10/06/2026
WANAWAKE DODOMA.
Mungu amewapa neema ya kumiliki miji msioijenga , nyumba msizonunua! Baraka yenu inatoka katika kumbu kumbu la torati 6. Je maana yake nini? Na je inatupasa kufanya nini ili tuweze kuona na kupokea tulichopewa siku ya leo?
KUMB 6:10 "Tena itakuwa atakapokwisha Bwana, Mungu wako, kukuleta katika nchi aliyowaapia babu zako, Ibrahimu na Isaka na Yakobo, ya kuwa atakupa; miji mikubwa mizuri usiyoijenga wewe,
11 na nyumba zimejaa vitu vyema vyote usizojaza wewe, na visima vimefukuliwa usivyofukua wewe, mashamba ya mizabibu na mizeituni usiyoipanda wewe, nawe utakula na kushiba;"
Neno linaimanisha baraka za Mungu hazitokani na nguvu zako peke yako, hayo unayopitia ni kwasababu unategemea akili zako mwenyewe. Mungu anaweza kukupa vitu ambavyo hujavifanyia kazi moja kwa moja. Mungu anaweza kufungua kufungua fursa au mafanikio ambayo yanaonekana kuzidi juhudi zako za kawaida. Ndio mana kuna wakati ukiangalia mali zako wakati mwingine unajiuliza imewezekanaje hauamini k**a ni wewe umetafuta! Ni kwasababu ni Yeye kafanya kwako, zaidi ya akili yako na ufahamu wako .
Unaweza ukawa na kazi na usimiliki chochote, Neno pia linasema asiyefanya kazi na asile kwa nini wewe ufanye kazi bado unalala njaa! Bado umepangisha! Na pengine unalipwa vizuri! Nguvu za utajiri ni Mungu anakupa havitegemeani na unafanya nini! Mama ntilie anaweza akajenga nyumba, banker hana why? Kwa sababu wanategemea akili zao na kazi zao. Ukimtegemea Mungu huwa anafanya zaidi ya fahamu zetu.
*JE MUNGU ANATAKA NINI KWETU?* ILI TUWEZE KUPOKEA HIZI MALI TUSIZOTAFUTA SISI.
1.Mche Bwana Mungu na kuzishika sheria zake na amri zake. Zipi hizo? kutokuabudu miungu wengine. Usiabudu Miungu wengine, usiwe mwizi mwizi, mjanjaja, Mjanjanjanja! Msizini ili mpate msivyotafuta! Wewe mpende kwa moyo wakowote, kwa akili zetu zote, na mawazo yetu. Na mengine mengi.
Unapoumcha Mungu kutakubadilisha The way you think, speak, you act , utakuwa na Mindset of a Believer: mindset of faith.
Atataka familia yakoz watoto wako wote umkabidhi yeye ili adui asipate upenyo kupitia kwako itakuzuilia kupokea.
Tena anasema atawasukumia mbali adui zakoKumb 6:19. "ya kuwa atawasukumia nje adui zako wote mbele yako, k**a alivyosema Bwana "
adui ni nani! Wale wanaleta Negative Influences, wana wivu, gossipers, criticisers, mockers ili wakutoe hapo. Watakuzuia kupokea baraka hizi kwa hiyo lazima akutenge nao. Katika Matthew 13:25-26. Wapo inasema walipolala adui akawavizi usiku akapanda magugu katikati ya shamba lao la ngano, akaenda zake. Cain out of jealously he killed abel, How many are jealous of you.?
Adui mwingine Nehemiah 4:1-3 “ Hata hiki wanachokijenga, angepanda mbweha, angeubomoa ukuta wao wa mawe. "
Watafanya kila jambo usione baraka wala kufikia hatma yako. Tembea na Kumb 6 yote uimbe kinywani kwako utakutana na baraka hii ya ajabu! Mambo ambayo hujawahi kufikiria Mungu anaenda kukupa.