Professor Jay

Professor Jay MIKUMI Stand UP�

Dada mkuu  KASHASEMA❤️❤️❤️❤️ "1st  May Ombi langu kuu ni mjitokeze kwa wingi sana kushuhudia ukuu wa Mungu.
19/04/2026

Dada mkuu KASHASEMA❤️❤️❤️❤️

"1st May

Ombi langu kuu ni mjitokeze kwa wingi sana kushuhudia ukuu wa Mungu.







"PROF JAY NI GIANT GORILLA WA BONGO FLAVAKUTAMBULISHA albamu ya Machozi, Jasho na Damu, ilitoka "Bongo Dar es Salaam", "...
17/04/2026

"PROF JAY NI GIANT GORILLA WA BONGO FLAVA

KUTAMBULISHA albamu ya Machozi, Jasho na Damu, ilitoka "Bongo Dar es Salaam", "Jina Langu", halafu "Ndiyo Mzee". Mikwaju mingine iliyofuata ni “Piga Makofi” aliowashirikisha Simple X na Sos B, “Niamini”, aliofanya na familia yake ya HBC, Big W***y na Fanani. “Tathmini” alibatua na Jay Moe, “Nawakilisha”, aliowaalika AY, Black Rhino, Complex na Adili.

Vyuma vingine ni “Na Bado”, “Salamu Bibi na Babu”, “Yataka Moyo” na “Machozi, Jasho na Damu”, uliobeba jina la albamu. Fanya mapitio upya kuanzia mwanzo. Hesabu ni tracks 11. Urefu ni dakika 53. Ukianza kusikiliza, hakuna kupeleka mbele wala kuskip, kila tufe lina-makes sense. Hii ndiyo mantiki huwa hakuna ubishi, Machozi, Jasho na Damu inapotajwa kuwa ni moja ya albamu bora kabisa za Bongo Flava.

Albamu mbili; Funga Kazi 2000, vilevile Machozi, Jasho na Damu, zilitosha kumpa Prof Jay legendary status si tu kwenye jumuiya ya Hip Hop Afrika Mashariki, bali kwa sanaa ya Afrika. Jay ni legend. Jay ni giant gorilla. Vyovyote unavyoweza kumtafsiri, Jay ni monstrous size kwenye utamaduni wa Bongo Flava.

Machozi, Jasho na Damu ilitoka Desemba 2001. Mwaka 2002, yalikuwa majuma 52 ya makusanyo kwa Prof Jay. Show mkoa kwa mkoa, hadi kuvuka mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Wakati huohuo ilikuwa miezi 12 ya hekaheka za jikoni, maandalizi ya pishi jipya, Bongo Records, kwa audio engineer, P Funk Majani.

“Priii priii eti promota anabeep, naamua kumpigia bila aibu anajisifu,” ilikuwa salamu ya Prof Jay, jina la wimbo ni “Promota Anabeep”, with Mgosi Mkoloni, michambo mikavu kwa Nyangema Promota aliyevaa suti na kandambili. Anamwahidi msanii paradiso, halafu anampiga kizinga cha nauli na kugongea fegi. “Nyambaaf”, kwa sauti ya Mkoloni. Ndivyo albamu “Mapinduzi Halisi”, ilivyotambulishwa.

Desturi ya Jay ilikuwa kuandika historia katika kila albamu, ndivyo alivyofanya kwenye “Zali la Mentali” ndani ya Mapinduzi Halisi.

Unaweza kuzuia mvua lakini siyo heshima ya Prof Jay kwenye Bongo Flava. Mei Mosi, 2026, Bongo Flava Honors itafanikisha the long overdue induction ceremony ya Jay. 710 Garden, Kawe historia itaandikwa. Sugu The Jongwe atasherehesha tukio.

Ndimi Luqman MALOTO".

"JAY ALIVYOTUNUKIWA UPROFESA WA BONGO FLAVA!MIEZI ya utawala wa Funga Kazi 2000 ilikoma mwaka 2001 ulipowasili. Jay haku...
09/04/2026

"JAY ALIVYOTUNUKIWA UPROFESA WA BONGO FLAVA!

MIEZI ya utawala wa Funga Kazi 2000 ilikoma mwaka 2001 ulipowasili. Jay hakutaka kingdom itetereke. Aliikabidhi domain albamu “Machozi, Jasho na Damu”, ikiwa solo project nje ya HBC. Introduction single ni “Bongo Dar es Salaam”. Again, storyteller N***a Jay, aliweza kuifanya Afrika Mashariki i-bow kulielekea jina lake, kwa jinsi alivyoisimulia Dar es Salaam na visanga vyake ndani ya beti tatu kwa ufundi wa hali ya juu. Lady Jaydee akanogesha hook.

Unauza cheni bandia, unalipwa pesa feki, mitaa ya Dar unakutana na bibi vizee wanafanya ukahaba, unapita Mwananyamala kizembe, unapigwa roba ya mbao, viwanjani unadata warembo wote bien, unashindwa kumtofautisha changudoa na mtoto wa kishua, katikati ya jiji unagongewa hadi mhuri wa Ikulu, halafu watu wanaendesha exotic cars, wakati maisha ya Mbongo ni danga-chee. Jay aliua kila line, beti kwa beti, visa na matukio yote, ndani ya Bongo Dar es Salaam.

“Jina Langu”, ni release namba mbili ya Machozi, Jasho na Damu. K**a kulikuwa na mtu aliyekuwa bado na shaka kuhusu utaalamu wa Jay kwenye mbanga za Hip Hop, basi Jina Langu ilimnyoosha. Kisha, bila huruma, Jay akaachia “Ndio Mzee” ft Juma Nature na Babu Ayubu. Jay alitumia sanaa kuionesha jamii kamba za wanasiasa vipindi vya uchaguzi.

Ndio Mzee ni pini lingine lililowalazimisha wazee kumpenda Jay. Alikuwa kijana mdogo, lakini akili na maarifa vilizidi umri. Ni hapo the everlasting DJ, John Dilinga Matlou, akahoji for what reason aendelee kuitwa “N***a Jay”, wakati kazi yake ina hadhi ya kiprofesa?

Pwani ya Mashariki hadi Lake Tanganyika. Kanda ya Ziwa mpaka Nyanda za Juu Kusini. Kilimanjaro na Meru, himaya za katani na korosho. Maskani za alizeti na zabibu, Unyanyembe na East Africa yote. Kauli ya DJ JD ilipokelewa unanimously. Mitaa ikanyoosha mikono kumtunuku Jay Uprofesa. Ni profesa wa muziki. Profesa wa Hip Hop. Profesa wa Bongo Flava. Fupisha, tamka Profesa Jay.

Jay ni foundational lifter of Bongo Flava. Do you still defy that? Mei Mosi, 2026, ni siku ya Bongo Flava Honors kudhihirisha kwa nini Jay anaitwa Profesa. Curator Sugu the Jongwe ataongoza shughuli. Makutano ni 710 Garden, Kawe Beach.

Ndimi

"Big vibes. Bigger energy. 🔥✨Deiwaka World Bongo Flava Honors – Season 4 is here! 🇹🇿🎶A night to celebrate the culture, t...
08/04/2026

"Big vibes. Bigger energy. 🔥✨

Deiwaka World Bongo Flava Honors – Season 4 is here! 🇹🇿🎶
A night to celebrate the culture, the sound, and the stars shaping Bongo Flava.

🎤 With Prof Jay
🎙 Hosted by Sugu
📅 May 01 | 8PM – 12AM

🎟 Grab your tickets now on the Tukiio App & website

".

PROF JAY ALIVYOWAPA UBATIZO WA LADHA WAPINGA RAPMAMSAP ni msamiati uliotumiwa na wanaume wa makamo na wazee, likimaanish...
04/04/2026

PROF JAY ALIVYOWAPA UBATIZO WA LADHA WAPINGA RAP

MAMSAP ni msamiati uliotumiwa na wanaume wa makamo na wazee, likimaanisha “mke”. Wimbo kuitwa “Mamsap”, iliwavuta hadi wenye mvi nyingi kusikiliza. That’s right, Jay aliwafuata wapinga Rap, akawaweka kwenye shabaha na kuwapa ubatizo wa ladha. Swahili Rap ikavunja dari ya kioo na kupaa kilometa milioni juu ya usawa wa bahari. Jay akaipeleka HBC to the next level.

Waasisi wa HBC ni Terry Msiagi (Fanani au Luna T), William Shundi (Big W***y au Crazy One), Ngida Raphael (KC1), Gabriel Kilunga (Tuff Jam), na Frank Korassa (Trigger F). Jay alijiunga na HBC baadaye, lakini akawa instrumental wa hits za crew hiyo, na albamu yao bora, Funga Kazi 2000, ambayo ni kazi ya mtu tatu; Jay, Fanani na Big W***y.

Mawe 10 yalikamilisha Funga Kazi 2000. “Funga Kazi” yenyewe, “Chemsha Bongo”, “Mamsap”, Jay alituhadithia kuwa yeye ni kichwa kidogo msuli mkubwa kwenye “Chuzi Limekubali”, kuna “Kubwa Kuliko”, “Eeh Mola”, “Fanani wa Uhakika”, “Pata Potea”, ung’eng’e mtupu katika “it’s Time 4 Action”, halafu tunaweza kubet kuwa verse bora kabisa ya Swahili Rap kupata kuandikwa ni ya Jay ndani ya “Nusu Peponi Nusu Kuzimu”.

Bongo Flava haikuwa liquid asset, lakini kuwapata HBC watatu kwenye show ilibidi ujipange. Jay alikuwa ofisa wa kampuni ya Mobitel, siku hizi Yas. Kituo chake cha kazi Tanga. HBC bila Jay ilikuwa sawa na The Wailers bila Bob Marley, walinena FA na Jay Moe, katika “Ingekuwa Vipi”. Ungetakiwa kulipa fee ya show, halafu ilikuwa lazima ukate tiketi ya ndege kwa ajili ya Jay, na uvizie weekend akiwa off. Jay aliset standards.

Ukuu wa Jay ni kipawa chake cha kusimulia kwa vina na mizani kwenye mdundo. Ana uwezo mkubwa wa kunyoosha topic, tajiri wa misamiati ya lugha fasaha na slang. Hakuna mada aliyoigusa akashindwa kuitendea haki. Anakupa details za kutosha, anakuburudisha kwa midondoko. Eneo hili ndilo linampa Jay turufu ya kutamkwa kuwa yeye ni bora wa muda wote. Jay is the Goat, no doubt!

Jay ni foundational lifter wa Bongo Flava, I told ya! Tunaiendea Mei Mosi, 2026, siku ya Bongo Flava Honors kumtunuku Jay heshima anayostahili. Ni 710 Garden, Kawe. Sugu the Jongwe ndiye curator.

Ndimi Luqman MALOTO

"CHEMSHA BONGO YA JAY ILILETA MAPINDUNDUZI YA UTAMADUNIN***A Jay, msongo ambaye maskani kwake ni Kimara, alibaini mapema...
01/04/2026

"CHEMSHA BONGO YA JAY ILILETA MAPINDUNDUZI YA UTAMADUNI

N***A Jay, msongo ambaye maskani kwake ni Kimara, alibaini mapema kuwa mwarobaini wa wapinga Swahili Rap ni maudhui ambayo wasingeweza kuyapinga. Kutoka Kimara mpaka Upanga, ndani ya familia kubwa ya Hard Blasterz Crew (HBC), The Scientist Prof Ludigo Bishota, alinyonga midundo, Jay akawa tonic kwenye albamu ya Funga Kazi 2000.

Ngoja kwanza, kabla ya kudurusu albamu, tuzungumze kuhusu Chemsha Bongo. Wimbo ni baraka kwa kila sikio. Ulikuwa chachandu kwa vipindi vyote vya redio. Uliongeza idadi ya wasikilizaji wa redio, ukakuza namba ya wafuasi wa Swahili Rap. Ukawapa wazimu vijana wengi, wakatamani kufanya muziki wawe k**a N***a Jay. Hili halibishiwi, Chemsha Bongo ilizalisha underground wengi wa Rap Afrika Mashariki.

Wazee wakaksi walinywea, wakatoa leseni kwa watoto wao waliorap. Wazazi wengine waliwauliza vijana, “wewe hufokifoki, hutaki kuwa k**a yule wa Chemsha Bongo?” Mabitozi kibao wakajiita “Jay Tunakuzimia”, na walifanikisha mitikasi ya pesa na kuchezea nyoyo za warembo waliompenda N***a Jay. Ilikuwa analogia. Anasikika redioni, picha yake haijulikani. Matapeli wali-take advantage.

Chemsha Bongo ilikuwa lead single ya Funga Kazi 2000, ingawa release namba moja ilikuwa “Chuzi Limekubali”. Halafu sasa, ikafuata “Mamsap”. Wahuni walilia mapenzi kwa unyenyekevu na uadilifu mkubwa. Jay alikamua beti mbili, romantic gangsta mwenzake, Terry Fanani, akaua moja ya kati. Mamsap ni kibali kwa gangstaz kunyenyekea na kulia mapenzi pindi nyoyo zinapok**atika.

Tazama akili ya Jay; watu wanasema Rap uhuni, yeye akatumia maarifa yake makubwa ya kusimulia, akatoa hadithi ya mwanampotevu kutoka familia ya kitajiri, aliyekataa shule, akaishi pepo ya mpito kwa sababu alikuwa na fedha. Ponda sana raha, hakusikia la mwadhini wala la mnadi sala. Mwisho, kijana anajuta na kutubu baada ya kufilisika. Je, nani angeweza kupingana na ujumbe huo wenye mafunzo? Chemsha Bongo ika-dominate.

Elewa tunaposema Jay ni foundational lifter wa Bongo Flava. Mei Mosi, 2026, 710 Garden, Kawe, Jay atasimikwa rasmi heshima ya Bongo Flava Honors. Madude ya Jay yatalia kwa live band. Sugu the Jongwe atakuwa mwenyeji.

Ndimi Luqman MALOTO".

"PROF JAY; THE FOUNDATIONAL LIFTER OF BONGO FLAVANyerereland ilikuwa tambarare utadhani uwanda wa chumvi wa Salar de Uyu...
29/03/2026

"PROF JAY; THE FOUNDATIONAL LIFTER OF BONGO FLAVA

Nyerereland ilikuwa tambarare utadhani uwanda wa chumvi wa Salar de Uyuni. Laini mithili ya jiwe la Talc. Mserereko k**a kutembea juu ya polished marble yenye povu la sabuni. Tanzania was beautiful, utamu wake ni saresare na Thaumatin.

Ukimwi ndiyo tu ulileta sokomoko, lakini raia walichagua kuishi nao. Ugonjwa hatari ulikuwa Malaria. Siyo sasa mabalaa ya magonjwa yasiyoambukiza, saratani, vifo vya ini na figo hadi kwa infants. Aisee, naimiss Bongoland ile, iliyokuwa na mguso halisi wa Kitanzania. Ukarimu, ushirikiano, mshik**ano, vilikuwa jadi. Mapenzi yalikuwa ya moyoni. Siyo sasa pesa ndiyo inaamua upendwe au utendwe.

Late Gen X na early Gen Y (Millennials), ndiyo makundi rika yaliyotengeneza vijana kwenye mzunguko. Ni kizazi cha mapinduzi ya sanaa na ajira. Wateule wachache walitambua mapema kuwa dunia inakwenda kasi, na sound mpya ya muziki ilihitajika kuhudumia kaumu.

Wape heshima yao. Ni business-minded cohort. Walikuwa mbele ya muda kung’amua kuwa sound mpya ingevutia halaiki, na hivyo ndivyo pesa hutegwa. Mchakato haukuwa rahisi. Kenge walijimiksi kwenye mishemishe za mamba. Kila kitongoji kikawa na underground rappers.

Jamii ikaacha kuwatafsiri wavuta bangi kwa moshi, kipimo kikawa Rap. Kila aliyerap, alitiwa hatiani kijamii kuwa mtumia mihadarati. Halafu sasa, vipaji vikachanganyika na vioja. Wenye vipaji wanarap, wa vioja wanatukana na kufokea watu. Haikuwa kazi rahisi kuifikisha Swahili Rap mainstream.

Stiff boycott ya wazazi. Hawakutaka watoto wao wafanye Rap. Waliorap walionekana broke dreamers. Hawakuwa na kitu, ila waliyaota maisha ya successful American rappers. Wapo waliotabiri wimbi la wagonjwa wa akili kupitia vuguvugu la Hip Hop Tanzania.

It takes a genius to make the impossible possible. Kijana mteule, aliyebarikiwa karama kubwa, jina lake Joseph Leonard Haule. Akitembea na monikers za Jay Hustle na N***a Jay. Kwa tungo moja tu, “Chemsha Bongo”, aliyeyusha kila neno lililotokana na fikra hasi kuhusu Swahili Rap.

Mei Mosi, 2026, Jay atatunukiwa hadhi ya Bongo Flava Honors, kutambua mchango wake wa thamani. Sugu the Jongwe will host. 710 Garden, Kawe, ndiyo spot.

Ndimi Luqman MALOTO".

MASKANI KIMARA watu kila siku Mamtoni, Jonas Kiwia wasalimie Washington, Ukiweza Pita Texas Mpe HI Chief SAM na mkumbush...
11/08/2025

MASKANI KIMARA watu kila siku Mamtoni,
Jonas Kiwia wasalimie Washington,
Ukiweza Pita Texas Mpe HI Chief SAM na mkumbushe uzushi wa BONGO DAR ES SALAAM💣💣💣🔥


Mungu ni mwema sana Jana Tar 16 July nimefanikiwa kupokea Tuzo yangu ya  kimataifa ya LIFETIME ACHIEVEMENT IN MUSIC (BON...
19/07/2025

Mungu ni mwema sana Jana Tar 16 July nimefanikiwa kupokea Tuzo yangu ya kimataifa ya LIFETIME ACHIEVEMENT IN MUSIC (BONGO FLAVA) kutoka HOLLYWOOD and African prestigious Awards (HAPAwards) katika ofisi za Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) jijini Dar as salaam.
Makabidhiano hayo yaliongozwa na mkurugenzi wa ukuzaji Sanaa wa BASATA Bwana Edward Buganga aliyenikabidhi kwa niaba ya katibu mtendaji wa BASATA Dkt Kedmon Mapana,
Shukrani za kipekee kwa waandaaji wa Tuzo hizi za HAPAwards, Mashabiki na wadau wangu wote kwa kunipa Heshima hii kubwa na ya kipekee sana kwangu, Pia naishukuru sana Serikali kupitia BASATA Kwa kuwezesha jambo hili kubwa kufanikiwa kwani Tuzo hii sio tu imeniheshimisha mimi tu peke yangu bali ni Heshima kubwa sana kwa tasnia nzima ya Muziki na Taifa languzima kwa Ujumla, Na imenipa nguvu zaidi ya kuendelea kufanya vema na kujipanga vizuri kwa mambo makubwa zaidi, ASANTENI SANA WOTE NA MUNGU AWABARIKI SANA🙏🙏🙏
STAND UP💪💪
🔥🔥🔥🔥

Tukiwa kwenye mwezi wa Figo duniani, K**a Mwenyekiti wa taasisi ya  inayotekeleza programu ya AFYA AWARENESS CORPORATE i...
03/03/2025

Tukiwa kwenye mwezi wa Figo duniani, K**a Mwenyekiti wa taasisi ya inayotekeleza programu ya AFYA AWARENESS CORPORATE itafayofanyika March 14, nimekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Masoko , Elimu ya afya kwa umma ni kipaumbele 2025/26
duniani.

Address

Morogoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Professor Jay posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to Professor Jay:

Share