Moody Economics Photo and Video Production

Moody Economics Photo and Video Production OUR SERVICES 1.PHOTO ENTRY 2. VIDEO DOCUMENTARY 3.PASSPORTSIZE EXPRESS

25/04/2025
21/04/2025

KARIBUNI SANA, BEI POA UBORA ULE ULE

Kilosa Moja hiyo
04/06/2022

Kilosa Moja hiyo

13/03/2022

RATIBA YA YANGA KUWASINDIKIZA RSB BARKANE AIRPORT.

SAA 3:00 kutembelea kiwanda cha Magodoro GSm

5:00- Kuvua Kambale uwanja wa Kaunda

7:00. - Msafara wa Yanga na Wenyeji wao kuelekea Airport

8:30 - Msafara kufika Airport na Msagasumu na Haji Manara kutumbuiza

9:00 Timu kupanda ndege.

Shime shime wana Yanga tujitokeze kuwasindikiza wageni wetu hawa Waarabu.

11/03/2022

Hii imetokea huko ujerumani ambapo daktari mmoja wa vichaa mwenye hospitali yake binafsi alikuwa anasafiri na vichaa

wake watatu wenye nafuu katika ndege ndogo toka mji mmoja kwenda mji mwingine.

Wakiwa hewani wagonjwa wawili walikuwa wanacheza cheza na kupiga kelele ndani ya ndege kwa nyuma wakati mmoja ametulia

kimya akiwa ameshika gazeti. Kelele zilikuwa zinasumbua kiasi fulandi ndipo Yule mgonjwa aliyekuwa kimya akaenda kwa

daktari mbele katika chumba cha kuongozea ndege na kuzungumza na daktari wao

Mgonjwa: Samahani dokta, nilikuwa nafikiri k**a tungewapa mipira wachezee ili wapunguze kelele

Daktari: Ni sawa haina tatizo, wazo zuri sana

Yule mgonjwa akarudi nyuma kwa wenzie kisha baada ya k**a dakika kumi hivi kule nyuma kulikuwa kimya kabisa. Daktari

akafurahishwa mno na ubunifu wa yule mgonjwa mmoja na kuona kuwa maendeleo yake ni mazuri.

Daktari akataka kuwapa pongezi kwa kukaa kimya, akamuita yule mgonjwa aliyetoa wazo na kumuuliza

Daktari: aisee! Wazo lako ni zuri sana, waambie wenzio kuwa tukifika nitawapa zawadi kwa utulivu wa leo

Mgonjwa: nilipata wazo zuri zaidi ya lile, nilipowapa mpira nikawafungulia mlango wakachezee barazani. Wakiingia ndani

nitawaambia. Shukrani dokta.

Jamaa alipita sehemu isiyoruhusiwa katika kambi ya jeshi na akapewa adhabu ya kuhamisha tofali 1000!Jamaa akajitahidi ak...
06/03/2022

Jamaa alipita sehemu isiyoruhusiwa katika kambi ya jeshi na akapewa adhabu ya kuhamisha tofali 1000!
Jamaa akajitahidi akabeba tofal 900 na akawa hoi! Na ghafla akakumbuka kuwa mkuu wa kambi ni rafik yake wamesoma pamoja,

akampigia simu.
Jamaa,”mkuu, vijana wako wamenipa adhabu ya kuhamisha matofali 1000!”
Mkuu,”hao wajinga kweli hawajui tunavyofahamiana! Wasikusumbue,mi ndo mkuu wao. Zirudishe palepale zilipokuwa mwanzo,

halafu uje ofisini tuonane.” Jamaa wacha alie.

06/03/2022

Jamaa yangu mmoja alikuja kunitembelea kule Mburahati Madoto. Sasa wakati namsindikiza tukafika kituo cha madoto mwisho

kusubiri daladala. Mara jamaa yangu akanyewa na kunguru kichwani. Jamaa akaangalia juu alivyogundua amenyewa akamuona

kungulu usawa wake, jamaa akaangua kicheko sana yaani. Mi nilikuwa naona yote yanayotokea nikamuuliza “sasa unacheka nini

ndugu yangu wakati umenyewa?” Jamaa akajibu “We acha tu, afadhali bata hawapai angani k**a kunguru”...................

06/03/2022

*Jeuri dawa yake kiburi;* 🤣🤣🤣🤣

Gari imeondoka KARIAKOO kufika MANZESE konda akauliza kuna mtu anashuka?

Abiria 1 akajibu: "Tumeziacha nyumbani tuna mitandio tu."

kufika mbele..

abiria mwenye nyodo akawa anashuka UBUNGO MAZIWA. Akasema;

"Konda nashuka maziwa."

Konda akamjibu;

"Itabidi urudi mjini ukanunue Sidiria."

19/02/2022

*MAMA ETI BABA YETU ATAKUFA LINI.?*

Hakuna siku niliyojisikia vibaya k**a siku moja nipo nyumban, k**a kawaida yangu nilikuwa nimelewa chakar, nimejilaza kwenye kochi. Hapo ni baada ya kumtukana mke wangu na kuwaambia wote waende jikoni.
Ilikuwa ni usiku, baada ya muda njaa ilinibana, nilinyanyuka na kuyumbayumba kwenda jikoni kudai chakula ambacho mke wangu amepika nikiwa sijui hata pesa katoa wapi kwani asubuh sikumwachia chochote.
Baada ya kufika mlangoni kabla sijapiga teke mlango k**a kawaida yangu, sauti ya mtoto wangu wa miaka minne ilisikika akimuuliza mama yake, "MAMA ETI NA SISI BABA YETU ATAKUFA LINI?"

Nilishtuka na kuanza kusikiliza walikuwa wanazungumza nini, "Wewe mtoto nyamaza usiseme hivyo ni vibaya, tema mate chini" mke wangu alimkemea lakini hakujali.
Sasa mbona dada amesema baba yake Jonas amekufa, ameenda kwa Mungu hatarudi tena, kwanini na sisi baba yetu asiende ili tubaki wenyewe?, mtoto aliongea. Mke wangu alijaribu kumkanya lakini hakusikia aliendelea.
Binti yangu wa miaka saba yeye alimkatisha kumuelewesha.

"Baba Jonas anaenda kwa Mungu kwa sababu ni mtu mzuri. Baba yeye hataenda kwa Mungu, ataenda kwa shetan, haendi Mbingun..." alimaliza kumuelewesha mdogo wake, mke wangu alichanganyikiwa zaidi alijaribu kuwakanya lakini yule mdogo aliendelea.
"Heri hata Baba afe maana anakupiga wewe kila siku na sisi, ningekuwa Rambo ningemuua Paap! Paaa! 🤓😳😳Pigo moja tu anakufa, nikiwa mkubwa namuulia mbali……". Aliongea kwa kujigamba.😎

Mtoto aliendelea kuongea kwa msisimko, nilijikuta nasimama wima, pombe ziliniisha, njaa ikakoma, nilianza kutambaa kurudi sebulen, nilishindwa hata kukaa. Niliingia chumban na kuanza kujiangalia kwenye kioo.
Nimefanya nini maisha yangu niliwaza nikikumbuka nilivyokuwa natamani kuwa na familia nzuri, mke mzur na watoto ambao wananipenda. Lakini mtoto wangu mwenyewe wa miaka minne anatamani mimi baba yake kufa! Nilitaman kulia lakin nilijua haitanisaidia, niliingia bafuni na kuanza kujitapisha, nilitapika pombe yote

REJAREJA TSH.10000.JUMLA TSH. 8000 for 6PCMOROGORO-KILOSA-UHINDINI-MTAA WA WAZEE KARIBU NA DUKA LA KANZU
12/01/2022

REJAREJA TSH.10000.
JUMLA TSH. 8000 for 6PC
MOROGORO-KILOSA-UHINDINI-MTAA WA WAZEE KARIBU NA DUKA LA KANZU

Address

KILOSA
Morogoro
620

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Moody Economics Photo and Video Production posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to Moody Economics Photo and Video Production:

Share