1009 Music

1009 Music We aspire to provide the right productions to the world - telling our African stories through art. We are an entertainment company that manages artistes.

We produce good music, shoot videos and also do gigs

Mcheshi anayejaribu kuwa k**a Ishowspeed, Vindee, jana amepigwa akiwa kwa upeperushaji huko Klabu Area, UON. I ni baada ...
26/02/2026

Mcheshi anayejaribu kuwa k**a Ishowspeed, Vindee, jana amepigwa akiwa kwa upeperushaji huko Klabu Area, UON. I ni baada ya kuanza kuongelesha wasichana waliokuwa kwenye njia na taa ya mwanga ya LED wanaoitumia kuwaangazia vijana wasiojulikana.
Baada ya purukushani ilionekana kumalizikia kwa mtu wake wa kamera kuumizwa Vindee alidai kuwa hawangeweza kumuibia simu kwa maana anawashinda na nguvu.
Je wewe waona ni haki kwa watu kuwasumbua wapepereshaji video ikiwa kamera zao zitawamulika wakiwa pahala pa umma

Rondo Retreat wamejipata kwenye shida la Uhusiano wa Umma baada ya kuonyesha mapendeleo ya rangi.Tukio hilo linalohusish...
07/01/2026

Rondo Retreat wamejipata kwenye shida la Uhusiano wa Umma baada ya kuonyesha mapendeleo ya rangi.

Tukio hilo linalohusisha muimbaji tajika Bien, mkewe, chiki na familia yao, limefanya Rondo retreat kuizima sehemu ya maoni kwa kurasa lao la instagram.

Hayo hayajazuia mashabiki wa msani huyo na wakenya kwa ujumla kuikashifu biashara hiyo. Kwenye google na tripstar wameizamisha kiwango kutoka 4.7 hadi 2.4 kwa masaa machache, na huenda kiwango hicho kikateremka ata zaidi.

Rondo retreat hivi sasa wamegundua ushawishi alionao msanii huyo na labda wanajutia tukilo hilo. Ila, hadi sasa hawajaomba msamaha wala kutoa ripoti yoyote.

Hadi na sisi tunakemea biashara yoyote inayoonyesha ubaguzi wa rangi. Washindwe

Rais wa Marekani ameionya NATO kuwa Urusi na China wanaigopa NATO kwa sababu moja tu; kuwa Marekani iko miongoni mwao.Kw...
07/01/2026

Rais wa Marekani ameionya NATO kuwa Urusi na China wanaigopa NATO kwa sababu moja tu; kuwa Marekani iko miongoni mwao.

Kwa posti ndefu alijisifia kuwa ameifanya Marekani kuheshimika kwa kuwekeza kwenye Ulinzi na Jeshi lao.

Amuisurutisha Jamhuri ya Norwey kwa kumnyima tuzo la nobel peace prize. Wengi wanasema hafai kupewa kwa kuwa, licha ya kujifanya hao ndo wanazima moto, ni wao wao wanaoakisha moto na kuiba rasilimali za nchi zingine.

Je waona kuwa Donald Trump yuko sawa?

Wanachuo wa awali wa shule ya upili ya Mang'u wamemkemea Naibu wa rais aliyetolewa, Rigathi Gachagua, kwa kile wanachoda...
07/01/2026

Wanachuo wa awali wa shule ya upili ya Mang'u wamemkemea Naibu wa rais aliyetolewa, Rigathi Gachagua, kwa kile wanachodai ni ukabila wa hali ya juu.

Kwa kauli walioipitisha mtandaoni, wamesema kuwa wanasikitika kwa wanasiasa kutumia shule na rasilmali za taifa katika siasa za utenganisho. Wakasema pia Mang'u ni shule ya jamhuri ya kenya na kila mtu ndani ya kenya ana haki ya kusomea huko ikiwa amehitimu.

Je wewe wadhani Rigathi Gachagua ako sahihi?

Mchezaji wa Ghana anayoichezea timu ya AFC bournemouth ya Uingereza, Antoine Semenyo, amekubali mkataba wa kujiunga na T...
07/01/2026

Mchezaji wa Ghana anayoichezea timu ya AFC bournemouth ya Uingereza, Antoine Semenyo, amekubali mkataba wa kujiunga na Timu ya Manchester City.

Semenyo anatarajiwa kufanya uchunguzi wa kitabibu hivi leo kwa matayarisho ya kujiunga na timu io ya Man City.

Mkataba huo unathaminiwa kuwa wa Euro millioni sitini na tano. Twamtakia mchezaji huyo heri na fanaka.

Wanasiasa wa mrengo wa ODM wameingia kwenye mtandao kufanya kumbukumbu kwa marehemu Raila Amolo Odinga kwa siku yake ya ...
07/01/2026

Wanasiasa wa mrengo wa ODM wameingia kwenye mtandao kufanya kumbukumbu kwa marehemu Raila Amolo Odinga kwa siku yake ya kuzaliwa.

Ila wengi wao wamekejeliwa kwa hizo jitihada za kujihusisha na marehemu kinara huyo wakiwaita mayatima wa kisiasa. Wengi wamewaelezea kuwa sasa hawatalitumia jina la Raila kupata viti, itabidi wadhihirishe utendakazi wao.

Je wewe waona ikiwa ni kumbukumbu la kweli ama ni mchezo wa kisiasa?

Mkimbizi bora zaidi afrika Ferdinand Omanyala amesema kuwa ako tayari kumenyana na mpeperushaji wa video wa Amerika Isho...
07/01/2026

Mkimbizi bora zaidi afrika Ferdinand Omanyala amesema kuwa ako tayari kumenyana na mpeperushaji wa video wa Amerika Ishowspeed.

Amesema kuwa licha ya kuwa hana maitaji mengi, ikiwa Ishowspeed ako radi kumpa kitita kisicho chini ya dola elfu hamsini za Marekani basi atamenyana naye.

Watu wengine wanamponza kwa kuwa walitaka afanye bure bilashi na wengine kumuunga mkono kwa kuwa kukimbia ni kazi yake na hakuna mtu hutaka kufanya kazi yake bila kulipwa. Wewe waonaje?

Rais wa Afrika Kusini ameikemea shambulizo na kuk**atwa kwa rais wa Venezuela Nicolas Maduro.Rais Ramaphosa amesema Rais...
06/01/2026

Rais wa Afrika Kusini ameikemea shambulizo na kuk**atwa kwa rais wa Venezuela Nicolas Maduro.

Rais Ramaphosa amesema Rais wa Muungano wa Amerika Donald Trump amekiuka kanuni za muungano wa Kimataifa.

Amesisitiza kuwa wizi wa rasilimali kupitia propaganda, na kuvunjwa kwa uhuru wa taifa la venezuela kunaacha mfano mbaya kwa mataifa mengine.

Timu ya Uingereza, Manchester united, yatarajiwa kumteua aliyekuwa mkufunzi wao wa Jadi Ole Gunnar Solsjaer. Ole gunnar ...
06/01/2026

Timu ya Uingereza, Manchester united, yatarajiwa kumteua aliyekuwa mkufunzi wao wa Jadi Ole Gunnar Solsjaer.

Ole gunnar alikuwa mkufunzi wa timu hiyo kuanzia mwaka wa 2018 hadi 2021alipoachishwa kazi. Hivi punde aliachishwa kazi na timu ya Besiktas baada ya msururu wa matokeo mabaya.

Akipewa kazi atamridhi Ruben Amorim aliyepigwa kalamu nyekundu baada ya kuzozana na mamlaka kuhusu mfumo wake wa uchezaji.

Siye twangoja tuone nani atachukua kiti hilo.

Timu ya Algeria imefuzu katika awamu ya robo finali baada ya kuipiga timu ya demokrasia ya Congo bao moja kwa nunge.Bao ...
06/01/2026

Timu ya Algeria imefuzu katika awamu ya robo finali baada ya kuipiga timu ya demokrasia ya Congo bao moja kwa nunge.

Bao hilo lilifungwa na Adil Boulbina katika dakika ya 119'.

Algeria itakutana na Nigeria ambayo iliiaibisha Mozambique kwa mabao manne mtungi hapo jana.

Wewe waona nani atafuzu kwa awamu ya nusu finali?

Kenya imeorodheshwa katika nafasi ya tatu kwa uzungumzaji wa kiingereza.Afrika kusini na zimbabwe zimeorodheshwa katika ...
06/01/2026

Kenya imeorodheshwa katika nafasi ya tatu kwa uzungumzaji wa kiingereza.

Afrika kusini na zimbabwe zimeorodheshwa katika nafasi ya kwanza na ya pili mtawalia.

Watumiaji mtandao wanausuka umuhimu wa kiingereza wakisisitiza kuwa nchi hizi zina lugha za kiafrika na hazifai zisifie kujua lugha za wakoloni

Mpepereshaji wa video wa marekani Ishowspeed amesema kuwa mpangilio wa kenya ni kutua mbunga ya wanyama.Amesema kuwa ana...
06/01/2026

Mpepereshaji wa video wa marekani Ishowspeed amesema kuwa mpangilio wa kenya ni kutua mbunga ya wanyama.

Amesema kuwa anatarajia Kenya itakuwa tofauti na Zimbabwe haswa kwa upungufu wa mimea na miti.

I ni baada ya Infuluensa wengi kwenye mitandao ya kijamii kujidai kuwa ni wao watakuwa wakimuongoza. I inaaenda tofauti sana na mipango yao na hivyo kuhakikishia watumiaji mitandao kuwa hao ni waongo na wanatafuta kiki na jina la ishowspeed.

Address

Kahawa Wendani
Nairobi

Telephone

+254113012736

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when 1009 Music posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to 1009 Music:

Share