Hadithi entertainment

Hadithi entertainment Ukurasa huu unahusu stori mbali mbali za maisha , mikaza ya kimapenzi, kisasi na mwisho kwa ujumla

buy the whole story, through m pesa , contact me with that number above,

price 1500/- TSH

wangapi mnakumbuka hii stori?je mnapenda kitabu kitoke?
20/05/2026

wangapi mnakumbuka hii stori?

je mnapenda kitabu kitoke?

Season two ije au
05/12/2024

Season two ije au

07/07/2024
SIKUTEGEMEA 01Dayo de AmosMaisha ni k**a mtihani usiokuwa na majibu ,Kuna wakati unaweza kudhani Duniani umebakia peke y...
14/04/2024

SIKUTEGEMEA 01
Dayo de Amos
Maisha ni k**a mtihani usiokuwa na majibu ,Kuna wakati unaweza kudhani Duniani umebakia peke yako, lakini sikuzote kwenye maisha urafiki ni zaidi ya ndugu wa damu, miaka hii wimbi la urafiki limekuwa tishio sana. Miaka iliyopita maisha yalikuwa marahisi kuliko sasa.
Miaka mitano iliyopita ilikuwa miaka mizuri sana Kwa bi dada Sheila maana alifanikiwa kupata kazi katika kampuni ya A-vision iliyokuwapo hapa nchini Tanzania. Na wakati huo alikuwa na miaka kumi na nane tu,
"Hongera sana dada yangu nimefurahi Kwa kuwa mwanamke wa kwanza kuwa na kazi nyenye mashahara mkubwa, aliongea rafiki yake Sheila aliyejulikana k**a Sakina.
"Hahaha Sakina bwana, ni juhudi k**a hutojali naweza kukutafutia kazi pale,,
"Hapana ,nitatafuta mwenyewe,,
"Sakina unajua ,tumekuwa pamoja Mimi nawewe tumekuwa pamoja Kwa mda mrefu sana, wewe SI rafiki tu Bali ni ndugu yangu kabsaa, ooh hafu nisindikize chuo cha NIT kwanza,,
"Ooh jamani ,unaenda Kufanya nini?,,
"Kuna mtu nataka nimuone kwanza,,
Basi safari ya kuelekea NIT ilitimia huku lengo la Sheila ni kumwona rafiki yake wa utotoni, ambaye Kwa maisha yake aliamua kujitolea kumsaidia, baada ya safari ya nusu saa hivi Walifika chuoni, Sheila akaenda Moja Kwa Moja kwenye idara ya uhariri. Baada ya kufika alimkuta kijana mmoja ambaye ,Sheila alimwangalia Kwa dakika moja bila kuongea....
"Hei dada ,vipi mbona unashangaa? K**a huna la kuongea ondoka hapa,,
Kitendo hicho Sheila hakukipenda sana hivyo akasema...
"Samahani kaka ,naitwa Mina nipo hapa kuonana na mkurungenzi wa chuo,,
"Ooh bi dada ,hukusoma hapo mlangoni?,, Nenda chumba namba Tano kulia utaona mlango,,
Sheila aliondoka huku akiwa Hana raha kabsa, mara baada ya kutoka akakutana USO Kwa USO na Sakina.
"Vipi mbona mnyonge hivo?"
"Hapana kitu, haya twende nyumbani kwangu,,
Safari ya kurudi nyumbani ikawadia mara hii Sheila hakuwa na furaha k**a mwanzo, baada ya kufika aliingia chumbani kwake, cha ajabu kila pembe ya chumba kulikuwa na picha ya mwanaume mtanashati.
"Wewe Sheila huyu ni nani tena?,,
"Ooh huyu ni mtu niliyeenda kumwona,,
"Nini kilitokea? ,mbona ulikuwa na hudhuni kiasi hicho? Na nilisikia hukumwambia jina lako Kwa nini?,,
"Ooh wewe ulijuaje ? Nilisikia jinsi mlivyokuwa mnaongea,,
"Ooh sawa , alionekana kunisahau kabsa hata hajui ni nani aliyemsaidia kufikia pale,,
"Ooh Sheila labda ungemwambia ukweli angekukumbuka,,
"Sitaki ajue Mimi ni nani k**a amesahau acha iwe hivyo tu,,
Mazungumzo yalikuwa k**a kwamba mwiba mzito ulikuwa ndani ya moyo wa Sheila, lakini Sakina yeye alionekana kuwa na hamu ya kumjua yule kaka. Baada ya hapo Sheila alimsindikiza Sakina kuelekea nyumbani kwao ,na Kisha naye akaelekea kazini kwake, alipofika kazini alimkuta msaidizi wake akiwa na barua mbili.
"Wewe Salma nini hicho,,
"Bosi niliambiwa Kuna barua hizi zinatakiwa kusainiwa ,,
"Sawa ,lete nizione ,hafu Kuna kitu nataka unifanyie ...
"Kitu gani tena ,bosi Sheila ?,,
"Hivi juzi tulijadiliana na mkurungenzi wa idara yetu Kuna nafasi ya kazi alitaka kuitafuta, k**a bado ipo uje unambie,,
Salma aliondoka kwenda kwenye ofsi ya mkurungenzi, wakati huo Sheila alikuwa akipitia barua hizo, mara baada ya kumaliza, Salma alirudi. Sheila alikuwa na hamu sana kujua k**a nafasi bado ipo. Kwa hiyo ilibidi kuumuuliza .
"Nambie bado ipo?, Sheila aliuliza.
"Ndio ipo ila Kuna barua mbili za maombi,,
Wakati hayo yakiendelea nyumbani Kwa Sakina naye alikuwa akijiuliza maswali mwengi sana hasa Kwa nini picha ya yule kijana ilikuwa mle?, Hakutaka kutulia hiyo alichukua tax kurudi chuoni, naye Moja Kwa Moja alienda kwenye chumba cha huyo dokta, mara hii hakumkuta isipokuwa alimkuta mfanya usafi.
"Dada samahani ,huyu bwana Yuko wapi?,, Sakina aliuliza.
"Samahani hatuna bwana hapa, kwanza wewe ni nani?,,
"Ooh samahani ,k**a akija mwambie rafiki yake Sheila alikuja hapa,,
Sakina aliondoka akiacha maagizo Kwa mfanya usafi wa ofsi .wakati huo sheila akiwa na Salma mara baada ya kugundua walituma nafasi ni wachache, ikabidi kumpigia Sakina rafiki yake.
"Haloo Sakina, uko wapi?,, Sheila aliuliza, swali Hilo lilimfanya Sakina kuwa na kigugumizi.
"Ni.....ni.....ni....nipo nyumbani hapa ,vipi kwani Kuna shida Sheila?,,
"Hapana nataka kukwambia kuwa zimebakia siku mbili kufanyika Kwa interview ya kumpata msaidizi wa kukusanya mapato, vipi upo tayari?,,
"Ooh jamani rafiki yangu ndio maana nakupenda, nawezaje kukosa kazi hiyo?, We niambie nini kinatakiwa?,,
"Nakutumia link Kwa whasap yako utaona nini kinatakiwa,,
Baada ya maongezi hayo simu ilikatika ,huku Salma akimuiliza bosi wake, "hivi unauhakika na huyu mtu, mbona anaonekana k**a mhuni mhuni tu"
"Ooh Salma Kwa nini unasema hivyo?,,
"Sheila hata namna anavyoongea tu ,anaongea k**a mtu aliyeridhika na maisha yake,,
"Salma huyu namfahamu vizuri mno, nimesoma naye ,tukaishi naye ,ni mtu mzuri sana, najua vyema anaweza kazi hiyo,,
"Sawa bosi, k**a upendavyo,,
"Sawa Salma niamini Yuko vizuri sana,,
Baada ya maongezi hayo, Salma aliondoka zake, wakati huo chuoni yule mhariri alikuja na alipoingia tu taarifa ikaja.
"Mkuu Kuna mtu alikuwa anakutafuta,,
"Nani huyo?...
"Anaitwa Sheila ...
"Nini Sheila yupi?"
"Mkuu sijui ila alijitambulisha Kwa jina la sheila,,
"Sawa hata simfahamu kabsaaa.,,
Yule Binti alitoka na kumwacha bwana huyo akitafakari Sheila ni nani ,na Kwa nini amtafute?,,
Tangu miaka kumi na nane hawajawahi kuonana na Sheila, wakati huo katika kampuni ya A-vision suala la kumpata msaidizi lilizidi kuwa na kasi ,mara hii Sheila alimpigia Sakina.
"Rafiki yangu ,kesho njoo kwenye interview,,
"Oooh waho! Sawa rafiki na kuna nini cha kuja nacho?,,
"Usijali nitakutumia kwenye whatsapp ,,
Simu ilikata, mara baada ya kukata ,salma akamuuliza tena bosi wake.
"Maadam sheila hivi, unauhakika na huyo mtu?,,
"Jamani, salma usijali bila shaka ukimuona utampenda yuko vema kabsa hana shida na mtu,,
"Sawa, lakini.......,,
"Lakini nini tena ,salma jamani?,,
"Shida sio kwamba sina imani naye sijawahi kumjua lakini ,mbona najisikia vibaya hivi?,,
"Hahahahhahaha,, sheila aliangua kicheko , jamani usihofu hakuna kitu kibaya kwake namwamini sana,,
Wakati hayo yakiendelea Sakina aligeuka kuangalia kwenye dressing yake ,kisha akachagua gauni moja matata, baada ya kulivaa simu ilianza kuita ,alichukua simu yake na kuipokea.
"Haloo, subiri natoka sasa hivi,, aliongea sakina. Kweli alifunga kabadi lake na kisha kuondoka kuelekea nje, alipofika alikuwa kuna gari moja mhimu lilikuwa limepaki.Aliingia kwenye lile gari kisha akaondoka haikujulikana wapi alielekea.
Wakati huo Sheila alimpigia baba yake ...
"Halooo baba ,
"Haloo mwanangu, unaelendeleaje huko?,,
"Baba sisi tuko wazima, sana,,
"Vipi mbona unaongea kinyonge hivyo?,,
" Baba ! Ulisema nikaonane na yule mtu, hanikumbuki kabsa, hata kujua mimi ni nani hakujisumbua kabsa,,
"Mwanangu ,sinauhakika k**a kweli unayoyasema, ulijitambulisha kwake?
"Aanh baba kiukweli hanitambui kabsa,,
"Sawa niachie mimi nitalifanyia kazi,,
Baba aliongea akiahidi mkumsaidia binti yake.
"Maadamu ,ulikuwa unaongea na nani?,,
"Salma usijali ni baba,,
"Maadamu wewe ni k**a dada kwangu siku ya leo hauko sawa ,shida nini?,,
"Salma hakuna shida pengine uchovu make mambo ya kushughulikia nayo ni mengi, ndio maana niko hivi,,
Sheila aliamua kutoka nje kupinga upepo huku akikumbuka njinsi alivyotolewa maneno na yule mhariri.
Akiwa pale simu iliita namba ilikuwa namba ya Sakina ,
"Sakina ,unasemaje kipenzi,,
"Uko wapi?, Nipo ofsini vipi kuna shida?,,
"Hapana ,ila nimeshindwa kukalili yale maswali ,nifanyie mpango wanipitishe free tu,,
"Sakina hiyo haiwezekani ,kumbuka kwamba mimi sio meneja wa hii kampuni, kwa hiyo nimekutumia maswali jiongeze na wewe,,
"Kuna kitu nakifatilia hapa, ndio maana nikakuomba,,
"Ok sawa nitajaribu,, Sheila alikubali hapo papo akainuka kuelekea kwa mkurugenzi wa kampuni. Bwana Albert
"Mkuu samahani ,aaaa nimeona nikueleze jambo mhimu sana, make nimejaribu kufanya utafiti juu ya hawa watahiniwa wetu, mmoja tu ndio naona mwenye vigezo,,
"Ooh sheila, unajua hatuwezi kufanya jambo kwa njia hii labda ni hakikishie unamwamini na anasifa zote tunazozihitaji?,,
"Bosi usijali k**a kuna changamoto juu ya utendaji kazi wake bila shaka nitakudhibitishia hujakosea kunchagua,,
"Sawa, lete jina lake,,
Sheila alimpatia form ya Sakina ,na kuondoka, alipotoka tu akakutana na Salma.
"Salma kuna nini?,,
"Hapana, nilitaka kujua uko sehemu gani?,,
"Oooh! Jamani usiwe na wasi wasi juu yangu, leo twende tukale cha kula jioni pamoja,,
"Sawa maadamu wangu"
Baada ya makubaliano hayo kila mtu alikuwa na furaha sana. Wakati huo sakina alikuwa zake maeneo ya resort akila bata.hakuwa na wasi wasi plani zake ni kumjua yule kaka na namna gani anahusiana na Sheila. Alikuwa akipiga picha namna ya kumvutia kijana yule, baada ya kufikilia kwa mda alipata jibu na aliamua kurudi nyumbani.
Ilipofika majira ya asubuhi sakina aliamka mapema alijiandaa kisha akaita tax na safari kuelekea A-vision iliwadia, baada ya kufika alimfuata Sheila ofsini kwake.
"Ooh sheila mambo vipi mwana?,,
"Sakina?, Umefika saa ngapi?,, Aliuliza sheila."
"Mda so mrefu, vipi hapa panaonekana full bata , pananifaa sana,, aliongea sakina.
Salma akatia neno."Ndugu samahani itabidi uende kule. Chini subiria tu huko tafadhali,,
Kitendo hicho hakukipenda sana bibie Sakina.
"Sheilaa hii ni nini?, Na huyu ni nani?,,
"Sakina, sikia nenda tu kule isije ikaharibu mpango wetu,, sheila aliongea. Hata hivyo sakina aliondoka kuelekea kwa watahiniwa wenzake. Baada ya mda wote waliitwa tayari kwa kufanyiwa interview, Baada ya interview Sakina alionekana kukosa furaha, Sheila alimfuata.
"Vipi tena mbona uko hivyo?,,
"Kwani wewe unataka niweje?, Mbona kila siku niko hivi?,, Alijibu sakina kwa dharau, hata sheila alilitambua hilo. Hata hivyo hakutaka kuendelea kumuuliza, aliondoka kuendelea na kazi zake baadae alikuja bwana Albert.
"Sheila mtu wako kajitahidi kwa kuwa uko hapa ni rahisi sana kwako kuangalia mwenendo wake,, aliongea bwana Albert.
"Hakuna shida boss ,najua utampenda,, alijibu sheila.
Baada ya maongezi hayo Bwana Albert aliitisha kikao cha dharula katika ukumbi wa kikao ,timu nzima ya A-vision ilifika,
"Nimewaiteni hapa kwa lengo moja tu ,hii weekend tutakuwa na tour tutaenda uturuki kwa ziara kwa hiyo kila mtu ajiandae na hili naliacha kwako Sheila,, aliongea boss Albert.
Baada ya kuongea hayo kila mtu alifurahi sana, wakiwa anapongezana alikuja Mariam msaidizi wa Albert.
"Sheila nataka kuongea na wewe, njoo ofsini kwangu,, baada ya kuongea hivyo aliondoka ,wakati huo John yeye alikuwa zake pembeni akiangalia mchezo kwa kuibia , baada ya kuona tukio la mariam alimfuata Sheila.
"Dada naitwa John ,bila shaka wewe ndo sheila?,,
"Ndio ,nambie,,
"Ooh ! Hongera sana ,sikuepo hapa kwa mda ,niko kitengo cha mawasiliano niko chini ya mariam,,
"Oooh sawa, nafurahi sana kukufahamu ,bila shaka tutakuwa timu,, aliongea sheila.
"Ndio bila shaka, kuwa makini,,
Baada ya maongezi hayo, sheila ilibidi kumfuata mariam, baada ya kufika.
"Sheila nimeandaa mipango yote ya safari ,kisha nimetoa order kwenye moja ya hotel iliyopo mji wa agharibi ,hii hoteli inagharama mzuri sana kwa siku wanatoza dola 1560$ tu,,
"Ooh sawa nimependa wazo lako lakini je boss atalikubali?,, Aliuliza Sheila.
"Kuhusu boss usijali ,mwambie ni mpango wangu atapenda mandhari ya hoteli hiyo wala usijali sawa?,,
"Sawa, k**a unavyotaka,,
"Nimefurahi kukujua natumai tutakuwa timu,, ( walishikana mikono kuonesha kuwa wamekubaliana).Baada ya hapo Sheila alirudi kwa marafiki zake, alipofika tu simu yake ikaita namba ilikuwa boss Albert, alipisha pembeni kuipokea, hakuchukua mda kisha akapanda kuelekea ofsini kwa boss.
"Mkuu nimekuja,, aliongea Sheila.
"Huyo mfanya kazi wako mwambie kesho aanze kazi mara moja, mpangie majukumu yake ipasavyo,,
Baada ya sheila kupokea maelekezo hayo alirudi kwa marafiki zake, salma alikuwa wa kwanza kutaka kujua alichoambiwa na boss.
"Maadam sheila nambie boss kasemaje?,,
"Salma usijali ni suala la kiofsi wala hakuna jambo geni kabsa,,
Wakati hayo yakiendelea ,sakina yeye alikuwa njiani kuelekea Chuoni kuonana na yule mhariri, baada ya kufika moja kwa moja alienda kwenye ofsi ya mhariri. Sakina alibisha hodi kisha sauti ikasikika
"Karibu, ingia,,
Sakina aliingia kwa macho ya soni.
"Mkuu habari,,... Sakina alisalimia
Yule mhariri hakuelewa shida ya yule mdada ambaye hakuwa kumuona hata siku moja.,kabla hajajibu msaidi wa mhariri akafika.
"Mkuu.....,ooh kuna mgeni kumbe,,
"Ooh hakuna shida sharifa, nambie kuna shida?,,
"Hapana ,ila ....ila.... Au malizana na mgeni wako kwanza,,
Sharifa aligeuka kuondoka kabla hajafunga mlango ,akasikia sauti ikimuuliza ...
"Sharifa huyu mdada unamfahamu?,,
Ndio bosi, ndo yule mdada aliyekuja siku za nyuma akikuulizia, anaitwa Sheila,, baada ya sherifa kujibu aliruhusiwa kuondoka.
"Kwa hiyo wewe ndo yule binti unayenitafuta?,,
"Aah! Ni.... Ni nikweli,,
"Sawa niko hapa sema sasa,,
"Aanh najiua umenisahau si rahisi kukumbusha kwa nini nimekuja kwako, tumetoka mbali sana labda je unanikumbuka?,,
"Aanh ndio ,nakumbuka lakini sheila siikumbuki sura yake, lakini huwa nasikia sheila kutoka kwa baba yangu ,tofauti na hapo siwezi kusema uongo simfahamu kabsa sheila alivyo,,
"Hahaha(sakina alicheka kidogo huku akinyanyuka kwenye kiti), nikweli kabsa lakini nambie nini kilitokea siku hiyo?"
"Siku gani? Na ilikuwaje?,, Mhariri alikuwa na hamu ya kujua
"Namba yangu hii hapa ( alitaja namba)"
Baada ya kutaja namba aliondoka kuelekea nyumbani, baada ya kufika alimkuta sheila akimsubiria.
"Ulikuwa wapi?, Nimekusubiria ,mbaya hupokei simu,, aliongea Sheila.
"Ooh samahani ,sikuiona missed call yako, hata hivyo usijali niko hapa sasa, nambie .......,

30/03/2024

Kuanzia tarehe 15th
SIKUTEGEMEA itaanza kuruka kila siku ya jtatu hadi jmosi hapa Hadithi za dayo entertainment.HD na Hadithi entertainment

SEHEMU YA TATUBaada ya mama Doto kutishiwa kuk**atwa alifanya uamuzi wa kumkataa Asheri, wakati huo Asheri hakujua,Wakat...
25/12/2023

SEHEMU YA TATU

Baada ya mama Doto kutishiwa kuk**atwa alifanya uamuzi wa kumkataa Asheri, wakati huo Asheri hakujua,
Wakati huo M***a na Sarah wakiwa wanarudi nyumbani,mambo yalikuwa hivi...
"Sarah hivi tulichofanya ni sahihi?,,
"Nafikiri ni sahihi , Asheri anatakiwa kurudi shuleni na sikufanya kazi za watu,,
"Sawa lakini ni k**a tumeharibu jambo,,
"Kivipi tumeharibu,
"Ooh kumbuka hana karo,,
"Oooh duh,any way wacha tutaona,,
Wakati huo Ayubu alikuwa anasikiliza maongezi ya mama yake pamoja na Habiba, hivyo akagundua kuna jambo linaendelea kati yao kuhusu Asheri na familia yake. Kesho yake ilipofika asubuhi na mapema alipokutana na wenzake ....
"Mnajua nini nahisi mama anahusiana na mambo ya Asheri,,
"Wewe umejuwaje, na kwanini afanye hivyo?,,
"Niliwasikia jana wakiwa wanajadili na mpangaji japo sikuwa na uhakika sana,,
"Mmh huo utani, aliongea M***a,,
Wakati huo Asheri alikuwa akielekea kazini kwake, baada ya kufika tu ...
"Binti sikutaki hapa ondoka,, aliongea mama Doto.
"Mama kwani kunaubaya nimefanya? ,,
"Wewe ni mwanafunzi si ndio?,,
"Hata k**a mbona ghafla hivyo ,,
"Sitaki kujua we ondoka ,,
"Vipi kuhusu mshahara?,,
"Mmh hata mwezi haujaisha unadai malipo, hayo hayapo kabisa we ondoka tu,,
"Mama ! Huna hata huruma nimefanya kazi mda wote huo ,mbaya unanifukuza bila hata taarifa huoni ni kinyume na haki za watu?,,
Kabla ya mama Doto kujibu ,alikuja mama mmoja ambaye alikuwa na gari ,alishusha kioo kisha akaanza kuita...
"Wewe binti aliyevaa gauni la njano, samahani njoo,,
Asheri aligeuka ,alipogeuka akakutana na gari aina ya range lover nyeusi, na sura ya mama wa makamo ikiwa imechungulia huku ikimuita. Asheri hakusita alimfuata ...
"Shikamoo,,
"Marahaba binti , kwanini unazonana shida nini?,,
"Mama ,nashindwa hata kuelezea ,huyu mama aliniajili kufanya kazi ,nimefanya kazi wiki tatu ,na leo nimerudi anasema nimefukuzwa kazi, nimemwambia anilipe hela yangu amekataa,,
"Asheri hakujizua kushusha machozi, kiasi cha kutia huruma,
"Basi sawa nyamaza binti ,ila k**a hutojali naweza kupafahu kwenu?, Ingia kwenye gari nikupeleke,,
Kweli Asheri aliingia na kisha gari likaanza mbio kuelekea nyumbani kwa akina Asheri...
"Karibu hapa ndio nyumbani ,,
"Ooh sawa ,hata hivyo sikujua nyumbani kwenu, unaitwa nani vile?,,
"Naitwa Asheri Baraka,,
"Ooh kumbe ndio wewe unayesoma na mpwa wangu Angel?,,
"Ndio ni mimi ,,
"Mara nyingi huwa asema unafanya vizuri sana darasani ,mbona leo hujaenda shuleni?,,
"Aah ni kawaida, sikwenda kwa sababu nili.....,,
Mama yake akamkatiza...
"Aanh hakwenda kwa sababu nilimuomba anisaidie
"Ooh sawa lakini mbona simuoni baba yuko wapi? , Aliuliza yule mama ambaye alijulikana k**a shangazi yake Angel,,
"Aanh baba alii....alik.... Alikuwa shambani,, aliongea Asheri akiwa na kigugumizi.
Mwisho Asheri aliingia ndani kuandaa chakula kwa ajili ya mgeni.... Huku nje nako maongezi yalikuwa k**a ifuatavyo...
" Bi Hawa, nilitoka kwenye maisha yenu kwa nini unafuata binti yangu?,, Aliongea mama yake Asheri.
"Mmh! Nikukumbushe tu biti yake kaka ndio huyu ,usinifanye mjinga mtoto anateseka sababu ya ubishi wako, angalia k**a usingechepuka na huyo muuaji wala usingekuwa na maisha k**a haya,,
"Hivi wewe, ulitaka ninyenyekee mali?, Najua shida zangu zinakuhusu nini? Isitoshe niliamua kuacha kila kitu sikuomba chochote k**a malipo kutoka kwa kaka yako,,
"Najua kwa sababu ulikuwa umepumbazwa na huyo mjinga, angalia binti wa kaka yangu anaingia ugomvi na ndugu zake, amefukuzwa shule sababu huwezi kumlea ,wacha nitamchukua mimi sasa,,
"Huwezi kumchukua mwanangu,,
"Wacha tuone k**a kweli siwezi, aliongea bi hawa.
"Unataka nini ? Na kwa nini unanitenganisha na mwanangu nitapiga simu polisi,, aliongea mama Asheri akiwa na jaziba.
"Haha nisikilize ,jaribu uonea , unataka binti ,yako ajue kuwa aliyeko jela si baba yake halisi?,,
Wakati hayo yakiendelea shuleni Angle na rafiki yake Loksini ....
"Sauti ikasikika.... siwezi ogopa tena nitaongoza darasa hadi mwisho,, aliongea Angle.
"Nakujua malkia wewe ni the best all over our School,,
"Haya twende tukawaone hawa mbweha,, aliongea Angle malkia ,, safari ilianza kuwatafuta marafiki wa Asheri mwisho waliwapata.
"Ooh! Naona watu wamekuwa wakiwa ghafla si mfurahie ?,, Aliongea Angle.
"Sote tunajua inatambua kabsa Asheri angekuepo nafsi ya pili ingekuhusu ,wewe mtu wa kupoteza hahahhaa,, aliongea Musa huku akicheka...
Kitendo hicho kilimkera sana Angle...kabla hajasema sarah akanena jambo...
"Angle! huu ni wakati wako sasa nilifikiri unaweza ukasaidia japo hata kidogo angalau Asheri arudi , ila ahsante kwa kuwa hii ndo nafasi yako,,
Baada ya sara kusema hayo aliondoka na kundi lake.
"Usiniambie kuwa unataka kusaidia Asheri arudi hapa tena,, aliongea Loksini..
"Sio hivyo wakati mwingine kuchukua nafasi ya mtu kwa njia hii sio vizuri kabisa,,
Wakati hayo yakiendelea kwenye mgahawa wa mama Doto wateja walianza kupungua siku hadi siku, kitu ambacho hata yeye hakuweza kuamini kitu hicho kutokea." Huyu mtoto atakuwa mchawi mbona wateja wameisha ghafla tu alipoondoka?"" Alijisemea moyoni.
Hata hivyo hakuwa na jibu zaidi ya kuwaza kuwa Asheri amefanya manyanga kwenye biashara yake. Wakati huo Asheri yeye ndio alikuwa anatenga chakula mbele ya mgeni wake, siku hiyo alipika ugali wa mhogo na nyama ya bata... Baada ya kumaliza kula bi hawa alishukuru kwa ukarimu wa binti Asheri.
"Asheri wewe ni sawa na wapwa wangu, Angle na wenzake ,tabia mnafanana sana,, aliongea bi hawa.
"Hapana mama, mimi na angle tuko tofauti sana, maana yeye hanipendi k**a mimi ninavyompenda,, aliongea Asheri akiwa na hudhuni.
"Aanh mwanangu , usijali labda Angle hakujii vizuri, nani anajua pengine mbeleni mkawa ndugu,,
"Ndugu? Mmh Angle hawezi kuwa ndugu kwa tabia ile ,ila tuombe iwe hivyo,, aliongea Asheri.
"Sasa Asheri nambie si unataka kurudi shule?,,
"Ndio nataka kurudi lakini...... Inaonekana juhudi zangu zimeishia hapa, k**a unavyoona mama hana uwezo wa kulipia karo tena,, aliongea Asheri akiwa na huzuni machoni mama akadakia..
"Usijali bi hawa... Nitamtunza asheri maisha sio kusoma tu,,
"Mama? Hivi.....,, Kabla hajasema kitu bi hawa akadakia.
"Asheri nipo tayari kukusaidia ,nitalipia ada zote we nambie tu lini unataka kurudi shuleni?,,
"Kesho.. kesho nitakuwa tayari,,
"Ooh waoh ndo maana ninakupenda, unajari sana elimu yako sio k**a huyu,, aliongea bi hawa.
"Huyu nani?, Mama au?,,
"Hapana sio mama kuna kijana wa kaka yangu amekataa kusoma anaendesha magari ya mizigo ya baba yake,, alijibu bi hawa.
"Aanhaa sawa, ahsante sana mama ,ipo siku nitakulipa ,, aliongea Asheri akiwa analia machozi ya furaha,,
"Asheri nisikilize hata mama yako nitamsaidia ,nitamtafutia nafasi kwenye kampuni yetu,, bi hawa aliendelea kutoa ahadi mbele ya asheri na kumfanya amwamini kwa asilimia zote, hata ungekuwa wewe mpenzi msomaji kwa dhiki aliyokuwa nayo Asheri usingekataa, kwa hiyo Asheri aliona k**a Masihi amesikia kilio chake.
Huku shuleni sarah,musa na Ayubu walimfuata mwalimu mkuu.
"Mwalimu tumekuja kwako tunaombi moja tu,, aliongea sarah kwa niaba ya wengine.
"Ombi gani hilo tena sarah?,alihoji mwalimu mkuu.
"Mwalimu maisha ya mwenzetu yanaharibika ,Asheri alikuwa mwanafunzi bora tangu tukiwa form one, leo tupo form three bado anafanya vizuri pamoja na kwamba anamatatizo anayopitia lakini bado anafanya vizuri, kwa hiyo tuko hapa kuomba kibali kwako kupitisha mchango kwa wanafunzi wote angalu tuokoe ndoto za binti huyo,, aliongea sarah.
"Sarah, nisikilize sina uhakika k**a jambo hili ni jema labda k**a bordi ya shule itakubali kwenye kikao cha kesho,,
"Mwalimu chukua uhusika wa Asheri hafu nambie ungefanya nini?, (Sarah alipa magoti kwenye miguu ya mwalimu) mwalimu tafadhali fanya jambo okoa ndoto za binti ambaye anapambana mitaani kusaka ada ,mwalimu tunaweza kusaidia kwa namna hiyo,,
"Sawa, binti nyanyuka sasa,( mwalimu akiwa na haya maana hakuwaza maisha ya binti huyo) sawa nenda kwa mkuu msaidizi mwambie bila kusahau mwalimu wa dhamu,,
Kweli safari ilimalizika kwa mkuu wa shule, sarah aliingia kwa msaidizi mwalim Tony.
"Sarah nini tena mbona unakuja kuvamia humu,,
"Mwalimu ,hatujavamia ila tu ,tumeagizwa na mkuu,,
"Mmeagizwa nini,?,,
"Utupe kibali kwa ajili ya kuomba mchango kwa ajili ya ada ya Asheri,,
"Sarah uko serious kweli basi sawa, mimi nitachangia Elfu ishirini,,
Wakatio maadamu stella akaingia (,mwalimu wa dhamu)
"K**a ni kuhusu Asheri nitatoa elfu ishirini pia,,
Kitendo hicho kimlifanya sarah kufurahi, basi baada ya kibali kutoka wakaenda sehemu kujadili namna ya kufikisha tangazo kwa wanafunzi wenzao.
"Nafikiri ,tufanye hivi tupite darasa hadi darasa hiyo itapunguza kelele za wapinzani wetu,, aliongea Ayubu. Kweli wazo lilikubaliwa na wote ,na kisha wakaanza na madarasa ya chini yaani form one.
"Ndugu wanafunzi wenzangu hamjombo?,(wote walikubali salamu ya sarah), wengi mnanijua naitwa sarah nasoma kidato cha tatu, nikombele zenu kuwashirikisha jambo furani, k**a mnavojua shule yetu imepokea tuzo takribani tatu kwa kutoa mwanfunzi bora kiwilaya na kimkoa, na tuzo hizo ndio zinazotupa sisi kujulikana kila pembe ya tanzania . Kivukoni ni shule inayojulikana na kila mtu wa mkoa huu, lakini ni mwanafunzi mmoja tu aliyetupa sifa hizo, nasikitika kusema amefukuzwa shule sababu ya ada , mimi k**a sarah sikupenda nikasema nitafanya ndoto za mwenzetu kuwa kamili, najua kila mwanfunzi ana ndoto ambazo anataka kuzitimiza akiwa hapa Kivukoni sekondari. Kwa hiyo nakuomba mwanfunzi mwenzangu uchangie kidogo kwa ajili ya Mwenzetu Asheri. Wasilisha mchango wako kwetu tunaptikana darasa la kidoto cha tatu ,kiasi chochote kinafaa,,
Baada ya tangazo hilo walipita kila darasa wak**aliza, wengi waliguswa mpaka na walimu pia walichangia,
Wakati huo Asheri akiwa na mama yake ,bi hawa alikuwa tayari ameshaondoka,,
"Mama hebu nambie , unamjua vipi huyu?,,
"Aanh sio kitu, wakati unapika aliniambia jina lake,, alijibu mama.
"Lakini mama kuna kitu nahisi k**a hakiko sawa,,
"Kitu gani hicho,,
"Sijui, ila nimefurahi angalau kuna mtu atanisomesha,,
"Mmh mwanangu, kuna mambo mengi unatakiwa kuyazingatia,,
"Mambo gani hayo mama?, Usiniambie unakataa msaada wa shangazi yake Angle,,
"Sina .maana hiyo ila kuwa makini usimwamini kila mtu haswa watu k**a hawa, hawachelewi kugeuza karata na kuwa fimbo ya kukuchapia,,
"Mmmh mama kwa shida tulizo nazo, itakuwa ujinga kukataa msaada tunaopewa, najua shangazi hawa hawezi kuniumiza,, asheri aliongea kwa imani kubwana sana,
Wakati mama alikuwa akiwaza k**a binti yake akijua ukweli kuhusu baba yake. Hivyo Asheri alijiandaa huku akiwa na furaha, mama yake alikuwa akimwangalia, ni kwa mda sasa hajawi kuona binti yake akiwa na furaha kiasi hicho.
Shuleni mkuu akiwa na staff yote walikuwa wakiajadili kitendo cha Sarah kujulikana na board ya shule.
"Walimu wenzangu mtoto mdogo ametuzidi ujanja na sasa bord ya shule inataka kumuona kumpongeza kwa juhudi hamuoni ni aibu hii?,,. Aliongea mkuu.
"Mkuu, mimi sizani k**a kunakosa hapo ,mtoto kafikiria tujivunie kwa kuwa maarifa tunayowapatia yanawasaidia kuthamini wenzao,, aliongea maadam stella
Hoja hiyo iliungwa mkono na kila mwalimu, lakini mkuu ilimfanya kuchukia kabsa.. baada ya kikao alimpigia baba yake Ayubu.
"Haloo ba Ayubu naona mpango wako unapingwa na wengi tumepoteza, aliongea mkuu.
"Mwalimu nilikwambia tangu siku ile ,hivi wewe umesahau nafasi uliyo nayo ni kwa sababu yangu?,,
"Siajasahau mkuu,,
"Kwa hiyo ndo malipo haya uliyoyaahidi?, Fanya kila njia sitaki Asheri arudi shuleni fanya kila njia,,
Simu ilikatwa ,na kumuacha mkuu akiwa hana namna, wakati bordi kuu ya shule kesho itakaa kwa dharura kuhusu suala la sarah.

SEHEMU YA PILIMwanangu usiseme hivyo, ipo siku Mungu atatufungulia njia ,sawa."Mama! Mama! Yote haya ni makosa yenu k**a...
20/12/2023

SEHEMU YA PILI
Mwanangu usiseme hivyo, ipo siku Mungu atatufungulia njia ,sawa.
"Mama! Mama! Yote haya ni makosa yenu k**a msingefanya uharifu hapo mwanzo , haya yote tusinge yapitia.
"Pumbavuuuuu , mama akawa makali. Hivi unajua unachokiongea? Mwanangu siku ukiwa mtu mzima utaelewa lakini mimi ndiye ninayejua ukweli, ukweli wenyewe ni huu. Mke wa anko yako ndiyo mpangaji wa yote haya kwa hiyo k**a kuna mtu wa kumlaumu basi ni mke wa mjomba wako, aliharibu maisha yetu kwa kunidanganya kipindi hicho sikuwa na uwezo wa kupata mimba ,ndipo akaniambia kwenda kwa mganga, unafikiri mimi nilipenda kuwa hivi?
Nenda Kalale naamini utaanza kujifunza namna ya kuamini watu bila kuwa na tathmini, ukiamka niulize habari nzima nitakusimulia.
Ilipofika kesho alfajiri na mapema Asheri aliamka k**a alivyokubaliana na mwajiri wake mama Doto kuwa anatakiwa kufika mapema kwa ajili ya kuandaa kifungua kinywa, hivyo ilipofika saa kumi na moja aliondoka alimuacha mama yake akiwa amelala. Akiwa njiani alikuwa akiomba Mungu amlinde baya lisimkute. Ni kweli alifanikiwa kufika salama na alikuta mfanyakazi mwenzake yule bubu akiwa asha anza kuandaa maandazi pamoja na chapati. Wakati huo mama yake aliamka huku akiwaza kuwa atamweleza je binti yake amueleweshaje kile kilichotokea miaka ishirini iliyopita,taratibu alisogea katika chumba chake na kuanza kuita.
"Asheri! Asheri amkaa kumekucha"
Baada ya kuita kwa mda aliamua kuingia ndani lakini hakumkuta ,mama yake Asheri hakuwa na namna zaidi ya kuomba Mungu aliko mwanaye awe salama.
Wakati huo mama yake Ayubu alikutana na dada yake Habiba ambaye alijifanya kukutana na mama yake Asheri.
"Dada mpango umetiki, ila Dah umegharimu ya mzee cha pombe,, aliongea Habiba.
"Ni sawa tu, ila kwa sasa ngoja tuone atafanya nini?, Naami ataniuzia mali zote kwa bei nafuu,
Aliongea mama yake ayubu, wakati huo mama yake Asheri aliamua kwenda kituo cha polisi kufuatilia kesi ya Mumewe. Baada ya kufika.
"Mama! Wewe unauhusiano gani na huyu mzee,,
"Huyu ni mme wangu,,
"Una habari anatuhumiwa kwa kosa la kuuwa,,
"Kwa kweli sina uhakika k**a alihusika na tukio hilo, mume wangu namjua vizuri,,
Kabla afande hajajibu ,sauti ikasikika ..."Ni bora afie jera mwanaharamu huu,, kila mtu aligeuka kutazama ni nani anayeongea maneno makali k**a yale, hakuwa mwingine bali alikuwa kaka yake na mama Asheri.
"Kaka! " Mama Asheri aliita....
"Dada nisikilize huyu mjinga muache yeye ndo sababu ya wewe kupitia magumu na mimi sitaacha mpaka afie huko jera,,
Mama yake Asheri alimtazama kaka yake na kisha akasema...
"Kaka ni jambo gani ambalo mme wangu amelifanyia?,,
"Dada kwa hujui? Nhee! Hujui baba na mama alikatisha maisha yao bila huruma kwa acha kumtetea kabsa yote haya ni kwa sababu yake, kipindi mlipokuwa na mali hukunijali kabsa,,
"Kwa hiyo unalipiza kisasi, basi ni sawa,,
Wakati huo Sarah na Ayubu pamoja na Musa mambo yalikuwa k**a ndo hayaeleweki kwao,
"Jamani tunafanya je sasa?,, Aliuliza Sarah .
"Ngoja nitaenda nyumbani kwako tukirudi nyumbani,, alijibu Ayubu.
"Vipi wewe mbona uko kimya unawazo gani ,aliuliza Sarah .. Musa akajibu, sina wazo lakini nahisi moyo kuumia sana, siamini k**a Asheri hayuko ,sijawahi hata kumweleza hisia zangu...
"Nini ? Ayubu na Sarah wote waliuliza kwa pamoja.
"Wewe jamaa ,binamu yangu ujue nilifikiri wewe ni rafiki kumbe mnafiki?,,
"Ayubu hebu tulia bwana ,kwani kunashinda gani?,,
"Sarah huoni huyu jamaa ana mhadaa binamu yangu,,
"Mmh sio kumhadaa ,ni yeye anavyojihisi si vibaya, basi yaishe hebu tufanye jambo ni vipi tutakusaidia?,,
Wote waliondoka kwenda darasani ,lakini Ayubu hakupendezwa na maneno ya M***a. Wakati huo Asheri yeye alikuwa Bize kuhudumia wateja, siku hiyo kulikuwa na wateja wengi kuliko siku zote, hadi majirani wakaanza kuona wivu.
"Asheri mwanangu leo sikutegemea k**a tungepata pesa nyingi kiasi hiki. Aliongea mama yake Doto.
" Mama samahani labda nisaidie hata huku ya nauli angalau niwahi kurudi nyumbani,,
"Umeanza kazi leo unadai nauli? Hiyo ni roho ya tamaa hujachangia chochote kwenye mgahawa huu,,
Asheri hakuwa na la kusema hivyo alitoka na kurudi nyumbani akiwa hoi kutokana na kusimama mda mrefu, alipofika hakumkuta mama yake kwani tangu aende mahakani aliendelea kusimamia kesi ya mumewe .
" Mama unanikumbuka?,, Aliuliza Habiba rafiki yake na mke wa kaka yake.
"Ooh binti yangu mme wangu kafungwa jera,, aliongea mama Asheri bila hata ya kuulizwa hukusu mama yake,,
"Ooh sawa ,sasa unampango gani?,,
'natafuta hela nimtolee dhamana, kaka yangu amefanya kitu kibaya kabsa,, aliongea mama Asheri
Habiba akauliza kana kwamba haelewi.
",Ooh kaka tena kaka yako nani? Kwa nini umesema kafanya vibaya?,,
"Kwa sababu anakinyongo naye, anadhani kwamba yeye ndiye muuaji wa baba na mama, wakati sote tunajua kabsa Mke wake ndiye mhusika mkuu ,,
"Pole sana mama ,nitakusaidia kwanza nioneshe kaka yako kwanza,,
"Ninashukuru sana mwanangu, kaka yangu yule kule mwenye shati la njano,, alionyesha kidole kumwonesha. Habiba alimfuata baba Ayubu na kisha kutoa faragha..
"Haya mpango wenu ukoje wa kumtoa mke wa dada yako,,
"Wewe binti kwanza wewe nani na kwa nini unafuatilia kesi isiyokuhusu?,,
"Samahani mimi ni wakili wa mrs baraka,,
"Sawa ila tu nakuonya, kaa mbali na hii kesi.
Kweli Habiba aliondoka na kwenda kumjulisha mama Asheri.
"Ndio kasemaje,, aliuliza mama Asheri,
"Kasema k**a utalipa milioni kumi atamsamehe,,
"Milioni kumi? Natoa wapi mimi masikini?,,
"Mama usijali labda unaweza kuuza vitu unavyomiliki k**a vile mashamba nyumba,,
"Sasa k**a nitauza na hali ngumu k**a hii duh,,
Wakati maongezi yakiendelea Asheri alifika ...
"Mama usiuze chochote tutaishi wapi najua mjomba k**a anania mbaya na familia yetu wacha afanikiwe na naamini Mungu atalipa,,
"Asheri huyu ni baba yako, unataka afie gerezani?,,
"Mama nielewe! Ukiuza tutakaa wapi?,,
"Kwa hiyo unataka baba yako aozee jera?,,
Kabla hajajibu ,Habiba akaingilia maongezi...
"Mdogo wangu, msikilize mama yako naamini mama yako yuko sahihi, hakuna namna au unataka baba yako aozee jera?,,
"Dada sikia haya ni mambo ya familia kwa nini unaingilia?, Kwanza wewe nani?,,
"Mwanangu Asheri acha ugomvi, punguzo hasira baba yako yuko ndani anahangaika ,najua hana hatia,,
"Mama tafadhali najua lakini, huwezi ukamtoa maana najua mchezo unaendelea!, Hebu twende nyumbani kwanza tutayajadili haya huko.,,
Kweli safari iliendelea na wakati huo baba yake Ayubu aliitwa na mkuu wa kituo cha polisi.
"Bwana najua hii sio nzuri nakuomba hebu achana nalo,,
"Mkuu nasema na bado najua mbeleni huyu binti yake atakuja kunilipizia kwa hiyo nitashughulikia kila kikwazo, nimekulipa pesa kwa hiyo fanya k**a tulivyokubaliana,,
"Sawa lakini tafadhali kuwa na huruma basi maana hawana kitu chochote na bado shida zinawandama,,
"Mkuu fanya kazi yako, mimi sijari kabsaa,,
Wakati huo Habiba alikutana na dada yake mke wa mjomba
"Haya nambie mambo yameendaje huko,, aliongea mama yake Ayubu.
"Dah ! Tumefeli tena ,ilibaki kidogo tu akubali lakini binti yake alikuja kutibua
"Dah! Huyu Asheri yeye ni nani hasa? Inawezekanaje kakuzidi ujanja?,,
"Dada alishtuka tu, ndio maana akamvuta mama yake nje,,
Wakati huo Ayubu aliingia na kukuta maongezi yanaendelea
"Mama nini kinaendelea?,
"Aah mwanangu ni huyu mama kaja anauliza nyumba za kupanga,,
"Aanhaa sawa,, Ayubu aliondoka huku akiwa na mashaka kile alichokisikia. Wakati huo mama na binti yake maongezi yanaendelea.
"Mama kwa nini unataka kuniumiza?, Hebu fikiria tukiuza hapa tutaishi wapi?,,
"Asheri mwanangu huwezi kumkatia tamaa baba yako,kwa nini unakuwa na roho mbaya hivyo?,,
"Ukweli ni kwamba nahisia mbaya kwenye hili, vipi ikiwa huyu mtu anafanya kazi na Mjomba,,
"Unataka kusema ,hayuko kwa ajili ya kutusaidia?"
"Sina maana hiyo, mama humjui, wala hatujui kwanini anaamua kutusaidia ghafla hivi?,,
Baada ya Asheri kuongea hivyo ndipo mama akarudi kwenye hakili yake.
"Sawa nimekuelewa binti yangu, maana hata mwenyewe sijui kwa nini alitaka kunisaidia mbaya pendekezo lake la kwanza ni kuuza mashamba, kuna kitu hakiko sawa,,
"Afadhali umenielewa ,wacha kwanza baba ateseke kwa mda naamini tutatoa,,
Wakati huo Musa alikuwa zake kijiweni akitafakari namna ya kumsaidia Asheri, wakati akifikiria Sarah akaja akiwa amevalia gauni ilimfanya aonekane mrembo zaidi...
"Hiki! Ni... Sarah ni wewe kweli?,,
"Musa unashida gani wewe?, Unamaana imenisahau? ,,
"Hapana! Sina maana hiyo isipokuwa umekuwa mrembo sana, enhe unaenda wapi?,,
"Naenda kumtafuta Asheri huku sokoni, nasikia anafanya kazi hotel ya mama Doto.,,
"Nini? Mama Doto huyu ninayemjua?,,
"Hapana nafikiri ,sio yeye, unaongea k**a kuna mama Doto mwingine anayeuza mgahawa, hebu twende,,
Safari ya kuelekea sokoni ikaiva maana kila mtu alitamani Asheri alirudi shule ,ila isipokuwa kundi la Angel na Loksini ambao hawakuwa kumpenda Asheri hata siku moja.
Baada ya kufika sokoni moja kwa moja hadi kwenye mgahawa wa mama Doto,
"Mama shikamoo,, mama doto aliitikia na kisha kuwauliza sababu ya wao kuwa pale.
"Mama naomba kuonana na Asheri Baraka mfanya kazi wako,,
"Mnashida gani naye?,,
"Sisi ni wanafunzi wenzake tuliambiwa anafanya kazi hapa,,
"Kwa hiyo k**a anafanya kazi hapa ,ninyi inawahusu nini?,,
"Mama k**a kuna chochote ,tunaomba mfute kazi yeye ni mwanafunzi, utak**atwa,,

Address

Dar Es Salaam Tz
Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Hadithi entertainment posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to Hadithi entertainment:

Share