01/12/2024
LESONI LEO, DEC 1-NIMEWAPA KIELELEZO
Katika sehemu hii ya dunia, katika siku za YESU, watu walivaa makubazi na wengine walitembea bila viatu. Miguu ilipata vumbi na kuwa na uchafu, hivyo ilikuwa ni desturi ya mtumishi ama mtumwa kuosha miguu ya wale wanaokuja kwa ajili ya mlo. Lakini, hakuna mtumishi aliyekuwepo wakati YESU na wanafunzi wake wanakuja kwa ajili ya mlo, maana ilikuwa ni wakati wa usiku.
Kwa sababu hiyo π, YESU mwenyewe anainuka kutoka chakulani na kuosha miguu yao wote (Yohana 13:4-12). Lilikuwa ni tendo la ajabu, la kushangaza na ambalo halikutegemewa na wanafunzi kwamba YESU angelifanya π maana alikuwa ni Bwana na Mwalimu wao (ndivyo walivyomuita, na ndivyo ilivyo)-Hivyo kwa Mwalimu na Bwana kunyanyuka na kuanza kuosha wanafunzi wake miguu, tena miguu iliyojaa vumbi na uchafu mwingi (maana tumeona walikuwa walikuwa wakivaa makubazi na wengine walitembea peku), Kwa Bwana kufanya tendo ambalo lilipaswa kufanywa na mtumishi wa chini kabisa (mtumwa) ilikuwa ni ajabu.
Bila shaka, ndiyo maana Petro anakataa na kumwambia, "Bwana huwezi kuniosha mimi miguu" (Yohana 13:6).
Petro anakataa kwa sababu mbili. Moja, YESU ni Bwana na Mwalimu π anawezaje kufanya hivyo. Lakini mbili, huenda pia miguu ilikuwa ni michafu mno, sasa kuoshwa tena na Bwana si ni aibu hii βΊοΈ.
Lakini YESU anamwambia hivi, "asipofanya hivyo basi yeye hana shirika naye" (Yohana 13:7-8).
Nimalizie kwa kusema hivi π meza ya BWANA ina mafundisho mengi. Lakini katika somo la leo YESU alitaka kuwafundisha wanafunzi wake kile ambacho kiongozi anapaswa kufanya. Tazama Lesoni leo inasema, walimuita Bwana na Mwalimu (jina ama vyeo vinavyoelezea mamlaka ama uwezo), hivyo YESU alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake kwamba, "uwezo na mamlaka, vinapaswa vitumike kwa ajili ya huduma", si kwa ajili ya kujitukuza!!!
TAFAKARI NJEMA SANA...