Story funzo

Story funzo Karibu katika ukurasa wa simulizi, riwaya na jumbe za maisha kutoka kwa mtunzi Daniford ben

share na kuinvite(alika) marafiki kulike page hii kwa ku click sehemu iliyoandikwa invite

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Mos Quito, Felistus Kim, Mligo John Vanny, Violeth Ndoss,...
24/12/2025

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Mos Quito, Felistus Kim, Mligo John Vanny, Violeth Ndoss, Thobias Wilison, Gideon Wabuge, Franco Bernard, Nassor Salim, Agnes Philimoni, Milaji Omari, Theophil Theofrey, New Mick Msuya, Abdhallah Kassim, Mzungu Jrii, Masuha Mataba, Republica De Mocambique, Ammir Ke, Bismark Naut, Rubare Kwetu RB, Hilarious Hillas, Joshua Mrema, Mandevu Jonas, Joseph Kiangi, Zacharia Stephano, Master Plane

SIMULIZI: MVUJA JASHOMTUNZI: DANIFORDY BENMAWASILIANO: +255711444410SEHEMU YA 03TULIISHIA.Jerinda amempeleka sofania mae...
23/12/2025

SIMULIZI: MVUJA JASHO
MTUNZI: DANIFORDY BEN
MAWASILIANO: +255711444410

SEHEMU YA 03

TULIISHIA.
Jerinda amempeleka sofania maeneo ya fordy bar baada ya kuagizwa na mama zurufa. Je ni mzigo gani anaufikisha eneo hilo kwa ujira mrefu?

SASA TUENDELEE.

Ama hakika waghani lugha hawakukosea kusema sura siyo roho, furaha ya sofania ni kupita na kuingia sehemu ghari k**a zile ambazo aliziona kwa mbali wakati wa matembezi. Furaha yake ilimkumbusha kila muda sura ya mama zurfa ambaye kwake ama hakika alikuwa mwema kila sekunde ubongoni mwake. Hakuna hata thumuni ya kosa ingethubutu kuchafua wema wa mama zurufa kwa sofania. Jerinda alitoa maelekezo ya ishara tu kumtambulisha sofania, k**a vile wapiga debe wafanyavyo stendi kwa ile kauli yao ya kusema hii ni namba yangu nimeichora kuashiria kuwa wammpigia debe mteja. Sofania hakutambua chochote kilichokuwa kikiendelea kwake, zaidi alipewa maelekezo ya kukaa katika kiti moja wapo ndani ya saloon ile iliyojazwa nakshi haswa.

Upambaji ulianza kwa binti yule ambaye alikuwa amebuka na maisha ya ufukara, licha ya kuoga kila siku lakini haikufanya apendeze kwa muonekano wake. Hivyo ilifaa apendezeshwe zaidi ili tu kufanania na kazi aliyokuwa akiifanya. Dakika za kuhesabu muonekano wake ulianza kubadirika na urembo wake ukaanza kujidhihirisha wazi. Wakati huo jerinda alikuwa ametoka na kujipakia katika gari lake na kuondoka, kabla ya muda mchache kurejea akiwa na mifuko miwili ambayo alifika na kuiweka katika kiti kisha akawaeleza wahudumu wale kuwa ni kwaajiri ya sofania na kumkabidhi begi ambalo aliambiwa anapaswa kulilinda sana, kisha akamwambia anamsubiri garini. Punde tu baada ya kumaliza kumremba sofania akarembeka ndipo walipomkabidhi mifuko ile na kumuelekeza mahali pa kwenda nayo. Ilikuwa ni mifuko yenye nguo ghari sana, nguo ambazo alipaswa kuzivaa kwa muda huu, amahakika zilikuwa zimempendeza ila tu. Hofu ilikuwa dhidi yake kwa muonekano ule wa suruali pekee kutembea nayo maana hakuwahi kabisa kuvaa hivyo.

Ila haikuwa na namna ilimlazimu, ijapo roho yake ilikuwa ikisita sana akaihisi kuwa uvaaji huo ni nje ya maadili aliyofunzwa, sofania alitoka ndani mule akiwa mtu mwingine kabisa. Alikabidhiwa begi lake na kisha safari ikaanza kulifuata gari, hakika alibadirika haswa hali iliyomfanya mpaka jerinda kuduwazwa na muonekano ule ambao hakuwa ameutegemea kabisa.

"You look great". Alizungumza jerinda na kumuacha sofania akiwa anatabasamu tu, asijue nini maana ya kile alichokuwa ameambiwa.

Jerinda aliwasha gari na kulisogeza mita kadhaa hapa ilikuwa ni nje kabisa ya fordy bar, mahali ambapo ndipo alipaswa kuupeleka mzigo ule ambao hakuwa akijua ni nini haswa kilichokuwa ndani yake. Alipewa maelezo nini akifanya pindi aingiapo ndani mule na ni code gani azitaje, hivyo hakuwa na muda wa kusubiri alitekeleza alichoambiwa na hatimaye baada ya kukamilisha biashara ile aliyoambiwa, alitoka akiwa amebarisha lile begi la mwanzo na kuwa na jingine jeusi la lezzer, hili lilikuwa zito kiasi lakini kwa masharti aliyopewa ndivyo ilibidi afuate, hakupaswa kufungua kabisa mzigo huo. Alirudi garini na jerinda akalichapa gear kuelekea kwa mama zulfa, lakini sasa haikuwa dukani pale tena zaidi sasa mwelekeo ulikuwa nyumbani.

Mbele ya uzio mkubwa wa jumba la kifahari kulipambwa na madhari nzuri sana, juu ya kuta za fensi kulikuwa na uzio wa umeme, na kwa mbali ungetazama kwa nje jengo hili lilikuwa la ghorofa. Muda wote sofania alikuwa kimya tu akijikagua kagua namna alivyokuwa amependeza siku hii hata hakuwa na umakini wa safari ni wapi ametoka na wapi aendako. Zaidi alish*tushwa ghafla na ulio mkali wa honi, yes ni nukta chache geti likasogea upande wa kulia taratibu na gari lao likaanza kuingia ndani ya mji ule wa gharama ya juu, ughari wa jumba lililokuwa mbele ya macho ya sofania ulijaza maswali lukuki unongoni mwake, kwa ile wazawazua ninani aishiye humo ndani.

Gari liliendeshwa taratibu na kupaki upande wa kulia wa jengo hili na jerinda ndiye alikuwa wa kwanza kushuka, kabla ya sofania kufuata. Sofania kila kitu kilimshangaza hasa pale alipokuwa akishangaa geti lililokuwa likijifunga pasi kuwapo mtu, hakika kwake hii aliona k**a mi ushirikina, ila tu alikosa wa kumuuliza swali kutokana na ubusy wa muda wote kwa jerinda Walipiga hatua za taratibu kuusogelea mlango lakini kabla hawajafungua konde zito lilitua kichwani mwa sofania ambaye taratibu macho yalipoteza nuru, nguvu zikamuisha na taratibu akashuka na kutua ardhini k**a mzigo.
ITAENDELEA.

JE! nini kitaendelea unadhani na nini hatima ya mkasa huu?
Basi usikose sehemu inayofuata

MTUNZI: DANIFORDY BENSIMULIZI: MVUJA JASHOMAWASILIANO: +255711444410SEHEMU YA 02TULIISHIA.Mama zurufa ameahidi kumsaidia...
20/11/2025

MTUNZI: DANIFORDY BEN
SIMULIZI: MVUJA JASHO
MAWASILIANO: +255711444410

SEHEMU YA 02

TULIISHIA.
Mama zurufa ameahidi kumsaidia sofania kwa masomo na maisha ila anamtaka afanye kazi yake kwanza ili tu kuulipia msaada ambao atapewa, je ni msaada gani atapata?

SASA TUENDELEE.

Hali ya woga ilizidi kutabakuru ndani ya sofania ambaye maswali yalizidi kuhanikiza akili yake ijiundie maswali mengi ya siyo majibu, kila alipofikiri kuanza moja mbili ilitangulia kutoa jibu lisilo na swali, uso wake ulidhihirisha fazaha ya waziwazi, na kujitwika dhunubu ya kukufuru juu ya muumbaji wake ambaye alikuwa akimpa mitihani isi kifani hasa kwa umri ule mdogo aliokuwa nao.

"Zurufa, nisikilize mwanangu. Ni kazi rahisi sana. Haina ugumu wowote naamini utaiweza na k**a ukifanikisha nitakulipa vizuri. Si hivyo tu vyote nilivyokuahidi nitakutekelezea".

Alimaliza mama zurufa kuelezea, ni dhahiri kile alichokuwa amekizungumza kilipenya sawia masikioni mwa sofania ambaye, tabasamu hafifu lilichanua usoni pake. Roho yake ililipalipa kwa shauku ya kutaka kujua kazi hasa pale aliposikia juu ya malipo, kwakuwa katika vitu alivyotamani kwenye maisha yake ni kupata pesa tu. Alikuwa amekaa kwa utulivu kusikiliza maelezo ya kazi nyepesi aliyoambiwa hata yeye anaweza kuifanya. Hivyo aliitikia kwa kutikisa kichwa na mama zurufa akaendelea.

"Kuna mzigo nitakupa utaupeleka mahali, na ukiufikisha ni pesa nyingi sana utalipwa".

Aliweka ukomo mama zurufa, na kukatisha mazungumzo yake baada ya simu kuita, naye bila kusubiri alitoa nywira na kisha akaipokea na kusikiliza kwa muda bila kuzungumza kisha akajibu.

"Ok sawa namtuma binti yangu sasa hivi, huu ni super sana sio k**a wa mwanzo nimeujaribu".

Alijibu mama zurufa kujibizana na mpigaji, kisha akatulia kusikiliza tena, wakati huo sofania akiwa amerulia tuli asisikie chochote kilichokuwa kikizungumzwa upande wa pili, ambapo aliishia kusikia jibu la sawa kutoka kwa mama zurufa ambaye alitoa simu yake sikioni na kumgeukia. Alimtazama kwa muda asizungumze jambo ni k**a alikuwa akitafakari jambo fulani. Kisha akaichukua simu yake na kupiga kwa mara nyingine, simu ilipokelewa upande wa pili.

"Hellow madam, habari?".

Ulianza kusalimu upande ule wa pili baada ya simu kuita kwa sekunde chache.

"Yes! Njoo dukani kwangu mara moja".

"Sawa".

Majibizano yaliyompa zumbukuku sofania asijiu ni nini kilikuwa kikiendelea.

"Hivi mpaka sasa unanidai shingapi?".

"Siku nne mama"..

Alijibu haraka sofania huku akidoya ili kuonesha unyenyekevu alio nao.

"Aaah sawa unamaanisha elfu nane?". Alihoji mama zurufa.

" Ndio mama".

" Usiniite mama toka sasa niite dada, sasa nitakupa elfu ishirini".

" Ahsante ma...Dada". Alijibu kwa kimuhemuhe binti yule.

Kabla mazungumzo hayajaendelea nje ya duka la mama zurufa ilipaki Subaru ya rangi ya zsmbarau na akashuka mwanamke mrembo aliyekuwa aliyekuwa amependezeshwa na mavazi nadhifu yaliyo ushika vyema mwili wake. Weusi wa asili usio vikwatuzi ulienda sawia na nywele zake za blash ungekufanya umtazame mara mbili ili ijapo ufanye ubashiri wa kazi yake. Mwanamke huyo akangia dukani mule na kummsalimia mama zurufa huku akimtazama sofania ambaye alikuwa bado ameganda na ufagio akimtazama mwanamke yule huku tamaa ya kuwa k**a yeye ikizidi, ni hakika alianza kujiona naye akiwa amependeza vile vile.

"Ok jerinda ongozana naye huyu, mpeleke fordy kasino. Kisha utamuacha pale aingie kupitia mlango ule wa saloon kwangu, nimeshawapa maelekezo".

Alizungumza mama zurfa akitoa maelekezo kwa dada yule mgeni huku akimkabidhi begi dogo la mgongoni, ambaye naye alipokea na kumtaka sofania amfuate kwa nyuma wakati akitoka dukani mule. Walipotoka ndani ya duka lile dada yule alitoa ishara kwa sofania kuingia mlango wa nyuma naye alitii haraka na kuingia garini, ni dhahiri hata kupanda gari kwa upande wake ilikuwa ni ndoto ya muda mrefu. Alitulia mule akivuta manukato mujarabu, gari lilipigwa gia na safari ikaanza kufuata uelekeo wa kuingia mjini. Safari ilikuwa yenye ukimya sana, jerinda alishupaza macho yake mbele kutazama barabara tofauti na sofania ambaye macho yaliambaza kila upande wa kioo kushuhudia magari, nyumba na watu wakirudi nyuma. Gari lilifika na kupaki katika moja ya saloon ambayo ng'ambo ndiko kulikuwa na ukumbi mkubwa wenye makasino, na uuzwajwi wa unyaji. Ambao ndani yake ungeweza kuhudumiwa kila kitu cha satarehe.
ITAENDELEA.

Je nini hatima ya sofania, mzigo gani amebeba na nikazi gani ya ujira mwingi. USIKOSE SEHEMU IJAYO.

MTUNZI:DANIFORDY BENMWASILIANO: +255711444410SIMULIZI: MVUJA JASHO.     Sifuni ni jina nililozawadiwa baada ya kilio cha...
15/11/2025

MTUNZI:DANIFORDY BEN
MWASILIANO: +255711444410
SIMULIZI: MVUJA JASHO.

Sifuni ni jina nililozawadiwa baada ya kilio changu cha kwanza ndani ya ulimwengu huu wa watu wa hira na wema, nakumbuka niliwahi sikia watu wakisema subira yavuta heri, na laiti ingelikuwa mtu anaweza kuona vilivyo mbele kabla ya uzao wake basi ningeomba kuzaliwa baadae na sio kwa wakati huu, na k**a tungepewa uwezo kuona mbele nadhani kuna vingi mwanadamu asingefanya ili kukwepa majuto yaliyopo mbele yake baada ya kufanya kosa, Na ile methali ya majuto ni mjukuu isingetamkika vinywani mwa watu daima. Lakini nani awezaye kugeuza jicho lake litazame kisogoni k**a kinyonga afanyavyo? Jibu hakuna ila tu tumejaliwa kuona vya nyuma baada ya kuvipita na kugeuka tuvitazame tena, na mara zote huwa vinaweza kuwa vyema au vibaya. Na k**a ni vibaya basi ni lazima utatamani upewe maaajabu ya mdudu kinyonga abadirikaye rangi aonapo hatari mbele yake, ijapo naye abadiri ubaya wake kuwa wema ili tu kurudisha imani na amani kwa walimwengu.

Jina langu linabeba uzani mkubwa wa kisichotikiswa wala kutetereshwa, nilitamani sana nifanane na ule mlima sayuni. Lakini chozi la maumivu lilininyong'onyesha kwa kushindwa kuhimiri mapito yangu. Uyatima ulinijenga kuwa jasiri wakati wa utoto, njaa haikuwa adhabu kwangu kwakuwa tayari nilishazoea mlo mmoja kwa siku kwenye maisha yale ya mahangaiko nikiwa na mama yangu, wakati tukiranda mtaani. Siku jua kuhusu A wala Be, ila nilijifunza kuokota vibuni, chuma na baadhi ya mabati ili tu nikauze ili tupate chakula. Mama yangu kuna muda tuliungana katika kazi hii, ila mara chache alipata day worker mashambani na kazi ndogondogo zilizohitaji usaidizi, hivyo aliniacha niendelee na vibuni. Kila kesho ya matarajio ilikuwa haina tofauti na jana ya bora liende.

Ni miaka michache sana ya upevukaji wangu ilitosha kujifunza vichache kutoka kwa mama yangu ambaye ndiye alikuwa baba na mama yangu, kwakuwa sikuwahi kuiona sura ya baba. Mama Hakuwahi kuniambia chochote kuhusu ndugu zangu katika siku zoye za uhai wake, zaidi nilisikia kwa majirani kuwa mama yangu alibakwa na mtu asiyemfahamu ndiyo ujauzito wangu ulipotungwa. Miaka 14 ilitosha kabisa kuishi ndani ya upendo wa mama ambaye hakupenda kuniona nalia naye akacheka, ila aliweza kulia ili tu mimi jicheke. Alikuwa tayari kulala njaa ilimradi mimi nishibe. Hivyo kwangu nilimpa heshima ya hayati, ijapo wengine waliona ni marehemu na kuna wachache walimjua k**a maiti.

Maisha ya mtaa yalinipokea na kunihifadhi ndani yake ili niyaishi. Kwa mwanzo majirani walikuwa ni sehemu ya maisha yangu ila kuna muda walibadirika na kuanza kuninyanyapaa, na hata walipoigiza kunipa msaada basi walihakikisha kuwa na ulipa kwa gharama kubwa, yenye maumivu na majuto ya kupokea msaada huo.

"Sifuni... Nipo tayari kukupa msaada wa elimu na maisha. Je upo tayari?".

Alihoji mama zurufa kwa sifuni ambaye sasa alikuwa sakara haswa kutokana na maisha yaliyomkokonya bila huruma.

"Nipo tayari mama yangu, nipo tayari na Mungu akubariki na kukuondolea dhunubu zote zilizo juu yako. Nitashukuru kwa wema huo".

Alizungumza sifuni wakati machozi yakianza kumlengalenga kwa furaha iliyotabakuru rohoni mwake. Alijikuta akihaha tu bila kujua apige goti ama abaki wima k**a mlingoti wa bendera, alikuwa akifurahia kwenda shule ambayo hata hakujua ni shule gani. Furaha iliyozunguka ndani ya roho na akili ilifanya hata njaa ikose nafasi mwilini mwake sasa alijihisi mtu alieshiba shibe ya kiwango cha juu tena yenye chakula ambacho alikipenda kula.

"Aaah sawa nipo tayari kukusaidia, ila tu ni kwa sharti moja tu! Na k**a utakubali nitakupeleka shule na pia nitakufungulia biashara yako binafsi, ili ikufae kwa mahitaji madogo madogo wakati ukiwa katika masomo yako".

Mama zurufa aliweka ukomo kiasi, kutoka katika maelekezo yake wakati huu akimeza funda zito la mate, sawia kabisa na kushusha pumzi ndefu ambayo iliashiria yajayo mdomoni mwake yalihitaji hewa nyingi ili kusukuma yatoke, wakati huo sifuni alitulia tuli kimsikiliza na ile furaha ya awali ilipungua, akibaki kumtazama mama zurufa. Mama aliyefahamika mjiji hapo kwa wengi kuwa ni mfanya biashara mkubwa wa nguo, vipodozi na pia mmiriki wa baadhi ya salon za k**e. Ni mama wa haja hasa aliyepewa urembo na umbo kubwa, muonekano na harufu yake ya marashi ilidhihirisha wazi ughali aliokuwa nao katika maisha hasa ungemkuta katika gari lake ameshika usikani, hakika usingehitaji kuelezewa kuwa yule ni mwanamke wa viwango vya juu.

"Lakini mama mimi siwezi kukusaidia vingine zaidi ya kuendelea kufanya usafi hapa kazini kwako, maana sina ujuzi mwingine wowote zaidi ya kuokota vibuni (makopo ya maji na soda), hivyo ndiyo mama yangu alinifundisha. Nitawezaje kazi nyingine na sijui hesabu wala kusoma? Harafu na muo.... ".

Alijieleza sifuni ambaye alikatishwa maongezi yake na mama yule wakati bado alikuwa na jambo la kuzungumza, msaada aliuhitaji wakati huo hofu ikianza kumuingia juu ya msaada atao upata. Ila kiroho alikumbuka neno lisemalo ogopa kupewa viatu na mtu aliyevaa kandambili. Ndani yake bado kuna nafsi ilikuwa inamsukuma kuwa bado anahitaji msaada hivyo hapaswi kuogopa changamoto.

"Tuliza munkari, nimekwambia nataka kukusaidia sasa izo fyokofyoko zinatoka wapi! Unanielezea kwani mimi sijui? Jishikilie vizuri nisije kudondosha kabla sijakaza nguo, sijui nimeeleweka..? "

Alimaliza mama yule kuzungumza. Sasa hata sura yake ilibadirika haikuwa na tabasamu tena k**a awali na kumfanya sifuni kuogopa kuzungumza zaidi ya kuwa msikilizaji wa kusubiri msaada wa mama zurufa.
ITAENDELEA.

Je! Nini hatima ya mkasa huu unadhani na nini kitaendelea kwa sifuni, msada gani anatarajia kuupata! Basi usikose sehemu ijayo.

Nisikilize Mwanangu…Dunia ya sasa imejaa watu wa hila, wasio thabiti, na wenye tabia ya kupita mbele kwa kudanganya. Mwa...
03/10/2025

Nisikilize Mwanangu…
Dunia ya sasa imejaa watu wa hila, wasio thabiti, na wenye tabia ya kupita mbele kwa kudanganya. Mwanangu, usidhani kila kicheko ni kweli, kila maneno ni ya dhahiri. Kuna wengine wanaonekana wema ili wakutaplishe, wawe na faida kutoka kwako, na kuondoka bila heshima.

Mwanangu, hekima yako ni silaha kubwa zaidi. Ukiishi kwa kuamini kila mtu anayeonekana mzuri, utapoteza heshima, pesa, muda, na wakati mwingine hata ndoto zako. Usikubali uongo wa wengine ukudanganye. Kujua kusoma tabia ya mtu ni ulinzi wa thamani zako.

Nisikilize vizuri mwanangu… Hakuna mtu anayekutumia vizuri k**a wewe mwenyewe. Hila na uongo wa wengine ni mwanga wa haraka – huanguka k**a jua linapochomoza na kuanguka. Lakini nidhamu, hekima, na ujasiri wako ni nguzo thabiti ambazo hazitazidishwa na dhoruba yoyote.

Mwanangu, fanya kila uamuzi kwa akili na moyo wako. Usikimbilie starehe za muda mfupi, mapenzi yasiyo thabiti, au mashindano yasiyo na maana. Hili ndilo somo kubwa la maisha ya sasa: dhahiri sio kila kitu kilicho mbele yako ni kioo cha kweli. Angalia ndani, hakikisha kila hatua unayoichukua ina maana halisi.

Mwisho, nisikilize tena mwanangu… Hila za wengine ni changamoto yako. Ukiweza kudumisha nidhamu, hekima na moyo thabiti, hakuna uongo wa mtu mwingine utakayekuondoa kwenye nafasi yako ya heshima. Dunia ya sasa inamheshimu yule anayejua thamani yake, anayesimama imara, na haachii mwingine akumwangamize.

🗣️Kikao kimeisha Mwanangu… sasa ni juu yako kulifanyia kazi somo hili. Usisahau kufollow channel yangu ili tuendelee kujifunza pamoja

TABIA 10 ZA SINGLE MOTHER ASIYE NA SHUKRANIKatika jamii za sasa, kuna wanawake wengi wanaishi k**a single mothers (wazaz...
29/09/2025

TABIA 10 ZA SINGLE MOTHER ASIYE NA SHUKRANI
Katika jamii za sasa, kuna wanawake wengi wanaishi k**a single mothers (wazazi wa k**e wanaolea watoto peke yao). Wapo ambao ni wenye hekima, heshima na moyo wa shukrani, lakini pia wapo wengine wanaoonyesha tabia za kutokujali na kukosa shukrani. Tabia hizi hujitokeza waziwazi, na huwaathiri wanaume wanaohusiana nao kwa namna tofauti.

Wanaume wa kiume wenye misimamo imara (masculine men) mara nyingi huwakwepa wanawake hawa, lakini wanaume tegemezi kihisia (emotionally dependent men) hujikuta wakiwapenda sana hata k**a wanateseka.

Hapa chini kuna ishara 10 za tabia za single mother asiye na shukrani, kisha tutajibu kwa nini wanaume wa kiume wanawakwepa, na kwa nini wanaume tegemezi kihisia huwapenda sana.

1. Kutojali Msaada Anapopewa

Single mother asiye na shukrani hupewa msaada wa kifedha, kimawazo au kimwili, lakini badala ya kushukuru, huona ni wajibu wa kila mtu kumsaidia.
Hii inamfanya mwanaume wa kiume ajisikie anadharauliwa na humkwepa. Lakini mwanaume tegemezi kihisia huamini atathaminiwa baadaye, hivyo ataendelea kumpa msaada bila kikomo.

2. Kuchukulia Wanaume K**a ATM

Wanawake wa aina hii huona mwanaume si mtu bali ni chanzo cha pesa. Hawana mapenzi ya kweli, bali hufikiria zaidi faida.
Mwanaume wa kiume atakimbia kwa sababu hataki kutumiwa. Lakini mwanaume tegemezi huamini akitoa pesa nyingi zaidi, ndipo ataaminiwa na kupendwa.

3. Kutoonyesha Shukrani Ndogo Ndogo

Hata mambo madogo k**a zawadi ndogo au msaada wa ushauri hawajali. Hakuna thank you, hakuna tabasamu, hakuna kuthamini.
Kwa mwanaume aliye na heshima ya kiume, hii ni ishara ya hatari. Lakini mwanaume tegemezi husema moyoni, “labda hajafurahishwa vya kutosha, ngoja nijitahidi zaidi.”

4. Kuwashutumu Wanaume Wote
Mara nyingi single mother asiye na shukrani huwa na historia ya kulalamika kuhusu wanaume wote: “wanaume hawana maana, wote ni wabaya, hakuna wa kuaminika.”
Mwanaume wa kiume atajua huu ni mtego na ataepuka. Mwanaume tegemezi huona ni nafasi ya kuthibitisha yeye ni tofauti na wengine.

5. Kujiona Mwathirika wa Maisha

Badala ya kuchukua jukumu la maisha yake, hujiona mwathirika kila mara – akilaumu ex wake, serikali, au mazingira.
Mwanaume mwenye nguvu ataona hana nafasi ya kusaidia mtu anayeishi kwenye lawama. Lakini mwanaume tegemezi hupenda nafasi ya kuokoa mtu, na hapo ndipo huingia kwenye mtego wa kihisia.

6. Kutumia Watoto K**a Silaha
Single mother asiye na shukrani mara nyingi hutumia watoto wake k**a chombo cha kulazimisha mwanaume kumpa msaada au kubaki kwenye uhusiano.
Wanaume wa kiume huchukia kutumia watoto k**a chombo cha maumivu. Lakini mwanaume tegemezi huona ni jukumu lake kufidia pengo na anajitolea kupita kiasi.

7. Kutokuwa Mwaminifu Katika Mapenzi
Kuna single mother asiye na shukrani ambaye hucheza michezo ya kimapenzi, huficha mambo, na mara nyingi hana uaminifu.
Mwanaume wa kiume hatakubali kudharauliwa kwa heshima yake, lakini mwanaume tegemezi hupuuza ishara zote, akijifariji kuwa mapenzi ya kweli ni uvumilivu.

8. Kiburi na Kudharau
Hutumia maneno ya dharau, hujiona juu ya kila mtu na hawezi kushuka kusamehe au kushukuru.
Mwanaume wa kiume huona kiburi ni sumu ya mapenzi, lakini mwanaume tegemezi huamini uvumilivu wake utabadilisha tabia hiyo.

9. Kukimbilia Haki Badala ya Wajibu
Wanadai haki zao kila mara (“nina haki ya kuheshimiwa, kusaidiwa, kufadhiliwa”), lakini hawatoi wajibu wala kushukuru.
Hii humkimbiza mwanaume wa kiume, lakini humvutia mwanaume tegemezi ambaye anaamini kutoa bila kikomo kutaleta upendo.

10. Kuwatumia Wanaume Wema K**a Daraja
Single mother asiye na shukrani hutumia wanaume wema kupiga hatua kimaisha, lakini akifanikiwa hutupa uhusiano huo k**a kiatu cha zamani.
Wanaume wa kiume wanagundua mapema na huondoka, lakini mwanaume tegemezi huendelea kuvumilia kwa matumaini ya kuthaminiwa baadaye.

Kwa nini wanaume wa kiume wanawakwepa?

Kwa sababu wanaume wa kiume wanajua thamani yao. Wanajua mapenzi ya kweli lazima yawe na heshima, shukrani na uwajibikaji. Wanapomuona single mother asiye na shukrani, wanajua ni hasara ya muda na nguvu.

Kwa nini wanaume tegemezi kihisia huwapenda sana?

Kwa sababu wanaume hawa mara nyingi hubeba White Knight Syndrome – hamu ya kuwaokoza wanawake waliojeruhiwa. Huamini wakijitolea vya kutosha, hatimaye watapendwa. Upweke wao wa ndani huwafanya kuvumilia maumivu makubwa kwa matumaini ya kupata uthibitisho wa upendo.

👉 Hii ni somo kubwa kwa wanaume wote: mapenzi ya kweli hujengwa kwa shukrani, heshima na uwajibikaji. Wanaume wenye nguvu wanajua hii, na wanaume tegemezi wanapaswa kujifunza kujithamini kwanza kabla ya kujitolea kupita kiasi kwa watu wasiothamini.

NIMEREJEA TENA. Tuendelee kusupport kwa kushare kazi zangu, nami nasema"Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo...
26/09/2025

NIMEREJEA TENA. Tuendelee kusupport kwa kushare kazi zangu, nami nasema

"Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo k**a ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga".

Yohana 14:27

Story picha: NGUVU YA PENZI(03)MTUNZI:DANifordy benMAWASILIANO: +255711444410Tuliishia marko anamuona mpenziwe baada ya ...
05/09/2025

Story picha: NGUVU YA PENZI(03)
MTUNZI:DANifordy ben
MAWASILIANO: +255711444410

Tuliishia marko anamuona mpenziwe baada ya kumsubiri kwa muda mrefu sana, lakini anatambua kuwa yuko tofauti na siku zote....

Sasa tuendelee

Wakati zuhura akitoka nyumbani alimuacha mamaye akijianda kuondoka kwa kuhakikisha mjukuze wote wanakula vyema ili asimpe mzigo mwanaye wa maandalizi ya chakula, kwakuwa aliufahamu utundu wao. Na baad ya kuondoka ndipo zuhura alipopata nafasi ya kutoka kwenda kwa marko.

Kadri zuhura alipokuwa akisogea ndipo marko alikuwa akiona alama za uvimbe mwilini mwa mpenziwe, jambo lililomshangaza mno ijapokuwa hakuthubutu hata kutamka neno mpaka zuhura alipomkaribia kabisa.

"Vip kipenzi changu mbona hivyo leo harafu..."

"Usiniite hilo jina tena marko umenisababishia nimepigwa mwenzio mpaka nimeumia hivi, tafadhari mimi na wewe mwisho sasa na naomba tuachane kuanzia leo".

"zuhura".

"Aah staki bwana, niache".

"Nisikilize basi nitakacho kukwambia ijapo kwa dakika moja tu zuhura, ina maana umesahau ahadi zako zote? Hivi unadhani nitaishije bila wewe na huku tulipanga kuwa pamoja daima. Unatambua kuwa sina tofauti kabisa na majivu ya karatasi mbele ya upepo muda wote nitaishia kupepea nikipurizwa, kwanini uniache naangamia kwa kiu ilihali uko na maji? Pole kipenzi changu kwani si kusudio langu kukufanya uumie ni maisha tu! Amini kuwa hakuna mafanikio bila mapito ya kukupa ujasiri na hili ni jambo dogo tu twaweza zungumza hapaswi kugombana".

Marko alitumia ulimi wake vyema kuhakisha nduru za filimbi zinamtoa nyoka ndani ya pango, kutokata kwake tamaa kulifanya faraja upya ndani mwa zuhura ambaye ni dhahiri kipigo kile kilifanya maamuzi magumu pasi fikra. Wakati huo zuhura alikuwa amesimama wima, kando ya marko aliyekuwa bado amekaa katika jiwe kubwa akimtazama marko kwa jasho lililojaa husda. Kislani alichokuwa nacho kilizidi hata kile cha uke wenza mbele ya mme kipenzi cha wote. Nguvu kubwa aliyoitumia marko katika ushawishi mbele ya binti yule mchomovu katika mahusiano hatimaye ilifanikiwa kumlaghai zuhura mwenye mapenzi ya dhati kwa marko, naye akaingia kingi na kurudi katika mstari ambapo baada ya mazungumzo ya muda yenye kufarijiana wawili wale waliirejesha furaha yao upya k**a zamani na kusahau maumivu, kisha marko siku hii aliamua kumsindikiza nyumbani zuhura. Na kwakuwa siku hii zuhura alimjuza marko kuwa mama na baba yake hawapo nyumbani basi, baada ya kufika walikaa nyumbani hapo wakipiga story za hapa na pale mpaka usiku ukawakuta hapo, mwisho stori hizo zilifanya tamaa ya kimwili kumuingia marko ambaye alianza kutamani kula tunda la mpenziwe zuhura.

"Zuhura tafadhari mpenzi wangu, si umesema mama na baba yako hawapo? Basi naomba leo ijapo nidodose dodo kidogo mwenzi nishapata mshawasha".

Alizungumza marko kwa sauti ya huba iliyokwaruza kiasi kufanya isik**e vyema masikioni mwa mpenziwe ambaye alikuwa ametulia tuli kumsikiliza.
ITAENDELEA

Je atafanikiwa mpango wake marko? Usikose sehemu ijayo

Story picha: NGUVU YA PENZI(02)MTUNZI: Danifordy benMawasiliano: +255711444410Tuliishia zuhura akimtafuta marko baada ya...
24/08/2025

Story picha: NGUVU YA PENZI(02)
MTUNZI: Danifordy ben
Mawasiliano: +255711444410

Tuliishia zuhura akimtafuta marko baada ya kuto muona eneo la makutano yao...

SASA TUENDELEE.

Zuhura hakuwa amajua ni nini kimemsibu mpenziwe alikuwa akiita kwa sauti ya chini mno(mnong`ono) ili kutosababisha watu wengi kusikia kijijini pale maana hawakuwa na siri hata kidogo.

"Marko..markooh uko wapi jitoke basi ijapo hata nikuone sura yako kipenzi changu hivi unajua nimekumiss sana".

Hakupata majibu yoyote kutoka upande wa pili zaidi alisikia msakanyo wa hatua zikikanyaga kutoka katika kichaka na kuelekea upande alio kuwako zuhura, hali ya woga ilianza kumtanda na kumfanya kupiga hatua za tahadhari kurudi nyuma ili tu! Kujitengenezea mazingira ya kutimua mbio.
"Zuu mpenzi usiogope ni mimi, nilitaka kujua k**a kweli unanipenda ndio maana nilijificha".

"Tookapa, umenipa wasiwasi mimi nikajua hujaja".

Aliongea zuhura kwa kujidekeza kabisa huku akichumpa kutoka ardhini na kumrukia marko kwa kumbato zito mno lenye kuambatanishwa na mabusu mfurulizo, baada ya kuzunguza k**a kawaida waliahidiana kukutana kisimani hapo siku ya jumamosi saa tisa alasiri kwani siku hii ilikuwa si siku ya shule kwa marko na wakaagana na kila mmoja alikuwa ameelekea kwao, kwa upande wa marko aliyekuwa akiishi na mama yake pekee hakukuwa na shida hata kidogo. Ila shida ilikuwa kwa zuhura ambaye alikuwa akiishi na baba pamoja na mama yake tena wakali mno.
"Leo maji ulipanda kuteka mlimani?".

Alihoji mama kwa ghadhabu huku mkononi akiwa ameshika bakora ndefu mbele ya mwanaye.
"Samahani mama kulikuwa na foleni hivyo nikawa nikisubiri zamu yangu ifike".

"Unayemdanganya nani hapa, si ulikuwa na kitoto cha mjane wewe undhani sijapata taarifa zako sio, sasa wacha nikufunze kuwahi ukitumwa".

Alizungumza mama zuhura, na bila kusubiri alizituliza bakora nyingi katika mwili wa mwanaye ambaye alilia kwa uchungu mno akiomba kisamehewa, lakini mama yake asimsikilize na alipo ridhia kwa adhabu aliyotoa alimuamuru bintiye kwenda kuoga haraka. Zuhura alipomaliza kila kitu alielekea kulala mapema mno kwani siku hii hakuwa na furaha kabisa na ndio siku aliyomchukia mno marko na kuahidi kuwa siku ambayo wangelikutana basi ndio angemjuza marko kuwa waachane.

Hakika usiku wa deni hauchelewi kukucha, kwani juma mosi ilitimia na marko ndiye alikuwa wa kwanza kufika mahali pa miadi akimsubiri zuhura ambaye alichelewa kufika saa zima, na wakati matumaini ya marko yakififia kumuona zuhura wake tayari kabisa kwa kuondoka, akamuona zuhura akija tena akiwa mnyonge mno..
ITAENDELEA.
https://youtu.be/4Ns614FnfCc?si=SPMf2nBIU36FgsId

Je zuhura atamwacha marko? Na itakuwaje unadhani!? Basi usikose sehemu ijayo

Story picha: NGUVU YA PENZI (01)Mtunzi: DANIFORDY BENMawasiliano:+ 255711444410Zuhura alikuwa ni binti pekee kwa mamaye ...
23/08/2025

Story picha: NGUVU YA PENZI (01)
Mtunzi: DANIFORDY BEN
Mawasiliano:+ 255711444410

Zuhura alikuwa ni binti pekee kwa mamaye pamoja na babaye, zuhura alikuwa binti mrembo mno kwa muonekano hata tabia yake pia. Ukweli ni kuwa alichechefya mioyo ya wengi mno mtaani kwao, shuleni hata mjini alikokuwa akielekea kuuza mboga za majani alizokuwa akizilima baada ya kutofanikiwa kuchaguliwa kuendelea na kidato chakwanza, hakuwa mtu wa majigambo juu ya umbo na sura yake alivyokuwa amejaliwa kwani alikuwa msikivu kwa kila aliyekuwa akizungumza naye bila kujari, rika, kabira wala jinsia.

Zuhura alikuwa ni muaminifu mno mbele ya kipenzi chake marko ambaye alikuwa akisoma kidato cha nne shuleni itebe, mkoani sawe nchini nyumba nitu. Ndoto za wawili hawa ilikuwa ni kuhakikisha kuwa wanakuwa pamoja katika maisha yao yote. Hivyo ikawa marko akitoka shule tu anakwenda kumsubiri zuhura karibu na kisima katika jiwe kubwa lililokuwa chini ya mbuyu.

Walikuwa wakifurahi kila wakikutana kwani walikuwa wakisimuliana vingi vya ndani na kupanga malengo yao. Siku moja zuhura aliaga kuwa anaelekea mtoni k**a kawaida yake ambapo alifika kisimani akaiweka ndoo na kuanza kuita kwa sauti k**a kawaida yake kumjuza marko k**a alikuwa amefika. Lakini hakupata majibu hivyo ikamlazimu kuanza kumtafuta mpenziwe huku moyoni akiwa na hofu kubwa mno...
ITAENDELEA

yuko wapi marko na nini hatima ya kisa kibwagizo hiki?

SIKU ZA UHAI WANGU (12)Na. Danifordy benMAWASILIANO: +255711444410TULIISHIA.Fatuma ameandika ujumbe katika karatasi na k...
19/08/2025

SIKU ZA UHAI WANGU (12)
Na. Danifordy ben
MAWASILIANO: +255711444410

TULIISHIA.
Fatuma ameandika ujumbe katika karatasi na kisha kuchukua simu yake na kuandika ujumbe kwa mama yake, huku kule kwa hance anapewa taarifa ya kuwa yupo huru pale hospital ila atatakiwa kuripoti polisi baada ya kupona.

SASA TUENDELEE.

Baada ya kumaliza kuandika ujumbe ule fatuma alisogelea kichupa kidogo kilichokuwa na dawa ndani yake, ilikuwa ni chupa ambayo ilikuwa na dawa ya kuua wadudu katika mazao. Aliitazama kwa muda kisha akaongeza na vidonge alivyokuwa navyo ndani mule ambavyo alivibugia na kushushia sumu ile kisha akaenda kulala kitandani. Alitulia pale kwa muda kisha akaanza kufurukuta kwa maumivu makali ya tumbo, maumivu haya aliyokuwa akiyagugumia chinichini pasi msaada na dakika 45 utulivu ulichukua nafasi, wakati huo rafikiye maria alikuwa akifika mlangoni na kubisha hodi kwa muda bila majibu, mpaka palr ilipomlazimu kuomba msaada wa boda aliyemleta wasaidiane kuuvunja mlango baada ya kutambua kuwa ulikuwa umefungwa kwa ndani. Nini kingefuata zaidi ya umati wawatu kushuhudia mwili mfu uliokuwa juu ya kitanda kilicholowa kwa povu zito lenye harufu mbaya. Hakika kilikuwa kilio chenye kuumiza hasa pale waliposoma ujumbe ule ulioachwa na fatuma kabla ya kufanya maamuzi magumu.

SIKU ZA UHAI WANGU.
Naacha ujumbe huu kwa kila aliyehai, kuna mengi nimefanya mema ila hili limeniumiza na nimeamua kujiondoa uhai k**a hukumu ya nilichofanya. Walimwengu kijana yule hana hatia ila mapenzi ndio yalipelekea nitake kuupoteza uhai wa mtu asiye na hatia. Ikawe hivyo aachiwe aendelee na maisha yake ya kuipambania kesho yake. Mimi natangulia kuwaandalia makazi.

Ulisomeka ujumbe huo ambao aliucha fatuma, na kule kwa mama yake ulisomeka ujumbe mfupi.

"Ulinifunza kuwa mwema, ila nimevunja kauli yako basi acha nijipe adhabu kabla ulimwengu haujaniadhibu".

Ilikuwa huzuni kwa wengi ila hakuna arudishae muda nyuma na parapanda ikalia kwa fatuma na taratibu zilifuatwa kisha fatuma akazikwa.

Habari hizi kwa hance zilikuwa mbaya ila haikuwa na namna ya kuzui zaidi ya kumuombea apunguziwe adhabu ya kaburi akapata ufufuo mapema mtu aliyempenda. Matibabu yalikwenda sawa na hance akaruhusiwa hospital akaelekea kituo cha polisi kufuta jalada la kesi yake na kurudi nyumbani akiwa chini ya ungalizi wa kitabibu na nesi sofia. Mawasiliano yao yalikwensa sawa na mwisho ukaribu wao ukaenda mbali zaidi na hatimaye wakawa wapenzi na sofia alimfungulia biashara hance, maisha ya kasonga nao wakafuata itifaki ndoa ikafungwa wakiwa tayari wana watoto wawili.
MWISHO.

FUNZO, Kuna mengi ya kufikiri kabla ya kufanya maamuzi ukiwa na hasira, hata wahenga walisema hasira hasara hivyo chunga hasira yako isije kukugharimu kesho.

Address

Njombe
Iringa

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Story funzo posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Establishment

Send a message to Story funzo:

Share