02/02/2026
TUSALI SALA YA ASUBUHI
+Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.
Ee Baba yetu Mungu mkuu,
Umenilinda usiku huu,
Nakushukuru kwa moyo,
Ee Baba, Mwana na Roho.
Nilinde tena siku hii,
Niache dhambi, nikutii.
Naomba sana Baba wee,
Baraka yako nipokee.
Bikira safi, ee Maria
Nisipotee nisimamie,
Mlinzi mkuu malaika wee.
Kwa Mungu wetu niombee
Nitake nitende mema tu,
Na mwisho nije kwako juu. Amina.
NIA NJEMA.
Kumheshimu Mungu wangu
Namtolea roho yangu,
Nifanye kazi nipumzike
Amri zake tu nishike.
Wazo, neno, tendo lote
Namtolea Mungu pote
Roho, mwili, chote changu,
Pendo na uzima wangu
Mungu wangu nitampenda,
Wala dhambi sitatenda.
Jina lako nasifia,
Utakalo hutimia.
Kwa utii navumilia
Teso na matata pia.
Nipe, Bwana, neema zako
Niongeze sifa zako. Amina.
โขSALA YA MATOLEO.
Ee Yesu, kwa mikono ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sala, matendo, masumbuko na furaha zangu zote za leo. Ee Yesu, ufalme wako utufikie. Amina.
BABA YETU.
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe. Ufalme wako ufike. Utakalo lifanyike duniani k**a mbinguni.
Utupe leo mkate wetu wa kila siku. Utusamehe makosa yetu, k**a tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina.
SALAMU MARIA.
Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu, mzao wa tumbo lako, amebarikiwa.
Maria mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
KANUNI YA IMANI.
Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi, Muumba wa mbingu na dunia; na kwa Yesu Kristo Mwanae pekee, Bwana wetu, aliyetungwa mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, akazaliwa na Bikira Maria, akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato, akasulubiwa, akafa, akazikwa, akashukia kuzimu; siku ya tatu akafufuka kutoka wafu, akapaa mbinguni; ameketi kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi; kutoka huko atakuja kuwahukumu walio hai na wafu.
Nasadiki kwa Roho Mtakatifu, Kanisa takatifu Katoliki, ushirika wa Watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili, na uzima wa milele. Amina.
AMRI ZA MUNGU.
1. Ndimi Bwana Mungu wako, usiabudu miungu wengine.
2. Usilitaje bure jina la Bwana Mungu wako.
3. Shika kitakatifu siku ya Mungu.
4. Waheshimu baba na mama; upate miaka mingi na heri duniani.
5. Usiue.
6. Usizini.
7. Usiibe.
8. Usiseme uongo.
9. Usitamani mwanamke asiye mke wako.
10. Usitamani mali ya mtu mwingine.
AMRI ZA KANISA.
1. Hudhuria Misa takatifu Dominika na Sikukuu zilizoamriwa.
2. Funga siku ya Jumatano ya Majivu; usile nyama siku ya Ijumaa Kuu.
3. Ungama dhambi zako walau mara moja kila mwaka.
4. Pokea Ekaristi Takatifu hasa wakati wa Pasaka.
5. Saidia Kanisa katoliki kwa zaka.
6. Shika sheria katoliki za ndoa.
1.MATENDO YA HURUMA KIMWILI NI:
-Kulisha wenye njaa
-Kuwanywesha wenye kiu
-Kuwavika walio uchi
-Kuwakaribisha wageni
-Kuwaponya wagonjwa
-Kuwatembelea wafungwa
-Kuzika wafu.
2.MATENDO YA HURUMA KIROHO:
-Kuwashauri walio mashakani
-Kuwafunza wajinga
-Kuwaonya wadhambi
-Kuwafariji waliojeruhiwa
-Kusamehe maovu
-Kuchukuliana kwa saburi na wale wanaotutendea maovu
-Kuwaombea walio hai na wafu
SALA YA IMANI.
Mungu wangu, nasadiki maneno yote linayosadiki na linayofundisha Kanisa Katoliki la Roma, kwani ndiwe uliyefumbulia hayo, wala hudanganyiki, na wala hudanganyi. Amina.
SALA YA MATUMAINI.
Mungu wangu, natumaini kwako nitapewa kwa njia ya Yesu Kristo, neema zako duniani na utukufu mbinguni, kwani ndiwe uliyeagana hayo nasi, nawe ni mwaminifu. Amina.
SALA YA MAPENDO.
Mungu wangu, nakupenda zaidi ya chochote; kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na jirani yangu k**a nafsi yangu, kwa ajili yako. Amina.
SALA YA KUTUBU.
Mungu wangu, nimetubu sana dhambi zangu, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukizwa na dhambi. Basi sitaki kukosa tena, nitafanya kitubio, naomba neema yako nipate kurudi. Amina.
SALA KWA MALAIKA MLINZI.
Malaika mlinzi wangu, unilinde katika hatari zote za roho na za mwili. Amina.
KUOMBEA NCHI YETU
(JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA)
Ee Mungu Mwenyezi wa milele, Baba wa mataifa yote na watu wote, utuangalie kwa huruma, sisi watu wako wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tunaohesabika kati ya mataifa ya dunia. Kwa baraka yako utuwezeshe kuishi maisha mema k**a iwapasavyo wana wa Mungu.
Wote. Uibariki Nchi yetu.
Uwaangaze viongozi wetu. Sheria wanazotunga zilingane na sheria zako wewe uliyetuumba kwa nchi yako.
Wote. Uibariki Nchi yetu.
Uwajalie watu wote paji lako la imani ya kuwa wewe ulikuwepo, upo na utaendelea kuwepo. Utupe hekima ya kuishi kwa uaminifu katika amri zako.
Wote. Uibariki Nchi yetu.
Uwashe moto wa mapendo yako ya kimungu mioyoni mwetu. Mapendo hayo yatusaidie kushinda utengano, ushindani na chuki ya ukabila au ya dini.
Wote. Uibariki Nchi yetu.
Utuunganishe sisi wote kwa muungano wa kindugu, tupate kuwa moja ndani yako wewe, Baba wa wote na ndani ya mwanga wako.
Wote. Uibariki Nchi yetu.
Ulibariki taifa letu liweze kusitawi na kuishi kwa amani na mataifa mengine.
Wote. Uibariki Nchi yetu.
Uwaongoze viongozi wetu wote ili watimize wajibu na kazi zao sawasawa. Wawasaidie raia wote kujipatia hali njema hapo walipo.
Wote. Uibariki Nchi yetu.
Utujalie sisi sote tuweze kufikia ukomo uliotutayarishia, yaani kuwa raia katika ufalme wa mbinguni, unapoishi na kutawala daima na milele. Amina.
MALAIKA WA BWANA
โขMalaika wa Bwana alimpasha habari Maria, Naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria mtakatifu Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
โขNdimi mtumishi wa Bwana, Nitendewe ulivyonena.
~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria mtakatifu Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
โขNeno wa Mungu akatwaa mwili, akakaa kwetu.
~Salamu, Maria, umejaa neema; Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria mtakatifu Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu. Sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
Utuombee Mzazi mtakatifu wa Mungu, tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe:
Tunakuomba, ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya malaika kwamba Mwanao amejifanya mtu, kwa mateso na msalaba wake utufikishe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.
BIKIRA MARIA MALKIA WA AMANI. UTUOMBEE
Tunawatakia siku njema, Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu.AMINA