17/06/2026
utafanyaje ukijikuta kwenye Hali k**a hii
unak**atwa na watu usiowajua wanakupeleka sehemu ambayo ata hujui wanakuingiza kwenye chumba ndogo wanakufunga.
wao wantoka nje lakini hawajafunga mlango lakini wamekufunga na chain ili usitoke.
ukakaa pale bila kujua kinachofuata, ukaskia usingizi ukajilaza baadae kidogo unashtuka unaskia joto na hewa imekuwa nzito pale ndani, unaamua kujifungulia ili utoroke unafanikiwa kufungua chain na kuanza kuelekea mlangoni ambako kunaonekana kuko wazi ,
Unafika mlangoni unataka kitoka tu unajikuta umejigonga ukutani
kumbe huwo sio mlango ni picha tu imebandikwa ikafanania mlango,
unachanganyikiwa unaanza kuwa na hofu unageuka huku na huko kutafuta pakutokea unaona kma vitobo vya kuingizia hewa unakimbilia kuvuta hewa unakuta nako hakuna
ivo vitobo ni michoro ilofanana na vishimo tu,
unazidi kuogopa na jasho linakutoka., hewa inazidi kuisha ndani unatamani kupiga kelele lakini nguvu zinakuishia kabisa
unaona kifo machoni bila kujua utafanyaje.
Unaanguka chini tayari kungoja tu mwili uzime upoteze maisha ,
kwa mbali ukiwa hoi unaskia sauti inakuongelesha ikikutaka utoe ushirikiano nae utaje namba ya siri ya accout yako ya Bank yenye taslim shilingi bilion 50 la sivyo utaachwa ufe kwa kunyimwa hewa
je utaamua nini kutoa usirikiano au bora ufe tu