Coprol

Coprol Digital creator

Mamlaka za afya nchini Ufaransa zimesema watu 5,764 wamefariki dunia kutokana na athari za wimbi kubwa la joto lililoiku...
23/07/2026

Mamlaka za afya nchini Ufaransa zimesema watu 5,764 wamefariki dunia kutokana na athari za wimbi kubwa la joto lililoikumba nchi hiyo huku vifo hivyo vikirekodiwa kati ya Juni 17 na Julai 2 mwaka huu.

Joto hilo limeathiri maeneo mbalimbali na kuongeza hatari kwa makundi yenye afya dhaifu hasa wazee na wenye magonjwa sugu.

Wataalamu wa hali ya hewa wanasema kuongezeka kwa mawimbi ya joto na matukio mengine ya hali mbaya ya hewa kunachangiwa kwa kiasi kikubwa na shughuli za binadamu, hususan uzalishaji wa gesi chafuzi unaochochea mabadiliko ya tabianchi.

Wamezitaka nchi kuimarisha hatua za kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa na kujiandaa zaidi kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Marekani na Saudi Arabia zimesaini makubaliano ya ushirikiano wa nyuklia yatakayowezesha Marekani kutoa teknolojia na ut...
23/07/2026

Marekani na Saudi Arabia zimesaini makubaliano ya ushirikiano wa nyuklia yatakayowezesha Marekani kutoa teknolojia na utaalamu wa kusaidia maendeleo ya mpango wa nyuklia wa Saudi Arabia.

Hata hivyo makubaliano hayo yamezua mjadala kutokana na hofu kwamba uwezo wa kurutubisha uranium unaweza baadaye kutumika kutengeneza silaha za nyuklia.

Kwa mujibu wa makubaliano hayo Saudi Arabia haitaruhusiwa kuendeleza au kununua teknolojia yake ya kurutubisha uranium kwa kipindi cha miaka 10.

Badala yake iwapo shughuli za urutubishaji zitaonekana kuwa na manufaa ya kibiashara kituo hicho kitajengwa na Wamarekani bila kuhamisha teknolojia nyeti kwa Saudi Arabia.

Waziri wa Nishati wa Marekani Chris Wright amesema makubaliano hayo yanazingatia viwango vya juu vya usalama wa nyuklia na kuzuia kuenea kwa silaha za nyuklia.

Rais Samia Suluhu Hassan amesema nchi za Afrika zinapaswa kuongeza uwekezaji wa ndani katika sekta ya afya ili kuhakikis...
22/07/2026

Rais Samia Suluhu Hassan amesema nchi za Afrika zinapaswa kuongeza uwekezaji wa ndani katika sekta ya afya ili kuhakikisha huduma za afya zinawafikia wananchi wote kutokomeza UKIMWI, kuboresha afya ya uzazi na kudhibiti magonjwa yasiyoambukiza.

Amesema hayo alipokuwa akihutubia Mkutano Maalum wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Umoja wa Afrika kuhusu Afya unaofanyika nchini Ghana.

Katika hotuba yake Samia amesema Tanzania imeendelea kuimarisha sekta ya afya kupitia uwekezaji katika viwanda vya dawa na vifaa tiba, kuongeza bajeti ya afya kila mwaka kutekeleza Bima ya Afya kwa Wote na kuboresha miundombinu ya huduma za afya huku akisisitiza kuwa nchi itaendelea kushirikiana na mataifa mengine kutafuta suluhisho la pamoja kwa changamoto za afya barani Afrika.


22/07/2026

Shamba la.mizeituni nchini italia lateketea kwa moto

Babu mmoja amesherehekea siku yake ya kuzaliwa ya miaka 105 kwa kufanya jambo ambalo wengi hawawezi kuthubutu hata wakiw...
22/07/2026

Babu mmoja amesherehekea siku yake ya kuzaliwa ya miaka 105 kwa kufanya jambo ambalo wengi hawawezi kuthubutu hata wakiwa vijana akiruka na parachuti akiwa na mwalimu wake huko Barre New York.

Familia na marafiki zake walikusanyika kushuhudia tukio hilo maalum na kuadhimisha hatua hiyo muhimu ya maisha yake.
Kwa kutimiza miaka 105 mwaka huu 2026 ina maana alizaliwa takribani mwaka 1921.

Neno moja kwa mzee wetu.


Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Arusha Saipulan Ramsey amesema tabia ya uchawa imekuwa ikiliharibu ta...
22/07/2026

Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Arusha Saipulan Ramsey amesema tabia ya uchawa imekuwa ikiliharibu taifa na haipaswi kupewa nafasi katika uongozi.

Amesisitiza kuwa viongozi wanapaswa kuzungukwa na watu wanaojitambua na wanaoweza kutoa ushauri wa kweli badala ya kusifia kila jambo bila msingi.

Ramsey amesema maendeleo ya taifa yanategemea viongozi kusikiliza maoni ya kweli na kukubali kukosolewa pale inapobidi, badala ya kutegemea watu wanaofanya uchawa kwa maslahi binafsi.


Rais wa Nicaragua taifa la Amerika ya Kati Daniel Ortega ametangaza kuwa nchi hiyo haitafanya tena uchaguzi hatua inayof...
22/07/2026

Rais wa Nicaragua taifa la Amerika ya Kati Daniel Ortega ametangaza kuwa nchi hiyo haitafanya tena uchaguzi hatua inayofunga mlango kwa upinzani kuwania madaraka baada ya muhula wake kumalizika mwakani.

Ortega ambaye amekuwa madarakani tangu mwaka 2007 amesema enzi za vyama vinavyoungwa mkono na mataifa ya nje kurejea kutawala zimekwisha.

Uamuzi huo umepingwa na Marekani ambapo Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio amesema unadhihirisha utawala wa kimabavu na kuwanyima wananchi haki ya kuchagua viongozi wao kupitia uchaguzi wa kidemokrasia.

Uchaguzi wa mwisho wa Nicaragua mwaka 2021 ulizua malalamiko makubwa baada ya wapinzani wengi kuk**atwa na sauti za ukosoaji kuzimwa kabla ya kupigwa kura.

Rais wa Marekani Donald Trump amesema huenda Marekani ikashambulia "Pickaxe Mountain" nchini Iran hivi karibuni akidai h...
22/07/2026

Rais wa Marekani Donald Trump amesema huenda Marekani ikashambulia "Pickaxe Mountain" nchini Iran hivi karibuni akidai hakuna kinachoweza kuzuia hatua hiyo.

Eneo hilo linadaiwa kuwa kituo cha siri kilichochimbwa chini ya mlima ambapo Israel inaamini Iran imehifadhi sehemu ya akiba yake ya urani iliyorutubishwa pamoja na mitambo ya kisasa ya kurutubisha urani.

Kwa upande wake Iran imeonya kuwa shambulio lolote la Marekani dhidi ya vituo vyake vya nyuklia litachukuliwa k**a upanuzi wa vita katika Mashariki ya Kati.

Onyo hilo limeongeza hofu ya kuongezeka kwa mvutano na uwezekano wa kuzuka kwa mapigano makubwa zaidi katika eneo hilo.


Meya wa Jiji la New York, Zohran Mamdani amesema baada ya kupitia ushauri wa kisheria na timu yake amebaini kuwa hana ma...
22/07/2026

Meya wa Jiji la New York, Zohran Mamdani amesema baada ya kupitia ushauri wa kisheria na timu yake amebaini kuwa hana mamlaka ya kisheria ya kumk**ata Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu iwapo atawasili New York licha ya hati ya kuk**atwa iliyotolewa na Mahak**a ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC).

Hata hivyo Mamdani amesema mamlaka hayo yapo mikononi mwa serikali ya shirikisho ya Marekani na ameitaka iunge mkono ICC pamoja na kutekeleza hati hiyo ya kuk**atwa.

Kauli hiyo inakuja siku chache baada ya Mamdani kusema alikuwa akitafuta njia za kisheria za kutekeleza kuk**atwa kwa Netanyahu kutokana na tuhuma za uhalifu wa kivita.


Bunge la Ufaransa limepitisha sheria mpya inayowazuia watoto wenye umri chini ya miaka 15 kutumia mitandao ya kijamii ha...
21/07/2026

Bunge la Ufaransa limepitisha sheria mpya inayowazuia watoto wenye umri chini ya miaka 15 kutumia mitandao ya kijamii hatua iliyoungwa mkono na Rais Emmanuel Macron ambaye anatarajiwa kuisaini kuwa sheria kabla ya kuanza kutumika mwezi Septemba mwaka huu wa masomo.

Serikali imesema lengo ni kulinda afya ya akili na maendeleo ya watoto dhidi ya athari za majukwaa ya kidijitali.

Sheria hiyo pia inapiga marufuku matangazo yanayowalenga watoto kutumia mitandao ya kijamii, yakiwemo ya influencers huku matangazo ya majukwaa hayo yakitakiwa kubeba onyo la kuwa ni hatari kwa watoto chini ya miaka 15.

Mamlaka ya mawasiliano ya Ufaransa (Arcom) ndiyo itasimamia utekelezaji wa sheria hiyo wakati serikali ikiendelea kutafuta mfumo wa kuthibitisha umri wa watumiaji.


Address

Mkuyuni
Mwanza

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Coprol posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category