata mwaomba, wala hampati kwa sababu mwaomba vibaya, ili mvitumie kwa tamaa zenu.

Kwa upande mwingine, Mungu hawezi kujibu maombi ya ubinafsi kwa ajili ya mambo ambayo tunayahitaji ili yatupe faida kwa tamaa zetu wenyewe .

1 Yohana 5: 14-15 maandiko yanasema;

14 Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia.

15 Na k**a tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba.

Kwamba K**a tunaomba kulingana na mapenzi ya Mungu, ndipo Yeye hupokea maombi yetu. Kwa hakika lazima tujue tunaombaje kulingana na Mapenzi ya Mungu?

Maandiko hapa chini yana fafanua vuzuri sana kile kinachotakiwa kufanyaika.
[ 1 Yohana 3: 21,22; John 14: 13.14, 15: 7.16; 16: 23,24,26] mfano katika 1 Yohana 3:21-22 ana sema;

21 Wapenzi, mioyo yetu isipotuhukumu, tuna ujasiri kwa Mungu;

22 na lo lote tuombalo, twalipokea kwake, kwa kuwa twazishika amri zake, na kuyatenda yapendezayo machoni pake.

Ukisoma kwa making utajua tu kuwa sio kila MTU anaomba na kujibiwa Bali ni wale wanaozishika amri za Mungu na kutenda mema.

Kadhalila katika Yohana 15:7 yanasema,

7 Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.

Kwamba kiwango cha kuomba lolote na likapata majibu ni lazima uwe ndani ya Yesu na maneno yake yawe ndani yako.

Tafsri rahisi ni kwamba uwe umetubu na kuacha dhambi na kwamba Yesu ni Bwana na mwokozi wako, na neno lake umelihifadhi ndani yako.

Kanuni nyingine ya kuomba na kujibiwa maombi ni kuzaa matunda. Tena matunda yatakayo kaa. Namaanisha kuwaleta wengine kwa Yesu nao wakae na kudumu ndani ya Yesu. Ndio maana yohana 15:16 anasema;

16 Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.

Maandiko pia hutufundisha kuwa tunapaswa pia kutoa shukrani kwa baraka zetu na maombi yetu tunayojibiwa:

Wafilipi 4: 6,7 anasema, haja
zetu na zijulikane na Mungu pamoja na shukrani.

1 Timotheo 2: 1 maandiko yana tufundisha kuwa, Sala kwa ajili ya wengine ni pamoja na kutoa shukrani kwa aajiri yao.

Waefeso 5:20 Maandiko yanatuelekeza Kutoa shukrani kwa Mungu siku zote na kwa mambo yote yanayotuzungukaikiwa in pamoja na Uhai na Afya njema tulizo nazo. Anasema;

19 mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;

20 na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo.

Vifungu hivi pia huonyesha umuhimu Wa kumshukuru Mungu na kwakweli ni tendon la imani kuomba na kushukuru kabla ya kujibiwa haja yako.

[1 Thesalonike. 5:18; Kolosai 4: 2; 2: 7; 3:17], Kolosai 4:2 anasema,

2 Dumuni sana katika kuomba, mk**esha katika kuomba huku na shukrani.

Nimuhimu kujua kuwa, maombi mara zote huenda sambamba na shukrani. Mara tu unapomaliza kutoa haja zako basi Mshukuru Mungu kwa kujibu haja za moyo wako, huku ukijua kuwa kila jibu unalohita bado ni kwa wakati ulioamriwa.

Mungu kwa upendo Mkuu anatualika wote kupeleka Haja zetu mbele zake lakini huchukizwa tena kwa kiasi kikbwa na watu wasio na shukrani. (Luka 17: 12-17).

Ebu soma hii hadithi uone shukrani inavyoweza kumuokoa mtu, nawe ujifunze kuomba na kushukuru.

12 Na alipoingia katika kijiji kimoja, alikutana na watu kumi wenye ukoma; wakasimama mbali,

13 wakapaza sauti wakisema, Ee Yesu, Bwana mkubwa, uturehemu!

14 Alipowaona aliwaambia, Enendeni, mkajionyeshe kwa makuhani. Ikawa walipokuwa wakienda walitakasika.

15 Na mmoja wao alipoona kwamba amepona, alirudi, huku akimtukuza Mungu kwa sauti kuu;

16 akaanguka kifudifudi miguuni pake, akamshukuru; naye alikuwa Msamaria.

17 Yesu akajibu, akanena, Hawakutakaswa wote kumi? Wale kenda wa wapi?

18 Je! Hawakuonekana waliorudi kumpa Mungu utukufu ila mgeni huyu?

19 Akamwambia, Inuka, enenda zako, imani yako imekuokoa.


Asope Family





https://youtu.be/E5ZZvo6u2L4
20/05/2023

https://youtu.be/E5ZZvo6u2L4

Sauti na maneno ya wimbo mkuu wa kihonda net event 2023,Ni rahisi sana kukariri Kwa kutazama video hii.Barikiwa.🙏

18/05/2023

BWANA NDIYE MCHUNGAJI WANGU
Zaburi 23:1 Bwana ndiye mchungaji wangu; Sitataka
Nataka tuangalie Zaburi 23.
Zaburi hii imekuwa ikizungumzwa katika mazishi na matukio mengi. Ni kile tunachoweza kukiita "Zaburi ya Kawaida." Wakristo wengi, na wasio wakristo, wanajua Zaburi hii. Lakini swali ni je, tunalijua hilo
Tuanze na mstari wa 1. "Bwana ndiye mchungaji wangu, sitaki." Fikiria juu ya hilo. Mfalme wetu mkuu na Bwana ni mchungaji kwetu. Mchungaji hutunza kondoo wake. Jambo moja ambalo ninajua kuhusu Yesu ni kwamba anatutunza. Anatuongoza na kutuongoza katika mwendo wetu wa maisha.mioyoni mwetu
Yesu anatuambia katika Yohana 10:11, "Mchungaji Mwema hutoa maisha yake kwa ajili ya kondoo." Alisema Mchungaji Mwema hutoka nje, bila kujali hali ikoje, na hutafuta kondoo mmoja aliyepotea. Alisema kwamba atatuongoza na kutukimu katika maisha yetu.
Fikiria chakula chote ambacho mchungaji wetu ametutengenezea, na aina mbalimbali. Angeweza kutupa mkate na maji na kusema hiyo inatosha, lakini si Yesu wetu. Alifanya mengi kiasi kwamba ni ya kushangaza tu! Umewahi kutazama mtandao wa chakula na kushangazwa na vyakula vyote tofauti vya dunia yetu?
Angeweza kuifanya dunia k**a sayari ya mars: tasa na tupu.Tena, Yesu hakufanya hivyo. Aliifanya dunia iliyojaa uhai na hazina kiasi cha kuishangaza akili! Je, umewahi kutazama "Sayari ya Dunia," na kukaa hapo huku kinywa chako kikiwa wazi kwa uzuri na maajabu ya viumbe vyake vyote?
Ningeweza kuendelea na kuendelea, lakini leo, tukumbuke kwamba Bwana ndiye mchungaji wetu. Hatutapungukwa, kwa sababu Anatutimizia mahitaji yetu yote. Yeye ndiye Mungu wa kufurika, Mungu wa ajabu na uwezo, na zaidi ya yote, Yeye ndiye MCHUNGAJI wetu MWEMA!
Bwana Yesu ndiye Mchungaji wangu Mwema. Yeye daima huangalia kila hitaji nililo nalo, na kukidhi mahitaji hayo kwangu. Mchungaji wangu Mwema ananipenda, na daima ana ubora wangu akilini.
Asoupe Family




14/05/2023

Tutafakari maneno haya , Binadamu huwa tunajisahu sana

14/05/2023

SIKU MOJA
Ukimya utatamalaki, upweke utashika hatamu na kila mtu atabaki kimya akitafakari siku hiyo.
Ndugu zangu wapo watakaosalimu amri kwa kuyaruhusu machozi yazitawale nyuso zao, wapo watakaoyasindikiza machozi yao kwa kwikwi na vilio vya hofu. Wapo watakao kuwa wakilia usoni lakini mioyoni mwao wakishangalia siku hiyo.
Nitakuwa kimya, nimetulia tuli na sitaweza kuziondoa pamba zitakazokuwa zimepachikwa katika matundu ya pua na masikio yangu. Naam, sitakuwa na uwezo wa kuchagua aina ya marashi yatakayo tumika kunipulizia kwa wakati huo.
Nitakuwa nimevikwa vazi jeupe p*e, vazi ambalo litashuhudia funza wakiushambulia mwili wangu chini ya mgongo wa ardhi. Nitakuwa ukisubiri kubeba mchanga tani sita katika shimo lenye urefu wa futi sita.
Siku hiyo nitakuwa pekee yangu , katika siku hiyo sitakuwa tena na manjonjo, kiburi ama maringo niliyonayo leo hii.
Pengine nimewahi kuwa na ahadi nyingi katika maisha za kuzitimiza lakini siku hiyo zote zitakuwa zimekoma
Ni siku isiyo na jina,ni siku isiyoepukika ila ni siku isiyo mbali
Jua huchomoza, mwezi hung'ara,mawio na machweo pia,vyote havitasogea kuilekea siku hiyo.
Ni katika siku hiyo ambapo pumzi na mwili wangu vitatengana,nafsi yangu itaelekea kusiko marejeo.

Tafakari Njema, Jumapili Njema

Imetayarishwa na kuletwa kwako na
Asoupe Family
Asoupestudioz
14/05/2024






Karibu ubarikiwe na wimbo huu Kutoka The Blessing Voice Singers (SYC) Kwaya ya vijana wa  kanisa la wasabato Seka-Musoma...
22/04/2023

Karibu ubarikiwe na wimbo huu Kutoka The Blessing Voice Singers (SYC) Kwaya ya vijana wa kanisa la wasabato Seka-Musoma
https://www.youtube.com/watch?v=hAVK5MGZQp4
Tutembelee katika youtube channel yetu kwa nyimbo zaidi.
Usisahau ku Subscribe,Comment na Share kwa kugusa link hii
https://www.youtube.com/
Ahsante

Barikiwa na wimbo huu wa Mtini kutoka kwa kwaya ya The blessing voice singers, ikiwa ni album yao ya kwanza, track 8.

HAKUNA HOFU2 Timotheo 1:7 Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.Tunaona kwam...
22/04/2023

HAKUNA HOFU
2 Timotheo 1:7 Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya moyo wa kiasi.
Tunaona kwamba si Mungu atoaye hofu. Mungu ametupa nguvu, upendo, na utimamu wa akili. Kwa hivyo hofu inatoka wapi? Hofu inatoka kwenye shimo la kuzimu. Watu wengi wako katika utumwa wa hofu nyingi katika maisha yao, na inawazuia kutoka kwa uwezo wao.
Tunaweza kuzungumza juu ya hofu tunayosikia mara nyingi, k**a hofu ya urefu au hofu ya buibui, lakini hofu zote hutoka kwa chanzo chao, na yote ilianza wakati wa kuanguka kwa mwanadamu. Katika uumbaji, Mungu hakuweka woga ndani ya Adamu au Hawa, lakini walipokula tunda lililokatazwa, hofu hii iliingia maishani mwao.
Angalia jinsi inavyoileta katika Mwanzo 3:8-10: “Kisha wakasikia sauti ya BWANA Mungu, akitembea bustanini wakati wa jua kupunga, Adamu na mkewe wakajificha usoni pa BWANA Mungu. kati ya miti ya bustani.
9 Ndipo BWANA Mungu akamwita Adamu, akamwambia, Uko wapi?
10 Akasema, Nalisikia sauti yako bustanini, nikaogopa kwa kuwa mimi ni uchi; nami nikajificha.”
Adamu anamjibu Mungu kwa maneno “Niliogopa,” ingawa kabla tu ya hili, tunaona kwamba Mungu alishuka kila siku wakati wa jua baridi ili kushirikiana nao, na ili wao wafurahie ushirika pamoja na Muumba.
Hofu ilikuja ulimwenguni wakati wa anguko, lakini sasa imetupwa nje kupitia kazi iliyokamilika ya Yesu pale msalabani.
Hatupaswi kuishi chini ya utumwa wa hofu. Tunaweza kuishi katika ushindi wa kazi iliyomalizika ya msalaba. Yesu ameziharibu kazi za shetani, na hofu ni mojawapo. Kwa hiyo leo, fanya uamuzi wa kutembea katika ushindi ambao Yesu Kristo amekushindia!

Asoupestudioz

Address

Musoma

Opening Hours

Monday 09:00 - 17:00
Tuesday 09:00 - 17:00
Wednesday 09:00 - 17:00
Thursday 09:00 - 17:00
Friday 09:00 - 17:00
Sunday 09:00 - 17:00

Telephone

+255626926340

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Asoupestudioz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to Asoupestudioz:

Share

Category