Shauri

Shauri Shauri

Amani ya kisiasa ni nguzo ya maendeleo ya taifa.Tofauti za kisiasa ni sehemu ya demokrasia, lakini hazipaswi kuwa chanzo...
18/12/2025

Amani ya kisiasa ni nguzo ya maendeleo ya taifa.
Tofauti za kisiasa ni sehemu ya demokrasia, lakini hazipaswi kuwa chanzo cha migawanyiko au vurugu. Kujenga amani kunahitaji viongozi na wananchi kuheshimu sheria, kukubali maoni tofauti, na kuweka maslahi ya taifa mbele ya maslahi binafsi au ya vyama. Bila amani ya kisiasa, haki, maendeleo na umoja wa kitaifa haviwezi kudumu.

Hii ndio Kampuni iliokua ikiuza na kusambaza mafuta miaka ya nyuma, hadi kufikia watu kuita jina la SHELL kila kituo cha...
10/12/2025

Hii ndio Kampuni iliokua ikiuza na kusambaza mafuta miaka ya nyuma, hadi kufikia watu kuita jina la SHELL kila kituo cha mafuta hapa Tanzania.
Ukweli kwamba sio kila kituo cha mafuta kinaitwa SHELL bali ni mazoea tulio zoea.
Kwasasa mtu akikwambia nipo shell ana maanisha yupo petrol station (kituo cha kuuzia mafuta ya magari

09/12/2025
28/08/2025

😁😘

MLANGONI KWA BABA YAGA – Sehemu ya Tatu: WalioitwaNilipoanza kuota tena, sikushangaa.Ndoto zilirudi polepole, k**a moshi...
07/04/2025

MLANGONI KWA BABA YAGA – Sehemu ya Tatu: Walioitwa

Nilipoanza kuota tena, sikushangaa.

Ndoto zilirudi polepole, k**a moshi wa uvumba unaozunguka kichwa chako mpaka huwezi tena kutofautisha kati ya hewa na kiini. Sauti ya Baba Yaga haikusema maneno, bali iliniacha na alama—mfumo wa hisia, ukumbusho wa giza, na mwanga mdogo unaokuongoza kuupitia.

> “Wapo wengine,” sauti ilinong’ona. “Waliopaswa kuona.”

Nilianza kuwaona.

Watoto k**a mimi. Walionyanyaswa kimya kimya. Waliosahaulika na dunia lakini si na msitu. Mmoja wao aliishi karibu na sokoni—mvulana aliyeficha michubuko ya nyumbani chini ya tabasamu. Mwingine alikuwa msichana aliyekuwa akizungumza na mawe; watu walimwita mwendawazimu. Lakini mimi niliona—mawe yalikuwa yanajibu.

Sikutumia nguvu. Sikutisha. Nilikaa nao, nilisikiliza. Na kisha nilisema:

> “Unakumbuka ndoto zako za usiku? Zile ulizokuwa huwaambii mtu? Ni milango. Ukiwa tayari, itafunguka.”

Walipoingia, walirudi wakiwa kimya. Lakini kimya tofauti na cha maumivu—kimya cha kuelewa.

Tulipoanza kuwa wengi, tuliitwa majina: Watoto wa uchawi, waletaji giza, waliochukuliwa. Lakini hatukujali. Tulikuwa tunajifunza kuona ulimwengu kwa macho mapya. Na zaidi ya hayo—tulikuwa tukijifunza kuubadilisha.

Lakini usiku mmoja, niliona moto msituni. Sauti ya Baba Yaga haikunong’ona tu—ililia. Nilijua maana yake.

> Mtu ameingia bila mwaliko. Na hajaja kujifunza. Ameleta sumu.

Ndoto zangu zikabadilika—zikawa kali. Kila aliyegusa nyumba ya Baba Yaga bila nia safi, hakurudi vile alivyoenda. Lakini sasa… mtu huyu alitaka kuvunja mlango.

Kwa mara ya kwanza, niliogopa.

---

Mwisho wa Sehemu ya Tatu

MLANGONI KWA BABA YAGA – Sehemu ya Pili: Macho ya MosiBaada ya kutoka kwenye nyumba ya miguu ya chuma, Mosi hakuwa yule ...
06/04/2025

MLANGONI KWA BABA YAGA – Sehemu ya Pili: Macho ya Mosi

Baada ya kutoka kwenye nyumba ya miguu ya chuma, Mosi hakuwa yule mtoto yule aliyepotea.

Aliwaona watu wakiwa na ngozi za mwili, lakini ndani yao walitembea kivuli—hofu, hasira, tamaa. Aliweza kusikia sauti ambazo watu wengine hawawezi: sauti za miti, vilio vya majivu, na nyimbo zilizopotea katika vumbi la historia.

Alikuwa kimya. Si kwa sababu hakuwa na maneno, bali kwa sababu alijifunza kwamba maneno ni vitu hatari—yanaweza kutengeneza au kuharibu dunia nzima.

Wakiwa wamehama Bwela, Amina alijaribu kumrudisha Mosi kwenye maisha ya kawaida: shule mpya, majirani wapya, chakula kizuri. Lakini kila usiku, Mosi alisimama mlangoni, akitazama msituni, k**a anasubiri kitu. Au mtu.

“Mama,” alisema kwa mara ya kwanza baada ya miezi miwili. “Je, watu wakubwa huwa wanajua wanachofanya?”

Amina alimtazama, machozi yakimjaa. “Sio kila wakati, mwanangu.”

Mosi akatikisa kichwa. “Baba Yaga alisema nimerudi nikiwa na zawadi ya kuona. Lakini pia ni laana. Kwa sababu sasa siwezi kupuuza ukweli.”

Aliwaona walimu wake wakitumia maneno k**a silaha. Aliwaona viongozi wakila zaidi ya walichotenda. Aliwaona watoto wakiugua roho kwa sababu ya chuki, kutoeleweka, na upweke.

Siku moja, alimuuliza mama yake, “Naweza kurudi kwa Baba Yaga?”

Amina alishtuka. “Kwa nini?”

Mosi alitabasamu kwa uchungu. “Kwa sababu nafikiri watu wengine wanahitaji kufundishwa — si kwa maneno, bali kwa safari k**a yangu.”

---

Mwisho wa Sehemu ya Pili

MLANGONI KWA BABA YAGAKatika mtaa wa Bwela Mtoni, kulikuwa na fumbo lililowatesa wakazi wake. Watoto walikuwa wakipotea,...
06/04/2025

MLANGONI KWA BABA YAGA

Katika mtaa wa Bwela Mtoni, kulikuwa na fumbo lililowatesa wakazi wake. Watoto walikuwa wakipotea, mmoja baada ya mwingine, kana kwamba hewa ya usiku ilikuwa inawameza kimyakimya. Hakukuwa na mlio, wala alama ya kuvunjwa kwa mlango—ni k**a walikuwa wakitoweka na dunia ikawa kimya.

Amina, mama wa mtoto mmoja aitwaye Mosi, alikuwa mmoja wa walioteseka. Mosi alianza kuota ndoto za ajabu:
“Anakuja mama mzee mwenye macho mekundu… anatembea juu ya sufuria inayoelea juu ya ardhi. Ana nyumba yenye miguu... k**a kuku.”

Amina alikumbuka hadithi ya bibi yake kuhusu Mama wa Milango—kiumbe aliyeishi msituni zamani, anayewachukua watoto ambao mioyo yao imechafuliwa na uovu au hofu. Hakuwahi kuamini, hadi usiku huo Mosi alipoweka viatu vyake nje ya mlango... na asubuhi akawa hayupo.

Kila mtu alikata tamaa. Polisi walishindwa. Wachawi wa mitaa walikaa kimya. Lakini Amina hakuweza kukubali. Alifuata ndoto za Mosi, zikimpeleka hadi pembezoni mwa msitu wa zamani, ambapo watu hawatembei tena.

Ndani ya ukungu mnene, aliona nyumba yenye miguu ya chuma ikining’inia juu ya dunia. Milango yake ilifunguka yenyewe, na sauti ya mzee ikaita:
“Karibu, mama wa mtoto mchafu.”

Amina aliingia, moyo ukidunda. Ndani, alikuta bibi mzee aliyevaa shungi iliyochakaa, macho yaking’aa kwa mwangaza mwekundu.
“Hukumu iko mikononi mwako,” Baba Yaga alisema. “Ni nani anastahili kuishi: mtoto, au dunia iliyomharibu?”

Katika majaribio ya kiroho yaliyojaza giza, Amina alilazimika kukumbuka ukweli wa maisha yake, makosa yake, na hali ya jamii. Alilia, akakiri, akaomba.

Hatimaye, nyumba ikatetemeka, na mlango wa nyuma ukafunguka. Mosi alitoka, akiwa mzima, lakini kimya — macho yake yaliona zaidi ya dunia ya kawaida.

Tangu siku hiyo, Amina na Mosi walihama Bwela. Lakini kila mwezi, Amina humpeleka msituni, kwa kimya. Sio kwa woga — bali kwa heshima.

Kwa sababu wale wanaojua, wanajua: Baba Yaga yupo. Na si kila mtoto hupotea — wengine hufundishwa.

Hiyo ndo P2 bhn 😀 kipenzi cha wadada ila majuto kwa baadhi ya wengi wa wanandoaKuna madhara yoyote yamekupata baada ya k...
19/03/2024

Hiyo ndo P2 bhn 😀 kipenzi cha wadada ila majuto kwa baadhi ya wengi wa wanandoa

Kuna madhara yoyote yamekupata baada ya kutumia vidonge vya p2...! Leo napenda nikupe somo kidogo

Sio wote hupata madhara ila baadhi yetu hivi vidonge vya dharura vya kuzuia mimba huja na mirejesho tofauti ndani ya miili yetu

Mfano, baadhi yetu huanza ku-exprience hali ya uchovu, kichefuchefu, maumivu ya nyonga, kizunguzungu, kuwahi kupata hedhi kabla ya wakati au hedhi kuchelewa kutoka, kutapika, kutoka jasho n.k hii ni kwa sababu p2 huachia dutu ambazo huenda kuvuruga mpangilio wa homoni za mwanamke, kuua mbegu za mwanaume na kuharibu mazingira ya uwezekano wa mimba kutungwa

Kuitumia kwa mara moja sio mbaya ila kuendekeza matumizi ya p2 mara kwa mara inaweza kupelekea tatizo sugu la mvurugiko wa homoni (homoni imbalansi) hiyo ikawa ndo mwanzo wa hedhi yako kuvurugika, kuwa na uchi mkavu, kukosa hisia, kukosa ute wa uzazi, mayai yako kusinyaa na kupelekea kushindwa kupevuka na kuwa mwanzo wa kutafuta mimba bila mafanikio au changamoto nyinginezo za uzazi

Kitaalam unashauriwa USIMEZE p2 zaidi ya mara mbili ndani ya mwaka mmoja (kwa usalama wa afya yako ya uzazi) sasa wale ndugu zetu ambao kila mkisex mnakimbilia p2 chukueni tahadhari, usiharibu kizazi chako kwa starehe ya muda mfupi

Nakukumbusha mambo muhimu hapa

• Hakikisha umekula na kushiba kabla hujameza p2

• Usimeze p2 k**a kuna uwezekano wa tumia kondomu

• Siku moja baada ya kumeza p2 jitahidi sana kupata vyakula vya kijani yaani hapa namaanisha tango, bamia, mboga za majani aina zote, brocolli pamoja na matunda kila siku walau kwa siku 7, hii itakusaidia mwili kurekebisha kiwango cha homoni zilizoshushwa na p2

• Ni muhimu kunywa maji mengi baada ya kumeza p2

• Ni muhimu kuwa mpenzi wa chai ya Tangawizi kali, mdalasini, iliki na mchaichai kwa wingi au Unaweza kutengeneza juisi ya ndizi mbivu na kunywa glass moja kila siku k**a unahisi p2 inakupa kichefuchefu, uchovu, kizunguzungu n.k

• K**a p2 imesababisha hedhi yako k

Maisha ya mwanaume duniani bila hela ni sawa na jehanamu. Mimi sijui kwa wengine, lakini kuishi duniani kwa mwanaume bil...
06/02/2024

Maisha ya mwanaume duniani bila hela ni sawa na jehanamu.

Mimi sijui kwa wengine, lakini kuishi duniani kwa mwanaume bila hela hata upendwe vipi na mwanamke mwenye pesa, kuna mateso ya kiume lazima uyapate. K**a una ego ya mwanaume huwezi kuishi kwa raha na mke, au girlfriend anayekulisha ...kuna maumivu makali sana ya kiume unless k**a akili za kichwani zimefeli . Wale wanaopitia maumivu hayo kwa muda wanaweza kusamehewa.

Ngoja nikuambie ukweli wapo binadamu wawili wanaoweza kupendwa bila sababu yaani with unconditional love:
# Mwanamke .
# Mtoto
Mwanaume anapendwa k**a ni provider. Mwanaume anapendwa k**a anahudumia. Mwanaume anapendwa k**a anasimamia.

Mwanaume asiye na uwezo wa kulea familia or kuhudumia hakuna upendo. Lazima uwe provider ili upendwe.
Fuatilia familia ambazo baba hakujipanga hata watoto wake wanamdharau.Ninaijua familia ambayo baba alitumia sana hela enzi za ujana akastaafu na kuishia kuwa na nyumba, mama akapambana watoto wakasoma na kuendelea…
Mama anaweza kuwapigia simu wanae na kuwaambia “baba yenu naona haeleweki. Naona anacheka na mama Joy, jirani”
Mtoto wa k**e anapiga simu na kumtukana baba yake “Baba acha tabia chafu. Hujachoka?”
Imagine. Baba anaomba msamaha. Hana sauti na hana ujasiri.
Ngoja nikupe mfano hapa;
Mwanaume ukipata mpenzi wa k**e swali gani la kwanza utaulizwa:
"Ni mzuri eeh? Tuone picha yake?"
Lakini Mwanamke ukipata mpenzi wa kiume swali gani la kwanza unaulizwa
"Anafanya kazi gani? "
Mambo ya sura yanafuata baadaye, kwanza wanataka kujua kipato chake.

Ukitaka kuishi kwa mateso duniani hasa wewe mwanaume lala usiwe na hela.
Imagine mwanaume unaachwa kwasababu huwezi kuhudumia unakimbilia kutafuta mwanamke mwingine utaachwa tena na tena mpaka ukumbuke kuwa hela ni kipaumbele.

Tafuta hela.
Kuwa addicted na ndoto kubwa.
Kuwa addicted na maisha makubwa.
Pigana kufa na kupona upate hela.
Imagine una mke na watoto halafu huna hela? Unless iwe ni temporary na mke ana matarajio

Know your worthWhen someone treats you like you're just one of many options, help them narrow their choice by removing y...
04/03/2023

Know your worth

When someone treats you like you're just one of many options, help them narrow their choice by removing yourself from the equation. Sometimes you have to try not to care, no matter how much you do. Because sometimes you can mean almost nothing to someone who means so much to you. It's not pride - it's self respect. Don't give part-time people a full-time position in your life. Know your value & what you have to offer, and never settle for anything less than what you deserve.

Love me or hate me All are the same Cause I don't have a heart n mind that gives a s**t about you anymore.
04/03/2023

Love me or hate me All are the same Cause I don't have a heart n mind that gives a s**t about you anymore.

Address

Tanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Shauri posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to Shauri:

Share