Bongo connect

Bongo connect BONGO CONNECT- Breaking News-Entertainment-Trending Stories
Follow kwa habari za uhakika na burudani kila siku.

05/09/2026

Wafanyabiashara wanaojishuhulisha na ukaangaji wa samaki katika soko la Ferry manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara wamegoma kukaanga samaki kwa kile wanachodai kuuziwa kuni kwa bei ya juu.

Mgomo huo umejiri September 5,2026 huku viongozi wakiendelea na jitihada za kuhakikisha changamoto hiyo inatatuliwa na huduma zinaendea k**a kawaida.

# bongo connect

05/09/2026

Fikiri Khamisi Masana aka Sir Lisco, aliingia South Africa mwaka 1993. Tanzania anatokea Manzese hila kiuhalisia anatokea Morogoro.

Sir Lisco ni mwanangu wa faida pia aliomba nimtafutie ndugu zake. Kisha nilifanya kazi hiyo mpaka nikafanikiwa kuwapata dada zake wawili Zuhura na Subra

Sir Lisco alijiandikisha vizuri tu kwa safari ya kutoka Cape Town kuja Tanzania 🇹🇿 kupitia ndege yetu ya Msaada wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Ubalozi wetu wa Watanzani South Africa 🇿🇦

Leo tarehe 4/9/2026 siku ya safari kaka mkubwa kagoma. Ikabidi kiongozi wangu Chichi katibu mkuu wa Tac Cape Town atumie nguvu.

Lakini walipo mfikisha sehemu husika tena mbele ya Mhe. Balozi James G. Bwana Balozi wetu wa Watanzania South Africa, Lisco aliondoka huku akiongea maneno makali sanak kiasi cha Mhe. Balozi James G. Bwana kuona sasa,huenda akaleta shida ktk ndege

Lisco ameondoka na kuingia mtaani kuishi maisha yake ya kulala nje tena na kupata tabu

Nimeumia sana kwa kweli, sema nini poleni sana viongozi wangu wote wa Cape Town ambao mlijitolea kumpambania Lisco kutoka moyoni kwenu, Lisco kaniumiza moyo wangu sana

04/09/2026

Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran IRGC,limeanzisha Mashambulizi mwengine kuelekea Kwenye Kambi za kijeshi za Marekani zilizopo nchini Jordan.

Taarifa kutoka Makao Makuu ya Jeshi hilo zinasema, Mashambulizi hayo yamefanywa ili kuiwahi Marekani aliyepanga kushambulia nchini Iran, kupitia Kambi zake zilizopo huko Jordan.


04/09/2026

HUWEZI AMINI HAPO WALIKUA NA WAZIRI KABISA TENA WALUKUA NDO WAMEWEKWA KIKAAANGONI 😂😂😂😂

04/09/2026

Miongoni mwa Watanzania waliorejea nchini kutoka
Afrika Kusini amesema anajisikia furaha kurejea Tanzania baada yabkukaa kwa muda nchini humo.

Kijana huyo amesema maisha nchini Afrika Kusini si rahisi kwa
wageni, akibainisha kuwa tofauti za elimu na hali ya uchumi ni
miongoni mwa mambo yanayochangia kuwepo kwa tofauti za
kitabaka katika jami.

Alfajiri ya leo, Septemba 4, 2026, kundi la Watanzania limewasili
nchini likitokea Afrika Kusini.

Kundi jingine la Watanzania linatarajiwa kuwasili nchini mchana wa leo, ljumaa, Septemba 4, 2026.

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda (UPDF), Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ameibua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kut...
04/09/2026

Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi ya Uganda (UPDF), Jenerali Muhoozi Kainerugaba, ameibua mjadala mkubwa mitandaoni baada ya kutoa kauli kuhusu uwezo wa wanaume katika tendo la ndoa na kupata watoto.

Kupitia ujumbe aliouchapisha, Jenerali Muhoozi amesema wanaume ambao hawawezi kudumu zaidi ya dakika moja wakati wa tendo la ndoa na kuwapa wanawake ujauzito wanapaswa kuk**atwa.

Jenerali huyo aliendelea kwa kutumia lugha kali, akidai kuwa wanaume wenye hali hiyo hawana faida.

Kauli hiyo imezua mijadala mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii, huku baadhi ya watu wakiichukulia k**a mzaha, wakati wengine wakipinga wakieleza kuwa uwezo wa mwanaume katika tendo la ndoa unaweza kuathiriwa na sababu mbalimbali za kiafya na kisaikolojia.

Wewe unaonaje kauli ya Jenerali Muhoozi?

Follow

Mamlaka za Usalama nchi Iran,zimechapisha Picha za wanajeshi sita  wa Iran,wakiwemo wanajeshi wa anga walio uwawa Katika...
03/09/2026

Mamlaka za Usalama nchi Iran,zimechapisha Picha za wanajeshi sita wa Iran,wakiwemo wanajeshi wa anga walio uwawa Katika mashambulizi ya Marekani yaliyofanywa siku Chache nyuma.


SOLO (1996)KUNA filamu za miaka ya 90 ambazo ukiangalia leo unaweza kugundua zilikuwa mbele ya wakati wao. Solo ni moja ...
03/09/2026

SOLO (1996)
KUNA filamu za miaka ya 90 ambazo ukiangalia leo unaweza kugundua zilikuwa mbele ya wakati wao. Solo ni moja ya hizo. Filamu hii inachanganya action na teknolojia, lakini kinachofanya iwe tofauti ni kwamba mtu tunayemfuata si mwanajeshi wa kawaida. Ni mashine iliyotengenezwa kwa ajili ya kuua, lakini baadaye inaanza kujifunza maana ya huruma na kuchagua yenyewe upande wa kusimamia.

Filamu inamzungumzia Solo, android ambaye ametengenezwa na jeshi kwa ajili ya mapambano. Ana nguvu kubwa, anaweza kutumia silaha mbalimbali na ameundwa kufuata amri bila kuuliza maswali. Anatumwa katika nchi ya Amerika ya Kati kwa ajili ya kukabiliana na waasi.

Lakini mambo yanabadilika baada ya Solo kushuhudia watu wasio na hatia wakiteswa na kuuawa. Kitu ambacho hakikupangwa kwenye mfumo wake kinaanza kujitokeza, anaanza kuwa na huruma na kutambua kuwa si kila mtu anayepaswa kupigwa risasi ni adui.

Hapo ndipo Solo anaanza kuasi amri za waliomtengeneza. Anakimbia na kuishi pamoja na watu wa kijiji ambao walikuwa wanateswa na kikundi cha wapiganaji kinachoongozwa na Rio.

Wanakijiji wanamchukulia k**a mgeni mwanzoni, lakini polepole Solo anaanza kuwa sehemu yao. Anakuwa mlinzi wao na kutumia uwezo wake kuwasaidia kujilinda dhidi ya watu waliokuwa wakiwashambulia.

Kijijini hapo, Solo pia anakutana na mtoto anayeitwa Miguel. Urafiki wao unakuwa muhimu kwa sababu Miguel anamfundisha mambo ambayo hayawezi kupatikana kwenye programu ya kijeshi, ikiwemo namna ya kuishi k**a binadamu na hata kutumia ujanja badala ya nguvu pekee.

Lakini jeshi haliwezi kumuacha Solo aende zake. Wanamtuma Colonel Madden pamoja na kikosi maalumu kumtafuta na kumrudisha. Madden anamchukia Solo kwa sababu anaamini teknolojia hiyo mpya inaweza kuwafanya wanajeshi k**a yeye wasiwe na kazi tena.

Hapo ndipo vita kubwa inaanza. Solo anajikuta akipambana na watu waliomtengeneza huku akijaribu kuwalinda wale ambao sasa amewaita marafiki zake.

Na k**a hiyo haitoshi, jeshi linatengeneza toleo jingine lenye nguvu zaidi, ambalo linatumwa kumuangamiza Solo. Sasa anakuwa anakabiliana na kitu kinachofanana naye, lakini kimeundwa bila huruma na kwa lengo moja tu, kumuua.

Tarehe 20 Desemba 2020, beki wa zamani wa Barcelona, Gerard Piqué, aliwahi kuonekana kwenye picha akiwa amevalia jezi ya...
03/09/2026

Tarehe 20 Desemba 2020, beki wa zamani wa Barcelona, Gerard Piqué, aliwahi kuonekana kwenye picha akiwa amevalia jezi ya Simba SC, jambo lililozua gumzo miongoni mwa mashabiki wa soka nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa mdau mmoja wa soka, ukubwa wa jina la Piqué hauishii kwenye mitandao ya kijamii pekee, bali ni miongoni mwa wachezaji waliowahi kutengeneza historia kubwa katika soka la dunia baada ya kucheza pamoja na mastaa k**a Lionel Messi, Xavi Hernández, Andrés Iniesta, David Villa na Sergio Ramos.

Mdau huyo pia amegusia maisha binafsi ya Piqué, akimtaja k**a aliyewahi kuwa mume wa mwanamuziki Shakira, ambaye amewahi kutumbuiza kwenye matukio makubwa ya Kombe la Dunia.

Akilinganisha hilo na kampeni za jezi za Yanga, mdau huyo amesema klabu hiyo imechukua baadhi ya mbinu ambazo Simba iliwahi kutumia katika kujenga chapa yake, akisema Yanga ingekuwa bora zaidi k**a ingetumia njia zake binafsi za ubunifu.

Aidha, mdau huyo ameibua mtazamo kwamba hatua hizo huenda zikawa zinatumika kuwafanya mashabiki wa Yanga kuelekeza nguvu kwenye mambo mengine, badala ya kuendelea kujadili suala la ujenzi wa uwanja.

✍️ Ameandika Mdau wa Mpira

👉 Je, unaunga mkono hoja za mdau huyu?

Jeshi la Walinzi wa mipaka ya Iran limesema,limek**ata Meli ya Mafuta kutoka nchi za ghuba iliyokuwa na lita 382,000 za ...
02/09/2026

Jeshi la Walinzi wa mipaka ya Iran limesema,limek**ata Meli ya Mafuta kutoka nchi za ghuba iliyokuwa na lita 382,000 za Mafuta na kuwashikilia wafanyakazi 11 wa kigeni waliokuwa kwenye Meli hiyo.


Address

Dar Es Salaam

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Bongo connect posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share