Gwiji wa Mashairi Kenya

Gwiji wa Mashairi Kenya Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Gwiji wa Mashairi Kenya, Poet, Eldoret.

TUWE WALEZI SIO WATESI.Watoto kwetu baraka, nawala sio laana,Hawafai kuteseka, au hata kuwakana,Kile wanacho kitaka, tuk...
19/05/2023

TUWE WALEZI SIO WATESI.
Watoto kwetu baraka, nawala sio laana,
Hawafai kuteseka, au hata kuwakana,
Kile wanacho kitaka, tukizingatie sana,
Tuweni kwao walezi, wala tusiwe watesi.

Kisha tusiwabague, misingi ya kijinsia,
Tena yapaswa tujue, si vyema kuwachukia,
Wakike tuwatambue, na wa kiume sawia,
Tuweni kwao walezi, wala tusiwe watesi.

Tuache kupendelea, tuwapeni haki sawa,
Tukome kuwaonea, nawala kutowagawa,
Hivyo nikuwakosea, majonzi hadi kujawa,
Tuweni kwao walezi, wala tusiwe watesi.

Wote tuwape upendo, tena uwe ni wa dhati,
Tofauti ziwe kando, mbele yao hatuteti,
Yawe mazuri matendo, Kisha kwa kila wakati,
Tuweni kwao walezi, wala tusiwe watesi.

Sikutaki!---------------------------------------Sikutaki,Waulize wajuao,Sikutaki,Hivyo wacha makisio,Sikutaki,Nakujuza h...
19/05/2023

Sikutaki!
---------------------------------------
Sikutaki,Waulize wajuao,
Sikutaki,Hivyo wacha makisio,
Sikutaki,Nakujuza hivyo leo,
Sikutaki,Mimi sili masalio!
-----------------------------------------------
Sikutaki,Hata najua mumeo,
Sikutaki,Asopitwa na viweo,
Sikutaki,Wewe kwake u pitio,
Sikutaki,Waulize wajuao!
-----------------------------------------------
Sikutaki,Sura k**a kipepeo,
Sikutaki,Rangi hizo upakao,
Sikutaki,Nani huyo atakao,
Sikutaki,Mla zake na wenzao!
----------------------------------------------
Sikutaki,Nina wengi wa chaguo,
Sikutaki,Nzuri sana sura zao,
Sikutaki,Wewe pia zako koo,
Sikutaki,Waulize wajuao!
-------------------------------------------------
Sikutaki,Nishafikia kituo,
Sikutaki,Sikutaki marudio,
Sikutaki,U kiumbe cha mgao,
Sikutaki,Wa mgao nenda nao!
-------------------------------------------------

NALISHWA VITU VITAMU.Nalishwa vitu vitamu, na tena vilivyo nona,Si eti ni vya msimu, wala vyakusumbuana,Salama havina su...
19/05/2023

NALISHWA VITU VITAMU.
Nalishwa vitu vitamu, na tena vilivyo nona,
Si eti ni vya msimu, wala vyakusumbuana,
Salama havina sumu, ndo mana navitafuna,
Si wa mama nitilie, au bandika bandua.

Mali yake nayasifu, hakika siyakinai,
K**a maji ya madafu, sikwamba ninajidai,
Nikitafuna minofu, utadhani ywazirai,
SI wa mama nitilie, au bandika bandua.

Chuchu zilivyo simama, huwa zanitekerenya,
Kwa nguvu huwa ywahema, ikiwa nazimumunya,
Nyundo kila ikizama, hunifungulia mwanya,
Si wa mama nitilie, au bandika bandua.

Kuna sehemu kifika, hunguruma k**a radi,
Kisha anatetemeka, nikipenyeza zaidi,
Kisawa namtandika, kana kwamba ni gaidi,
Si wa mama nitilie, au bandika bandua.

Mtunzi
Gwiji wa Mashairi
Eldoret Kenya

Address

Eldoret

Telephone

+254719402224

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Gwiji wa Mashairi Kenya posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to Gwiji wa Mashairi Kenya:

Share

Category