17/03/2026
JUA NAMNA YA KUMSHINDA ADUI YAKO.
Adui yako huishiwa nguvu tu pale unapokamilisha mambo ya maana, lakini k**a una adui halafu hana mambo ya maana unapoteza nguvu zako bure, kati yako na adui yako lazima kuwe na kitu chaku compete! Huwezi mwambia mtu ni adui halafu hakuna chochote. Adui jicho lake lipo kwa Unachokifanya, adui ni mharibu yupo hapo kuhakikisha anakumaliza, adui ni mtu hatari wa ubadae wako.
Nehemia 6:16
16 Ikawa adui zetu wote waliposikia, ndipo makafiri wote waliotuzunguka wakaogopa, nao wakakata tamaa sana machoni pao wenyewe; maana waliitambua kazi hiyo ilivyotendwa na Mungu wetu.
Hawa ndio maadui kina tobia, Angalia waliposikia Nehemia kajenga ule ukuta mrefu uliobomoka miaka mingi, wakaogopa, wakataa tamaa sana machoni pa wenyewe. Hakikisha unamshinda adui kwa kufanya mambo makubwa, hatushindani na adui kwa maneno, kwa sababu adui anayo maneno ya kutosha atakushinda, wakamwambia hako ka ukuta hata mbweha akikasukuma kanaanguka, adui atakufanya hujione hufai na huwezi, lakini leo nakwambia dhamiria kufanya mambo makubwa hata maadui zako watakuja upande wako. Focus, songa mbele, utafika. Maneno, condemnation, accusations, ni maneno madogo madogo wakati mwingine tutayafunua, leo nataka kukwambia adui yako mfanye k**a lift awe sababu ya wewe kufanya mambo makubwa, ukikumbua una adui fanya mambo makubwa atakuja kukuheshimu