04/10/2025
8~~~9
*SEHEMU YA 08*💔
MAMA ALIVYOTOKA KIMAPENZI NA MCHUMBA WANGU
Jenny alibaki amejishika shavuni akiugulia maumivu baada ya kuzabwa kofi asilolitarajia kutoka kwa baba yake,
"Safi sana, hayo ndiyo mambo sasa" mwanamama Sofia aliongea kimoyo moyo huku akitabasamu
"Mjinga kabisa wewe, unataka kuishi k**a upo kwako hapa, nitakurudisha kwa mama yako kule ukakae nae"
"Samahani baba" Jenny aliongea kwa sauti ya chini, akiwa ameinamisha uso
"Basi baba Jenny msamehe binti yako amekosea"
"Potea mbele ya uso wangu!" aliambiwa kwa ukali akatikisa kichwa na kuondoka taratibu kuelekea chumbani kwake huku machozi yakimlenga lenga machoni....
Upande wa pili Henry alikuwa bado amelala kitandani chumbani kwake, akijigeuza geuza kulia na kushoto huku akiwa amejifunika shuka gubi gubi tangu kwenye miguu mpaka kichwani, mlango wake ukagongwa
"Nani?" aliuliza kiuchovu lakini hakujibiwa, ukaendelea kugongwa huku yeye akijigeuza geuza na hatimae mgeni mwenyewe hakusubiri kufunguliwa mlango ambao kumbe haukufungwa, akaingia taratibu, alikuwa ni rafiki yake mwingine
"Oya umelala mpaka saa hizi, una maisha mazuri sana?"
"Hamna nimechoka tu aisee"
"Kilichokuchosha nini demu nini?"
"Hamna jimama moja hivi nimegaragara nalo usiku mzima"
"Jimama tena na siyo Jenny ninaemfahamu mimi?"
"Nilikuwa na mama yake"
"Mama yake tena, kulikoni?"
"Stori ndefu, niambie mzee ume..." kabla hajamalizia sentensi yake akiwa pale pale amelala kitandani, mlango uligongwa tena, rafiki yake akaufuata kwenda kuufungua na kukutana na mwanadada Jenny aliyekuwa anaelekea kazini, akipitia kwa mchumba wake huyo kumuona baada ya kuona simu anazompigia na meseji zake hazijibiwi
"Karibu shem"
"Asante shem, za leo?"
"Salama"
"Sijui Henry yupo ndani?"
"Eeh yupo karibu, pita tu ndani"
"Asante" Jenny alijibu kwa sauti ya chini na kuingia taratibu huku Henry akiwa anatazama amjue mgeni huyo aliyeingia chumbani kwake alipoona ni Jenny akakaa kitako huku uso ukimbadilika kwa hasira
"Kwanini umemruhusu aingie ndani?" alimwuliza rafiki yake
"Sasa ulitaka nifanyaje Henry, kwani si shemeji yangu au, kuna shida gani kwani?"
"Ungeniuliza kwanza"
"Siyo kosa langu" rafiki yake alijibu huku Jenny akishangazwa na maneno hayo ya mpenziwe,
"Kwa hiyo kuingia chumbani kwako nahitaji ruhusa Henry?"
"Ndiyo utaratibu mpya, kilichokuleta?"
"Umepatwa na nini Henry mbona kauli zako sizielewi elewi, simu zangu hupokei na meseji haujibu, nilikuja hapa usiku kujua una tatizo gani sijakukuta naambiwa umeondoka na mwanamke, huyo mwanamke ni nani?"
"Unauliza yote hayo ili?"
"Nipewe majibu, nini shida?"
"Shida siyo mimi, shida ni wewe Jenny, siku hizi unalewa, unalala kwa mwanaume hulali nyumbani sasa unadhani shida ni nani kati yangu mimi na wewe?"
"Unaongea kuhusu nini, mimi nimefanya lini mambo ya ajabu hayo na nani aliyekuambia ujinga huo?"
"Unadhani mimi mjinga mpaka nimtaje aliyeniambia habari hizo, wewe elewa tu kuwa najua mambo mengi sana ambayo wewe huyajui"
"Hata sielewi unachokizungumza Henry"
"Utanielewa tu, naomba mlango ulioingilia ndiyo huo huo utokee"
"Henry, makosa ufanye wewe halafu unihukumu mimi, kosa langu ni nini kwani?"
"Oi jamaa yangu msikilize basi shem mbona ni mdada mmoja yuko poa sana hana mambo mengi?" alitetewa na rafiki wa Henry
"Mimi simtaki sasa k**a wewe unamtaka freshi tu"
"Ndo maneno gani hayo rafiki yangu?"
"Henry unankvunjia heshima sasa, nimekusikiliza na nimechoka kuendelea kuvunjiwa heshi..."
"Samahani, wangu wa ubani ananipigia kidogo hapa" alimkatisha Jenny na kupokea simu huku akiweka sauti ya juu (loud speaker) ili wote wasikie
"Babe umeamkaje?" sauti ya mwanamke ilisikika ikiongea kwa kudeka
"Nimeamka vizuri tu nambie mamy?"
"Nimekumisi tu natamani tuonane k**a jana"
"Waaoooh hata mimi nimekumisi pia tena usinikumbushe zile raha za jana, za moto sana, mwanamke umeniweza wewe" Henry aliongea kwa makusudi huku akimtazama Jenny ambae alikuwa ameshikwa na hasira na machozi yanamlenga lenga
"Sawa Henry, asante, nashukuru sana, nashukuru" Jenny aliongea huku akijifuta futa machozi akageuka kuanza safari ya kutoka chumbani humo
"Shem Jenny, subiri kwanza" rafiki wa Jenny alijitahidi kumzuia
"Niache shem imetosha" alimzuia huku akitoka na kuubamiza mlango
"Umefanya nini sasa Henry mbona unakua k**a haujakua kiakili vile?"
"Dawa ya moto ni moto kaka" alijibu huku akikata simu ya mwanamama Sofia ambayo ilikuwa hewani bado, rafiki yake akatikisa kichwa kumsikitikia....
*SEHEMU YA 09*💔
Jenny alifika kwenye kibarua chake kipya tayari kuanza kazi, moja kwa moja akaongoza mpaka ofisini kwa meneja akabisha hodi na kukaribishwa ndani alimomkuta kwenye kiti chake k**a kawaida anaongea na simu kwa sauti ya chini ikionyesha anazungumza na mwanamke huku akizunguka zunguka kwenye kiti chake,
"Sema" alimwambia alipomaliza kuongea na simu
"Habari ya saa hizi?"
"Njema kabisa mrembo, karibu"
"Ndo nimekuja kuanza kazi"
"Oooh sawa nenda kaanze"
"Bado sijaelewa utaratibu wa hapa na ofisi yangu ni ipi?"
"Oooh utaratibu ni mdogo tu, ni wewe kuchukua sare zako za wahudumu na kuzivaa kisha kwenda kuungana na wenzako kuhudumia wateja, simple tu"
"Lakini bosi, kazi niliyokuja kuomba mimi siyo ya kuhudumia wateja ila ni ya utunza fedha, k**a kumbukumbu zako ziko vizuri na ndivyo jana ulivyoniahidi nikija leo nianze kazi"
"Kwa hiyo hutaki kazi?"
"Hapana siyo kwamba sitaki kazi ila..."
"Ila nini?"
"Sawa nimekuelewa"
"Nenda huko kaulizie sare zilipo uvae uanze kazi, mengine tutaongea baadae"
"Sawa, samahani" Jenny alijibu kiunyonge na kugeuka taratibu akiondoka huku bosi huyo akimsindikiza kwa macho ya uchu mpaka alipotoka ofisini kwake humo, kwenye korido akakutana na muhudumu aliyevalia sketi fupi ili juu ya magoti tena yenye mpasuo, mapaja yote yakiwa nje, akipita
"Dada samahani" alimsimamisha
"Shida yako?" mwanadada huyo alimwuliza
"Naulizia zinapopatikana sare zenu za kazi, bosi kaniambia nami nivae" Jenny aliongea, mwanadada huyo akamtazama kwa kumpandisha na kumshusha kabla hajamjibu chochote
"Mimi nikadhani una kitu cha maana cha kuniambia, sare si uzitafute" alijibiwa kwa nyodo
"Sasa na wewe Tunu kibaya kipi, si unamwelekeza tu mtu anakuelewa kuliko kuanza kumchamba dada wa watu mgeni?" muhudumu mwenzake alimshangaa alipowakuta
"Mwelekeze wewe kwani huna mdomo au?" alimjibu na kuwaacha
"Usijali shoga yangu ana mastress yake tu yule, ulikuwa unaulizia sare?"
"Ndiyo dada, shikamoo"
"Marahaba, naitwa Farida, wewe unaitwa nani?"
"Naitwa Jenny"
"Ooh Jenny, jisikie huru kabisa, na twende nikakuonyesha zilipo sare ukabadilishe uanze majukumu yako"
"Asante dada" walishikana mikono wakaondoka kuelekea kwenye chumba cha kubadilishia nguo, walipoingia alimpa sketi na blauzi nyeupe akavaa, sketi ikiishia juu ya magoti, mapaja yote yakiwa wazi
"Umependeza sana?"
"Mh siwezi fupi sana"
"Aaah mbona ndo nzuri na hakuna nyingine na ndo sare ndo hizo"
"Mh mimi nguo za aina hii sivaagi, siziwezi"
"Ndo ujaribu, vaa tu kwani shida iko wapi, usichokizoea unajifunza" Farida alimwambia, Jenny akaanza kutembea kwa wasiwasi na taratibu kutokana na sketi hiyo fupi na ya kubana iliyomshika mwili wake, hakuwa na namna zaidi ya kukubaliana na hali halisi na muda huo huo simu yake iliita akapokea na kumuomba radhi Farida kisha akaenda pembeni ili kuzungumza, alikuwa ni rafiki yake aliyemuelekeza kwenye kazi hiyo
"Vipi Jenny, kimya shoga yangu au ndo ushapata tena kazi niliyokuunganisha, umuhimu sina?"
"Mh ndo maneno gani hayo wakati tangu jana usiku mpaka leo asubuhi nimekutafuta lakini hupatikani kwenye simu jamani?"
"Halafu kweli, simu yangu iliingia maji hapa penyewe, vipi kazi inaendaje?"
"Kazi yenyewe uliyoniambia mbona siyo yenyewe jamani, nimekuwa muhudumu tena?"
"Muhudumu, hajakuweka kwenye uhasibu?"
"Wewe hukuongea nae labda"
"Atakuweka tu, wewe zuga zuga kidogo si unajua tena, kwani chuo hujaenda eeh?"
"Sijaenda chuo na sitoenda tena tulishamaliza mitihani ilikuwa ni kujisomea somea tu na kwa sababu sikuwa na ishu"
"Sasa mambo si ndo hayo, poa nitakucheki baadae wangu nina kazi hapa naimalizia"
"Sawa best ila asante kwa connection hata hii niliyopata"
"Usijali Jenny" rafiki yske alijibu na kukata simu
"Umemaliza twende zetu?" Farida alimwuliza alipomaliza kuongea na simu
"Nimemaliza dada twende" waliongea wakiongozana taratibu huku Jenny akitembea taratibu na kwa kunyata kutokana na sketi iliyoishia mapajani ambayo pia ilimbana, walipokatiza karibu na ofisi ya meneja, Farida akamshika mkono kumzuia ili wasimame
"Kuna nini dada Farida?"
"Sikiliza vizuri" alimwambia wote wawili wakatega sikio
"Uuuuuwiii meneja jamani jamani mh taratibu!" walisikia mayowe ofisini ya Tunu akilalamika kimahaba
"Mtoto mtamu sana wewe, ooosh aaaah!" meneja nae alisikika ikionekana walikuwa bize kunyanduana ndani ofisini
"Sitaki kuzunguka kwa wateja nataka nikae nihesabu hela tu"
"Hiyo imeisha Tunu, tukitoka hapa tu unaanza kazi, inua mguu kidogo ooooh yeaaaah" Meneja aliongea huku akiguna na mihemo ikiendelea kati yao
"Umesikia hiyo Jenny, hapo sahau kuhusu kuwa muhasibu, sahau kabisa!" alimwambia
"Ooooopppsss!" Jenny akashusha pumzi aliposikia habari hiyo kuwa tayari kuna mtu anatoa kitu ofisini ili kuipata nafasi hiyo hiyo ambayo yeye ndiye ameahidiwa.
ITAENDELEA...