18/03/2020
Mambo mengi sana yanazungumzwa kuhusu huu ugonjwa au maambukizo ya virusi vya corona, China na Marekani wanatuhumiana kuwa mwenzake kuvitengeneza virusi vya corona,
Ukweli uko wapi? Sisi hatutaki kujua nani katengeneza tunataka tiba na kinga km mlitegeneza harafu mkashindwa kutengeneza kinga au tiba hii inamaanisha aliyetengeneza hakujua km taifa lake litakuwa na janga hili sasa wanahaha kuinusuru dunia.
Kwa mawazo yangu finu na yasiyo timamu, ni kweli wamekosa tiba au wanataka tupungue duniani vile tumekuwa wengi?
Sitaki kuamini km kihama kimekaribia km baadhi ya watu wanavyosema japo mambo km haya yameandikwa na yalitabiliwa km magonjwa yasiyo na tiba, baba kuzaa na binti yake, mama kuolewa na kijana wake, mivurugano kati ya taifa na taifa kabila na kabila, jamaa na jamaa, ndugu kwa ndugu nk,
Lkn hii ni dalili tuu na hayana budi kutokea.
Bado mambo machache tuu yalisalia km vile mvua kubwa ya mawe mawe makubwa mfano wa talanta tetemeko kubwa ambalo halijawahi kutokea toka kuumbwa kwa misingi ya dunia hapo ndio visiwa vitahana kutoka shehemu moja kwenda nyingine,Milima na vilima navyo vitahana, na kabla ya hapo mambo mengi yatokea.