30/03/2022
GLORIOUS MISSION - 03
Ndugu msomaji k**a hukusoma sehemu ya kwanza na ya pili bonyeza hapa
GLORIOUS MISSION - 01
https://web.facebook.com/simastories/photos/a.115692673481442/327083862342321/
GLORIOUS MISSION - 02
https://web.facebook.com/simastories/photos/a.115692673481442/334739901576717/
AU ENDELEA NA GLORIOUS MISSION - 03
ILIPOISHIA
Na ni kweli, yule askari akasema “naomba niingie dakika moja tu!” Akaruhusiwa kuingia, akaomba anikague kujiridhisha kiusalama. Basi akanikagua na hakukuta silaha wala kitu chochote chenye kuleta mashaka. Kisha akaangalia angalia pale ndani na hakuona dalili yoyote ya kuwepo kwa silaha. Mwisho macho yake yakatua kwenye maboksi mawili, moja lilikuwa na madawa na lingine lilikuwa na vifaa vya huduma ya kwanza na matibabu ya dharura. Akawaambia wale madaktari wafunue boksi moja la mbele ya lingine. Wakafunua, akachungulia kisha akatulia k**a sekunde ishirini hivi, kisha akatikisa kichwa na kusema “samahani sana kwa kuingilia kazi yenu, nilikuwa tu nahakikisha usalama wenu. Samahni sana kwa usumbufu pia ahsanteni kwa ushirikiano wenu na mko salama hivyo wawaisheni hawa watu hospitali” “aaaah haina shida usijali” akajibu Bamdogo Kasim huku akiondoa gari haraka kutoka langoni pale na kuitafuta barabara kuu kwa kasi kubwa sana. Baada ya dakika k**a tatu hivi tulipishana na ambulance halisi ikienda eneo la tukio. Hapa sasa alianza kuendesha gari k**a mwehu huku pikipiki niliyokuja nayo ikitufuata nyuma. Nilihisi kabisa ni mtu wetu pia japo hata sikujua Kasim alimpa funguo muda gani mtu huyo. Tukiwa tunakimbia kwa kasi ile, niliwaza sana, wamejuaje k**a nimetingwa? Ni nani huwa ananifuatilia kwenye misheni zangu wanazonipa? Tunaenda wapi mda huu? Inakuwaje polisi wakijua gari yetu ilikuwa ambulance feki? Bamdogo kaitoa wapi? Pastor Enock tunampeleka wapi? Je yuko upande wetu au ni adui yetu? Vipi yule dada niliyemuacha pale uwanjani hana fahamu yuko salama? Nitamuona vipi tena? Sikupata jibu hata moja, nikasubiri muda uamue.
……………………………………………………..
ENDELEA….
Tukiwa tumeshika barabara ya kwenda Mbeya mjini, bamdogo aliendesha gari kwa kasi kubwa huku akiwa amezima kelele na taa za kuwaka waka za ambulance ile. Yule mtu aliyetufuata kwa pikipiki naye hakuwa nyuma alikimbiza kiasi kwamba akatupita na kuwa mbele yetu, nadhani alijua mpango mzima wa tukio lile. Nikiwa naendelea kujiuliza nini kinafuata baada ya kuchomoka uwanjani, na kulikumbuka tukio lile zima lililokuwa k**a picha ya video, nilishuhudia ghafla yule mwenye pikipiki mbele yetu alikatiza kuingia kibarabara kidogo pale njia panda iendayo mlima Rungwe. Ni njia iliyokuwa na kimsitu cha kiasi mwanzoni kabla ya msitu uliomnene mbele yake. Tuliposogea mbele kidogo, yule mtu alisimama na kutuonesha ishara ya kusimama. Bamdogo Kasim alisimamisha gari na kushuka haraka kisha kutuambia nasi tushuke haraka. Tukashuka na zile siraha na kila kitu chetu. Wakati huo mchungaji Enock alikuwa tayari ameshakuwa wa baridi, miongoni mwa wale madaktari hakukuwa na mtaalamu hata mmoja, wote walikuwa ni wataalamu bandia hivyo hakuna msaada wowote alioupata, mchungaji akaaga dunia.
Tuliposhuka, pembeni nikaiona gari nyingine aina ya BMW X7 nyeusi, ambayo nadhani ilitusubiri. Tuliposhuka tu ikawashwa, kulikuwa na mtu ndani ya gari hiyo tayari. Tukapanda kisha ikaondolewa kurudi barabara kuu. Ile ambulance tuliiacha pale pale kichakani na mchungaji akiwa amepumzika ndani yake, alipumzika milele. K**a kawaida yule jamaa aliyeendesha pikipiki yangu alitangulia mbele kwa mwendo wa kasi sana. Sisi tulienda mwendo wa kawaida sana, wala dereva yule hakukimbiza sana. Baada ya dakika chache yule jamaa wa pikipiki akapotea kabisa kutokana na mwendo wake kuwa mkali. Kwenye gari hii sasa tulikuwa k**a watu saba, dereva mpya, bamdogo Kasim, wale watu wanne waliojifanya madaktari na mimi. Tukiwa viti vya nyuma ya gari, Kasim alianza kunihoji maswali kwa ghadhabu sana, “kwani unamfahamu yule binti uliyekuwa unamsaidia pale uwanjani? si ungeua wote wawili? Nakuuliza unamfahamu?” aliuliza kwa hasira. “Sasa hapa nijibu ndio au hapana!, wamejuaje yote haya?” nikawaza. Hapo sasa nikatambua hata hawakuwa mbali na nini, walikuwa karibu sana na mimi wakati wa tukio zima bila mimi kujua. Nadhani waliambiwa na mzee kwamba waje kunipa ‘backup’ k**a nitaelemewa.
Nikiwa natafakari haya na bado sijajibu swali, gari mbili za polisi zilitupita kwa kasi. Kila mtu alitulia ghafla na kusubiri nini kinajiri. Muda wote huo sikuwa na maamuzi yoyote katika yaliyofanyika nilikaa kimya kuangalia mipango ilivyopangika. Nikadhani labda kwa sababu wameshatupita na wamepotea basi dereva angebadiri mwelekeo au hata kuficha gari mahali kwa muda. Cha ajabu hata hakuwa na wasi wasi, ndo kwanza akanyanyua mkono wake wa kushoto na kunyoosha kidole cha kati kwenye kioo cha mbele cha gari yetu huku akicheka kwa dharau. Muda wote alivaa ‘earphones’ na kuimba kwa sauti wimbo mmoja uliojirudia mara kwa mara. Ulikuwa ni wimbo wa kimarekani na nadhani aliupenda sana. “I don care.. eeeh eeeh, I don care.. eeeh eeeh, I don care.. eeeh eeeh, life’s fu***ng tough, Ago make’t easy…wana drive.. wana drive to the hell… tomorrow is not there.. use this moment en make it funny” Haya ni baadhi ya maneno ya wimbo ule alioonekana kuupenda sana. Alionekana mtu mwenye uzoefu mkubwa sana wa kukimbiza magari, na hakuwa na hofu.
Baada ya mwendo kidogo, Bamdogo Kasim alipigiwa simu na yule jamaa aliyetangulia na pikipiki. Alimwambia hali ya barabarani, mita k**a mia tano kutoka tulipo sisi kuna askari wa barabarani wanafanya msako. Yeye jamaa wa pikipiki alipapita hapo na aliona moja ya zile gari za polisi imepaki pembeni. Nilianza kuogopa maana yule askari aliyenikagua kwenye ambulance kule uwanjani aliiona vizuri sura yangu na sidhani k**a atakuwa amenisahau. Nikawaza k**a atakuwepo miongoni mwa askari waliobaki na ile gari basi nitaweza kuk**atwa. Kasim akamwambia dereva asimamishe gari, wala hakusikia aliendelea kuimba wimbo wake ule kwa sauti. Staili yake ya Maisha ilinishangaza sana, nadhani aliiga huko kwenye filamu za kimarekani. Mara ya pili Kasim akavuta earphones na kumwambia mbele kuna ukaguzi wa gari zinazopita. Yule jamaa akamgeukia kwa jazba kisha akacheka kwa dharau kiasi kwamba sikuelewa ni mtu wa namna gani. “unaua vibe babu” ndo sentensi yake fupi aliyojibu huku akiendelea kuendesha gari. Ghafla akafunga break, akageuka nyuma akawapa ishara wale madaktari, nao wakavua mavazi yao haraka na kuwa na muonekano wa tofauti kiasi. Nguo zao za kidaktari, vifaa pamoja na miwani zao kubwa vyote vikawekwa kwenye mfuko mmoja na kutupwa haraka sana mtaroni pembeni mwa barabara. Baada ya kuwa sawa, dereva alitoa bahasha nne kwenye kidroo cha dashboard ya gari na kumkabidhi kila mmoja cha kwake kisha wakashuka na kupanda dala dala tofauti kila mmoja.
Baada ya kuwashusha madaktari wale sasa tukabaki watatu, mimi, Kasim na dereva mwenyewe. Tukaendelea mbele na safari, mwendo kidogo mbele sikuelewa alichofanya dereva, alicheza na ile gari na ndani ya sekunde chache akasimamisha gari. Mara hii hakusimamisha kwa taratibu za kawaida za barabarani bali aliiweka katikati ya barabara imegeuka k**a inaingia mtaroni, ilifunga barabara yote. Muda huu hapakuwa na magari, Akashuka, akafungua buti la nyuma la gari na kutoa boksi la vifaa vya ufundi wa magari na ovaroli. Akafungua boneti pale mbele ya gari kisha akaingia chini kwenye uvungu wa gari, baada ya dakika chache niliona moshi ukitoka kwenye boneti. Sikujua hata alifanya nini, japo nilikuwa na uhakika kabisa ule moshi haukuwa wa tatizo. Niliwaza kuna mchezo anacheza ila upi? nia yake ni nini? Sikupata jibu. Bamdogo naye alionekana kupata wasiwasi kiasi na inawezekana ile haikuwa sehemu ya mpango wao.
Baada ya mda mfupi akatoka uvunguni na kufunga buti na boneti kisha akaingia kwenye gari akiwa na vibati vyenye usajili wa gari ile. Hapa sasa nikaanza kutambua kuwa huyu hakuwa dereva tu ila mharifu mwenye akili nyingi. Japo swali langu bado halikupata jibu kamili bado, mpango wake ni nini? Alipofika kwenye gari alifunga vioo vyote vya gari. Vilikuwa ni vioo ambavyo mtu wa nje hawezi kuona waliondani ya gari. Tulikaa kimya kwa dakika k**a tano hivi huku yeye akiendelea kuufuatisha wimbo wake ule na moshi mkubwa ukiendelea kufuka kutokea chini ya gari. Muda wote huu bamdogo aliangalia saa yake, ambapo mwishoni uvumilivu ukamshinda, akamshutua jamaa huku akiuliza unafanya nini?. Dereva hata hakujibu kitu bali akapozi wimbo wake ni kufanya shiiiiiiiiii!!! huku ameweka kidole kwenye mdomo wake k**a vile mtu anayesema tulia usipige kelele utanipeperushia ndege wangu. Tukatulia tena huku yeye akishusha kitu k**a kipazia cheusi pale mbele kwake, akaziba kioo cha mbele. Dakika chache baadaye alitengeneza msongamano mkubwa wa magari njia zote mbili hakuna gari kushuka wala kupanda. Watu wengi kwenye magari walishuka kuja kuangalia kilichotokea. Waliojaribu kuchungulia ndani hawakufanikiwa kuona kitu. Haikueleweka kimetokea nini, wengi wao niliwasikia wakijadili kila mtu akitoa maoni yake. Wakati wote huo sisi kwa ndani tunawaona. Baadhi ya waendesha magari walionekana kukasirishwa sana na hali ile ndipo dereva mmoja wa daladala aliponyenyua simu na kuwapigia askari barabarani wa kile kituo cha mbele kilichokuwa kinafanya ukaguzi. “Hallo afande….., freshi tu kaka….., ndio nimepita hapo sio mda ila hapa mbele kuna tatizo…….., hapa mbele karibu na kona kuna gari imetelekezwa katikati ya barabara njia haipitiki kwenda wala kurudi mzee….. poa poa njooni.” Alisikika dereva yule wa daladala akiongea na askari huku akijaribu kuchungulia ndani ya gari yetu. Sijui hata alisikiaje na spika zake ndogo alizokuwa amevaa masikioni mwake, dereva wetu alipiga tena wimbo wake aliokuwa ameupozi uendelee kuimba, akiwa anapandisha sauti ya kiredio chake kidogo cha mfukoni, akasema “Let the game begin mother f**kers”. Akimaanisha “ mchezo uanze ’ Alionekana ni kijana wa kitanzania mwenye mapenzi sana na umarekani, hasa kwa jinsi alivyojaza matusi ya kizungu kwenye kila sentesi iliyomtoka mdomoni mwake. Alicheka kwa dharau kisha kuiwasha gari na kupiga muungurumo mkubwa huku tairi zikizunguka kwa kasi na kutoa moshi uliongezeka kwenye ule aliousababisha chini ya gari. Hii hali ilifanya watu wote waliokuwa wameizunguka gari ile kusambaratika pembeni na kuipisha. Aliizungusha na kuiweka sawa kuelekea mbele kisha akaiondoa kwa kasi kubwa. Nilishangazwa sana na ujuzi wake wa kucheza na gia na usukani kwa pamoja ndani ya muda mfupi sana. Nilipogeuka nyuma niliona kidude kidogo mithiri ya kibaruti kikiwa chini kinatoa moshi, mpaka leo sijawahi kujua alikuwa amewasha nini kutoka kwenye lile boksi la vifaa. Watu walibaki midomo wazi na mikono kichwani kwa spidi aliyoondoka nayo. Muda huu gari ilitembea kwa kasi kubwa kiasi kwamba ilikuwa k**a inaelea matairi hayagusi barabara. Mbele kidogo baada ya kuimaliza foleni aliyoitengeneza tulipishana na gari zote mbili za polisi nazo zikiwa kasi kurudi kuja sehemu ya tukio. Sijui ni kwa nini hawakutuzingatia, pengine walidhani tumetokea karibu kwa hiyo ile foleni haikutuhusu. Ndani ya hizo gali walikuwa ni wale askari waliotupita mwanzo pamoja na wale wa barabarani. Hata hawakuwa makini na sisi maana sidhani k**a waliona kwamba gari yetu haikuwa na ile pleti ya usajili. Hapa sasa nilipata picha halisi ya plani yake hasa tulipopita kwenye kile kituo cha ukaguzi bila kukuta askari yeyote. Muda wote huu aliendelea kuimba wimbo wake huku akiichochea gari ile ambayo nadhani ilikuwa imefanyiwa maboresho kiufundi ili ikimbie zaidi ya kawaida bila kuchemka. Alipishana na magari mengine k**a vile apishanavyo na mtu anayetembea kwa miguu. Kutokana mwendo ule mkali, sijui k**a tulifuatiliwa tena na wale askari au lah! Maana muda mfupi tulifika karibu kabisa na Mbeya mjini ambapo kukwepa maaskari wa vituo vingine vya mjini aliingia kibarabara cha mtaani na kula kona nyingi mpaka tukaingia kwenye geti moja ambamo alipaki na mlango ukafungwa.
Tukashuka na kuingia ndani. Nilishangaa sana baada ya kuingia ndani ya jumba lile la kifahari. Nilimuona mzee wangu akiwa na kiongozi mmoja mkubwa wa siasa hapa nchini, waziri ninayemjua kupitia vyombo vya habari na mitandao. Niliendelea kujilundikia maswali kichwani yasiyo na majibu. Hapa mzee kafuata nini? Ina maana na huyu waziri naye anafanya biashara haramu? Kwa nini anafanya biashara ya madawa ya kulevya wakati yeye ndio alipaswa kupambana nayo? Ina maana naye anahusika kusafirisha nyara mbalimbali za serikali? Au ndiye huwa anayemsaidia baba yangu kusafirisha zile pembe za ndovu kwenda nje ya nchi na kuleta madawa? Ana njaa gani huyu waziri mpaka ajihusishe na biashara hizi haramu? Sikupata jibu la maswali yote haya. Nikiwa mkimya nisiyeongea lolote, baba aliniuliza, “Jamin nilikwambiaje kuhusu Jackline?, eeeh nawe ulijibu nini?” Kabla sijajibu kitu, baba mdogo Kasim akadakia.. “kijanaako amezama tena kwenye mapenzi hadi anaharibu kazi” huku akifungua friji lililokuwepo ndani hapo na kutoa pombe kali. “Mapenzi…. Mapenzi… mapenzii.. hahahahaha” aliongea Joseph Charles baba yangu ambaye pia ni bosi wangu huku akicheka kwa ghazabu kubwa. Alinisogelea kwenye sofa niliyokuwa nimekaa, “who is she?, eeeeeeh nilikutuma kumpenda Jackline au ukamuue?”. “hata sio Jack bro” alidakia Kasimu baba mdogo akiwa anajimiminia pombe ile kali k**a anakunywa maji. “ooooh a new girl!!! Bravo” akapiga makofi kunipongeza kwa hasira huku akinizunguka. Aliponizunguka kwa nyuma nilishtukizwa na kofi moja zito alilonipiga kisogoni, pwaaaah!!!! Kofi lile lilinishusha kutoka kwenye sofa mpaka chini ambapo nilifikia magoti. Nikiwa nimebaki nimepiga magoti bila kuongea kitu nimeinamisha kichwa chini, bosi alikuja mbele yangu akatoa bastola na kuniinua kichwa kwa siraha hiyo akiniangalia kwa hasira kali hasa aliposikia neno mapenzi limeharibu hazi aliyonipa. Hapa niliwaza naweza kuuawa kweli japo imani yangu iliniambia baba hawezi kuniua hata iweje. Japo upande mwingine niliogopa kwa jinsi alivyokasirika. Niliwaza siraha zangu sina hata moja mambo yakibadilika kabisa pale ndani. Tuliacha kila kitu kwenye ile gari pale nje. Nilipotupa macho kwa dereva yule ambaye sikumjua hata kwa jina tu, alikuwa anaendelea kuimba kwa sauti huku akiangalia runinga iliyokuwa ikionyesha mashindano ya mbio za magari. Alionekana kufurahia sana bila hata kujali kilichokuwa kikiendelea pale ndani. Yule waziri aliingia chumbani na kutoka na kibrifkesi kidogo kisha kumkabidhi dereva, ambaye aliondoka huku akiimba tu wimbo wake na kutikisa kichwa akionekana kuufurahia kweli kweli. Mzee akiwa ameniwekea bastola kwenye paji langu la uso, akaniuliza tena ni nani huyo mwanamke?? Sikujua cha kumwambia maana binti yule niliyempenda ghafla pale uwanjani hata simfahamu. Nikimjibu hivi mzee angeniona muongo na bado naleta mapenzi kwa kumlinda mtoto wa k**e kitu ambacho kwake ni sumu kwenye kazi. Ikanibidi tu nikae kimya. “Nakupa dakika moja ya kuchagua aidha mapenzi nikumalize mda huu au familia uishi, nakuuliza tena, ni nani huyo binti na nampataje??” Kwa hasira isiyopungua, bosi aliongea.
…………………………………………………………………..
ITAENDELEA…..…..
Ahsante kwa kusoma mpaka hapa, usikose sehemu ya nne ya simulizi hii nzuri…
Je nini atafanyiwa Jamin?, Jackline ni nani? Yule binti vipi?..
Kupata muendelezo wa stori hii au episode iliyopita kwa urahisi tufollow Instagram, Facebook, Twitter, Youtube.. zote jina ni .
Maoni/Ushauri: Whatsapp/Text/Call +255766511619