FKGstories

FKGstories Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from FKGstories, Art, Arusha.

Karibu katika ukusa huu wa FKGstories ukurasa unaokupa wakati mzuri wa kujifunza kupitia makala na hadithi mbalimbali za kubuni na zinazohusu maisha halisi ya mTanzania na dunia kwa ujumla.

Leo ni siku ya kuzaliwa ya mwasisi wa  page yetu ya FKGstories. Happy Birthday broπŸ’πŸ’
15/09/2023

Leo ni siku ya kuzaliwa ya mwasisi wa page yetu ya FKGstories. Happy Birthday broπŸ’πŸ’

Fikra Huru........MnyarugandaNelius Trazias 0748254542Mnyaruganda... Siku ukipata nafasi ya kukutana na   mwanao John  m...
08/10/2022

Fikra Huru........Mnyaruganda

Nelius Trazias 0748254542

Mnyaruganda... Siku ukipata nafasi ya kukutana na mwanao John mkumbushe

1. Mkumbushe kuwa mwanamke ni kiumbe chenye huruma sana ila asitumie mlango huo k**a fungulia Mbwa, machozi ya mwanamke ni sumu inayoua taratibu.

2. Mwambie John kuwa akila akaondoka akumbuke kuna wengi wamevimbiwa hata baada ya kula, hivyo asijisifu sana hata matokeo hutoka baada ya kufanya mitihani.

3. Mkumbushe John kuwa mwanamke ni kiumbe kinachoamini sana katika uongo kuliko hata ukweli ila haitaji longolongo , hivyo asipende kutembea katika maisha ya kuigiza akivaa raba na suruali za kuazima mwisho wa siku ataumbuka.

4. Mkumbushe John kuwa hakuna mwanamke msaliti hapa duniani ila mwanamke anataka apewe upendo wa kweli na matunzo kidogo ili asimame daima k**a ukuta wa Berlin. Ila wanaume wengi wa sasa kupenda kukwepa majukumu wamegeuza kibao na kuanza kuwaita wanawake Malaya. Duuuuuuh Mungu wa Isaka

5. Mkumbushe John kuwa kila anapomuona mwanamke ampe heshima yake maana kila mwanamke amebeba maono ya dunia. Mara ndiye mwalimu wa familia, mara mwanasheria kwa watoto wake, mara mhasibu akilinda uchumi wa familia, mara Daktari kumuangalie anayeumwa , mara mwandishi akatoe habari na mwenendo wa familia yake n.k, . Mwanamke jipige kifua sema " wanawake jeshi kubwa ".

6. Mkumbushe John kuwa mwanamke ni sawa na bustani ya mbogamboga huitaji kumwagiliwa kila siku hivyo akiacha ikauke wenye uhitaji wa kula mboga za majani ni wengi hivyo amlinde Mwanamke k**a mboni.

7. Mkumbushe John kuwa wabeba maono ni wengi siku hizi, hivyo amtangulize Mungu asije kuliwa kichwa na madanga wa mjini.

8. Mkumbushe John kuwa kila akimuona mwanamke analia asimuone k**a muigizaji bali kupitia kulia kwake mwanamke hujiongezea siku za kuishi kwa kuondoa machungu na mwanaume hali hii ndiyo mara nyingi humuondoa uhai kwa sababu ya kuyakumbatia machungu leo hii wanaume wengi hufa mapema na kuwaacha wake zao.......

03/10/2022
MWANAUME KUFA MAPEMA HAIEPUKIKIFikra Huru....... MnyarugandaUkizaliwa mwanaume  jua fika wewe ni mfia watu, ndipo naliku...
29/09/2022

MWANAUME KUFA MAPEMA HAIEPUKIKI

Fikra Huru....... Mnyaruganda
Ukizaliwa mwanaume jua fika wewe ni mfia watu, ndipo nalikumbuka neno la Wahenga lisemalo "Ukimuona Nyani mzee jua amekwisha kwepa mishale mingi". Mnyaruganda wape hai wanaume wote wanaolelewa wambie sio UWANA huo. Leo hii watoto katika familia nyingi wanayajua mabaya ya baba zao kuliko mazuri yao, hii ni kwa sababu Mama zetu hupenda kuyasimulia mabaya ya waume zao kuliko mazuri yao. Wanaume wengi hunyamaza kwenye familia zao si kwamba hawawezi kuongea ila siku zote wao huitamani kesho yao. Kasome Mwanzo 2:24

Bro usimrudishe nyumbani mke wako kwa sababu anaongea sana. Mwanamke kwa siku ana uwezo wa kuongea maneno 7,000 na mwanaume amejitahidi Sana ni maneno 4,000 kwa siku. Wale waliokwenda shule nisaidieni hiyo hesabu, jamani Mungu amempendelea mwanamke katika kunena. Leo hii ukipita mtaani wanawake walioachwa na waume zao ni wengi kuliko wanaume walioachwa na wake zao. Mke wa Nyerere mama Maria yupo mpaka leo, mke wa Mkapa mama Anna Mkapa yupo na mke wa Magufuli mama Janeth Magufuli yupo.

Ujue lile neno lisemalo mtu akikupiga shavu la kulia mpe hata na lile la kushoto lina maana kubwa mno. Mwanaume anaweza mpenda binti na kumlipia Ada ya shule ila binti akimaliza masomo humchagua mwanaume atakayemuoa maana yawezekana alikuwa akihitaji msaada kwa sababu ya ugumu wa maisha ya kwao wakati huo. Mmmmmmmm mwanaume hapo kwanini asiife mapema kwa hizo stress.

Mnyaruganda... ujue yule msanii liyeimba wanaume tumeumbwa mateso alisitahili kujengewa sanamu tena pale posta. Ila ni kawaida ya wanadamu kutambua mchango wa mtu akishakufa. Mwambie mwanaume k**a akitoa pesa k**a zawadi kuwanunulia watoto wake nguo basi pesa asiiache pale mezani awaite watoto wake na mke wake awakabidhi hiyo pesa watoto wakiona ili wajue ni baba yao amewapa zawadi ila ukiacha pesa pale mezani watoto wataamini mama yao ndio huwatunza kwa kila kitu na badae watakula kichwa ndio maana familia nyingi sasa watoto huwapenda mama zao kuliko baba ukiachana na tafiti za kibayologia.

Mnyaruganda ... mwambie binti asitake kuachika mapema, Hamsini 50% kwa 50% Ni mfumo wa Ulaya na serikalini ila kwenye ndoa za Kiafrika wazee wanaukataa mfumo, basi k**a unayabishia maneno yangu nenda pale Ikulu ukamuone mama Samia na mumewe. Mwambie Mhe.Dkt Mwigulu Nchemba waziri wa fedha apunguze utitili wa kodi za tozo maana anaendelea kumchimbia kaburi mwanaume taratibu kwa sababu huku kwenye familia wanaume wana ushuru wa kila aina Mara ushuru wa kila siku awe anaumwa au laah ataulizwa matumizi tu (tax table).
Jipatie nakala ya Kitabu changu "UTUMWA ULOJAA UDI" sh.5,000 tu.
0748254542

Ndugu Mabibi na mabwana wapenzi wa ukurasa wetu wa FKGstories napenda kumleta kwenu mwandishi nguri wa simulizi na makal...
29/09/2022

Ndugu Mabibi na mabwana wapenzi wa ukurasa wetu wa FKGstories napenda kumleta kwenu mwandishi nguri wa simulizi na makala mbalimbali zinazoaksi uhalisia wa maisha ya kila kila siku, si mwingine nae ni Nelius Trazias πŸ’₯πŸ’₯πŸ’₯πŸŽŠπŸŽŠπŸŽŠπŸŽ‡πŸŽ‡πŸŽ‡

Address

Arusha

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when FKGstories posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to FKGstories:

Share

Category