31/08/2022
STORY 04: KISA CHA MFALME NA WAKE ZAKE WANNE
Hapo zamani za kale palikuwapo na mfalme mwenye nguvu aliyeishi katika nchi tajiri sana. Mfalme huyu alikuwa na wake wanne. Kati ya wake zake wote, alimpenda na kumjali sana mke wake wa nne. Alimununulia vitu vya dhahabu, almasi na mavazi ya kifahari. Kiufupi mfalme alimpa mke huyu wa nne kila kitu alichotaka na kumfanyia chochote kile alichoweza kufanya.
Lakini pia alimpenda sana mke wake wa tatu. Mke huyu alikuwa mrembo sana, hivyo mfalme alimfurahia na kujivunia kujionesha nae pindi alipokuwa anatembelea nchi jirani. Atahivyo, mfalme aliamini mke huyu atakuja kumuacha na kumwendea mtu mwingine katika siku za usoni.
Vilevile, mfalme alimpenda mke wake wa pili. Mke huyu alikuwa mwelevu na mtu anaejali sana hivyo mfalme alimchukulia k**a mshauri na msiri wake. Pindi mfalme alipopata shida au ugumu wowote katika suala zima la maamuzi, aliweza kumshirikisha naye aliweza kumsaidia mfalme kuvuka mazito na mgumu alokuwa anapitia.
Na mke wa kwanza wa mfalme alikuwa mke mwaminifu sana na alikuwa mke pekee aliyekuwa na mchango mkubwa katika kutengeneza na kudumisha utajiri wa mfalme pamoja na ufalme wake. Mke huyu alimpenda sana mfalme lakini mfalme akuonesha kumpenda, kumuheshimu wala kumjali k**a alivyokuwa akfanya kwa wake wengine, hivyo badala yake alimpuuzia.
Siku moja, mfalme aliugua sana, akawa hoi taabani kiasi cha kukaribia kufa. Mfalme akayawazia sana maisha yake ya kifahari na kustahajabu kwa kusema “hivi sasa nina wake wanne wakinifariji, lakini pindi nitakapokufa nitakuwa pekee yangu”. Mfalme akahofia kuwa mpweke katika maisha yake baada ya kifo, hivyo akamuuliza mke wake wa nne kwa kusema “nilikupenda sana zaidi ya wote, nikakupamba kwa mavazi ya kifahari na nikaonesha kukujari sana wewe. Sasa, niko karibu kufa, je utafuatana nami katika maisha yangu baada ya kifo?” Hakuna namna, siwezi kwenda na wewe” alijibu mke wake wa nne na kisha akaenda zake bila kusema neno jingine. Mfalme akuwaza k**a mke aliemjali sana angeongea maneno k**a hayo, hivyo alihuzunika sana kwani majibu ya mke wake wa nne yaliukata moyo wake k**a vile kisu chenye ncha kali.
Mfalme akiwa kwenye huzuni nyingi baadae akamuuliza mke wake wa tatu kwa kusema “nilikupenda sana katika maisha yangu yote na sasa nina kufa, je utaenda nami na kuwa pamoja katika maisha yangu baada ya kifo?” “Hapana” mke wa tatu alijibu “maisha ni matamu sana na pindi ukifa nitaolewa na mtu mwingine”. Moyo wa mfalme ukazama na kuwa wa baridi sana.
Mfalme akamuuliza mke wake wa pili “Umekuwa ukinipenda, ukinishauri, ukinitia moyo na kuwa msaidizi kwangu, nami nimekuwa nikikugeukia kwa kukuomba msaada nawe umekuwa nami bega kwa bega wakati wote. Sasa ikitokea nimekufa utafuatana na kuwa pamoja nami katika maisha baada ya kifo?” mke wa pili akamjibu “Samahani sana mfalme wangu, wakati huu siwezi kukusaidia tena, lakini nitakachoweza kukifanya ni kuandaa kila kitu kwa ajili ya mazishi yako na mimi kuwepo mbele yako mpaka pale utakapozikwa” . jibu lake mke wa pili lilitoka k**a shaba ya umeme na hivyo kuharibu kabisa moyo wa mfalme.
Sasa, mfalme akabaki mkiwa na mnyonge kwani alikuwa amepoteza matumaini ya kumpata mweza katika maisha yake baada ya kifo. Hii ni kutokana na kukosa ushirikiano kutoka kwa wake zake aliowapenda na kuwajali sana. Mfalme akiwa amebaki mkiwa, mara sauti ikatoka na kusema “Nitaenda na kufuatana nawe mahali popote pale bila kujali ni wapi hata k**a ni katika maisha yako baada ya kifo.” Mfalme akaangalia huku na kule na kumbe ilikuwa sauti ya mke wake wa kwanza ambaye alimjali wa mwisho katika wake zake wote. Alikuwa hana mvuto na amekondeana k**a vile ana utapiamlo. Mfalme akiwa na huzuni zaidi alijisikia aibu na kusema “Nisamehe sana, ninajuta kwamba sikukujali. Nilipaswa kukujari sana pindi nilipokuwa na nafasi na nilitakiwa kukupa umakini na kipaumbele cha kwanza katika maisha yangu.”
Funzo la hadithi hii ni kwamba wote tuna wake wanne katika maisha yetu ya kila siku.
1. Mke wa nne anawakilisha mwili wetu. Tunaupenda na kuupamba kwa mapambo, vipodozi na mavazi mazuri. Tunatumia muda na jitihada nyingi kuufanya uonekane vizuri lakini hautaenda na sisi pindi tutakapo kufa bali utaenda zake bila kusema neno lolote k**a vile mke wa nne alivyofanya.
2. Mke wa tatu anasimama kwa niaba ya vitu tunavyovimiliki k**a vile mali, vyeo, wadhifa, umaarufu au utajiri. Vitu hivi havitafuatana nasi pale tutakapo kufa, bali vitagawanywa na kupewa watu wengine k**a vile mke wa tatu alivyosema kwamba atakwenda kuolewa na mtu mwingine.
3. Mke wa pili anawakilisha familia, ndugu, jamaa na marafiki. Tunawapenda, tunawaamini na kuwashilikisha matatizo yetu kwa ajili ya kutushauri, kutufariji na kutusaidia. Haijalishi ni kwa muda gani watakuwa pamoja nasi lakini kikomo cha kuwa pamoja nasi ni pale tu watakapotuzika. Wanaweza tu kwenda na sisi kwenye maziko yetu na kutuaga k**a vile tu mke wa pili alivyosema atakwenda kuanda mazishi ya mfalme na atakuwepo katika siku ya kumsindikiza na kumzika.
4. Na mke wa kwanza anasimama kwa niaba ya roho zetu. Mara nyingi tunapuuzia kujali roho zetu kwa kujifanya tuko bize na kutafuta maisha, utajiri, furaha na nguvu lakini roho ndiyo kitu pekee kitakachofuatana nasi kwenye maisha yetu baada ya kifo.
Hivyo tuijali miili yetu kwa kuifanya nadhifu na yenye afya. Tufurahie vitu tunavyovimiliki na faraja inayotokana na vitu hivyo. Tuthamini familia, ndugu, jamaa na marafiki kwa upendo na msaada wanaotoa. Lakini tusisahau kujali roho zetu kwa kujikabidhisha kwa Mungu kwa kufanya ibada, dua, toba na utu wema.
Asante
Usisahau kulike na kushare.