31/07/2021
🙏🏽🙏🏽 FARHAN M KIHAMU] ..Hivi sasa ni saa 3:53 Usiku kwa saa za Afrika Mashariki, nikiwa hapa mizani ya Mikese Mji kasoro Bahari Morogoro njiani kurejea Jiji la Lawama
Pembeni yangu namuona Mama mmoja na mtoto mmoja mgongoni na mmoja kamshika mkono, kichwani ana sinia la machungwa, hawafanyi biashara kujenga bali tu kupata kula yao ya siku
Kwenye fikra zangu yupo yule Kaka na Dada yangu aliehitimu UDSM, UDOM au SUA! Ni mwaka wa tano sasa, amebadili sana bahasha, ameandika sana proporsal ila "samahani hatuna kazi" imekuwa ringtone kwake
Kwenye maombi yupo yule Kijana mdogo mwenye ndoto kubwa! Ila kila akibisha hodi maofisini anaulizwa k**a ana uzoefu na kazi, ataupatia wapi k**a kila mlango unafungwa? Kila siku ni afadhali ya jana
Nipo pamoja nawe uliesoma kwa kuunga unga, wazazi waliuza kila kitu, wakiamini siku unahitimu ni mwanzo wa historia mpya ya maisha yao, ila hawakujua ndio mwanzo wa stress mpya za maisha yao, ngumu kila sehemu
Nasema nawe pia Mwanangu wa bodaboda! Boss anataka kipande chake ila bado umelipa faini, abiria hawapatikani kila kitu ngumu, Mchumba nyumbani anataka chips kuku na pesa ya saloon
Nasema nawe Mwanangu unaepambania penzi kwa gharama yoyote, Mchumba anataka iPhone wewe una Infinix, Mchumba anataka lunch Samaki Samaki wewe unaishi kwa pass ndefu, life is not fair
Unajitahidi kujikwamua, umechora proposal zako za kiharakati unampa Boss akuvute ila blue tick zimesoma na Boss kakuzimia simu na kesho unaikuta inatumika, komaa na jikaze dunia sio yetu
Nasema nawe Mwanangu wa chini ya dollar moja, Kaka, Dada, Baba na Mama! Popote ulipo endelea kuamini kwenye kesho yako! In Africa we are not living we are surviving 💪
Mungu awape wepesi wana wa Adamu, k**a bado tuko hai basi hakuna Uchawi
🎶Faraja nakuita Faraja, upo wapi Faraja🎶
credit: FARHAN M KIHAMU]