23/02/2024
FAHAMU KUHUSU MALARIA KUPANDA KICHWANI
Wengi wetu tumekua tukisikia mitaani kuhusu malaria kupanda kichwani, hii malaria kupanda kichwani ni nini hasa na ni kweli inatokea malaria kupanda kichwani?
Ipo hivi;vimelea vya malaria vinavyojulikana k**a plasmodium huingia mwilini na kwenda moja kwa moja kwenye red blood cells(seli hai nyekundu za damu) na kukutana na Haemoglobin ambazo huzishambulia kwani ndio hula na kuendelea kuzaliana na ndivyo huzidi kula haemoglobin nyingi zaidi na malaria kuzidi kua kali. Haemoglobin ndizo ambazo huungana na oksijeni na kuisafirisha katika sehemu mbali mbali za mwili.
Sasa haemoglobin zikishapungua kwa wakati huo haziwezi kuungana na oksijeni ya kutosha zilizobaki na kuisafirisha sehemu mbali mbali za mwili ikiwemo ubongo ambao hutumia oksijeni kufanya kazi zake k**a vile kufikiria, kukumbuka na kutafsiri taarifa zinazoletwa kupitia mfumo wa neva.
Hivyo haemoglobin zinashindwa kupeleka oksijeni ya kutosha kwenye ubongo na hivyo ubongo unashindwa kufanya kazi zake katika kiwango chake na ndipo hapo mgonjwa wa malaria anaonekana k**a amepandwa na kichaa na kuchanganyikiwa na ndipo hapo tunasema sasa malaria imepanda kichwani.
Tafadhal follow page yangu na kualika wengine pia ili kuendelea kupeana madini mengi ya kutosha kuhusu afya, fedha, maisha na maendeleo binafsi. Hapa ni kupeana ujuzi na elimu tu. Ahsante.
Imeandaliwa nami yaz lee jr..