Pastor fide.

Pastor fide. Pastor

WANAWAKE DODOMA.Mungu amewapa neema ya kumiliki miji msioijenga , nyumba msizonunua! Baraka yenu inatoka katika kumbu ku...
10/06/2026

WANAWAKE DODOMA.

Mungu amewapa neema ya kumiliki miji msioijenga , nyumba msizonunua! Baraka yenu inatoka katika kumbu kumbu la torati 6. Je maana yake nini? Na je inatupasa kufanya nini ili tuweze kuona na kupokea tulichopewa siku ya leo?

KUMB 6:10 "Tena itakuwa atakapokwisha Bwana, Mungu wako, kukuleta katika nchi aliyowaapia babu zako, Ibrahimu na Isaka na Yakobo, ya kuwa atakupa; miji mikubwa mizuri usiyoijenga wewe,
11 na nyumba zimejaa vitu vyema vyote usizojaza wewe, na visima vimefukuliwa usivyofukua wewe, mashamba ya mizabibu na mizeituni usiyoipanda wewe, nawe utakula na kushiba;"

Neno linaimanisha baraka za Mungu hazitokani na nguvu zako peke yako, hayo unayopitia ni kwasababu unategemea akili zako mwenyewe. Mungu anaweza kukupa vitu ambavyo hujavifanyia kazi moja kwa moja. Mungu anaweza kufungua kufungua fursa au mafanikio ambayo yanaonekana kuzidi juhudi zako za kawaida. Ndio mana kuna wakati ukiangalia mali zako wakati mwingine unajiuliza imewezekanaje hauamini k**a ni wewe umetafuta! Ni kwasababu ni Yeye kafanya kwako, zaidi ya akili yako na ufahamu wako .

Unaweza ukawa na kazi na usimiliki chochote, Neno pia linasema asiyefanya kazi na asile kwa nini wewe ufanye kazi bado unalala njaa! Bado umepangisha! Na pengine unalipwa vizuri! Nguvu za utajiri ni Mungu anakupa havitegemeani na unafanya nini! Mama ntilie anaweza akajenga nyumba, banker hana why? Kwa sababu wanategemea akili zao na kazi zao. Ukimtegemea Mungu huwa anafanya zaidi ya fahamu zetu.

*JE MUNGU ANATAKA NINI KWETU?* ILI TUWEZE KUPOKEA HIZI MALI TUSIZOTAFUTA SISI.

1.Mche Bwana Mungu na kuzishika sheria zake na amri zake. Zipi hizo? kutokuabudu miungu wengine. Usiabudu Miungu wengine, usiwe mwizi mwizi, mjanjaja, Mjanjanjanja! Msizini ili mpate msivyotafuta! Wewe mpende kwa moyo wakowote, kwa akili zetu zote, na mawazo yetu. Na mengine mengi.

Unapoumcha Mungu kutakubadilisha The way you think, speak, you act , utakuwa na Mindset of a Believer: mindset of faith.

Atataka familia yakoz watoto wako wote umkabidhi yeye ili adui asipate upenyo kupitia kwako itakuzuilia kupokea.

Tena anasema atawasukumia mbali adui zakoKumb 6:19. "ya kuwa atawasukumia nje adui zako wote mbele yako, k**a alivyosema Bwana "

adui ni nani! Wale wanaleta Negative Influences, wana wivu, gossipers, criticisers, mockers ili wakutoe hapo. Watakuzuia kupokea baraka hizi kwa hiyo lazima akutenge nao. Katika Matthew 13:25-26. Wapo inasema walipolala adui akawavizi usiku akapanda magugu katikati ya shamba lao la ngano, akaenda zake. Cain out of jealously he killed abel, How many are jealous of you.?

Adui mwingine Nehemiah 4:1-3 “ Hata hiki wanachokijenga, angepanda mbweha, angeubomoa ukuta wao wa mawe. "

Watafanya kila jambo usione baraka wala kufikia hatma yako. Tembea na Kumb 6 yote uimbe kinywani kwako utakutana na baraka hii ya ajabu! Mambo ambayo hujawahi kufikiria Mungu anaenda kukupa.

Hivi  unawezaja kuacha kumtegemea Mungu aliyekuumba kwa kusudi ye ndiye anayejua hatima yako halafu ukaanza kumtegemea M...
31/05/2026

Hivi unawezaja kuacha kumtegemea Mungu aliyekuumba kwa kusudi ye ndiye anayejua hatima yako halafu ukaanza kumtegemea Mganga wa kienyeji, una akili timamu kweli! Anakuomba kafala ya mmeo ya watoto wako vile uvipendavyo upo tuu humo unawaza hela huku unatembea na maumivu kibao nusu mfu nusu mtu. Hela zenyewe za masharti. Amesema Mimi ni BWANA, Mungu wako, nikufundishaye ili upate faida, nikuongozaye kwa njia ikupasayo kuifuata. Sasa unatafuta faida wapi wewe? Mwanamke amka amelaaniwa amtegemeaye mwanadamu na kumfanya kuwa kinga yake, moyoni mwake kamwacha Mungu. Ingia toba niite tuchome mikoba yako uanze na Mungu. Trust him fully. Wengine mmefilisika mmekata tamaa amka mwamini Mungu k**a fedha ilishapita kwenye mikono yako jua ipo... Mahala mkondo wa maji yanapita hata mvua ikikata miaka 100 siku ikinyesha yatapita hapo, wewe ni mkondo wa i hela zilipita hapo zitapita tena dabo, hata k**a hujawahi shika fedha leo tunatengeneza mikondo zitarudi hapo double. Acha kuwaza fedha ni kitu kidogo kwa Mungu, anachotaka kwako mtegemee tu. Mpe nafasi Mungu.

Aksanteni sana Namanga super kwa kunialika. Tuendelee kuomba hata nyumba kwa nyumba mpaka tunatoboa, hatuwezi kuishia popote tutaishia pale Mungu amekusudia

Wakati Mwingine unahitaji tu kunyamaza kimya  na kumwimbia Mungu Zaburi ya 25. Awatazame adui  zako kwa namna wanavyokuc...
21/05/2026

Wakati Mwingine unahitaji tu kunyamaza kimya na kumwimbia Mungu Zaburi ya 25. Awatazame adui zako kwa namna wanavyokuchukia kwa ukatili mwingi.

Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na...
20/05/2026

Wafilipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lo lote; bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu.

MAMBO MUHIMU MATANO UNAYOPASWA KUYAZINGATIA  UNAPOOMBA MUNGU AKUPE SPEED/KASI  KATIKA MAMBO YAKO.Ukimuomba Mungu akupe s...
18/05/2026

MAMBO MUHIMU MATANO UNAYOPASWA KUYAZINGATIA UNAPOOMBA MUNGU AKUPE SPEED/KASI KATIKA MAMBO YAKO.

Ukimuomba Mungu akupe speed/kasi katika maisha yako , mafanikio yako, utumishi wako, na mengineyo mengi maana yake unaruhusu nguvu ya Mungu kuingilia kati kwenye mambo yako mambo yaende kwa kasi sana. Ni ombi zuri sana na Mungu humpa mtu anachotaka, ukiomba mkate utapewa mkate.

Sasa hii kasi ya Mungu husababisha mambo kukimbia sana. k**a ukitafuta kazi miaka basi ni siku au masaa Mungu akiweka kasi yake, k**a ni biashara basi itaenda haraka kiasi cha kushangaza na wengine wanaweza wasielewe k**a ni kweli inawezekana. Kasi ya Mungu itatokea kwako iwapo tu utazingatia mambo yafuatayo.

1. ONDOA SPEED GAVANA
Wakati unaenda na kasi ya Mungu sio wewe unayepaswa kupunguza mwendo sababu anayeuongoza mwendo ni Mungu. Speed yake ni ile ile haijalishi kuna milima, mabonde, mashimo, we nenda ukijua ndio speed yenyewe na mwenye speed ni Mungu, jikane. Kuna mahali Mungu atakwambia nenda usianze kuweka gavana zako, nitaingiaje pale, nitafikaje pale just gooo...
Eliminate your fear, doubt, negativity. These are spiritual speed gavanas that slow down your progress and block your faith.

2. TEMBEA NA IMANI WAKATI WOTE.
Lolote asemalo Mungu we fanya hata k**a haliwezekani hata kidogo, we fanya! Changamoto yoyote isikuzuie fanya kwa Imani, we angalia mwisho unachokitaka usiangalie na unayokutana nayo. We jua kusudi inatosha. keep the same level of faith and consistency.

3. AMINI UELEKEO MUNGU ANAOKUPA.
K**a ni Mungu anaongoza safari yako muamini yeye, mbele zake hutaangamia, hata utupwe kwenye tanuri la moto hutateketea. His guidance gives protection, wisdom, and strength even in difficult seasons.

4. USISHIKE BREAK POPOTE
Ukishakuwa katika kasi ya Mungu, ziko break nyingi usizishike nazo ni kuruhusu maoni ya watu na kuacha kile Mungu anakwambia, Mungu wakati wote ni Mungu wa kuyaweza yasiyowezekana, sasa mwanadamu atakuhesabia hili unaweza, hili huwezi, watakukwamisha. Njia za Mungu hazichunguziki. Too many brakes destroy God’s speed and delay your purpose

5. ZINGATIA NA UOMBE.
Omba pasipo kuchoka mpaka hicho ambacho umehitaji Mungu aweke mkono wake na akuongezee mwendo/ kasi ya kutimia kipate kutimia. Usipoe mpaka ufike mahali umetaka kufika.

Pastor Phide
Call/Whatsapp
0764 151543.

Zaburi 125 :1-2 " Wamtumainio Bwana ni k**a mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.K**a milima inavyouzunguka Y...
14/05/2026

Zaburi 125 :1-2 " Wamtumainio Bwana ni k**a mlima Sayuni, Ambao hautatikisika, wakaa milele.K**a milima inavyouzunguka Yerusalemu, Ndivyo Bwana anavyowazunguka watu wake, Tangu sasa na hata milele."

Katika mitandao ya kijamii hii tunayotumia, unaweza kumuogopa mtu ambaye unapaswa kumhurumia. Tena kumhurumia sanaaaa......
12/05/2026

Katika mitandao ya kijamii hii tunayotumia, unaweza kumuogopa mtu ambaye unapaswa kumhurumia. Tena kumhurumia sanaaaa.... Hata katika maisha tunayoishi unaweza kumuogopa sana mtu mwenye mali lakini katika uhalisia wake unapaswa kumhurumia na kumuombea kwa namna anavyozipata. Wengine huua, wengine wanateseka kuzitafuta. Mungu awape kuona utajiri alionao wa fedha na dhahabu.

Mungu aendelee kuwatunza na kuwabariki. Awajibu k**a alivyomjibu Yabesi, alimbariki, akatanua mipaka yake na kumlinda.

KUMCHA BWANA NI CHANZO CHA MAARIFA.Utajua unamcha Bwana kwa sababu akili yako haiwezi kuwa ile ile, ufahamu wako hauwezi...
10/05/2026

KUMCHA BWANA NI CHANZO CHA MAARIFA.

Utajua unamcha Bwana kwa sababu akili yako haiwezi kuwa ile ile, ufahamu wako hauwezi kuwa uleule. Tabia yako haiwezi kuwa ile ile, lazima vitu viongezeke kwako sio kupungua, ukiona kuwa vile vile au kupunguka. Jua kuna mahali humtii Mungu. Kwa sababu kumcha Mungu ni kumtii na kumtegemea yeye.

Mithali 1:17 Kumcha Bwana ni chanzo cha maarifa, wapumbavu hudharau hekima na adabu.”

Ukishakuwa na Mungu jikane, itakusaidia ujue Mungu anataka kuwekeza nini ndani yako. Kwa sababu, Mungu hawezi kukaa ndani yako na mambo yako ya kale. Amesema lazima atafanya jambo jipya ndani yako, kwa hiyo akiingia ndani yangu si mimi tena bali ni Mungu, kwa hiyo kila nitakalofanya litangatia ni Mungu anayepaswa kuonekana, k**a ni tabia aonekane Mungu, k**a ni mavazi aonekane Mungu, chochote nifanyacho nitafanya Mungu akionekana.

Using'ang'ane na ufahamu ule ule na akili ile ile. Acha akuonyeshe baada ya yeye kuingia ndani yako, nini anaenda kubadilisha, ndio maana ya kujikana, wewe ufe yeye afufuke ndani yako. La sivyo Utaendelea kumuona Mungu vile vile. Mungu hazoeleki ana jambo jipya kila siku.

Nimekutana na watu wengine wanauliza siku hizi hatukuoni huku na huku. huvai nguo za kubana tena?, huvai vigauni vifupi, kuna mmoja kaniuliza leo. Nikapata na somo la kufundisha, jamani jibu ni ndio kwa sababu game changer Mungu mwenyewe yuko ndani yangu anabadilisha systems. So kaeni kwa kutulia bado mtaona mambo ambayo macho hayajawai kuona wala masikio hayajawahi kusikia, Mungu kabeba chombo chake.

Halafu Mungu hagawani utukufu na Mtu. Akisema hata k**a utachekwa, watakubeza we fanya utukufu ubaki kwake. Ukianza kupima pima na wanachokwambia maana yake unataka kugawa utukufu utashindwa.

Isaya 42:8 a"Mimi ni Bwana; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine........

ukaamua kumcha Mungu kweli kweli, ukaongozwa na yeye, ukajikana na kuruhusu yeye awe ndani yako na kufanya anayotaka wewe, huwezi kuwa na akili ile ile. Ukiona unamtumikia Mungu akili ile ile, ufahamu ule ule, ukipewa maagizo unaanza kupima ya Mungu na wanayokwambia watu my friend akili mpya utaisikia mbinguni. Tulia kwanza mche Mungu akupe maarifa.

Nya 7:14 "Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia ...
08/05/2026

Nya 7:14 "Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao."

Nyenyekea na kuomba, ntafute Mungu anapatikana, usikae na mambo magumu, usikae na millima mirefu, usikae na giza, usikae na mauti, mtafute Mungu hulitazama neno lake na kulitimiza. Acha kutenda dhambi, mambo ya kale mambo yasiyo ya utukufu wa Mungu, amua kubadilika sasa, naye Mungu atabadilisha maisha yako.

Be humble!Watu wakikuheshimu, wakikupenda wakikuchagua wakakupa zawadi, be humble usiinue mabega juu, usiwadharau yote y...
07/05/2026

Be humble!
Watu wakikuheshimu, wakikupenda wakikuchagua wakakupa zawadi, be humble usiinue mabega juu, usiwadharau yote yamefanyika kwa neema ya Mungu.

Mithali 16:18 "Kiburi hutangulia uangamivu; Na roho yenye kutakabari hutangulia maanguko."

Address

Sakina
Arusha

Telephone

+255764151543

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Pastor fide. posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to Pastor fide.:

Share