07/12/2025
Kaburi la Mzee Martin Kiyeyeu aliyefariki mwaka 1974, k**a linavyoonekana katika picha kando ya barabara ya Iringa-Mbeya
Kaburi la Kiyeyeu lipo katika Njiapanda ya Mlolo, pembezoni mwa barabara kuu iendayo Mbeya ukitokea Iringa, upande wa kulia ndani ya Halmashauri ya Wilaya ya Iringa. Ni kaburi la mganga maarufu wa jadi aliyewahi kuhudumu katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo. Ingawa alifariki miaka mingi iliyopita, kaburi lake linaonekana k**a limejengwa jana kutokana na uimara na muonekano wake.
Inasemekana kuwa baada ya kifo chake alizikwa kwa kufuata taratibu za kimila za Machifu, ambapo alizikwa akiwa ameketi na akiwa amesindikizwa na mtu aliye hai aliyejitolea kuzikwa naye. Hadi leo, kaburi hilo limeendelea kuwashangaza watu wengi kutokana na maajabu yanayolizunguka.
Moja ya matukio yaliyowahi kutokea na kush*tua wengi ni wakati Shirika la Umeme (Tanesco) lilipokuwa likiweka nguzo za umeme kando ya barabara hiyo. Nyaya za umeme zilipofikishwa eneo lililopakana na kaburi la Martin Kiyeyeu, nguzo zilipita eneo hilo na nyaya zika pita juu ya kaburi hilo chakushangaza ni kwamba umeme ulipita vizuri kabla na baada ya eneo la kaburi, lakini juu ya kaburi hilo pekee hakukuwa na msongo wowote wa umeme. Tukio hilo liliwashangaza hata wahandisi wa Tanesco, na hatimaye wakaamua kuhamisha baadhi ya nguzo ili kulipisha eneo hilo.
Inadaiwa pia kwamba kulishindikana kuliondoa kaburi hilo mara mbili, na katika majaribio hayo watu wawili walipoteza maisha mmoja akishambuliwa na nyuki, na mwingine kufariki ghafla akiwa anaendesha tingatinga kwaajili ya kuliing’oa kaburi hilo. Baada ya matukio hayo, mila na matambiko yalifanyika, na hatimaye kaburi hilo pamoja na mengine 21 yaliyokuwa eneo hilo yalihamishiwa upande wa pili wa barabara, ambako tayari kulikuwepo kaburi la mtoto wa k**e wa Kiyeyeu.
Hadi leo, simulizi la Kaburi la Kiyeyeu limeendelea kuwa miongoni mwa masimulizi yanayovutia watu wengi kutokana na maajabu na ya eneo hilo