Malindi show biz

Malindi show biz Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Malindi show biz, Art, Malindi.

πŸ”₯ Breaking News | Podcasts | Interviews | Gossip | Business Advaticement
πŸ“ž +254768482846πŸ“²
Whatsapp channel

https://whatsapp.com/channel/0029Vb89pXCAzNbwn8Yewp2v

πŸ—οΈ KITUO MAALUM CHA KULINDA HAKI ZA WATOTO KINAJENGWA MALINDIKila mtoto anastahili kusikilizwa, kulindwa na kutendewa kw...
26/06/2026

πŸ—οΈ KITUO MAALUM CHA KULINDA HAKI ZA WATOTO KINAJENGWA MALINDI

Kila mtoto anastahili kusikilizwa, kulindwa na kutendewa kwa heshima. Hili linawezekana kwa kuhakikisha kunakuwa na mazingira salama ambapo watoto wanaweza kueleza changamoto zao bila hofu.

Ujenzi unaoendelea wa Kitengo Maalum cha Kulinda Haki za Watoto (Child Protection Unit) katika Kituo cha Polisi cha Malindi, unaofadhiliwa kupitia Malindi NG-CDF, ni hatua muhimu katika kuimarisha huduma za ulinzi na usalama wa watoto katika eneo hili.

Kitengo hicho kitakuwa na mazingira rafiki kwa watoto, kikiwemo maktaba na ofisi maalum zitakazowezesha maafisa kushughulikia kwa haraka na kwa weledi kesi zinazohusu unyanyasaji, ukatili na unyonyaji wa watoto.

Mradi huu unalenga kuhakikisha watoto wanapata ulinzi, haki na msaada wanaostahili katika mazingira salama na yenye utu.

β€” Mheshimiwa Mbunge Hon. Amina Mnyazi - M.P Malindi
Malindi show biz

🚨 ZILIZOTUFIKIA HIVI PUNDE! πŸ˜₯Mwanaume huyu alinaswa jana mjini Malindi, eneo la Al-Noor Plaza karibu na Roundabout, akid...
26/06/2026

🚨 ZILIZOTUFIKIA HIVI PUNDE! πŸ˜₯

Mwanaume huyu alinaswa jana mjini Malindi, eneo la Al-Noor Plaza karibu na Roundabout, akidaiwa kupatikana akiwa na baiskeli ya muuzaji wa maziwa ambayo ilikuwa imevunjwavunjwa na ikisemekana alikuwa akiipeleka kuuzwa k**a chuma chakavu (scrap).

Kwa mujibu wa taarifa zilizotufikia, tukio hilo lilisababisha muuzaji wa maziwa kupoteza ajira yake, jambo lililoumiza wengi.

Wananchi wanahimizwa kutafuta riziki kwa njia halali na kuepuka vitendo vya wizi vinavyowaumiza wenzao.

Kumbuka: Mtu anayeshukiwa kwa kosa hubaki mshukiwa hadi pale mahak**a itakapothibitisha hatia yake.

Je, una maoni gani kuhusu ongezeko la visa vya wizi mjini Malindi? Tuambie kwenye maoni. πŸ‘‡
Malindi show biz

🚨 TAHADHARI KWA WANANCHI WA MALINDI!K**anda wa Polisi mjini Malindi, Moses Kosgei, amekanusha vikali uvumi unaosambaa ku...
26/06/2026

🚨 TAHADHARI KWA WANANCHI WA MALINDI!

K**anda wa Polisi mjini Malindi, Moses Kosgei, amekanusha vikali uvumi unaosambaa kuhusu madai ya wanaume kupoteza sehemu zao nyeti akisema taarifa hizo si za kweli.

Akizungumza kuhusu suala hilo, K**anda Kosgei amesema hakuna tukio lililoripotiwa na kuthibitishwa linalounga mkono madai hayo, na hivyo kuwataka wananchi kuacha kusambaza habari ambazo hazijathibitishwa.

Aidha, amesisitiza kuwa yeyote atakayebainika kueneza uvumi au taarifa za uongo zinazoweza kuzua hofu miongoni mwa wananchi atachukuliwa hatua za kisheria kwa mujibu wa sheria.

πŸ—£οΈ Wananchi wanahimizwa kupata taarifa kutoka vyanzo rasmi na kuepuka kusambaza uvumi unaoweza kupotosha umma au kusababisha taharuki.

Je, una maoni gani kuhusu hatua kali dhidi ya wanaoeneza taarifa za uongo? Tuambie kwenye sehemu ya maoni. πŸ‘‡
Malindi show biz

Ningependa kuweka jambo hili wazi.Baada ya kuchapisha taarifa kuhusu madai ya deni yaliyokuwa yakizungumzwa hadharani, n...
26/06/2026

Ningependa kuweka jambo hili wazi.

Baada ya kuchapisha taarifa kuhusu madai ya deni yaliyokuwa yakizungumzwa hadharani, nilipigiwa simu na Mheshimiwa Rose akinitaka niondoe chapisho hilo akidai linamuaibisha. Kwa heshima niliamua kuliondoa.

Baadaye nilipigiwa simu tena na Hon Rose wakinitishia kuwa wako katika ofisi za DCI Kilifi na nikatishiwa kuwa nisipoomba msamaha kupitia video, hatua zingechukuliwa dhidi yangu kupitia simu .

Nina heshimu taasisi zote za usalama, sio vyema na watu wote kulitumia jina la DCI au kutaka taasisi nyingine za serikali k**a njia ya kutisha au kushinikiza watu wanapokosa na ikiwa hakuna hatua rasmi zinazohusika.

K**a mwandishi wa habari Au content creator, nitaendelea kufanya kazi yangu kwa kuzingatia ukweli, ushahidi na maadili ya taaluma. Niko tayari kuwajibika pale ninapokosea, lakini staki kukubali mtu anitishie akitumia jina la taasisi za serikali zikihusishwa katika migogoro ya kibinafsi bila kuwajulisha.

Mwisho, kiongozi anapaswa kuwatumikia wananchi kwa uwazi, kutimiza ahadi walizotoa, na kujibu hoja kwa njia ya heshima na ukweli.

Asanteni.
Malindi show biz 360 Online Tv

🚨 TETESI ZAZUA MJADALA SABAKI BAADA YA KIFO CHA EVANS THETHE 😒Tetesi zimeibuka katika eneo la Sabaki baada ya baadhi ya ...
25/06/2026

🚨 TETESI ZAZUA MJADALA SABAKI BAADA YA KIFO CHA EVANS THETHE 😒

Tetesi zimeibuka katika eneo la Sabaki baada ya baadhi ya wanajamii kujadili kupitia makundi ya WhatsApp kuhusu madai kwamba marehemu Evans Thethe, ambaye ameaga dunia leo, alikuwa akimdai kiongozi wa Sabaki , Rose .

Kwa mujibu wa ujumbe unaosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, marehemu inadaiwa aliwahi kuwasilisha suala hilo kwenye kundi la WhatsApp siku chache zilizopita. Hata hivyo, hatua hiyo ilizua hisia tofauti ambapo baadhi ya wanakundi walikemea na kusuta kitendo hicho, huku wengine wakitoa maoni kwamba ikiwa kweli deni hilo lipo, lingefaa kulipwa ili kusaidia familia katika maandalizi ya mazishi.

Kwa sasa, madai hayo yameendelea kuzua mjadala mkubwa miongoni mwa wakazi wa Sabaki, huku wengi wakitaka ukweli wa suala hilo ubainishwe wazi ili kuondoa sintofahamu zinazozidi kusambaa mitandaoni.

❓ Je, wewe una maoni gani kuhusu suala hili? Unadhani madai k**a haya yanapaswa kujadiliwa hadharani baada ya kifo cha mtu, au ni vyema familia na wahusika wakayatatua kwa njia nyingine?
Cc: Coast Gossip club Habari za Tetesi

360 Online Tv

Huyu jamaa unaezasema alikua anasema Nini?πŸ˜…πŸ˜­πŸ˜­πŸ˜­
25/06/2026

Huyu jamaa unaezasema alikua anasema Nini?πŸ˜…πŸ˜­πŸ˜­πŸ˜­

Hii style huyu jamaa amechapwa Kwa miguu inaitwajeπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚????
25/06/2026

Hii style huyu jamaa amechapwa Kwa miguu inaitwajeπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚????

25/06/2026

Kanairo πŸ˜‚πŸ˜‚ unapelekwa kihuti ukiconectiwa direct to station πŸ˜‚πŸ˜‚
Niko hapa nyumbani Malindi watching liveπŸ˜‚

🚨 HABARI ZA HIVI PUNDEMwanaume anayejulikana kwa jina la Shee kutoka Ganda amefariki dunia baada ya kushambuliwa na wana...
25/06/2026

🚨 HABARI ZA HIVI PUNDE

Mwanaume anayejulikana kwa jina la Shee kutoka Ganda amefariki dunia baada ya kushambuliwa na wananchi wenye hasira katika eneo la Wananchi, Malindi, kwa tuhuma za wizi.

Polisi tayari wamefika eneo la tukio na kuuchukua mwili wake. Tukio hili ni la kusikitisha sana.

Wizi haufai. Vijana tujitahidi kutegemea jasho letu. πŸ•ŠοΈ Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.


Malindi show biz

25/06/2026

Nairobi kulikucha πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Malindi show biz

Address

Malindi

Telephone

+254768482846

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Malindi show biz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category