13/12/2025
HATIA
SEHEMU YA 2
MTUNZI: EDWARD BALELE
ILIPOISHIA
Thomas anatoa karatasi kwenye mfuko wake wa suruali,anachukua kalamu na kuandika maneno juu ya karatasi kwa herufi kubwa,"NISAMEHE SANA" kisha anafungua dirisha la chumba hiki kilichopo ghorofa ya sita ya hoteli hii na kujirusha.
ENDELEA....
Bibi harusi Paulina bado yupo bafuni akijitazama na kufurahia jinsi alivyoumbika pengine hii ndio sababu iliyofanya vijana wengi wa kiumbe kuongoza kwa idadi kubwa k**a wafuasi wake mtandaoni.
"Baby,mbona unachelewa,mwenzako nina hamu na wewe nataka nikupe vitu adimu na motomoto"Paulina aliendelea kuongea kwa sauti nyororo yenye uwezo wa kumtoa nyoka pangoni na kumleta wazi mbele ya kadamnasi ya watu lakini licha ya kujibebisha kiasi hicho hakupokea jibu lolote kutoka kwa Thomas.
Uso wake ukaanza kubadilika ni k**a sasa ameanzw kukasirika maana ni dakika kadhaa zimepita na mumewe bado hajaiingia bafuni. Paulina alitoka bafuni kwa hasira,"Thomas kwani unafanya nini mpaka saa hizi huja...."maneno yalishindwa kutoka kinywani baada ya kugundua kuwa alikuwa anaongea peke yake muda wote aliokuwa bafuni.
"Ameenda wapi huyu,usiku huu?"alijiuliza na kisha upepo ukampuliza mwili na wake na kufanya agundue kuwe dirisha lao liko wazi. Paulina alisogea kwenda kulifunga na kwa bahati anaona umati wa watu wakiwa wamemzunguka mtu aliyekuwa amelala chini na huku baadhi ya watu wakiwa wananyooshea vidole vyao kuelekea dirisha lake lilipo.
Uchungu unamwingia haraka na kupiga kelele,"Thomassss....."anaeguka na kuchukua shuka na kujisitiri mwili wake na kwa bahati mbaya Ile karatasi yenye ujumbe inaanguka chini na upepo unaipuliza na kupotelea chini ya kitanda.
Paulina anateremka chini na shuka lake watu wanamshangaa lakini hajali,machozi yanamtoka. Muda wote analiitajina la mpenzi wake ,ambaye ni mwanaume aliyempenda sana,Thomas.
Anafika chini na kwa nguvu zake anajipitisha katikati ya umati wa watu uliozunguka mwili wa Thomas. Masikini Paulina hofu na mashaka yake vimegeuka kuwa kweli ,ni kweli kuwa aliyelala hapa chini ni mumewe,Thomas Mbuge.
***************************************
NYUMBANI KWA MR MBUGE
K**a nilivyokuambia tangu mwanzo kwamba huu ni usiku mkubwa na sio rahisi kwa wazee wenye umri k**a wa Mr Mbuge kuwa macho hadi muda huu.
Mr Mbuge na mkewe wamelala kitandani,niamini mimi kuwa inahitaji moyo na uvumilivu wa hali ya juu kulala karibu na mwanamume huyu kwani Mr Mbuge k**a usingemjua ungezania kuwa kuna simba ndani ya nyumba hii kwa sababu ya sauti yake ya kukoroma.
Simu yake inaanza kuita na kuwashtua wote wawili. Mr Mbuge anaichukua na simu yake. "Nani tena huyu anayekupigia usiku huu?"aliuliza mkewe,mama yake na Thomas
"Ni mkweo"anajibu Mr Mbuge
"Nani,Paulina?"aliuliza tena mama Thomas
"Ndio,kwani una mkwe mwingine zaidi yake?"
"Anataka nini usiku huu?"
"Sijui,ngoja tumsikilize"
Mr Mbuge anapokea simu na hapo hapo simu inamdondoka mkononi mwake na mshangao mkubwa unajaa kwenye sura yake,Mama Thomas haelewi anamshangaa tu.
ITAENDELEA
simulizi hii itakuwa inakujia Kila baad ya siku moja baada ya sehemu Moja kutoka. k**a unavutiwa na kisa hiki na unapenda kiendelee kupostiwa humu ndani basi usisite ku-like,share na comment ili kunitia moyo zaidi wa kuendelea kufanya hiki ninachokifanya.