23/04/2026
Nimefanikiwa Kutembelea Basketball Hall of Fame, Massachusetts USA, ilikuwa ndoto iliyotimia. Nilicheza sana kikapu na Safari yangu ya basketball ilianza nikiwa nasoma Consolata Seminary Mafinga O-Level, Ruaha Sec Iringa, Galanos Sec, Club ya Hotspring Iringa na leo nimefika sehemu yenye historia ya magwiji niliyokuwa nawafuatilia tangu zamani.
Picha hii nikiwa mbele ya sanamu la Dr. James Naismith, mwanzilishi wa mchezo wa basketball mwaka 1891 hapa Springfield, Massachusetts, inanipa hisia kubwa sana. Hapa ndipo chimbuko la mchezo huu ulioleta furaha kwa dunia nzima, ndiyo maana sehemu hii huonekana k**a nyumbani kwa basketball.
Ndani ya Hall of Fame nimeona historia za legends k**a Michael Jordan (6× NBA Champion, 5× MVP), LeBron James (all-time leading scorer, 4× NBA Champion) na Kobe Bryant (5× NBA Champion, 81 points in one game), pamoja na wengine wengi walioweka records zisizofutika.
Nimevutiwa sana kuona namna credits, records na mafanikio ya wachezaji yanavyotambuliwa na kuheshimiwa. Hii imenikumbusha kuwa kazi nzuri, nidhamu na juhudi huwa hazipotei. Ndoto yangu ilikuwa kufika hapa… leo imetimia. 🏀🇺🇸✨ Legends BasketballJourney