STORY ZA SOA

STORY ZA SOA � �

The way life is… not every victory needs noise,some grow in silence… yet their impact is powerful 💭✨
11/04/2026

The way life is… not every victory needs noise,
some grow in silence… yet their impact is powerful 💭✨

08/04/2026

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Omar Morgan Ali, Gerrishon Mwiti, Silvester Rono, Jøsę Yen, Hezron Hezron, Abdala Mwinyiheli, Doreen Wamalwa, Bonistar Mweene, Amad Dialo, Selector Carlos, Jose Kijanaa, Mie Emour, Ni Abed, Kanduyi Tiwayi Be, Simon Pala
Thanks to follow me welcome 😊😊😊😊😊😊😊😊😊😊😊😊😊

30/03/2026
nikiwaza namimi nitaambiwa namna hii jamani👉 Mungu ailaze roho ya Marehemu  mahala pema peponi  nakumbuka kufanya mema n...
16/11/2025

nikiwaza namimi nitaambiwa namna hii jamani👉 Mungu ailaze roho ya Marehemu mahala pema peponi nakumbuka kufanya mema na kukubali msemo wa Dunia tunapita
Rest in peace MC PILIPILI 🙏🏿 😢😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭😭 imetugusa wengi na tumeamini kufa lazima kuishi ni bahati

HADITHI:KISASI CHA SABINA AUTHOR:SOA SEHEMU YA :59     INAENDELEA.........Basi usiku uliingia kwenye  jengo la Mama Vero...
12/11/2025

HADITHI:KISASI CHA SABINA
AUTHOR:SOA
SEHEMU YA :59
INAENDELEA.........Basi usiku uliingia kwenye jengo la Mama Vero Vero alipelekwa na best yake akiwa amelewa sana alimshikilia mpaka ukumbini
"Naa nini kimetokea tena?"
"Amelewa sana alikua kachukia tu"
"Vero"
"Niachieni "
Aliondoka akipepesuka na Mama yake alimfata tu ndani alipanda kitandani na kulala tu Mama Vero alimfunika shuka na kumshika Naa.
"Kwanini kalewa k**a mjinga"
"Nilimuona kalewa tu na niliona sio vizuri kumuacha pekeake pale lolote baya lingemtokea ndiomana nikamleta lakini sijui tatizo lake kwa sasa"
"Sawa "
Basi Naa aliondoka tu siku ilipita Asubuhi Sabina alianza kuandaa vitu vyake kazini na Mara alimuona Raj alishangaa tu na kuendelea na kazi zake alimfata
"Usinikwepe sijaja kuongea chochote nitakaa tu"
"Kwahiyo hapo umekaa na uongei "
"Nakaa sitaki uache wateja kwasababu yangu nakaa nikichoka natoka tu"
"Sawa kaaa tu"
Boss Raj alikaa na Sabina aliendelea na kazi zake aliwakaribisha wateja wengi na Raj alikaa tu akimtizama hakuna alichoweza kuongea mpka mda uliisha na kufunga biashara.
Basi Sabina alibeba mkoba wake kuanza kuondoka na Raj alimfata.
Wakati huo Rey alikuwa na Mama Sabina wakiongea.
"Umenijuaje kam Mama Sabina"
"Nakujua tu naweza kuongea na Sabina uanze nae ukurasa mpya kam kweli umebadilika"
"Kweli muulize rafiki yangu basi tumehama na nyumba zile tunaishi vyema kabisa"
"Naogopa kumkosea tena yeye ni mwema sana"
"Niamini "
"Nakuamini sitaki lolote baya kuna vingi nimejifunza kwa binti yako nataka ubadilike kweli astahili vile"
"Sawa nisaidie "
"Sawa kwaherini "
Aliondoka wakati Sabina alisimamisha bajaji nakupanda na Boss Raj alipanda pia Sabina aliposhuka nayeye alishuka.
"Kwanini unanifata"
"Siku tuliachan sikukusikiliza kabisa"
"Raj mimi sijui chochote unachoongea fanya k**a ni mfanyakazi wako ulienifukuza kazi tu sina mahusiano nawewe kabisa"
"Niambie ni hasira tu .......
Itaendelea like na comment yako ni faraja kwangu

05/11/2025

MUNGU IBARIKI TANZANIA 🇹🇿 MUNGU IBARIKI AFRIKA
🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿🙏🏿

HADITHI: A TEST OF LOVEAUTHOR: SOASEHEMU YA: 4Siku zilikuwa zinaenda, na kila moja ilikuwa k**a ukurasa mpya wa kitabu k...
28/10/2025

HADITHI: A TEST OF LOVE
AUTHOR: SOA
SEHEMU YA: 4

Siku zilikuwa zinaenda, na kila moja ilikuwa k**a ukurasa mpya wa kitabu kisichoandikwa. Neema aliendelea kujipa nguvu kuendesha mgahawa huku akijitahidi kuweka mbali hisia zake zinazomchanganya. Wakati huo, Amani alikuwa bado yule yule mwenye tabasamu la kudumu, mwenye huruma kwa kila mmoja, na mwenye upendo wa kimya kwa Neema.

Furaha, bila kujua kilichoendelea ndani ya mioyo ya marafiki wake wawili, aliendelea kuamini kuwa Amani alikuwa wake. Alimtambulisha kwa marafiki zake, wakapiga picha, wakaweka mitandaoni. Kwa wengi, walionekana k**a wanandoa wa baadaye. Lakini Amani hakuwa anaweka moyo wake huko, alikuwa akicheka kwa heshima, si kwa mapenzi.

Usiku mmoja, mvua ilinyesha kubwa. Neema alibaki mgahawani kusafisha, akiwa hana mwavuli. Amani alifika akiwa na mwavuli mkubwa, akatulia mlangoni kimya. “Nilihisi utakuwa bado hapa,” alisema kwa sauti ya upole. Neema alimtazama kwa macho ya shukrani isiyo na maneno.

Walitembea pamoja chini ya mvua, bila kusema mengi, lakini kila tone la mvua liliongeza ukaribu wao. Walipofika kwao, Neema alisimama kidogo kabla ya kuingia. “Kwa nini husemi chochote?” aliuliza ghafla. “Wewe huoneshi chochote… lakini unajali sana. Unanifanya nijisikie salama na pia kuchanganyikiwa.”

Amani alimwangalia kwa macho ya utulivu. “Neema, si kila upendo hupaza sauti. Mwingine unajengwa kwa vitendo vidogo, siku baada ya siku. Sitaki kukulazimisha. Nipo tu. Hadi moyo wako utakapokuwa tayari.”

Neema hakujibu. Aliingia ndani na kufunga mlango taratibu, akiegemea mlango kwa ndani, huku moyo wake ukipiga kwa nguvu. Hakujua k**a alikuwa na hofu, au furaha, au vyote kwa pamoja.

Na mvua iliendelea kunyesha… ikiosha uchungu wa zamani, ikimwagilia mbegu mpya za hisia zisizotajwa…

HADITHI: A TEST OF LOVEAUTHOR: SOASEHEMU YA: 3Neema alianza kugundua kuwa kila mahali alipogeuka, alikuta Amani. Asubuhi...
16/10/2025

HADITHI: A TEST OF LOVE
AUTHOR: SOA
SEHEMU YA: 3

Neema alianza kugundua kuwa kila mahali alipogeuka, alikuta Amani. Asubuhi anakuta ameshawasha taa ya mgahawa kabla hata hajafika. Mchana yuko sokoni akinunua mboga kwa niaba ya Bi Mariam. Jioni, anasikia sauti yake ikichekesha watoto wa jirani na kucheza nao rede. Neema alijaribu kujitenga, lakini kivuli cha Amani kilimfuata kimya kimya, si kwa lazima bali kwa tabasamu lake lisilochosha.

Wakati huo, Furaha alikuwa akimkaribia Amani kwa kasi ya ajabu. Alimwalika kunywa kahawa, wakatembea ufukweni mara kadhaa, na hata akamchukua kwao kwa chakula cha jioni. Amani alifurahia urafiki wao, lakini macho yake yalikuwa mbali yalikuwa kwa Neema. Alifahamu fika kuwa Furaha alikuwa anampenda, lakini moyo wake haukupiga kwa jina hilo.

Siku moja jioni, Neema alichelewa kufunga mgahawa. Amani, akiwa tayari amemaliza shughuli zake, alimsubiri bila kusema neno. Walipokuwa wakifunga, Neema alihisi ukimya uliojaa maswali. “Mbona unajifanya rafiki wa kila mtu? Hata wale wasiokuhitaji?” alimuuliza ghafla.

Amani alitabasamu. “Siwezi kulazimisha urafiki. Lakini moyo wa mtu ukiona huzuni, hauwezi kukaa kimya. Nilikutana na watu hapa, lakini huzuni yako ilivuta moyo wangu.”

Neema alitetemeka. Maneno yale yalimgusa k**a upepo baridi wa usiku. Alijua hajawahi kuambiwa maneno yenye upole k**a hayo. Lakini kabla hajajibu, Furaha aliwasili, akiwa na mkoba wa vyakula, tabasamu kubwa usoni. “Jamani! Mbona hamcheki leo?”

Hali ilibadilika. Neema akarudi kuwa mkimya. Amani akaweka uso wa kawaida. Na Furaha, bila kujua alichovuruga, aliendelea kucheka akiwatazama wote kwa upendo usio na masharti.

Katika giza la jioni, walitembea watatu kuelekea nyumbani, lakini mioyo yao mitatu ilikua na mwelekeo mitatu tofauti…

ITAENDELEA..

HADITHI: A TEST OF LOVEAUTHOR: SOASEHEMU: 2Songa nayoo...Siku moja, mvua ndogo ikinyesha Dar, gari dogo jeupe liliingia ...
15/10/2025

HADITHI: A TEST OF LOVE
AUTHOR: SOA
SEHEMU: 2

Songa nayoo...
Siku moja, mvua ndogo ikinyesha Dar, gari dogo jeupe liliingia kwa kasi mtaa wa Neema. Majirani walitazama kwa mshangao. Kutoka ndani, alishuka kijana mwenye tabasamu lisilokoma. Alikuwa na miwani meusi, saa ya gharama mkononi, na rangi ya chocolate iliyoambatana na ucheshi wa aina yake. Jina lake ni Amani.

Amani alikuwa ametoka Arusha, akija kuanza maisha mapya Dar es Salaam baada ya kupata kazi katika shirika la misaada ya kijamii. Jirani mpya huyo alikodisha nyumba karibu kabisa na familia ya kina Neema. Hakuwa mgeni wa kukaa kimya alianza haraka kujumuika, kusaidia pale mgahawani, na kuchekesha kila mtu. Bi Mariam alianza kumzoea, na hata Bibi Zubeda, kwa mara ya kwanza, alionekana kutabasamu mbele ya mtu mpya.

Neema, kwa upande wake, hakupendezwa na usumbufu wa Amani. Alimwona kuwa mzungumzaji kupita kiasi, mwenye tabia za kuingilia mambo ya watu, na mara nyingi alimpuuza. Lakini haikumpa Amani sababu ya kukata tamaa. Kila alipomwona Neema, aliongea kwa furaha, akifanya utani wa kiswahili uliochanganya ucheshi na busara. Neema alimwona k**a msumbufu, lakini Furaha alishaanza kumuona kuwa mtu maalum.

Katika mgahawa wa Bi Mariam, maisha yalionekana kubadilika. Wateja walikuwa wanaongezeka. Amani alikuwa anasaidia kupiga muziki, kuwahudumia wageni, na mara nyingine kucheka na watoto waliokuwa wakicheza pembeni. Mara kwa mara aliketi na Bibi Zubeda, wakibishana kuhusu siasa au chakula, na kutengeneza hali mpya ya upendo.

Lakini Neema alibaki na maswali. Huyu kijana ana furaha ya wapi? Mbona kila mtu amemkubali isipokuwa mimi? Na kwa nini moyo wangu unaanza kutetemeka kila anaponiangalia kwa macho yale ya upole?

Ndani ya moyo wake, pasipo kujua, mlango mdogo wa matumaini ulikuwa umefunguliwa...
ITAENDELEEA

HADITHI: A TEST OF LOVEAUTHOR: SOASEHEMU YA 1.Jijini Dar es Salaam, katika mitaa ya Kinondoni, anaishi binti aitwaye Nee...
15/10/2025

HADITHI: A TEST OF LOVE
AUTHOR: SOA
SEHEMU YA 1.

Jijini Dar es Salaam, katika mitaa ya Kinondoni, anaishi binti aitwaye Neema, msomi wa chuo na mwenye ndoto kubwa, lakini moyo wake umezama kwenye huzuni isiyoisha. Maisha ya familia yao si rahisi mama yake Bi Mariam anaendesha mgahawa mdogo uliorithiwa kutoka kwa marehemu mume wake. Bi Mariam ana mzigo mzito wa madeni na lawama kutoka kwa mama mkwe wake mzee Bibi Zubeda, ambaye hamwelewi kabisa.

Kila siku ni vita ya kuamka, kwenda chuoni, kusaidia nyumbani, na kuvumilia mgogoro wa kifamilia. Neema hana marafiki wengi zaidi ya Furaha, rafiki yake wa karibu, na Salim, kijana mwenye akili sana, mtaalamu wa IT, lakini mwenye mapenzi ya siri kwa Neema. Yeye hujituma kwa bidii, lakini mara nyingi huzama kwenye ndoto za mapenzi ya upande mmoja.

Katika jiji hili la kelele na pilika za maisha, Neema hupita siku zake akiamini kuwa hakuna nafasi ya furaha ya kweli kwake. Hata anapoandika kwenye daftari lake la siri, huandika: “Pengine furaha haikuumbwa kwa ajili yangu." Hajui kuwa maisha yake yanakaribia kubadilika kabisa… mtu mpya anakuja mtaani mwao – mtu atakayeingiza mwanga penye giza, lakini pia machozi penye tabasamu.

ITAENDELEA... Nifollow please 🙏.

HADITHI:KISASI CHA SABINA AUTHOR:SOARSEHEMU YA :58       SAMAHANI  KWA KUICHELEWESHA.........INAENDELEA.      Reyla alia...
03/10/2025

HADITHI:KISASI CHA SABINA
AUTHOR:SOAR
SEHEMU YA :58
SAMAHANI KWA KUICHELEWESHA.........INAENDELEA.
Reyla aliachwa pekeake hapo akujua afanye nini.usiku ulipita Asubuhi Sabina alikuwa kazini na Miss julliette alifika.
"Sabina binti yangu"
"tafadhali usiniite hivyo "
"kwanini?kwani wewe sie mwanangu kumbuka tulipotoka sasa kumbuka"
"sitaki kukumbuka Mama nimechoka kukumbushwa mambo mabaya niache na maisha yangu jamani "
"Sasa hivi mimi siwezi kuwa yule kabisa mimi nimebadilika"
"kipi mbona ni yule yule Miss Julliette alienifata mjini na kunidhalilisha .unajua sikuizi nikipita watu wananiita vipi"
"basi basi(akitokwa machozi) nilikosea na sitamani kuwa karibu yako lakini siwezi "
"natamani machozi yako yaseme ukweli "
"najutia vitendo vyote"
"natamani hiwe hivyo lakini uongo mtupu"
aliondoka na Madam Julliette alikaa hapo tu akimtizama vile akifanya kazi zake siku nzima .basi wakati ulipita Boss Raj alikua ofisini na Vero aliingia.
"Boss "
"nini"
"k**a ukinipa nafasi tena sitawai kukusaliti Raj "
"hakikisha unaelewa ninayokuambia leo"
Raj alimshika mkono wake Vero na kumuambia
"Nampenda yule msichana sijui kwanini lakini wewe kila nikijaribu kuwa nawe karibu sioni mapenzi kati yetu. Wewe ni binti mzuri na umejutia makosa naomba nisahau nione k**a Boss wako tu "
"Unamaanisha.. unitaki mimi?"
"ustahili kuambiwa hivyo lakini sitaki kukudanganya "
"Kwasababu yake najua najua tu lakini nitamuonyesha yule mjinga"
aliondoka kwa hasira Boss Raj alikaa kimya Basi Sabina akiwa anaendelea na kazi hapo alifika Reyla.
"Reyla"
"Sabina nimekuja kuomba msamaha kila kitu kilichotokea naomba nisamehe "
"ujanikosea wewe ni maisha yangu Reyla tangu nipo mdogo nilisemwa vile"
"lakini nilitakiwa nifikirie yale maneno kabla sijasema nimesababisha ukae mbali na Raj nisamehe"
"sawa lakini kumbuka kusamehe pia waliokukosea "
"wewe ni mtu mwema sana "
"Asante "
"ila kwanini Madam Julliette utaki kumsamehe ..... itaendelea like na comment yako ndio furaha yangu

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when STORY ZA SOA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share