24/09/2022
MUNGU ATENDAE YASIYOWEZEKANA.
TWENDE PAMOJA.
๐๐๐
Kutoka 14:10-16,18,21-22,24-25
[10]Hata Farao alipokaribia, wana wa Israeli wakainua macho yao, na tazama, Wamisri wanakuja nyuma yao; wakaogopa sana; wana wa Israeli wakamlilia BWANA.
[11]Wakamwambia Musa, Je! Kwa sababu hapakuwa na makaburi katika Misri umetutoa huko ili tufe jangwani? Mbona umetutendea haya, kututoa katika nchi ya Misri?
[12]Neno hili silo tulilokuambia huko Misri, tukisema, Tuache tuwatumikie Wamisri? Maana ni afadhali kuwatumikia Wamisri kuliko kufa jangwani.
SOMA HAPO JUU TENA NA KURUDIA RUDIA MARA KADHAA.... WAISRAEL WALOKUWA WATUMWA MISRI WAMEPATA NAFASI YA KUTOKA UTUMWANI, LAKINI PAMOJA NA KUTOKA WAMETEMBEA WAKAFIKA SEHEMU WAKAWEKA KAMBI NA KUSEMA WACHA TUMPUZIKE KIDOGO HAPA...MARA WANAONA WAMISRI WAKIJA JESHI KUBWA. WAKAANZA LAWAMA,
UNGETUACHA TUFIE MISRI,
BORA KUWA WATUMWA KULIKO KUFIA JANGWANI,
WAMESAHAU MAKUU ALOTENDA BWANA HADI WAKATOKA UTUMWANI.
Siku zote unapoamua kuachana na dhambi bado tuu shetani atakuja na vitisho mbele yako ili kukukatisha tamaaa,
Atakufanya ufukuzwe kazini,
Atakufanya ulale njaa,
Atakufanya uumwe.
LAKINI SIKIA RAFIKI USIOGOPE SONGA MBELE.
[13]Musa akawaambia watu, Msiogope, simameni tu, mkauone wokovu wa BWANA atakaowafanyia leo; kwa maana hao Wamisri mliowaona leo hamtawaona tena milele.
MUSA ANAWATIA MOYO WAISRAEL KATIKA MAMBO YASIWEZEKANA KWAO,
MSIOGOPE MAANA HILI JESHI HAMTALIONAAAA TENA,
HALELUUUYHAA๐๐
JESHI LINAKUJA NYUMA, MBELE KUNA BAHARI,PEMBENI NI MILIMA,
HAKUNA NJIA YA KUWAKIMBIA LAAAAKINI BWANA ANASEMA KUPITIA MUSA KWAMBA MISOGOPE.
SONGENIIII MBELE,
INAWEZEKANAJE KUSONGA KWENYE BAHARI ILIYO JAA MAJI TENA YENYE KINA KIREFU, TENA UPITE KATIKATI??
LAAAKINI BWANA AKIWA MBELE YAO UOGA WOTE UKATOWEKA.
LEO BWANA ANASEMA NAWE RAFIKI USIOGOPE
WEWE MAMA USIOGOPE,
WEWE KIJANA USIOGOPE,
HIVI VITISHO VYA MAISHA UNAVYOVIONA LEO VITATOWEKA VYOOOOOTE MAISHANI MWAKO MPKA USHANGAE.
WAISRAEL WANAMLILIA MUSA,
MUSA ANAMLILIA MUNGU,
HEBU TUONE MAJIBU YA MUNGU HAPA.
๐๐
[14]BWANA atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.
[15]BWANA akamwambia Musa, Mbona unanililia mimi? Waambie wana wa Israeli waendelee mbele.
[16]Nawe inua fimbo yako, ukanyoshe mkono wako juu ya bahari, na kuigawanya; nao wana wa Israeli watapita kati ya bahari katika nchi kavu.
[18]Na Wamisri watajua ya kuwa mimi ndimi BWANA, nitakapokwisha kujipatia utukufu kwa Farao, na magari yake, na farasi zake.
BWANA ANAMWAMBIA MUSA USINILILIE MIMI.
TENA BWANA HAMWAMBII MUSA WALILIE WAISRAEL,
HAPANA.
BWANA ANAMWAMBIA MUSA WAAAMBIE WAISRAEL WAENDELEE MBELE.
HAIJALISHI KUNA MAJI MBELE YAO LAKINI WAENDE MBELE,
MAJARIBU YANAPOKUJIA HAKUNA WA KUYAONDOA MBELE YAKO ISIPOKUWA NI WEWE PEKE YAKO NA MUNGU WAKO.
HAIJALISHI KUNA MAWINGU MBELE YAO LAKIN WAENDE MBELE,
HAIJALISHI KUNA DHORUBA MBELE YAO LAKINI WAENDE MBELE.
RAFIKI NI BAHARI IPI ILIYO MBELE YAKO.
JE HUPATI MCHUMBA MPAKA LEO NA UZEE UNAINGI,
JE BAHARI YAKO NI NDOA INATIKISWA,
JE BAHARI YAKO NI KAZI HAUNA,
JE BAHARI YAKO NI KAZI UMEFUKUZWA,
JE BAHARI YAKO NI SHULE ADA HAKUNA,
JE BAHARI YAKO NI MADENI YAMEKUSONGA,
JE BAHARI YAKO NI NINI RAFIKI.
WEWE WAJUA.
LEO BWANA ANASEM SONGA MBELE.
HATA LIKIWA KUBWA KWA KIWANGO GANI WEWE SONGA MBELE.
MIBARAKA ITAKUKUTA NJIANI RAFIKI SONGA MBELE.
MUNGU WA MAMBO YASIYOWEZEKANA ANASEMA SOOOOOONGAAA MBELE.
HALELUUUYAH.
NIMEAMUA KUSONGA MBELE,
IWE IWEJE NASONGA MBELE,
NIMEGUNDUA MBELE KUNA TUMAINI,
NIMEGUNDUA MBELE KUNA MEMA,
NIMEGUNDUA MBELE KUNA FURAHA,
NIMEGUNDUA MBELE AMIRI JESHI WA BWANA AMETANGULIA.
OOOH YESU NENDA PAMOJA NA WATU WAKO.
LEO BWANA AKUFANYIE WEPESI KWA JINA LA YESU.
AAAMEN
BARIKIWA UNAPOTAFAKARI
๐๐๐