Kwaya ya Yesu Kristo Mfalme-Nyasubi Kahama

Kwaya ya Yesu Kristo Mfalme-Nyasubi Kahama WAIMBAJI WA MUZIKI MTAKATIFU WA KIKATOLIKI KUTOKA PAROKIA YA MT. STEPHANO SHAHIDI-JIMBO LA KAHAMA

Tunawatakia Wakristo Wote Kipindi kizuri cha Kwaresma.
18/02/2026

Tunawatakia Wakristo Wote Kipindi kizuri cha Kwaresma.

11/02/2026
11/02/2026

Baasi buana Fr. J Msaiye akawa na haya Radio Waumini 88.3FM Beno Mkatoliki JUGO MEDIA Kwaya Katolikitza Vijana Jimbo Katoliki Moshi Radio Maria Tanzania Radio Mbiu

05/02/2026

Tunajivunia Kuwa nanyi Watumishi wa Mungu
Sifa na Utukufu ni kwake Mwenyezi Mungu๐Ÿ”ฅ๐Ÿ”ฅ

02/02/2026

TUSALI SALA YA ASUBUHI

+Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.

Ee Baba yetu Mungu mkuu,
Umenilinda usiku huu,
Nakushukuru kwa moyo,
Ee Baba, Mwana na Roho.
Nilinde tena siku hii,
Niache dhambi, nikutii.
Naomba sana Baba wee,
Baraka yako nipokee.
Bikira safi, ee Maria
Nisipotee nisimamie,
Mlinzi mkuu malaika wee.
Kwa Mungu wetu niombee
Nitake nitende mema tu,
Na mwisho nije kwako juu. Amina.

NIA NJEMA.
Kumheshimu Mungu wangu
Namtolea roho yangu,
Nifanye kazi nipumzike
Amri zake tu nishike.
Wazo, neno, tendo lote
Namtolea Mungu pote
Roho, mwili, chote changu,
Pendo na uzima wangu
Mungu wangu nitampenda,
Wala dhambi sitatenda.
Jina lako nasifia,
Utakalo hutimia.
Kwa utii navumilia
Teso na matata pia.
Nipe, Bwana, neema zako
Niongeze sifa zako. Amina.

โ€ขSALA YA MATOLEO.
Ee Yesu, kwa mikono ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sala, matendo, masumbuko na furaha zangu zote za leo. Ee Yesu, ufalme wako utufikie. Amina.

BABA YETU.
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe. Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani k**a mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku. Utusamehe makosa yetu, k**a tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina.

SALAMU MARIA.
Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu, mzao wa tumbo lako, amebarikiwa.
Maria mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

KANUNI YA IMANI.
Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi, Muumba wa mbingu na dunia; na kwa Yesu Kristo Mwanae pekee, Bwana wetu, aliyetungwa mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akazaliwa na Bikira Maria, akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato, akasulubiwa, akafa, akazikwa, akashukia kuzimu; siku ya tatu akafufuka kutoka wafu, akapaa mbinguni; ameketi kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi; kutoka huko atakuja kuwahukumu walio hai na wafu.
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu, Kanisa takatifu Katoliki, ushirika wa Watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili, na uzima wa milele. Amina.

AMRI ZA MUNGU.
1. Ndimi Bwana Mungu wako, usiabudu miungu wengine.
2. Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako.
3. Shika kitakatifu siku ya Mungu.
4. Waheshimu baba na mama; upate miaka mingi na heri duniani.
5. Usiue.
6. Usizini.
7. Usiibe.
8. Usiseme uongo.
9. Usitamani mwanamke asiye mke wako.
10. Usitamani mali ya mtu mwingine.

AMRI ZA KANISA.
1. Hudhuria Misa takatifu Dominika na Sikukuu zilizoamriwa.
2. Funga siku ya Jumatano ya Majivu; usile nyama siku ya Ijumaa Kuu.
3. Ungama dhambi zako walau mara moja kila mwaka.
4. Pokea Ekaristi Takatifu hasa wakati wa Pasaka.
5. Saidia Kanisa katoliki kwa zaka.
6. Shika sheria katoliki za ndoa.

1.MATENDO YA HURUMA KIMWILI NI:
-Kulisha wenye njaa
-Kuwanywesha wenye kiu
-Kuwavika walio uchi
-Kuwakaribisha wageni
-Kuwaponya wagonjwa
-Kuwatembelea wafungwa
-Kuzika wafu.

2.MATENDO YA HURUMA KIROHO:
-Kuwashauri walio mashakani
-Kuwafunza wajinga
-Kuwaonya wadhambi
-Kuwafariji waliojeruhiwa
-Kusamehe maovu
-Kuchukuliana kwa saburi na wale wanaotutendea maovu
-Kuwaombea walio hai na wafu

SALA YA IMANI.
Mungu wangu, nasadiki maneno yote linayosadiki na linayofundisha Kanisa Katoliki la Roma, kwani ndiwe uliyefumbulia hayo, wala hudanganyiki, na wala hudanganyi. Amina.

SALA YA MATUMAINI.
Mungu wangu, natumaini kwako nitapewa kwa njia ya Yesu Kristo, neema zako duniani na utukufu mbinguni, kwani ndiwe uliyeagana hayo nasi, nawe ni mwaminifu. Amina.

SALA YA MAPENDO.
Mungu wangu, nakupenda zaidi ya chochote; kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na jirani yangu k**a nafsi yangu, kwa ajili yako. Amina.

SALA YA KUTUBU.
Mungu wangu, nimetubu sana dhambi zangu, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukizwa na dhambi. Basi sitaki kukosa tena, nitafanya kitubio, naomba neema yako nipate kurudi. Amina.

SALA KWA MALAIKA MLINZI.
Malaika mlinzi wangu, unilinde katika hatari zote za roho na za mwili. Amina.

KUOMBEA NCHI YETU
(JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA)

Ee Mungu Mwenyezi wa milele, Baba wa mataifa yote na watu wote, utuangalie kwa huruma, sisi watu wako wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunaohesabika kati ya mataifa ya dunia. Kwa baraka yako utuwezeshe kuishi maisha mema k**a iwapasavyo wana wa Mungu.
Wote. Uibariki Nchi yetu.

Uwaangaze viongozi wetu. Sheria wanazotunga zilingane na sheria zako wewe uliyetuumba kwa nchi yako.

Wote. Uibariki Nchi yetu.

Uwajalie watu wote paji lako la imani ya kuwa wewe ulikuwepo, upo na utaendelea kuwepo. Utupe hekima ya kuishi kwa uaminifu katika amri zako.

Wote. Uibariki Nchi yetu.

Uwashe moto wa mapendo yako ya kimungu mioyoni mwetu. Mapendo hayo yatusaidie kushinda utengano, ushindani na chuki ya ukabila au ya dini.

Wote. Uibariki Nchi yetu.

Utuunganishe sisi wote kwa muungano wa kindugu, tupate kuwa moja ndani yako wewe, Baba wa wote na ndani ya mwanga wako.

Wote. Uibariki Nchi yetu.

Ulibariki taifa letu liweze kusitawi na kuishi kwa amani na mataifa mengine.

Wote. Uibariki Nchi yetu.

Uwaongoze viongozi wetu wote ili watimize wajibu na kazi zao sawasawa. Wawasaidie raia wote kujipatia hali njema hapo walipo.

Wote. Uibariki Nchi yetu.

Utujalie sisi sote tuweze kufikia ukomo uliotutayarishia, yaani kuwa raia katika ufalme wa mbinguni, unapoishi na kutawala daima na milele. Amina.

MALAIKA WA BWANA
โ€ขMalaika wa Bwana alimpasha habari Maria, Naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.

~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria mtakatifu Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

โ€ขNdimi mtumishi wa Bwana, Nitendewe ulivyonena.
~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria mtakatifu Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

โ€ขNeno wa Mungu akatwaa mwili, akakaa kwetu.
~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria mtakatifu Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

Utuombee Mzazi mtakatifu wa Mungu, tujaliwe ahadi za Kristo.

Tuombe:
Tunakuomba, ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya malaika kwamba Mwanao amejifanya mtu, kwa mateso na msalaba wake utufikishe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.

BIKIRA MARIA MALKIA WA AMANI. UTUOMBEE

Tunawatakia siku njema, Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu.AMINA


Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard!Denis Wambali, Nickostrates Thomas
29/01/2026

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard!

Denis Wambali, Nickostrates Thomas

25/01/2026

Kwaya KatolikitzaRadio Waumini 88.3FMJUGO MEDIABeno MkatolikiVijana Jimbo Katoliki Moshi

30/12/2025

๐— ๐—”๐—˜๐—ก๐—˜๐—ข ๐Ÿฑ ๐—ฌ๐—” ๐—›๐—œ๐—๐—” ๐—ฌ๐—” ๐—ž๐—œ๐—ž๐—”๐—ง๐—ข๐—Ÿ๐—œ๐—ž๐—œ ๐—ฌ๐—”๐—ก๐—”๐—ฌ๐—ข๐—ง๐—˜๐— ๐—•๐—˜๐—Ÿ๐—˜๐—ช๐—” ๐—ญ๐—”๐—œ๐——๐—œ ๐——๐—จ๐—ก๐—œ๐—”๐—ก๐—œ

๐Ÿญ. โ€‹๐Ÿ‡ฒ๐Ÿ‡ฝ GUADALUPE (MEXICO)
๐Ÿฎ. โ€‹๐Ÿ‡ป๐Ÿ‡ฆ MTAKATIFU PETRO (VATICAN)
๐Ÿฏ. โ€‹๐Ÿ‡ง๐Ÿ‡ท APARISIDA (BRAZIL)
๐Ÿฐ โ€‹๐Ÿ‡ฎ๐Ÿ‡น PADRE PIO (ITALIA)
๐Ÿฑ. โ€‹๐Ÿ‡ซ๐Ÿ‡ท LOURDES (UFARANSA)

โ€‹๐—จ๐—™๐—”๐—™๐—”๐—ก๐—จ๐—ญ๐—œ

๐Ÿญ. โ€‹๐Ÿ‡ฒ๐Ÿ‡ฝ ๐—š๐—จ๐—”๐——๐—”๐—Ÿ๐—จ๐—ฃ๐—˜ (๐— ๐—˜๐—ซ๐—œ๐—–๐—ข):
Hupokea wageni milioni 20โ€“25 kwa mwaka.

๐‘ผ๐’Ž๐’‚๐’‚๐’“๐’–๐’‡๐’–: Ni kituo cha kihistoria kilichojengwa baada ya Bikira Maria kumtokea Juan Diego mwaka 1531, ambapo vazi lake lenye picha ya muujiza limehifadhiwa bila kuchakaa kwa karne tano.

๐Ÿฎ. โ€‹๐Ÿ‡ป๐Ÿ‡ฆ ๐— ๐—ง๐—”๐—ž๐—”๐—ง๐—œ๐—™๐—จ ๐—ฃ๐—˜๐—ง๐—ฅ๐—ข (๐—ฉ๐—”๐—ง๐—œ๐—–๐—”๐—ก):
Hupokea wageni milioni 10โ€“18 kwa mwaka.

๐‘ผ๐’Ž๐’‚๐’‚๐’“๐’–๐’‡๐’–: Hiki ndicho moyo wa Kanisa Katoliki duniani, mahali ambapo Mtakatifu Petro alizikwa na makao makuu ya Baba Mtakatifu yanayounganisha mamilioni ya waumini.

๐Ÿฏ. โ€‹๐Ÿ‡ง๐Ÿ‡ท ๐—”๐—ฃ๐—”๐—ฅ๐—œ๐—ฆ๐—œ๐——๐—” (๐—•๐—ฅ๐—”๐—ญ๐—œ๐—Ÿ):
Hupokea wageni milioni 12โ€“13 kwa mwaka.

๐‘ผ๐’Ž๐’‚๐’‚๐’“๐’–๐’‡๐’–: Ni kanisa kubwa zaidi la Bikira Maria duniani lililojengwa kwa ajili ya sanamu ndogo ya bikira Maria iliyopatikana na wavuvi mtoni, ikigeuka kuwa alama ya umoja na imani kwa nchi ya Brazil.

๐Ÿฐ. โ€‹๐Ÿ‡ฎ๐Ÿ‡น ๐—ฃ๐—”๐——๐—ฅ๐—˜ ๐—ฃ๐—œ๐—ข (๐—œ๐—ง๐—”๐—Ÿ๐—œ๐—”):
Hupokea wageni milioni 6โ€“7 kwa mwaka.

๐‘ผ๐’Ž๐’‚๐’‚๐’“๐’–๐’‡๐’–: Mahali hapa huheshimiwa kwa ajili ya mwili wa Mtakatifu Padre Pio ambao haujaharibika, mtakatifu aliyekuwa na alama za mateso ya Kristo (stigmata) na karama ya uponyaji.
๐Ÿฑ. โ€‹๐Ÿ‡ซ๐Ÿ‡ท ๐—Ÿ๐—ข๐—จ๐—ฅ๐——๐—˜๐—ฆ (๐—จ๐—™๐—”๐—ฅ๐—”๐—ก๐—ฆ๐—”):
Hupokea wageni milioni 5โ€“6 kwa mwaka.

๐‘ผ๐’Ž๐’‚๐’‚๐’“๐’–๐’‡๐’–: Eneo hili ni maarufu kwa chemchemi ya maji ya muujiza yaliyotokea baada ya Bikira Maria kumtokea Mtakatifu Bernadette, likiwa kimbilio kuu la wagonjwa wanaotafuta uponyaji wa kiroho na kimwili.

Copy from

Address

Nyasubi
Kahama

Telephone

+255629209000

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kwaya ya Yesu Kristo Mfalme-Nyasubi Kahama posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category