HolySmile

HolySmile HolySmile is a non-governmental organization that specializes in arts, culture and entertainment services, mobilization, event planning, marketing strategy.

MDAU SHUPAVU AWARDS🎯 DINNER GALA – LAKE ZONEπŸ“ HOLYSMILENi usiku wa kipekee wa heshima, shukrani na kutambua mchango wa W...
06/02/2026

MDAU SHUPAVU AWARDS
🎯 DINNER GALA – LAKE ZONE

πŸ“ HOLYSMILE

Ni usiku wa kipekee wa heshima, shukrani na kutambua mchango wa Wadau Shupavu waliobadilisha maisha ya jamii na kuleta maendeleo ndani ya Kanda ya Ziwa. Unaokutanisha Wadau Shupavu Kutoka Mikoa Sita ya Kanda ya ziwΓ  Katika Jukwaa Moja....

πŸ“ VENUE: Goldcrest Hotel – Mwanza Jiji

πŸ“… TAREHE: 16 February, 2026
⏰ MUDA: 18:00 – 00:00 EAT
πŸ‘” DRESS CODE: Black β€’ Gold β€’ White

🎟 TICKETS:
❇️ 100,000/= Normal
❇️ 200,000/= VIP
❇️ 1,000,000/= – Meza ya Watu 5
❇️ 2,000,000/= – Meza ya Watu 12.

πŸ“ž MAWASILIANO ZAIDI:
0756 254 146 | 0622 891 972
πŸ”— Mitandao ya Kijamii: |

Tukuthamini kwa mchango wako, tukuheshimu kwa uthubutu wako.

Jifunze kuheshimu mahusiano ambayo umetambulishwa na mtu mwingine. Mtu anapokutambulisha kwa mtu katika mzunguko wake, i...
27/12/2024

Jifunze kuheshimu mahusiano ambayo umetambulishwa na mtu mwingine. Mtu anapokutambulisha kwa mtu katika mzunguko wake, inamaanisha amekuamini sana. Ni muhimu kutokuwa na haraka ya kujenga mahusiano ya karibu na huyo uliyetambulishwa bila kumhusisha aliyekutambulisha.

Kwa nini? Inawezekana huyo uliyetambulishwa haumjui k**a rafiki yako anavyomjua. Watu wengi wameingia matatizoni kwenye pesa, biashara, au mahusiano kwa kudhani wanamjua mtu kuliko aliyewaunganisha.

Pia, ni heshima kubwa kumfahamisha aliyekutambulisha juu ya kinachoendelea kati yenu. Hii hujenga imani na kumfanya aendelee kukutambulisha kwa watu wengine muhimu. Ukifanya mambo kwa kificho bila kumjulisha aliyekutambulisha, tambua kuwa mara nyingi wanarudi kumwambia kwa sababu walijuana kabla wewe hujawa sehemu ya uhusiano huo.

Kutunza mahusiano kunahitaji hekima na ukomavu. Bila hivyo, unaweza kupoteza wengi walio tayari kukuamini.

Mkurugenzi wa Taasisi ya HolySmile, Arnold Andolin Bweichum Usiku wa Wadau Shupavu Wilaya ya Kahama.
27/12/2024

Mkurugenzi wa Taasisi ya HolySmile, Arnold Andolin Bweichum Usiku wa Wadau Shupavu Wilaya ya Kahama.

27/12/2024

MATABE (NIMEKOMA) AMVUNJA MBAVU MKUU WA MKOA WA SHINYANGA! NA WADAU USIKU WA MDAU SHUPAVU WILAYA YA KAHAMA 2024 🀣

08/11/2024

HIGHLIGHTS | USIKU WA WADAU SHUPAVU KAHAMA HOLYSMILE MRATIBU Mr. Bweichum HolySmile

08/09/2024

MTOTO MWENYE KIPAJI CHA AJABU KWENYE HESABU

ZAWADI ZA SHYCOM ALUMNI MARATHON 2024  Shycom Mapendo sports Promotion Kwa Kushirikina na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shiny...
08/09/2024

ZAWADI ZA SHYCOM ALUMNI MARATHON 2024

Shycom Mapendo sports Promotion Kwa Kushirikina na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga inakuletea... 🎢

πŸ“’ *Shycom Alumni Marathon!* πŸ“’

πŸ“… Lini? Jumamosi, tarehe 21 Septemba 2024.
πŸ“ Wapi? Shinyanga Mjini, Uwanja wa CCM Kambarage.
πŸ’° Usajiri? Shilingi 35,000/- tu! Utapata T-shirt na Medali!

πŸšΆβ€β™‚οΈ Tutakuwa na mbio za *Kilomita 5, Kilomita 10, na Kilomita 21!* Pia, kutakuwa na michezo maalum na michezo kwa watoto. *Zawadi kubwa kwa washindi zitatolewa!*

JINSI YA KUJISAJIRI SHYCOM ALUMNI MARATHON
1. WhatsApp: Hifadhi namba hii 0754 241241 Tuma neno Shycom kisha fuata maelekezo.
2. Lipa kwa Simu: Kwa malipo ya Shycom Alumni Marathon kupitia Tigo Pesa

- Piga *150*01 #
- Chagua No. 5 (Lipa kwa Simu)
- Chagua 6 (Tickets)
- Chagua 1 (Marathon)
- Chagua 5 (Endelea)
- Chagua No. 1 (Shycom Alumni Marathon)
- Fuata maelekezo zaidi.

πŸ“ž Kwa maelezo zaidi na nafasi za udhamini, piga simu 0756 254146 au 0713527808

🎢 *Shycom Alumni Marathon 2024, hii ni yetu sote!* 🎢

Karibu sana mdau shupavu! πŸ’ͺ

Imedhaniwa na
1. Jambo Group
2. Tigo.

HOLYSMILE - TANZANIA...............................12 MEI 2023..............................Kwa niaba ya HolySmile, Mkur...
13/05/2023

HOLYSMILE - TANZANIA...............................
12 MEI 2023..............................
Kwa niaba ya HolySmile, Mkurugenzi wa anaungana na Watanzania wote kutoa pole kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia kifo cha Kiongozi Shupavu na Mzalendo wa kweli kwa Tanzania, Ndg. Bernard Kamillius Membe.

Bernard Kamilius Membe alizaliwa tarehe 9 Novemba, 1953, Rondo, Chiponda, katika Mkoa wa Lindi, akiwa ni mtoto wa pili kati wa watoto saba (7) waliozaliwa katika familia ya Mzee Kamillius Anthony Ntachile na Mama Cecilia John Membe.

K**a ilivyo desturi ya Wamwera, watoto hutumia jina la ukoo wa Mama. Hivyo watoto wote saba wa familia hii ya Mzee Kamillius wamekuwa wanatumia jina la upande wa mama yao, Cecilia, yaani Membe. Aliwahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania kuanzia mwaka 2007 hadi 2015. Pia aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Mtama kuanzia mwaka 2000 hadi 2015.

Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi, Amina.

.............................
Imetolewa na Kitengo cha mawasiliano HolySmile

Mdau wa Maendeleo kutoka Kampuni ya  Arnold Bweichum Mdau shupavu (kushoto) akikabidhi Tuzo ya  kwa wachimbaji wadogo wa...
12/03/2023

Mdau wa Maendeleo kutoka Kampuni ya Arnold Bweichum Mdau shupavu (kushoto) akikabidhi Tuzo ya kwa wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu Mwakitolyo namba 5 kutokana na kuwa na mchango mkubwa Serikalini wa ulipaji mapato na kuzalisha madini kwa wingi, (kulia) ni Mwenyekiti wa wachimbaji wadogo Mathew Tune

Wadau wa madini wakiwa kwenye Mkutano wa wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu Mwakitolyo wa usomaji mapato na matumizi...
12/03/2023

Wadau wa madini wakiwa kwenye Mkutano wa wachimbaji wadogo wa madini ya dhahabu Mwakitolyo wa usomaji mapato na matumizi.

Maisha ya kila mtu ni matokeo ya akili na utashi wa kila mtu katika maisha yake. Kwa maneno mengine maisha yetu ni zao l...
11/03/2023

Maisha ya kila mtu ni matokeo ya akili na utashi wa kila mtu katika maisha yake. Kwa maneno mengine maisha yetu ni zao la akili yetu na utashi wetu. Kwanini nimesema hivyo, naamini kila mtu ana mawimbi ya akili ambayo hutengeneza program fulani ambazo hushughulika na maisha ya kila siku. Hivyo k**a mtu akijaza program hasi kwenye akili yake atatoa kitu hasi, vivyo hivyo mtu akijaza program chanya atatoa kitu chanya, kwa wataalamu wa kiingereza wanatumia istilahi ya 'GIGO' yaani Good in, Good out. Bila kupoteza muda napenda kuzungumzia mambo matano unayohitaji ili kubadili maisha yako.

Mambo matano (3) unatohitaji ili ubadili maisha yako.

Β Kuwa na Imani ( believe )
Hakika katika maisha kuna changamoto nyingi; kukatishwa tamaa, kuibiwa, kudharauliwa, kukataliwa n.k. katika haya yote amini kuwa kuna muda,namna na jinsi ya kuondokana nayo. Ni lazima uwe na imani na kile unachofanya, uwe mnyoofu na kuyapokea yote huku ukiwa na imani kuwa ipo siku ndoto na malengo yako utayafikia Imani ina nguvu sana katika masomo yako,katika biashara yako, katika ndoa yako, katika utumishi wako, katika uongozi wako kwani kwa kuamini tu binafsi naamini unapata asilimia fulani ya kile unachotaka unapokea.

Tamko: Imani inaumba na kujenga kitu halisi katika ulimwengu halisi kutoka fikra au mawazo ya mtu.
Β 

Kujitoa ( commit )
Nafikiri ili nieleweke vizuri hapa, niseme kujitoa ni kusema kuwa mimi nahusika na jambo au shughuli husika wala si mwingine yeyote. Kujitoa ni kuchukua jukumu moja kwa moja bila kudhania kuwa kuna mtu atakusaidia. Ili kutengeneza maisha yako chukua jukumu kusimamia maisha yako yasiharibike au kuharibiwa na yoyote. Hakuna mtu aliyejitoa kikamilifu akashindwa kupata kile anachotafuta. Shida ya watu wengi huwa tunafanya mambo bila dhati ya moyo yaani ilimradi yaende.Ikiwa kweli una kiu kubwa ya kutaka uzee wako uonekana wa maana, basi unalazimika kujituma sana kwenye kila jambo unalolifanya. Ikiwa hutajituma na kuweka misingi imara wakati ukiwa kijana, sahau kuwa na mafanikio uzeeni na zaidi utalalamika na kujutia uzee wako wote.
Β 

Kuthubutu (dare )
Kuthubutu ni kuwa na moyo au kumua kufanya kitu hususani chenye changamoto. Hii ni nguzo muhimu sana.

Aliye anzisha masomo hakuwa na nia mbaya, tatizo ni yule aliyeanzisha mitihani na wote tuna akili, tatizo lipo kwenye ku...
03/03/2023

Aliye anzisha masomo hakuwa na nia mbaya, tatizo ni yule aliyeanzisha mitihani na wote tuna akili, tatizo lipo kwenye kuwa na akili timamu. Sir

Address

HolySmile HQ
Kahama
37302

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when HolySmile posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share