29/05/2026
DODOMA: KAMISHNA Jenerali wa Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas Lyimo, amesema mikoa ya Morogoro, Mara na Tabora ndiyo inaongoza kwa kilimo cha bangi nchini kufuatia mabadiliko ya maeneo ya uzalishajl.
Akizungumza na waandishi wa habari bungeni jijini Dodoma, Lyimo amesema hapo awali Mkoa wa Arusha ulikuwa kinara, lakini baada ya operesheni kubwa za Serikali, uzalishaji ulipungua na kuhamia katika mikoa hiyo mitatu.
Ameeleza kuwa Serikali kupitia DCEA imeendelea kuimarisha operesheni za kudhibiti kilimo hicho haramu kwa kushirikiana na vyombo vya usalama, ikiwa ni pamoja na kuongeza ufuatiliaji katika maeneo yanayohusishwa na uzalishaji wa bangi.
Aidha, amesema Tanzania imepiga hatua katika kudhibiti usambazaji wa dawa za kulevya za viwandani k**a he**in, co***ne, methamphetamine na mandrax, huku akibainisha kuwa ongezeko la waraibu wanaojitokeza kupata matibabu linaashiria kupungua kwa upatikanaji wa dawa hizo mitaani.