Simulizi Za Kusisimua Tz

Simulizi Za Kusisimua Tz It all about only stories. By Cleverley From Arusha

30/05/2019

Story: NISAMEHE
Contact us: 0659146373
Author: Cleverley
Sehemu ya 4
Ilipoishia sehemu ya 3;
Wakati mama John anainua simu kujaribu kumpigia mume wake, ghafla ilisikika mlio wa mlango mtu akiwa anagonga ikifuatiwa na sauti iliyo jawa na hofu.
“Hodi, nifungulie” hii ilikuwa sauti ya k**e
“Hee! Kuna nini mbona mbio hivyo?” aliuliza mama John baada ya kufungua mlango huku akiwa katika hali ya kutaharuki
“Umepata taarifa ya mumeo (Baba John)?” aliuliza mama huyo
“Hapana kuna nini? Nini kimetokea?” yalikuwa na maswali mawili yaliyofatana kutoka kwa mama John.
********************­****
Endelea………….
Asubuhi ya siku inayofata k**a kawaida kila mtu akiwa katika mihangaiko yake ya kujitafutia riziki lakini ilikuwa tofauti katika familia yake John ambao yeye pamoja na mama yake na mdogo wake walikuwa katika hospital ya kijiji kwaajili ya kumuona baba yao akiwa amelazwa.
Saa tatu kamili asubuhi ndio mda maalumu wa kuruhusiwa kuwaona wagonjwa, mama John na wanae waliruhusiwa kuingia wodini.
“Habari za asubuhi mume wangu” alisalimia mama John huku akiwa anatoa chupa kwenye mfuko
“Ah! Salama tu, mmeamkaje?” alijibu baba John na kuwatupia swali
“Shkamoo baba” walisalimia watoto kwa pamoja
“marahaba hamjambo” alijibu Baba John
“Hatujambo” walijibu watoto
“Enhe! Nini kilitokea” aliuliza mama John huku akikaa kitandani
“Dah! Wakati narudi jana usiku nilikutana na vibaka watatu ila mmoja sura yake siyo ngeni kwangu lakin sikumbuki wapi nlishawahi kumuona, wameniibia simu pesa na pia walinipiga k**a unavyoona wameniumiza mguu lakini namshukuru mungu naendelea vizuri kwa sasa japo daktari amesema nimepata hitilafu kidogo kwenye mfupa lakini haujavunjika kabisa” alisema baba John wakati huo watoto wake wakiwa katika utulivu na kwenye sura za kuonesha huruma kwa baba yao
“Pole, utakuwa sawa tu karibuni. Ngoja nikuwekee chai basi” alisema mama John huku akitoa kikombe katika mfuko na kumimina chai katika chupa.
Naam ulikuwa ni muda wa mapumziko, watoto walionekana baadhi wakicheza baadhi wakiwa kantini na wasiokuwa na hela walibaki darasani japo siyo kwa kupenda kwao. Steve k**a kawaida yake alikuwa uwanjani wakicheza mpira na wenzake ilisikika sauti ya k**e ikimuiita na alipogeuka alikuwa ni Vanessa.
“We nitafute baadae bana sasa hivi nacheza” alijibu Steve huku akiwa amegeuka kwaajili ya kurudi uwanjani lakini Vanessa alimuita tena,
“Njoo mara moja nikuulize basi” alijibu Vanessa kwa sauti kubwa na yenye ukali ndani yake
“Haya sema haraka haraka” alijibu Steve huku akijikung’uta suruali yake
“Wewe mwenzio (John) leo vipi mbona hajaja” aliuliza Vanessa
“Hata sijui maana leo sijapitia kwao, atakuwa kalala huyo maana ili mvua ya saa kumi na mbili siyo mchezo” alijibu Steve kimasihara
“Haha leo si utapitia kwao ukiwa unarudi nyumbani?” aliuliza Vanessa
“Nadhani” alijibu Steve
“Basi ukifika msalimie alafu mwambie akumbuke Ijumaa mechi aje” alisema Vanessa huku akigeuka kuondoka
“poaaaaaaaaaaa” alijibu Steve nae akigeuka ili kurudi uwanjani lakini muda ulikuwa umeenda na kengele ya kuashiria muda wa kurudi darasani ulikuwa umefika, kitendo hicho kilimfanya Steve akunje sura na kutoa sauti ya hasira.
Ilitimia Saa kumi na mbili jioni, Baba yake John aliruhusiwa kurudi nyumbani ila kwa masharti ya kutokuutumia mguu huo kwa kutembele ndani ya muda wa mwezi mmoja ndipo aanze mazoezi ya kuukanyagia chini.
“Itabidi tutafute baiskel ya kukufikisha nyumbani sisi tutakuja kwa miguu maana hela niliyonayo haitoshi kupanda gari” alisema mama John huku akimpungia mtu wa baiskel k**a ishara ya kumuita.
***********
Kengele iligongwa na kufanya wanafunzi wakimbie kuelekea eneo la matangazo(mstarini).
“Hamjambo” ilikuw sauti ya mwalimu Adamu mwalimu wa michezo
“Hatujambooo, shkamoo mwalimu” baadhi ya wanafunzi waliitikia na baadhi yao walikuwa kimya
“Natoa dakika kumi ya kufanya usafi kabla ya kengele ya pili kwaajili ya kukutana kuelekea uwanjani kwenye mechi na wageni wameshafika. Haya tawanyika isipokuwa wachezaji tuu ndo wabaki hapa”alisema mwalimu huyo na kufanya wanafunzi hao waanze kukimbia kuelekea sehemu zao za kufanya usafi
“Captain” aliita mwalimu Adamu baada ya kubaki na wachezaji tu
“Naam” alijibu Captain aliyefahamika kwa jina la Abduli
“Waongoze wenzako nilipokuelekeza alafu pitia jezi pale stoo mvae kabisa, mnisubiri nakuja” alisema mwalimu huyo na kuondoka.
Baada ya dakika 15 kengele ilipigwa tena na mda huu mwalimu aliwaamrisha wanafunzi watangulie uwanjani.
“haya kipa utakuwa wewe maana mwenzako leo hajaja” mwalimu wa michezo alianza kutoa namba za kucheza kwa wachezaji
“namba mbili, tatu, nne na tano wataongozwa na captain akifatia Juma, Khamisi na Hamadi” aliongezea mwalimu
“Upande wa kushoto na kulia ni James na Peter alafu viungo namba sita ni Kelvin na namba nane ni Joshua” alisema mwalimu huku waliotajwa wakianza kuchukua jezi
“Namba tisa na kumi ni Petro na Lucas wengine tutaanzia nje” alimaliza mwalimu na kusababisha Steve kucheka kuguna baada ya yeye na mwenzake John kutokutajwa katika kikosi kitachoanza.
Wachezaji walielekea uwanjani na kuwakuta timu pinzani wachezaji wa shule ya sekondari Manjangu wakiwa uwanjani wakipasha misuli yaani (warm up) na wao walianza kupasha misuli na kunyoosha viungo vyao kabla ya kipenga cha muamuzi wa mchezo huo kupulizwa mpira uanze. Wachezaji wa timu zote mbili walijipanga uwanjani tayari kwa kuanza mchezo huo.
“prrrrrrr” ilikuwa ni mlio wa filimbi ya muamuzi kuashiria mpira uanze na shule ya manjangu ndio walianzisha mpira huo ulioanza kwa kasi ya wachezaji wao, wachezaji wa timu ya manjangu wakionekana wako vizuri pia ukilinganisha na maumbo yao makubwa tofauti na wachezaji wa shule ya sekendari ya Mwanzini
Mpaka dakika ya arobaini na tano ya kipindi cha kwanza timu zote mbili zilichoshana nguvu kwa kutoka sare ya kutokufungana japokuwa timu wenyeji walionekana kutawaliwa kipindi cha kwanza.
“Poleni kwa mchezo, tuna mapungufu kwenye nafasi za ushambuliaji pia viungo mmepoteana na kusababisha kushambuliwa sana. Nitafanya mabadiliko kidogo kwenye nafasi ya ushambuliaji.” Aliongea mwalimu Adamu na kuwaruhusu kurudi uwanjani. Punde kipindi cha pili kilianza
Hamad!
Dakika ya sitini shule ya manjangu wanajipatia goli kutokana na mpira wa kona uliochongwa vizuri na kumkuta Bakari bila kuangalia goli aliutumbukiza nyavuni kwa kichwa maridadi. Mashabiki wa timu ya manjangu wanashangilia sana kwa goli hilo huku mashabiki wa timu ya Mwanzini wakiwa wanyonge ndani ya uwanja wao.
Dakika ya sabini na mbili timu zote zinafanya mabadiliko ya wachezaji huku timu wenyeji wakifanya mabadiliko ya wachezaji watatu kwa wakati mmoja wakiingiza washambuliaji wawili John na Steve pamoja na kiungo mmoja ambae Shabani mashabiki wa timu wenyeji walionekana kurudi kwa kushangilia baada ya mabadiloko hayo.
Inapigwa pasi maridadi kutoka kwa Steve inamkuta John ndani ya kumi na nane akibaki na kipa tu. “Prrrrrrrr” ni kipenga cha mwamuzi kuashiria ile ni penalt, ni baada ya John kuangushwa na golikipa baada ya kumpiga chenga, mashabiki wa Mwanzini wanaonekana kushangilia sana na penat inaenda kupigwa na Captain Abduli. Mwamuzi anaruhusu kwa filimbi penal ipigwe “Goooooooooooooal” ni kelele za mashabiki wa timu ya shule ya sekondari ya Mwanzin Abduli anaipatia timu yake bao la kusawazisha mnamo dakika ya themanini na tatu Mwanzin sekondari 1 na Manjangu sekondari 1.
Zimesalia dakika tatu mpira kuisha timu zote zikionekana kutawala mchezo kwa zamu, pasi inatoka kwake Petro inafika na kumkuta John, John anakokota mpira anapiga pasi inamkuta Steve “prrrrrr” Steve anachezewa madhambi karibu na penalt box inakua ni faulo kuelekea timu ya Manjangu zikiwa zimesalia sekunde kadhaa mpira kuisha. Anachukua John na kuutenga mpira kwaajili ya kupiga….. Mwamuzi anaruhusu mpira kupigwa na John anaupiga moja kwa moja “Goooooooooal” ni goli la pili kwa timu wenyeji linaloandikwa kupitia kwa mshambuliaji wao John, mashabiki wanaingia uwanjani kwa furaha.
Mpira unaekwa kati kwaajili ya kuanzishwa na hauchukui muda mwamuzi anamaliza mpira na timu wenyeji wanatoka na ushindi wa mabao mawili kwa moja dhidi ya timu ya Manjangu, John anaonekana akibebwa na wenzake juu juu kwa furaha.
“Hongera John” ilikuwa ni sauti ya Vanessa akimwambia John huku akimkumbatia kwa furaha kitendo hicho kilishuhudiwa na wanafunzi wengi, ilisikika sauti ikisema
“Nyie” sauti hiyo iliwafanya wawili hao kugeuka.
Je nini kitatokea? Kaa tayar kupata muendelezo usikose
********************­********************
Itaendelea...Kesho(I­jumaa)
Toa maoni yako kwa kucomment au katika namba hizi 0659146373
Nisaidie kushare ili na wengine wapate kuisoma, pia usiache kulike na kucomment ikiwa k**a support yako kwangu.
Like page yetu Simulizi Za Kusisimua Tz

30/05/2019

Habari wapendwa wa page hii. Napenda kuwataarifu saa kumi kamili Leo tutatoa muendelezo sehemu ya nne ya simulizi yetu ya NISAMEHE kaa tayari.
Ahsante

28/05/2019

Story: NISAMEHE
Contact us: 0659146373
Author: Cleverley
Sehemu ya 3
Ilipoishia sehemu ya 2;
“oh samahani” alisema Vanessa huku akitoa kitambaa katika sketi yake na kuanza kumfuta John mapajani katika suruali yake, kitendo hicho kilimfanya john abaki akimkodoloea macho Vanessa na kufanya wote wawili waangaliane hadi pale waliposhtushwa na sauti ikisema “Hamjambo?”.
********
Endelea na sehemu ya 3;
“Shkamo” John alisalimia huku akijitoa mikononi mwa Vanessa, “shkamo mama” Vanessa nae alisalimia huku akiangalia chini. “Marahaba, poleni na masomo” alijibu Mama Vanessa huku ak**eti chini “ahsante” walijibu kwa pamoja.
Mama Vanessa alielekea jikoni na kumuita Vanessa kwaajili ya kuandaa chakula cha mchana japokuwa muda ulikuwa umesogea sana, waliandaa chakula na kula pamoja. Baada ya chakula John aliaga na kuondoka kulekea nyumbani kwao.
“Ulikuwa wapi mda wote na nlikuambiaje kuhusu kumuacha mdogo wako mpaka anarudi nyumbani pekee yake? Umeanza tabia ya kuzurura kwenye nyumba za watu sio?” huyo alikuwa mam yake John akimuongelesha John baada yakufika nyumbani huku uso wake ukionesha Dhahiri kuwa kachukia “ samahani mama tulipitia uwanjani kulikuwa na mechi” alidanganya John huku akiangalia chini na alitambua endapo akisema kwel ingeweza kuwa shida kwake,
“Haya ndani upesi ubadilishe hizo nguo uje uende dukani” alijibu mama John huku akiendele kuwasha moto.
John aliingia ndani haraka akiwa mnyonge na baada ya dakika kadhaa alitoka akiwa kavaa nguo za nyumbani na kuagizwa na mama yake.
********************­**
Ikiwa imetimia majira ya saa mbili na nusu usiku, hali ya hewa ikiwa bado ya ubarid japokuwa mvua ilitulia kwa mda bila kunyesha.
“Acha kwanza taarifa ya habari iishe utaangalia hivyo vitu vyako” alisema mzee wa makamo akimwambia mwanae.
Alifahamika k**a Baba Frank lakini akizoeleka kwa jina la zimba, jina hili lilitokana na kipato chake pamoja na utajiri alio nao mzee huyo mwenye mtoto mmoja tu aliyeitwa Frank.
Familia ya mzee Frank inajumuishwa na mama pa moja na wafanyakazi wawili yaan house girl pamoja na dereva. Mzee Frank na mkewe walibahatika kupata mtoto mmoja tu ambae ndo huyo Frank na walimuonesha mapenzi yote na kumpa kila hitaji alilotaka na alilostahili.
Frank alikuwa anasoma kidato cha 3 katika shule ya st.August(ENGLISH MEDIUM) akiwa na miaka 17, kijana huyu alikuwa watofauti na baadhi ya vijana wengine kutokana na malezi anayoyapata kumpelekea kuwa na dharau inayomfanya ajione ni bora kuliko wengine na pia kuchaguwa marafiki walio katika usawa wake. Frank halikuwa na uwezo mkubwa darasani japo nae alijaaliwa kuwa na uwezo wa kucheza mpira, alikuwa mkorofi na mwenye kiburi ambacho kilifanya baadhi ya watoto wengine wamchukie.
“Haya njoo ule mwanangu, homework umeshamaliza?” mama Frank alikuwa akimwambia mwanae
“nimeshamaliza mamy” alijibu Frank kwa kudeka baada ya kunyimwa kubadili channel,
“We nae unadeka kitu kidogo ushavuta mdomo” mama Frank alimtania mwanae
“Dawa yake ni Boarding tu ili asahau tv maana kajiendekeza vibaya” alisema baba Frank
“muache mtoto ndo muda wake” mama Frank alimtete mwanae
“haya yangu macho” alisema baba Frank akiinuka kufata meza ya chakula ilipo,
“em, nenda kamuite kaka(dereva) chumbani kwake aje kula” mama John alimuagiza mwanae alieamka kwenye kochi kivivu. walijumuika pamoja katika chakula cha usiku.

Huku upande mwingine John akiwa anamsaidia mdogo wake kazi za darasani wakati huo wanasubiri chakula ambacho mama yao alikuwa bado anapika.
“Mama” aliita John
“Umeshamaliza kumsaidia mdogo wako?” lilikuwa swali badala ya kuitika k**a ilivyozoeleka kwa baadhi ya akina mama kuwa na tabia hiyo
“Ndio nimemaliza” alijibu John huku akivuta kigoda akae
“Baba yako mpaka sasa hivi hajafika kupatikana hapatikani kwenye simu sijui anashida gani?”
Aliongea mama John
“Mh tumsubiri, ila mama ninaombi” alisema John huku akimwangalia mama yake
“Usinambie tu habari ya hela” alisema mama John huku akikaa vizuri kumsikiliza mwanae
“ijumaa tuna mechi ya kirafiki ya shule kwahiyo nitaenda kucheza nadhani nitachelewa kurudi” alisema John
“Na mdogo wako” aliuliza mama John huku ukimwa ukitawala kwa dakika kadhaa bila John kujibu
“Atakuja kibandani kwako ili mrudi wote” alisema John
“Sawa sasa fanya hivi mkitoka tu shule utamleta alafu wewe urudi kwenye huo mchezo wako, sawa” alisema mama John
“Ndio nimekuelewa mama” alijibu John huku uso wake ukitawaliwa na tabasamu
Wakati mama John anainua simu kujaribu kumpigia mume wake, ghafla ilisikika mlio wa mlango mtu akiwa anagonga ikifuatiwa na sauti iliyo jawa na hofu.
“Hodi, nifungulie” hii ilikuwa sauti ya k**e
“Hee! Kuna nini mbona mbio hivyo?” aliuliza mama John baada ya kufungua mlango huku akiwa katika hali ya kutaharuki
“Umepata taarifa ya mumeo (Baba John)?” aliuliza mama huyo
“Hapana kuna nini? Nini kimetokea?” yalikuwa na maswali mawili yaliyofatana kutoka kwa mama John.
Je nini kimetokea? Kaa tayar kupata muendelezo
********************­********************
Itaendelea...Kesho(J­umaTano)
Toa maoni yako kwa kucomment au katika namba hizi 0659146373
Nisaidie kushare ili na wengine wapate kuisoma, pia usiache kulike na kucomment ikiwa k**a support yako kwangu.
Like page yetu Simulizi Za Kusisimua Tz

28/05/2019

Hello. Poleni kwa majukumu, napenda kuwataarifu kuwa ifikapo leo usiku tunatarajia kuendeleza story yetu ya NISAMEHE ambayo ilisimama kwa muda mrefu. Samahani kwa kuichelewesha na pia tutajitahid angalau kwa wiki tuitoe mara nne (JumaNne,JumaTano,Ijuma na Jumapili) mungu akipenda.
Tafadhali nisaidie kushare ujumbe huu na wengine wapate pia like na usiache kucomments maoni yako ni muhimu kwetu.
Ahsante
Mawasiliano: 0659146373

07/04/2018

Karibu katika page yetu ya Simulizi za Kusisimua Tz, napenda kuitambulisha story mpya itakayowajia hivi sasa hivi, support yenu inahitajika.

Story: CHOZI LENYE HATIA
Author : Glory
Contact : 0659146373

Sehemu ya kwanza....

Sitaki kuamini kwamba ipo siku dunia itatoa haki. Tangu nipate ufahamu sikuwahi kusikia matajiri wakinung’unika kwa kunyimwa haki, lakini watu walio wanyonge na masikini siku zote ndio wanaolia na kunung’unika kwa suala la kukandamizwa kunyimwa haki zao au kudhulumiwa.
Siwezi kusahau udhalimu uliobadilisha historia nzima ya maisha yangu. Ni vigumu kuelezea. Nilizaliwa katika mazingira na hali duni na mama asiyejulikana. Niliokotwa pembezoni mwa nyumba iliyokuwa ukiwa kwa miaka mingi nilipokuwa nimetelekezwa.

Niliokotwa na bibi mmoja aliyekuwa akiishi na Mume wake kwa miaka mingi bila kufanikiwa kupata mtoto. Walikuwa ni fukara tena waliojawa na simanzi kutokana na upweke waliokuwa nao.
Maisha yalikuwa magumu tena yasiyoelezeka. Ukizingatia nilikuwa mdogo sana, niliugua ghafla na kukatisha tamaa kutokana na kuwa sikuwahi kupatiwa chanjo yoyote tangu nilipozaliwa. Walezi wangu walihangaika huku na huko kuhakikisha napata nafuu. Kinachosikitisha zaidi na kutia huzuni ni kuwa hata lile eneo dogo walilokuwa nalo walinyang’anywa.
Babu yangu hakuwa na tegemezi lingine isipokuwa hicho kieneo kidogo tu alichonyang’anywa, alichokuwa akijihusisha nacho kwa kilimo ili kukidhi mahitaji madogomadogo ya nyumbani angalau kwa uchache.

Huu ni utangulizi wa story ya CHOZI LENYE HATIA

Itaendele.....
Please like, comments na share ili upate muendelezo na pia wengine waipate.

18/10/2017

Habari za usiku? Napenda kuwapa taarifa kesho simulizi ya NISAMEHE itaendelea. Samahani kwa kutokuitoa ila tulipata matatizo kidogo na pia nawakumbusha page hii ni mpya hivyo tunahitaji support yenu kwa kulike, comments na kushare ili wengine wasome. Na k**a unasimuliizi yako wasiliana nasi tutaipost katika page yetu .
Ahsante

16/10/2017

Story: NISAMEHE
contact us: 0683756035
Author : CJ1

Sehemu ya 2

Ilipoishia sehem ya 1.

"Jana nilisahau kuwapa mtihani yenu ya hesabu.... Hongereni" alisema Vanessa huku akiwapa mitihani yao huku Vanessa akimkazia macho John.
John alicheka huku na kumwambia Steven
"Nlisema lazima nikuongoze kwnye mathematics "
"Ah umenipita maksi tano tu, tisini na sita kwa tisini na moja zote ni A" alijibu Steven akiwafanya John na Vanessa kucheka.
"Vanessa umepata ngapi? " aliuliza Steven
"Tisini na nane" jibu hili la Vanessa liliwafanya Steven na John kugeuka mbele na mda huo mwl. wa English alikuwa akiingia darasani.

Endelea sehemu ya 2.

Baada ya mwalimu kuingia wanafunzi wote waliamka na kusalimia kwa pamoja k**a ilivyoada na kisha masomo yaliendelea k**a kawaida.

*****************************************-
"Fundi umenifanya nichelewe kwenda kazini kisa kiatu changu" alisema dada mmoja akimwambia mzee Jacob ambae mda huo alikuwa akipaka rangi viatu.
"Jana niliwahi kufunga kutokana na mvua ila kipo tayari unaweza kuchukua" alijibu mzee Jacob huku akimpa dada yule kiatu chake.
"Si ni elfu moja" dada yule alimuuliza mzee Jacob huku akiendelea kukitazama kiatu chake
"Hahahahaha nilikuambia elfu na mia tano, au umesahau? " mzee Jacob alijibu
"Ntakupitishia baadae hiyo mia tano" alijibu dada yule huku akimkabidhi mzee jacob noti ya elfu moja na kisha kuondoka.
"Ndo hivo bwana" alisema mzee mmoja aliekaa karibu na mzee Jacob
"Baadae itabidi nikafatilie mwenyewe maana yule kijana simuamini" alisema mzee Jacob huku akiendelea kupaka kiatu rangi
"Basi sawa ngoja niwahi kufungua duka, baadae tukutane pale kwenye kijiwe cha kahawa" alisema mzee yule huku akianza kupiga hatua akiondoka
"Sawa sawa" alijibu mzee Jacob.

Upande wa mama john alikuwa akiosha matunda na baadhi ya mboga kisha kupanga kwaajili ya kuuza. Biashara hii kwake aliizoea kwan aliona faida yake.
"Shkamoo, maembe hamna? " aliuliza binti mmoja na kumfanya mama John kuacha kazi zingine
"Yapo, ndo naosha. Unahitaji ya bei gani" aliuliza mama John huku akiosha maembe haraka haraka
"Nichagulie ya juice ya 300" alijibu binti huyo
"Naomba na ndizi za 1500,parachichi ya 2000 na nanasi moja" aliongezea binti huyo. Baada ya muda binti alikanidhiwa mfuko ulio na matunda
"Bei gani" aliuliza binti akitoa noti ya elfu kumi
"Elfu nane na mia tano" alijibu mama John
"Mama Sarah naomba tano mbili" mama John aliomba change kwa jirani yake.
" Hii hapa change, asante na karibu tena" alisema mama John huku akimpa binti yule change
"Haya asante" alijibu binti huyo huku akiondoka.

Baada ya vipindi vya asubuhi kuisha ulifika muda wa mapumziko, wanafunzi walitoka darasani kwaajili ya kwenda kunywa chai k**a ilivyo kawaida ya shule za sekondari.
"Chukua utaenda kumlipa" alisema Vanessa huku akimpatia John hela ya kwenda kumlipa yule muuza genge k**a walivyosema wao kuwa anawadai.
"Asante" alipokea John na kumshukuru Vanessa.
Baada ya Vanessa kuwaacha darasani Steven akamwambia John kwa shaulu kubwa
" Si unaona? Tatizo lako we muoga. Twende tukanunue chipsi. " alisema Steven
"Ila huon k**a ni vibaya kumdanganya mtoto wa watu na wakati hatudaiwi? " alijibu John
"Hana shida yule, we mwenyewe si unaona maisha yao yalivyo? Kila siku mwenzio anachukuliwa na baba ake na gari we mara ya mwisho kupanda gari si siku ile ya mechi. Acha uwoga" alisema Steven huku akiamka kwny dawatai. John nae aliamka na kutoka nje kwaajili ya mambo mengine.
Ni kweli Vanessa ni mtoto anaetoka katika maisha ya kitajiri akiwa k**a mtoto wa tatu na wa mwisho huku akiwa ametanguliwa na kaka pamoja na dada yake.
Vipindi viliendelea baada ya mapumziko, na kisha ikafika mda wa saa nane mchana ikiwa ni mda wa kutoka shule. Wanafunzi waligawanyika wengine alikuwa wakideki madarasa na vyoo, wengine wakipiga story na wengine wakicheza huku wote wakiwa na lengo la kusubiri kengele ya kwenda mstarini kusikiliza matangazo nabkisha kuondoka nyumbani.
John, Steven na wenzake walikuwa wakicheza mpira,
"Hivi huyu kaka anaitwaga nani?" Alikuliza msichana mmoja aliekuwa amekaa katika kundi la kina Vanessa wakiangalia watu wakicheza mpira kutokana na kuupenda kwao.
"Yupi? " alijibu mwingine
"Huyo, huyo aliefunga goli? " alijibu yule msichana na kumfanya Vanessa amwaangalie usoni na kumjibu
"Anaitwa John"
" Jamani nnavyompendaga" alisema yule msichana huku akitambasamu
"We nae, si unae yule sharobaro wako? " alijibu msichana mwingine
"Napenda mwaume wa namna hii yule kazubaa sana" alijibu huku akicheka.
Kengele ilisikika na kuwafanya wanafunzi wote wakimbie kuelekea mstarini.
Mwalimu wa matangazo alifika na kuwapa matangazo kesho wawahi na pia Ijumaa ya wiki hiyo kungekuwa na mechi baina ya shule yao pamoja na shule ya sekondari ya manjangu. Wanafunzi walishangilia baada y kusikia uwepo wa mechi maana wengi wao walipenda kuangalia na baadhi yao walikuwa wachezaji.
" Lazima niwafunge hata goli moja ili waache kujitamba " alisikika John akimwambia Steven
"Siku hiyo hatutaruhusu wapate goli ili waache majivuno" alijibu Steven
Ilionekana wawili hao ni wachezaji. Mara ghafla mvuli ilianza kunyesha na kumfanya mwalimu kuwaruhusu wanafunzi kwenda nyumbani. Walioishi karib na shule ilikuwa rahisi ila kwa wale wanaoishi mbali wengine walikaa kwnye kibaraza c ha nje ya shule na wengine wliingia darasan kukwepa mvua, Steven alitengana na John yeye alikuwa darasani wakati mwenzake alibaki kibarazani nje ya shule.
" pipiiiiiip" ilisikika honi ya gari lililopaki mbele ya kibaraza cha shule.
"Jamani kwaherini "aliaga Vanessa baada ya kuona ni baba yake ndo alikuwa akipiga honi. Alikimbia huku akiingia kwenye gari, lakini punde kioo cha gari kilifunguliwa
"John" aliita Vanessa
John aliekuwa kajikunyata kwa baridi aligeuka kichovu na kumuona Vanessa akimpa ishara ya kwenda kwenye gari, bila kuchelewa alikimbia na kuingia ndani ya gari.
"Hujambo John" alisema mzee yle wa makamo na kumfanya John ajiulize kajulia wapi jina lake, alisahau kuwa Vanessa mda mfupi uliopita alimuita kwa saut na ingekuwa rahisi mzee huyo kulijua jina lake.
"Sijambo shkamoo" alijibu John huku akimuangalia Vanessa na kupokelewa na tabasamu kutoka kwa binti huyo mrembo.
"Itabidi tuende nyumbani kisha baadae mvua ikiacha ndo uende nyumbani maana hiyo njia ya kwenda kwenu kuna maji mengi gari haliwezi kupita na pia huwezi kupita kwa miguu maana mvua itakunyeshea" alisema mzee yule akimwambia John. Vanessa alionekana kufurahishwa na kitendo kile kwan alitabasamu na kumnyooshea John kidole gumba.

Baada ya dakika tano gari lilikuwa mbele ya geti la jumba la kifahari na kumfanya John kuchungulia kwa dirishani. Alibaki kuduwaa maana nyumba k**a hizo aliziona katika movie na leo kwa mara ya kwanza anaingia ndani.
"Karibu ndani" Vanessa alikuwa akimkaribisha John ndani. Waliongozana hadi sebuleni ambapo palipambwa kwa makochi mazuri ukijumlisha na tv iliyomfanya John aishangae kwani kwao haikuwepo. Baba yake Vanessa aliingia chumbani na Vanessa aliingia jikoni akatoka na juice kwenye kikombe na kumkabidhi John ila wakati John anapokea ilimwagika kidogo katika mapaja yake.
"Oh samahani" alisema Vanessa huku akitoa kitambaa katika sketi yake ya shule nakuanza kumfuta John mapajani kwenye suruali, kitendo kile kilimfanya John kubaki kumkodolea macho Vanessa na kuwafanya wote wawili waangaliane hadi pale waliposhtushwa na sauti ikisema
"Hamjambo? " ilikuwa ni sauti ya mama yake Vanessa.

Itaendelea...

Nisaidie kushare ili na wengine wapate kuisoma, pia usiache kulike na kucomment ikiwa k**a support yako kwangu.

Like page yetu Simulizi Za Kusisimua Tz

15/10/2017

Vp wadau? Story ya Nisamehe mpo tayar niachie sehem ifuatayo? Toa comments au like nijue tupo pamoja

Toa utabiri wako katika mechi hii leo saa nane na nusu.  Liverpool FC vs Manchester United
14/10/2017

Toa utabiri wako katika mechi hii leo saa nane na nusu.
Liverpool FC vs Manchester United

13/10/2017

Story: NISAMEHE
Contact us: On Simulizi za kusisimua Tz
Author : CJ1

Sehemu ya 1.

Mvua kiasi ilikuwa inanyesha ikiambatana na barid kali wakati huo wa asubuhi ya jumatatu ya tarehe 25 mwezi wa 6 mwaka 1985. Wapo walioamka kuendelea na majukumu yao ya kila siku wakiwemo wanafunzi na pia walikuwepo ambao bado walikuwa wakizidi kuvuta mashuka yao kitandani ili kujikinga na baridi hiyo.
"John amka, mwamshe na mdogo wako sasa ni muda wa kwenda shule. "Ilikuwa sauti ya mwanamke mmoja akiwaamsha wanae kwaajili ya kwenda shule.
John ni mtoto wa kwanza akiwa na miaka 16 katika familia ya mzee Jacob wakiwa watoto wawili katika familia hiyo akiwepo mdogo wake Fabian mwenye miaka 14. Familia hiyo ikijumuishwa na wazazi wote wawili ilikuwa familia ya aman na pia yenye furah na kuridhika kwa kile walichokipata. Japo kuwa maisha yao yalikuwa duni lakini mungu aliwapa upendo na ndicho kicho ifanya familia hyo isiwe na kutokuelewana.
Walikutana mezani kwa pamoja ili kupata kifungua kinywa, wakati huo John alikuwa akisoma shule ya secondari mwanzini akiwa kidato cha pili huku mdogo wake akiwa darasa la saba katika shule ya msingi luanga. Mzee Jacob alikuwa fundi viatu na utengenezaji wa baiskel huku mke wake Bi. Maria ama mama John k**a alivyozoeleka kwa jina hilo mitaan yeye alihusika na biasha ya kuuza matunda na mboga sokoni.
"Jitahidin kusoma, John mfundishe mdogo wako endapo utapopata mda si unajua ndo anakaribia kumaliza? Sitaki kuona anakaa nyumbani kwa kufeli na pia sitaki wanangu mje kufanya kazi nnayofanya mimi. " aliongea mzee Jacob ikiwa k**a husia kwa wanae. Ni kwel aliwapenda sana.
"Hilo halina shida hatutowaangusha wazazi wetu" alisema John huku alikwa anavaa begi mgongoni kwaajili ya kuondoka.
"Msubiri mdogo wako muende pamoja si unajua mwamvuli upo mmoja tu. " alisema mama John, mwanamke mkarimu sana kwa mume wake akiwa na miaka 45 nyuma miaka mitano ya mumewe.
Muda wa kuondoka uliwadia huku kukiwa na manyunyu, John aliongozana na mdogo wake maana shule zao zilikuwa karibu na kisha kila mmoja akifuata geti la shule yake.
"Dogo simama" alisema kijana mmoja aliekuwa nyuma ya John.
"Hahahahaha aisee sijapata kuona mtu muoga kawa wewe" alijibu John baada ya kugeuka na kumuona aliekuwa akimuita, huyu ni Steven rafiki mkubwa kwa John maana waliishi pia mtaa mmoja.
"Muoga hafi mapema sasa wewe jifanye jasiri uone" alisema Steven huku kwa pamoja wote wakicheka.
Waliongozana hadi darasani na kuweka mabegi yao na kwenda mstarini kwaajili ya kusikiliza matangazo, na baada ya dakika 15 walikuwa darasani kwaajili ya kusubiri vipindi vianze.
John na Steven walikaa dawati mmoja darasani na hicho ndo kiliwafanya wawekaribu mda mwingi.
"John? " aliita binti wa miaka 15 aliekaa dawa la nyuma alilokaa John .
"Ahh! Mambo Vanessa" alisema John huku akijikuna kichwa kutokana na aibu aliyokuwa nayo kwa wanawake, wakati huo Steven alikuwa akimfinya John kwa chini ikiwa k**a ishara wanayoijua wao.
"Poa, mbona jana mlikuwa mnamkimbia yule muuza genge? " aliuliza Vanessa.
John alionekana akibabaika lakini Steven akadakia. "Alikuwa anatudai tu"
"Siyo vizuri kumkimbia, shingapi anawadai? " aliuliza tena Vanessa
"Mia mbili tu" alijibu John kwa aibu.
"Basi unikumbushe baadae break nikupe" alisema Vanessa huku akitoa karatasi kwenye begi lake.
"Jana nilisahau kuwapa mtihani yenu ya hesabu.... Hongereni" alisema Vanessa huku akiwapa mitihani yao huku Vanessa akimkazia macho John.
John alicheka huku na kumwambia Steven
"Nlisema lazima nikuongoze kwnye mathematics "
"Ah umenipita maksi tano tu, tisini na sita kwa tisini na moja zote ni A" alijibu Steven akiwafanya John na Vanessa kucheka.
"Vanessa umepata ngapi? " aliuliza Steven
"Tisini na nane" jibu hili la Vanessa liliwafanya Steven na John kugeuka mbele na mda huo mwl. wa English alikuwa akiingia darasani.

Itaendelea...
Huo ni utangulizi wa simulizi hii ya NISAMEHE.
Like na kucomment k**a kuna mapungufu au ushauri kwa mwandishi, pia usisahau kushare ili na wengine wasome.
Onyesha support yako.

12/10/2017

Karibu katika simulizi za kusisimua kupitia kwa mtunzi wenu. Page hii ni mpya hivyo soon mtapata simulizi za kweli katika maisha na za kusisimua. Support yako inahitajika ili kutimiza malengo yetu. Ahsante

Address

Liverpool

Telephone

0659146373

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Simulizi Za Kusisimua Tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category