19/06/2020
RIWAYA: PANDORA.
MWANDISHI: Octa PK.
UMRI: 18+
Mawasiliano: +255624102400.
+255746318516.
WhatsApp:+255746318516.
*****SEHEMU YA KUMI NA NNE*****
ILIPOISHIA...
"Asante, yaani umekuwa binti mkubwa sasa hivi." Alizungumza Ramia huku akitabasamu na wakati yeye akiendelea kuzungumza Sia alienda kwa Jaran na kumshika mkono kisha wakatoka nje huku wakiwaacha wengine waliendelea mazungumo yao.
"Yaani Sia, nazungumza nae hata hajali, akili yake yote ipo kwa Jaran." Alilalama Ramia.
"Wewe acha tu, kila kukicha analazimisha tuje Kisan nia yake ikiwa kumuona Jaran. Hapo atakuwa amefurahi kweli." Alizungumza Niaya na kuwafanya wote waliokuwa mule wacheke.
"Ehe, naomba mniambie kulikoni na mizigo hiyo msiyohitaji ishushwe?" Aliuliza Dahil.
ENDELEA...
"Ndugu yangu, ujio wetu mahali hapa ni kuja kusema kwaheri, kwani muda wetu wa kurudi Pandora, sasa umewadia." Aliongea Lutas.
"Mbona mapema sana mmeamua kurudi huko, hamuoni kwamba inaweza kuwa hatari kwenu?" Aliuliza Dahil kwa mshangao.
"Hilo lisikupe shaka shemeji. Hatuendi moja kwa moja kwenye jumba la ufalme. Tutaenda kuishi Kijiji cha mbali na jumba la ufalme." Alizungumza Ramia.
"Sasa k**a ni hivyo, kwanini msiendelee kuishi huku, ikiwa hakuna mnachokwenda kufanya huko? Au kuna jambo hamkupendezwa nalo jamani?" Alilalama Niaya.
"Hapana mdogo wangu, tumeamua kufanya hivyo ili Jaran akaendelee kujifunza na kuzizoea mila na desturi za Pandora. Sasa hivi Jaran ana umri wa miaka kumi na moja, na pia mnafahamu yeye ni mzaliwa wa kifalme, hivyo kwa umri wake huo ni vyema akaenda kuishi huko." Alijibu Ramia.
"Sawa, lakini inawabidi mkae hapa usiku huu, harafu kesho muendelee na safari, hakuna haja ya kuwa na haraka kiasi hicho." Alizungumza Dahil na wao hawakuwa budi kukubakiana nao.
Kesho yake kulipo pambazuka walianza safari ya kuelekea Pandora huku wakiiacha familia ya Dahil ikiwa na majonzi kwani walizoeana kuishi na kutembeleana kila mara ndani ya ardhi ya Gulu. Sia yeye ndio wakati wote machozi yalikuwa yanamtoka maana alijua hivi sasa itakuwa ngumu sana kwake yeye kuonana na Jaran k**a ilivyokuwa hapo awali. Waliondoka mahali hapo huku wakiahidiana kutembeleana kila wakati panapo majaaliwa.
Safari ilikuwa ndefu kiasi, na hawakuhitaji kujificha wapitapo mipakani kwakuwa walikuwa na vitambulisho vya Gulu ambavyo vilikuwa ni majina yaliyokuwa juu ya vibao vilivyochongwa kwa usatadi wa hali ya juu huku vikiwatambulisha kuwa ni wafanyabiashara kutoka Gulu. Na kwakuwa ni miaka mingi imepita, haikuwa rahisi kwa wanajeshi wa Pandora waliokuwa mipakani kuweza kuwatambua na hata hivyo wanajeshi wachache sana waliokuwa wakiwakagua, na hao pia hawakuwa makini na maeneo ya mipaka hiyo kwakuwa walikuwa wanakagua watu wanaoingia huku wakiwa katika hali ya ulevi wa kiasi.
Hali ya mahali hapo pa mpakani haikuwa nzuri kabisa hasa upande wa ulinzi k**a ilivyokuwa miaka mingi iliyopita. Wengine walikaguliwa lakini wengine hawakukaguliwa kwakuwa walitoa kiasi kidogo cha sarafu na kuruhusiwa kupita pasipo kukaguliwa.
"Inabidi tuelekee Kijiji cha Kismani, huko hakuna atakayeweza kutugundua na pia ni mbali kabisa na makao makuu ya ufalme wa Pandora." Alizungumza Latus.
"Hapana, kwa hali ninayoiona ndani ya taifa hili. Ulinzi umedorola sana na sio rahisi wao kufahamu uwepo wetu, hivyo nashauri twende tukaishi humo humo Doma, ila iwe pembeni ya mji huo. Na nafikiri itakuwa vyema k**a tutaenda kuishi kijiji cha Zabi." Alizungumza Zulam Maluñ.
"Nahisi wewe pombe bado zinakuendesha kichwani." Yaani unataka tukaishi ndani ya mji mkuu, huoni hiyo ni hatari kwetu? Twendeni huko Kismani ndio pazuri na ni salama kwetu." Alizungumza Ramia.
"Mimi nadhani, alichokiongea Mzee Zulam ni sahihi kabisa, na hiyo itakuwa ni rahisi kwetu kuzifahamu nyendo za maadui kwa sasa. Pia kijiji cha Zabi kipo pembeni kidogo ya mji mkuu wa Doma." Alizungumza Lutas.
"K**a ninyi mnaenda mji mkuu basi tunaachana hapa, mimi na mwanangu tunaenda Kismani, ninyi nendeni huko Doma. Jaran Twende mwanangu." Alizungumza Ramia huku akianza kumuhimiza farasi wake kuondoka, lakini alishangaa Jaran hata hajisumbui kumfuata.
"Wewe Jaran, hujanisikia? Hebu twende."
"Ukiona hivyo ujue, Jaran hahitaji kwenda huko. Twendeni tumuache yeye aende Kismani." Alizungumza Zulam Maluñ ama Zuma k**a alivyokuwa akijulikana Gulu, huku Jaran na Lutas pia wakaanza kumfuata Mzee Zulam wakimwacha Ramia aliyekuwa amesimama peke yake akitazama njia ya kuelekea Kismani.
Ramia hakuwa budi kumgeuza farasi wake na kuanza kuwafuata wenzake huku akiwa hataki hata kusemezana na wenzake kwakuwa hawakumsikiliza. Njiani Lutas, Jaran na Mzee Zulam walikuwa wakifanya mazungumzo lakini Ramia alikuwa kimya.
"Naona roho ya hasira na uchungu wa kulipiza kisasi uliyoiacha miaka ile ulipoondoka Pandora imekutambua baada ya kukanyaga ardhi ya Pandora. Mimi nilifikiri kwakuwa ni miaka mingi imepita basi itakuwa imekusahau, Kumbe bado inakukumbuka?" Lutas aliuliza kwa kumtania Ramia hali iliyopelekea Ramia amtazame kwa jicho la hasira huku akiwa ameuvuta mdomo kwa mbele.
"Mwache, itakuwa tumefanya makosa kuingia hivi ndani ya Pandora, ilibidi tuchinje kuku kuitoa roho hiyo kabla hatujaingia Pandora." Alitania Zulam na kuwafanya wote wacheke isipokuwa Ramia.
"Naona mnataka kuniudhi." Alizungumza Ramia.
"Sio sisi tunaokuudhi, ila itakuwa ni hiyo roho aliyosema Lutas." Zulam alikazia utani wake.
"Mzee Zuma, hivi unajua nimekustahi muda mrefu? Naona hizo pombe zako bado zinakuzuzua akiri. Niache!" Alizungumza kwa hasira Ramia.
"Usiniite Zuma nimeshakuambia, sasa hivi niite Zulam Maluñ, hilo ndilo jina langu. Zuma nimeshaliacha kwakuwa pombe nimeshaacha pia."
"Hahaha, yaani wewe uache pombe? Hilo gudulia la pombe linalokupa mahaba kila siku mpaka unaweseka kila unapotembea, leo useme umeliacha?" Alizungumza Ramia.
"Ndio, nimeliacha Sasa. Tena nataka nikifika Pandora naoa kabisa binti mbichi hivi, ili anizalie watoto." Alimzungumza Zulam na kuwafanya wote wacheke.
"Khaa, kwa uzee huo ni nani ataweza kukubali kuishi na wewe? Huyo atakuwa hajielewi kabisa, na amekosa mwanaume wa kumuoa." Ramia alimtupia neno hilo Zulam.
"Aliyekuambia Mimi ni Mzee nani. Unafikiri sura yangu kuwa hivi ndio kusema mimi ni Mzee?"
"Kwani Mzee Zuma una miaka mingapi?" Aliuliza Jaran aliyeonekana kuwa mkimya muda mrefu.
"Mimi nina miaka kumi na mbili tu." Alizungumza Mzee Zulam na kuwafanya wote waangue kicheko.
"Halafu na wewe, nimesema usiniite Zuma." Alikazia zaidi Zulam baada ya Jaran kumuita jina asilolihitaji kwa wakati huo huku wenzake wakiendelea kucheka.
"Wewe, tena mimi nitaendelea kukuita Zuma na ninashangaa wewe kujiita Zulam Maluñ wakati mimi nilikuwa najua maana tofauti na hiyo." Alizungumza Ramia.
"Ulifikiri maana ya Zuma ni nini?" Aliuliza Mzee Zulam.
"Nilijua maana ya Zuma ni Zulia la Mavi." Alizungumza Ramia hali iliyopelekea Mzee Zuma aongeze mwendo wa farasi wake kwa kasi pasipo kujibu kitu huku na wengine wakianza kufuata kwa kasi huku wakicheka kwa maana aliyoitoa Ramia. Kasi hiyo iliwafanya waufikie mji mkuu wa Doma majira ya jioni ya siku hiyo.
Baada ya kufika Doma ambao ndio mji mkuu wa taifa la Pandora, walielekea moja kwa moja kwenye Kijiji cha Zabi kilichopo pembezoni mwa mji mkuu wa Doma. Walitafuta nyumba ya wageni wakaweza kuipata.
"Ikiwezekana kesho inabidi tutafute nyumba ya kuishi, na pia tunatakiwa kupata vitambulisho vya uraia wa Pandora kwa majina tofauti na tunayoyatumia, vinginevyo hatutaweza kuishi kwa amani ndani ya mji huu." Alizungumza Lutas baada ya kushusha vitu vyao.
"Hilo nitalishughulikia mimi japo mimi siwezi kubadili jina kwakuwa sina ubaya na mtu huku, lakini pia ili kupata nyumba ya kuishi ni vyema tukazungumza na wahudumu wa hapa." Alizungumza Mzee Zulam.
"Sawa, Jaran hebu muite mhudumu wa hapa." Alizungumza Lutas na kumfanya Jaran akamuite mhudumu wa eneo hilo.
"Samahani, kuna nyumba za kununua ndani ya Kijiji hiki?" Aliuliza Lutas.
"Kabisa, tena mna bahati sana. Mjomba wangu anadaiwa na serikali kodi baada ya kushindwa kuilipia biashara yake ushuru ambao serikali ilikuwa imemwambia kulipa, hivyo kuna nyumba yake iko pembeni kidogo mwa Kijiji hiki." Alizungumza mhudumu wa nyumba ile ya wageni.
"Unaweza kutupeleleka sasa hivi.? Aliuliza Lutas.
"Sasa hivi hapana, maana bado nipo kazini. Nitaagiza mtu akamwambie aje hapa, na ninajua atafika mahali hapa maana ana uhitaji mkubwa sana wa pesa."
"Basi, tunaomba utusaidie kwa hilo."
"Sawa." Alijibu mhudumu kisha akaondoka na alilosema alilitimiza kwani majira ya usiku, mjomba wake na yule mhudumu alifika kwenye nyumba hiyo ya wageni, ambapo mhudumu alimpeleka walipokuwa watu wanaohitaji nyumba.
"Huyu ndio mjomba wangu anayeuza nyumba, nadhani mnaweza kuzungumza nae." Aliongea mhudumu yule kisha akaondoka.
"Karibu sana. Sisi ndio tuliokuwa tunahitaji nyumba ya kuishi na bahati nzuri huyo mhudumu ametuambia kuwa wewe unayo na unatafuta mtu wa kuununua." Alieleza Lutas.
"Ninyi mmetokea wapi?"
"Tumetokea Kismani." Alidanganya Lutas ili kuondoa maswali mengi kwa yule mtu.
"Sawa, nyumba ipo lakini inahitaji maboresho kidogo lakini nadhani mtaipenda. Mimi naitwa Jecca, ningependa kuwafahamu majina yenu pia." Alizungumza Mzee Jecca ambapo Lutas alianza kufanya utambulisho kwa majina ya uongo isipokuwa jina la mazee Zulam Maluñ ambaye yeye hakukuwa na tatizo hata k**a atajulikana.
"Sawa, nashukuru kuwafahamu. Kesho nitakuja kuwachukua ili nikawaonyeshe nyumba hiyo."
"Tunashukuru sana, kesho utatukuta mahali hapa." Alijibu Lutas.
"Samahan pia, Jana wakati tunakuja bahati mbaya tulikutana na vibaka wakatupokonya baadhi ya mizigo yetu, ambapo ndani yake kulikuwa na vitambulisho. Tutawezaje kupata vitambulisho vingine?" Aliuliza Mzee Zulam.
"Vitambulisho vinapatikana k**a ukihitaji. Ni pesa yako tu, maana ndivyo tunavyoishi sasa hivi, ukiwa na pesa basi hakuna unachoshindwa kukipata ndani ya mji huu."
"Tutavipata kwa muda gani k**a tukihitaji sasa hivi.? Aliuliza Ramia.
"Mkihitaji sasa hivi, kesho asubuhi mnavipata. Na k**a mna kiasi cha sarafu hamsini au kipande kimoja cha dhahabu, mnapata vitambulisho kwa idadi yenu." Alijibu Jecca.
"Unaweza kutusaidia kuvipata vitamvukisho hivyo?"
"Inawezekana, lakini kila kimoja inawabidi muongeze sarafu tatu. Jumla ziwe sarafu kumi na mbili ikiwa ni sehemu ya malipo yangu."
"Sawa, tunaomba ufanye sarafu kumi kwa vitambulisho vyote." Alizungumza Lutas.
"Sawa." Alijibu Jecca na kumfanya Lutas ampatie sarafu sitini ikiwa ni gharama za kutengeneza vitambulisho na malipo yake.
"Asante, nitakuja navyo kesho." Alizungumza Jecca kisha akanyanyuka na kuondoka eneo hilo.
Kila mmoja alielekea kwenye chumba chake kwaajili ya kupumzika, na kulipo pambazuka Jecca alifika mahali hapo akiwa na vitambulisho vinne vikiwa na majina tofauti na majina yao halisi huku Mzee Zulam Maluñ akiendelea kutumia jina lake halisi.
Baada ya makabidhiano hayo walienda kwenye hiyo nyumba wanayoihitaji kuinunua huku wakiwa wameongozana na Jecca. Nyumba ilikuwa nje kidogo ya Kijiji cha Zabi lakini yalikuwa ni maeneo ambayo kuna makazi mengine ya watu japo hayakuwa karibu karibu Sana. Waliipenda nyumba, na kuamua kufanya makabidhiano ya kimaandishi na muuzaji huku majirani na uongozi wa kijiji wakiwa mashahidi wa makabidhiano hao.
"Tunashukuru sana Jecca." Alizungumza Lutas.
"Nashukuru pia, na k**a kutakuwa jambo lingine lolote msisite kunijuza. Nitawasaidia."
"Sawa." Alijibu Lutas kisha wakaagana. Maisha mapya ya wale wanne yalianza ndani ya Kijiji cha Zabi uliopo Doma ambao ndio mji mkuu wa Pandora.
*****MWAKA MMOJA BAADAE*****
Ni majira ya usiku wa manane, mazoezi makali sana yalikuwa yakiendelea ndani ya msitu wa Imnwe uliopo nje kidogo ya kijiji cha Zabi. Alikuwa ni Jaran na Máulus mmoja wakiambaa angani juu ya msitu ule huku wakiendelea kupigana. Wote walionekana kwenda sambamba lakini mwalimu atabaki kuwa mwalimu tu, kwani Jaran alizidiwa na kupigwa pigo lililomtoa angani na kumpeleka chini, lakini hakuweza kudondoka vibaya kwakuwa alijizungusha kiustadi na kwenda kutua pasipo kuumia.
"Kidogo, umeanza kuwa imara sasa." Alizungumza Máulus yule.
"Aisee, haya mazoezi magumu sana." Alijibu Jaran.
"Usijari, utayamudu vizuri Sana na itafikia wakati ambao hata mimi sitaweza kupigana na wewe tena." Alijibu Mzee Zulam.
ITAENDELEA...
Haya Sasa, Jaran ndani ya Pandora na tayari mazoezi yameshaanza. Unafikiri atakuwaje baada ya mazoezi hayo? Endelea kufuatilia simulizi hii hadi mwisho.
***
SUPPORT NI NDOGO SANA WADAU, WATU WENGI HAWAJISHUGHULISHI NA KUSHARE SIMULIZI. ILA WAPO WACHACHE TU WANAOJISHUGUKISHA NA KUSHARE.
NITAKUWA NATOA POST PALE MUDA NINAOHISI MIMI NDIO UNAFAA KUPOSTI. MTU ASINIFUATE INBOX KUNIULIZA KUHUSU STORY WADAU.
NAWASHUKURU WANAOSHARE LAKINI MUDA SIO MREFU NITAANZISHA GROUO LA BURE HAPA HAPA FB KWA WALE WANAOSHARE NA KULIKE TU, MIMI NAWAONA WOTE WANAOSHARE NA KULIKE NINAWAONA WOTE HUKU.
KWAHIYO WIKI IJAYO WANAOSHARE ILI KUSUPPOT KAZI NDIO NITAKAOWAUNGA KWENYE GROUP LA BURE, NA NINYI MNAOINGIA NA KUSOMA TU MTABAKI HAPA NA STORY ZITATUMWA KWA MUDA NITAKAOUHITAJI MIMI. LAKINI MTAKAOKUWA KWENYE GROUP LA BURE MTAENDELEA KUPATA STORY ZOTE KWA WAKATI.
SIMLAUMU YEYOTE KWA KUWA SIO LAZIMA KUSHARE, NA WALA STAMDAI YEYOTE PESA KWA KUTOKUSHARE, ILA LAZIMA WAFUATILIAJE NDIO WANUFAIKE ZAIDI YA WANAOINGIA KUSOMA NA KUTOKA NDANI YA PAGE HII PASIPO KUSHARE.
ASANTE.
***
Share kadri uwezavyo ili wengine wajue pia kilichomo ndani ya page yetu. Pia hakikisha unawaalika marafiki zako wajongee kwenye ukurasa wetu.
***
Ukitaka uwe wa kwanza Kupata episode ya mbele ni sh. 200/= tu. Na malipo yote yanafanywa kupitia namba zilizopo hapo juu na utatumiwa Riwaya kwa njia ya Whatsapp au inbox kwa upande wa facebook.