Chuma 255

Chuma 255 Page hii ni kwa ajili ya Habari na Elimu. [email protected] +255 712 222244

Cool and respectfull life time, out going,down to earth love making friends,i love all hate me?

01/06/2026

Usiku wa Tarehe 29 mei 2026, Mwanamuziki wa alipiga bonge la Show Mkoani Morogoro .
Katikakati ya Show akampandisha Mdau maarufu na muuza magari maarufu Ndugu yetu na kuanza kumpa Heshima na shukrani zake Kutokana na mchango mkubwa wa Fuko Magari Kwake na wasanii wengine hasa wa Singeli wakifika Morogoro na hata nje ya Morogoro

31/05/2026

Unapajua huko

29/05/2026

Mbunge wa Jimbo la Morogoro Mjini Mh. Dr.
Abdul-Aziz Mohamed Abood amehoji juu ya waathirika wa Mafuriko katika Jimbo hilo, Serikali Ina Mpango gani wa kuwapatia Fidia?

29/05/2026

DODOMA: KAMISHNA Jenerali wa Tume ya Kudhibiti Dawa za Kulevya (DCEA), Aretas Lyimo, amesema mikoa ya Morogoro, Mara na Tabora ndiyo inaongoza kwa kilimo cha bangi nchini kufuatia mabadiliko ya maeneo ya uzalishajl.
Akizungumza na waandishi wa habari bungeni jijini Dodoma, Lyimo amesema hapo awali Mkoa wa Arusha ulikuwa kinara, lakini baada ya operesheni kubwa za Serikali, uzalishaji ulipungua na kuhamia katika mikoa hiyo mitatu.
Ameeleza kuwa Serikali kupitia DCEA imeendelea kuimarisha operesheni za kudhibiti kilimo hicho haramu kwa kushirikiana na vyombo vya usalama, ikiwa ni pamoja na kuongeza ufuatiliaji katika maeneo yanayohusishwa na uzalishaji wa bangi.
Aidha, amesema Tanzania imepiga hatua katika kudhibiti usambazaji wa dawa za kulevya za viwandani k**a he**in, co***ne, methamphetamine na mandrax, huku akibainisha kuwa ongezeko la waraibu wanaojitokeza kupata matibabu linaashiria kupungua kwa upatikanaji wa dawa hizo mitaani.

29/05/2026

Hali ya taharuki imetokea katika Kata ya Sokon 1, Jijini Arusha, baada ya baba mmoja kudaiwa kumfanyia ukatili
mtoto wake kwa kumfunga kwa minyororo nje ya nyumba yake
kwa zaidi ya saa nne.
Tukio hilo limeibua huzuni na maswali kwa wakazi wa eneo hilo, ambao wamesema kitendo hicho si cha kawaida na kimezua wasiwasi kuhusu usalama na haki za watoto katika jamii.
Inadaiwa kuwa baba huyo alichukua hatua hiyo akidai mtoto wake ana tabia ya ukorofi, huku baadhi ya wananchi wakieleza kuwa si mara ya kwanza kwa mtoto huyo kudaiwa
kudhalilishwa na kufanyiwa ukatili.
Wananchi wamezitaka mamlaka husika pamoja na vyombo vya ustawi wa jamii kuchukua hatua za haraka ili kulinda haki za watoto na kuhakikisha malezi yenye usalama na upendo.

28/05/2026
27/05/2026

Waumini mbalimbali wa Dini ya Kiislamu Mkoani Iringa wameungana kuswali Swala ya Eid Al-Adh’ha katika Msikiti mpya wa F***j uliojengwa na Familia ya ASAS na
kufunguliwa rasmi leo Mei 27, 2026.

Hafla hiyo iliyoshuhudiwa na Viongozi wa Serikali, Viongozi wa Dini pamoja na Wananchi mbalimbali ilienda sambamba na ibada ya kuchinja Wanyama kwa mujibu wa mafundisho ya Kiislamu k**a sehemu ya maadhimisho ya Eid Al-Adh’ha.
Akizungumza katika hafla ya ufunguzi huo, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Kheri James alisema Taasisi za Kidini zina mchango mkubwa katika kujenga jamii yenye maadili mema, mshik**ano na amani.

Alisema uwepo wa Masjid F***j utasaidia kuimarisha umoja wa
Wananchi pamoja na kuwa Kituo muhimu cha ibada na
mafunzo ya dini kwa kizazi cha sasa na kijacho.
“Ni matarajio yangu kuwa Masjid F***j utaendelea kusimamia
misingi ya umoja, upendo na kusaidia kukuza maadili mema katika jamii,” alisema Kheri James.
Kwa upande wao, baadhi ya Waumini walieleza furaha yao kwa kukamilika kwa Nyumba hiyo ya ibada wakisema itakuwa sehemu muhimu ya kuimarisha mafundisho ya dini pamoja na kuwaunganisha Wananchi kupitia shughuli mbalimbali za Kijamii na Kiroho.

26/05/2026

Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara imetoa wito kwa
Kiwanda cha Magari cha .ltd Corporation Limited kushirikiana na Serikali kuongeza mnyororo wa thamani kwa kuchochea uanzishwaji wa viwanda vidogo na vya kati vya vipuri nchini.

Hayo yamesemwa na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe.
Judith Kapinga (Mb), wakati akiweka Jiwe la Msingi la Kiwanda kipya cha kutengeneza magari madogo ya mizigo aina ya pick-up, cha kampuni hiyo huku akibainisha kuwa mkakati huo utaleta ajira kwa Watanzania, kuimarisha ujuzi wa kiteknolojia, na kujenga uchumi wa kisasa wenye
ushindani wa kimataifa.

Aidha, Waziri Kapinga amepongeza mchango wa kiwanda hicho kiuchumi kupitia ulipaji wa kodi na tozo za halmashauri takriban Bilioni 1.5, zinazosaidia huduma za kijamii, huku akiwahakikishia wawekezaji kuwa Serikali inafanyia kazi
changamoto zilizowasilishwa, zikiwemo za miundombinu ya
barabara, kodi ya magari, na ufanisi wa bandari ili kuendeleza uzalishaji huo.

Address

Morogoro

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Chuma 255 posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to Chuma 255:

Share