04/01/2024
Shirikisho la Soka barani Afrika (“CAF”) leo limetangaza ongezeko la 40% la Pesa kwa Bingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika la TotalEnergies (“AFCON”) Côte d'Ivoire 2023.
Bingwa wa AFCON Côte d'Ivoire 2023 atapokea USD 7 000 000 sawa na takriban Shilingi Billioni 17.
Mshindi wa Pili wa AFCON Côte d'Ivoire 2023 sasa atapata USD 4 000 000. Kila mmoja wa Washindi wawili wa Nusu Fainali atapata USD 2 500 000 na kila mmoja kati ya wanne waliofuzu Robo Fainali, USD 1,300,000.
Rais wa CAF Dk Patrice Motsepe alisema: “CAF imepata maendeleo makubwa katika kipindi cha miaka miwili iliyopita katika kuongeza Pesa za AFCON na mashindano yake mengine yote makubwa. Tumeongeza Pesa ya Tuzo ya Mshindi wa AFCON hadi USD 7 000 000 ambayo ni ongezeko la 40% kutoka Pesa ya awali ya Tuzo ya AFCON. Nina imani kuwa sehemu ya Pesa ya Tuzo itachangia katika kuendeleza soka na pia kuwanufaisha wadau wote wa soka, pamoja na kusaidia Vyama vyetu vya Wanachama katika tawala zao.”